Dar es Salaam: Mchakato wa ufuatiliaji simu zilizoibiwa kupitia Vituo vya Polisi una ‘harufu ya michezo michafu’

Kuipata simu yako iliyoibiwa ni kazi rahisi sana ila Kwa Sasa polisi ndio wanafanya kazi ionekane ngumu

Kuitrack simu iliyoibiwa sio lazima TCRA hata mitandao ya simu Kwa kushirikiana na polisi simu inapatikana tu kirahisi

Mbaya zaidi kibaka amekuibia simu ukilipoti polisi na polisi nae anakuibia tena simu hiyo hiyo
 
Wanachofanya polisi ni kufuatilia hizo simu kisha wanajimilikisha wao wenyewe na ndiyo maana hata uhangaike vipi huwezi kuzipata
Kwa simu za maana, ama wanajimilikisha au wanauza katika mtindo ambapo hazitakamatwa tena hasa kama mmiliki wa simu aliyeibiwa ni raia tu wa kawaida. Mmiliki akiwa mtu mkubwa, simu inapatikana haraka na kurudishwa kwake.

Simu za hovyo hovyo na zenye ubovu fulani, zinalundikwa kwa pamoja, halafu raia wanaitwa kuja kutambua simu zao, huku camera za waandishi wa habari zikiwa on. Hii ni kwa ajili ya kuuaminisha umma kuwa jeshi linafanya kazi kwa kwa uaminifu.
 
Mwenye simu aliyeibiwa anaombwa rushwa na simu hapewi. Aliyeiba au kuuziwa simu akikamatwa anazushiwa kesi ngumu kama mauaji au uporaji na anipa pesa ndefu kujinasua. Ndiyo maana mshahara wa polisi haufiki one million, lakini anajenga nyumba kwa miezi 3 anahamia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…