Dar: Inasemekana tukio hili la utekaji limetokea Kiluvya, kutokana na uzito wa jamaa walishindwa kumchukua. Hakuna aliyetoka kumsaidia

Tlaatlaah Muda SI mrefu mtaanza kuokota mizoga ya mno watuma.
jambo la kwanza hakuna mtekaji kati ya hao. ni genge la visasi tu hilo dhidi ya dhuluma au madeni

Lakini jambo la pili,
ukiwa mkorofi na mbabe mwenye dharau mtaani hakuna atakae thubutu kusaidia hata wakukute umegongwa na gari unakata roho.

Jambo la tatu,
unaweza kua jeuri na mbabe kwenye eneo lako la kujidai na kuonea wanyonge wako. Nje ya hapo vitoto vidogo tu vinakutoa jasho jitu zima na miguvu yako. Mathalan huyo jamaa atakua anatetemeka na kuvibrate miguu kama kiswaswadu..


Ishi vizuri na watu,
achana na kumendea mendea vitu vya watu ikiwa ni pamoja na wake zao, acha dhuluma na ubabe ambao ni useless 🐒
 
ni muhimu sana kuishi na watu vizuri, mtaani na popote pale.

ubabe, dhuluma, dharau na mizaha kwa mali na wake za watu vina matokeo mabaya sana hasa kwa wasiopenda kuongea bali kutenda.

heshimu wengine nawe utaheshimiwa na kusaidiwa ikiwa unahitaji msaada. vinginevyo watakutazama kama movie tu na kiburi chako unavyo nyoroshwa na wababe wako.

epuka tamaa, yatakutokea puani 🐒
 
ndani ya gari kulikuwa na mtu ,na mtekwaji alivyomwona tu SAUTi yakuomba msaada ilikuwa kubwasana .....pasiposhaka yule dogo white ameonekana vizuri sana..
 
Endelea kujidanganya
Je,Huyo Mtu kajulikana?
Je ni kwa sababu zipi walitaka kumteka?
Je alikuwa anatumia mtandao gani kwenye simu?
Je alikuwa anatumia social media gani kwenye mtandao (kisiasa) Instagram, Twitter, Facebook, au JF?

Bora uongelee Miziki, Simba, Yanga, Pombe au msambwanda n.k ili wasikuteke.

Muda umefika Mungu aingilie kati.
 
Tusishabikie kila kitu nakubpost pamoja na makosa mengine uhalifu umekuwa mkubwa sana kwa kiwango cha kutisha huko mbeleni watu watapigwa risasi live sitaki kuamini huyu ni mtu wakisiasa lazima atakuwa kuna jambo anafanya na walikuwa wana msaka.
Nje ya siasa uhalifu dhidi ya Taifa lako ni jambo la hatari kwa maisha yako. Mama mkanye mwanao mama mkanye mwanao.
 
kama kuna jambo wanamsaka, si wamkamate kisheria? unafika pale, umevaa nguo za kipolisi, unampa tuhuma yake, na kumwambia wende polisi kwa sababu upo chini ya ulinzi.

kumkamata kinguvu hivyo ni kwa sababu watanzania hawajaamka, kuna siku watakuja kuchomwa moto hao.
 
Nje ya siasa nilazima kila Raia wa Taifa hili ajuwe yeye na kizazi chake crime is dangerous and it can end you are life.
Nimeweka hii video kuonyesha vile huko Kenya watu walikuwa wana uwawa live kwa uhalifu.
Hatuwezi kuruhusu Taifa hili kuwa lamajangili ni hatari kwa uwepo wetu. Uhalifu wa aina yeyote hauwezi vumiliwa. Yaani kama mnafikiri huyu mama mtamgeuza kama chapati basi msije jishangaa mkageuzwa kama chapati.
 
Yaani mtu anatekwa mchana kweupe halafu raia wanatazama tu😬 Ubishi wa wabongo ni kwenye Simba na Yanga tu
 
Nimpe pole jamaa kunasuka hapo, maana wange mu RIP, pili inasikitisha sana wabongo hawasaidii wanamuangalia mtu akiwa matatizoni, baadae watume RIP

Aisee jamii inahitaji revolution , hii ni zaidi ya ukondoo
Ila angalau aliyepiga picha na video katusaidia kuwajua..Tunasubiri ufanafanuzi wa jeshi la polisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…