Kibali cha kurusha hiyo Helcopiter wanacho tangu tarehe 4/09/2020 mpaka 30/10/2020 ila tatizo lao ni rubani. Pia wamiliki wa hiyo ndege hawakuwa na plan ya kupaa leo. Inaonekana Chadema hawakuambiwa hali halisi na mmiliki wa ndege kuwa wamenyimwa waiver ya kumtumia rubani aliyezidi umri wa miaka 65. Lakini nasikia tatizo lingine Chadema hawajamlipa pesa huyo mmiliki wa ndege hivyo amewapiga chenga ya mwili mpaka walipe advance. Chadema waishukuru TCAA kwa kukataa rubani huyo aendeshe ndege na kufuata sheria tuliojiwekea. Pia na shangaa kwa nini Chadema waliwadanganya watz kuwa ndege imenyimwa kibali cha kuruka wakati wakijua sababu ya ndege hiyo kutokuruka??