Daniel Chongolo awa Katibu Mkuu CCM

Daniel Chongolo awa Katibu Mkuu CCM

Halafu anawaambia yeye na nanii ni kitu kimoja [emoji23][emoji23]
😄😄😄
202104340340.jpg
 
Kutanguliza maccm badala ya Nchi ni makosa makubwa sana na itaendelea kuigharimu sana Tanzania kwa miaka mingi ijayo.
Realistically, Samia hana option nyingine ila kuweka chama mbele ama sivyo watamtema! Kule ccm hana budi kuwa beneti na Mangulla asikubali aondoke haraka haraka kabla hajakisoma chama vizuri; watamkorofisha!
Give her the benefit of doubt !
 
yaani konda boy kila sehemu huwa amenyea kambi...., kwa VP mpango alinyeaga kambi wakati anamkoromea inshu ya makontena yake bandarini kodi..., haya huku tena kwa SG Chogolo alishamkoromeaga....kwa PM Maja pia alishanyeaga kambi....
Orodha ni ndefu sana, hata waliompa ifadhi wakati amefukuzwa shule baada ya kuwa RC alikuwa hapokei simu zao.
 
Petty issues
Mshikaji amekulia eneo fulani linaitwa Twico kwenye kiwanda cha mbao cha Sao hill- Mafinga.

Ametoka kwenye media akiwa mwandishi wa habari wa gazeti la Uhuru. Amejitahidi kutatua changamoto za ardhi akiwa Longido kbl ya kuhamishiwa Dar.

Yupo humble, si mtu wa majidai, mwenye uwezo fulani wa kutatua changamoto.

Tukiondoa ujuaji uliopo CCM kwamba wapo wenye CCM yao dogo anaweza kumudu!

KILA LA KHERI
 
Zambia na Zimbabwe kuna vivuli vya uchaguzi tu. Ni udikteta mtupu.
Ndugu, kama humjui Chongolo ungekaa kimya.
Kalelewa ndani ya CCM kuanzia akiwa UVCCM na akina Nape, Nchimbi, Bashe nk. Ndie aliekuwa master mind wa kampeni za kuhuisha chama kwenye ziara ya miaka mitatu waliyofanya kuzunguka nchi nzima kipindi kile wakiwa na katibu Mkuu Abdulrahmani Kinana na Nape Nnauye. Ana masters ya uongozi kutoka Mzumbe University na kapata mafunzo maalum ya siasa na uongozi Urusi. Amekuwa akitumwa kwenye uangalizi wa chaguzi mbalimbali nje ya nchi kama mwakilishi wa CCM, zikiwemo Zambia, Zimbabwe, Malawi nk. Usimchukulie kirahisi rahisi namna hiyo mazee.

NYONGEZA
Kabla hajateuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Longido mnamo 2016, alikuwa ndie Mkurugenzi Mkuu wa vombo vya habari vya CCM kwa maana ya Magaeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani na redio Uhuru. Alipoteuliwa akaacha ukurugenzi na kwenda kutumika Longido mkoani Arusha, kisha akahamishiwa Kinondoni. Siri yake kubwa ni kwamba anapenda kufanya mambo yake KIMYA KIMYA sana, huwezi kujua kirahisi. Hata kwenye chama hana umaarufu mkubwa wa kelele kama akina Nape, Makonda, Gambo, Kheri James na wengine.
Sasa mtu aliyeaminiwa kiasi hiki hawezi kuwa mwepesi mwepesi.
 
CCM ya zamani wanawajua wote walio wa kwao, ya Mwendazake ndio ilikuwa ikichukia watu huku na kule kuwaleta chamani. Leo tuko na raha tele!
yaaa,
Jamaa ni silent operator, ndio sababu watu wanadhani ni mgeni kule CCM. Hawajui kwamba ndie aliekuwa mkurugenzi wa media za CCM, redio na magazeti na yuko chamani kitambo sana
Halafu huyu jamaa anakipenda chama balaa,mimi mwenyewe nilikuwa sijui kana ana nafasi gani chamani.Ila nakumbuka siku moja mke wake alilazwa kwa ajili ya kujifungua yeye akiwa kwenye shughuli za chama huko Shinyanga,alivyotaarifiwa kuwa mkeo amelazwa,alimuomba bro ake mmoja aendelee na hilo yeye alisema mpaka amalize shughuli za chama kule ndiyo anaweza rejea.nakumbuka ilikiwa ni kipindi kile Mzee Lowasa anakimbiza show ya uchaguzi dhidi ya Mwendazake.Kila mtu alimshangaa Daniel.
 
Achana naye huyu YEHODAYA. Ukifuatilia comments zake humu utagundua ni Mtu aliye panic sana, nahisi Ni mmoja wa waliokuwa wanategemea hiyo nafasi na kama sio yeye basi alitegemea atateuliwa mmoja katika Timu yake.

KAJAA WIVU BALAA
Nina wasiwasi isije ikawa ni bashite maanake inaonekana kamaind big time.
 
Back
Top Bottom