TANZIA Dar: Pacha Rehema aliyebaki baada ya kutenganishwa naye afariki dunia

TANZIA Dar: Pacha Rehema aliyebaki baada ya kutenganishwa naye afariki dunia

Pole kwa wafiwa.

Madaktari wasivunjike moyo, hata mbuyu ulianza kama mchicha, ni kweli kibinadamu inaumiza kuna watu watahisi madaktari wanachezea uhai wa watu.

Ila hakuna mafanikio bila majaribio kadhaa yaliyoshindikana, inaumiza tu kwa kuwa ni binaadamu mwenzetu, hata huko kwa wenzetu yanatokea, si kila wanalofanya wanafanikiwa.

Watanzania tujifunze kupunguza lawama, tunawavunja moyo watu wanaojaribu kutafuta namna ya kutuponya hapa hapa nchini.
Umeandika vema, lakini tuna madaktari hapa Tanzania nadhani hizo lawama zinawahusu,, mimi ni mhanga wa moja wa madaktari hao.. Afya imekua biashara na sio huduma tena
 
Wangewaacha tu pengine wangeishi maisha marefu tu kama wale Maria na Consolata.

Mbwembwe kibao,makamera chumba cha upasuaji na battalion ya mabingwa room imefulika km Simba day.
 
Pole kwa wafiwa.

Madaktari wasivunjike moyo, hata mbuyu ulianza kama mchicha, ni kweli kibinadamu inaumiza kuna watu watahisi madaktari wanachezea uhai wa watu.

Ila hakuna mafanikio bila majaribio kadhaa yaliyoshindikana, inaumiza tu kwa kuwa ni binaadamu mwenzetu, hata huko kwa wenzetu yanatokea, si kila wanalofanya wanafanikiwa.

Watanzania tujifunze kupunguza lawama, tunawavunja moyo watu wanaojaribu kutafuta namna ya kutuponya hapa hapa nchini.
Trials + Errors=Perfect
 
Katika ya sekta ya afya, idara iliyo nyuma sana ni clinical care baada ya operation.

Hapo ina maanisha clinical service, nursing na kwa ujumla uangalizi wa mgonjwa baada ya operation.
Hapa Tanzania tuko nyuma sana.

Ni heri hao watoto wangetenganishwa na kubaki India.
 
RIP Pacha. Hivi Madaktari wa bongo wamesomea nn?
No, tusianze kuwalaumu madaktari wakati hatujui muunganiko wa watoto hao ulikuwaje. Yawezekana kulikuwa na utata (complication).
 
Taarifa mbaya kabisa hii.

Apumzike kwa amani binti yetu
 
No, tusianze kuwalaumu madaktari wakati hatujui muunganiko wa watoto hao ulikuwaje. Yawezekana kulikuwa na utata (complication).
Kama kulikua na utata why walifanyiwa operation?huwezi aka bet kwenye uhai wa binadamu, nchi zinazojielewa permits za madakitari hawa zingesimamishwa hadi tume huru ya wataalamu ije na mrejesho, huyu mama mfiwa iM sorry hakuna kitakachofanyika kwake, Angelus kwenye nchi zinazojielewa ,angemfungulia kesi ya madai waziri wa afya, hospital iliyo fanya operation hii,na madakitari, but bongo land hawa doctors maisha yao yanaendelea Maana wao na familia zao ni matibabu UK,India, US au Millpark med clinic
 
View attachment 2321684
Mtoto Rehema ambaye ni pacha aliyekuwa amesalia baada ya mwenzake waliyetenganishwa kufariki dunia, naye ameaga Dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), jana Agosti 11, 2022.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa MNH, Aminiel Aligaesha amesema: "Ni kweli amefariki jana saa tano asubuhi".

Watoto hao walifanyiwa upasuaji wa kutenganishwa Julai Mosi, 2022, pacha wa kwanza, Neema alifariki Julai 10, 2022.

Pia soma:
Pacha waliotenganishwa, mmoja afariki dunia
Tangu awali binafsi nilisema kutenganishwa na kufanikiwa kwa iparesheni ni mambo mawili tofauti, hats hivyo haukupita muda mmoja alifariki na sasa huyu naye amefariki!, pole mama mzazi wa mapacha hawa.
 
Wenzetu nchi zile juzi tu wametenganisha watoto walioungana ubongo! Sisi bado sanaaa!
 
Back
Top Bottom