Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amesema Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeanza mchakato wa kuboresha sekta ya usafiri wa bodaboda kwa kusajili madereva, kuwapatia namba za utambulisho, vituo rasmi vya kuegesha, na mavazi yatakayoongeza imani na usalama wa huduma wanazotoa.
Akizungumza katika kongamano maalum la maombi na dua kwa madereva wa bodaboda na bajaji, lililofanyika jijini Dar es Salaam, Mpogolo amesisitiza umuhimu wa sekta hiyo katika uchumi wa miji na usafiri wa kila siku. Ameeleza kuwa hatua hizo ni sehemu ya juhudi za serikali kuhakikisha huduma za usafiri wa bodaboda zinakuwa salama, nadhifu, na zinazoaminika zaidi kwa wananchi.
Katika kongamano hilo, Mpogolo ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanailinda amani ya taifa, hasa katika kipindi hiki cha maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Akizungumza katika kongamano maalum la maombi na dua kwa madereva wa bodaboda na bajaji, lililofanyika jijini Dar es Salaam, Mpogolo amesisitiza umuhimu wa sekta hiyo katika uchumi wa miji na usafiri wa kila siku. Ameeleza kuwa hatua hizo ni sehemu ya juhudi za serikali kuhakikisha huduma za usafiri wa bodaboda zinakuwa salama, nadhifu, na zinazoaminika zaidi kwa wananchi.
Katika kongamano hilo, Mpogolo ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanailinda amani ya taifa, hasa katika kipindi hiki cha maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.