TRA Tanzania
Senior Member
- Jul 16, 2022
- 128
- 370
Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Doto Biteko ameshuhudia utiaji saini wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania, (TCCIA) katika kuboresha uhusiano na walipakodi. Halfa hiyo imefanyika hivi karibuni wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa TCCIA uliofanyika jijini Dar es Salaam.