mafinyofinyo
JF-Expert Member
- Nov 29, 2012
- 4,404
- 3,275
Wenye macho na masikio tutajifunza kitu!Najaribu kuwaza tu
Hivi ikafika mwakani na mange akafa ama akadhurika
Faida yake nini,
Sifa zitamuendea Mungu ama shehe, ama uchawi?
Mange alikunywa kikombe cha babu wa loliondo halogekiFor sure hichi kimange sikipendi kabisa akiroge kisitukane watu tena
Kiroge tu Shekhe kikome
Ungekuwa wa kujibu ungeanza kujibu wewe niliyekuhoji ina maana kwavile Mange kasema ndo basi tena unakubali kila kitu bila kutumia uelewa wako mwenyewe!!!Nijibu ninacho uliza
Hii lawama ya kuchanganya dini Na siasa nalaumu mm ama aliongea mange?
Alijua atafanya hivyo anavyofanyaKule kwa Mange ni hatari tupu. Shehe anarushiwa kashfa za kufa mtu. Kama kashfa ni za kweli shehe ataumbuka sio mda mrefu. Wale waliowahi kufanywa wanaweza kumtumia Mange video na mapicha
Shekh ungesimama kwenye haki haya yasinge kukuta,ungekuwa pia yanapotokea manyanyaso ya watu wasio na makosa,kama tungesikia unatoa kauli kuwa serikali ina kalia demikrasia,serikali inawanyanyasa wananchi wanayoikosoa na kuwaonea wapinzani,na pia alipo pigwa risasi Lissu ungetoa kauli basi Leo hii usingeyapata haya,simama katika surati mustakim kuwa mkweli hayo ndio mafunzo ya mtume hakuwa mnafiki,ndio maana mpaka Leo anaheshimika,
Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhad Mussa Salim hivi sasa anazungumza na waandishi wa vyombo vya habari kuhusiana na kuhusishwa na kampeni zinazoendelea katika Jimbo la Kinondoni.
=====
Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Mussa Alhad ameelezea picha inayosambaa kwenye mitandao inayomuhusisha yeye kufanya kampeni ambayo yumo yeye na pembeni kuna mgombea wa CCM jimbo la Kinondoni, Maulid Mtulia akila chakula pamoja na wenzake wa CCM. Amesema picha ilipigwa akiwa kwenye maziko ya Sheikh Masoud Ismail, amesema yeye ni kiongozi na mtu yeyote anaweza kupiga picha na yeye.
Amedai Mange Kimambi amekuwa akitukana viongozi mbalimbali kwenye Instagram na kusema pia alimtukana mufti wa Tanzania baada ya kuipongeza serikali na Rais John Magufuli.
Sheikh Alhad amesema ametukanwa kwa dhulma na uadui na kudai Mange anautumia ulimi na mikono yake vibaya kudhulumu watu(Heshima zao).
Alhad amesisitiza huu ni mwaka wa mwisho kwa Mange na baada ya mwaka huu hatamtukana mtu yeyote kwa kutumia ulimi au mkono wake kwa sababu amejihalalishia mwenyewe maangamizi kwa mkono wake. Amesema atamshtaki kwenye mahakama ya Mbinguni.
Juu ya tuhuma za Sheikh kushiriki siasa, soma => Picha za Sheikh Alhad Mussa na makada wa CCM zinatoa tafsiri gani? BAKWATA toeni ufafanuzi
Amesema kuna watu walimpa rai asimjibu kwani atamtukana sana na kudai wao wanataka aendelee kutukana na hatasikia sauti yake baada ya leo ikimjibu na yeye andelee kutukana.
Alhad amesema hawezi kujiingiza kwenye kampeni ya kuipigia debe CCM, amesema CCM ina kawaida ya kualika viongozi wa dini na chama chochote kinaweza kumualika kwenye jambo lake. Amesema ajabu, picha zake ndio zinaanikwa lakini za viongozi wengine hazianikwi.
Katika hatua nyingine, Sheikh ameiambia NEC kuhusu JamiiForums ambao wameandika kwamba sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam: Hivi mnajua kama anafanya kampeni Kinondoni! Alhad amesema watachukua hatua za kisheria ili wathibitishe sheikh wa mkoa wapi amefanya kampeni, kwa kuhudhuria kwenye maziko au sababu ya picha!.
Hivyo kuhusu JamiiForums, wataona namna gani ya kushughulika nao kisheria na wengine wote ambao kwa namna moja au nyingine, wajiingiza katika jambo hilo kichwa kichwa bila kulijua ili kuvunja heshma zao.
Kwa hiyo yeye alianza zamani kuchanganya siasa na dini! Hapa kinachokera ni kwa nini awatuhumu wenzie (kina Bagonza ) wakati yeye ni mdau mkubwa wa kuchanganya?? Angepiga kimya kama alijua kuwa si msafi katika hili na hakuna ambaye angejali!Ungekuwa wa kujibu ungeanza kujibu wewe niliyekuhoji ina maana kwavile Mange kasema ndo basi tena unakubali kila kitu bila kutumia uelewa wako mwenyewe!!!
In short, huna cha picha wala nini ila unashindwa tu ku-admit kwamba umelishwa matango pori... umewekewa picha za February 2014 nawe ukaamini kwamba ni za sasa simply because Mange ndiye aliyeweka hizo pics!
Stay blessed!!!
Hakuna lolote hapo,Mange hafi na hakuna kitakacho mpata,huyo alisema hayo hana lolote,Kama angekuwa yeye mungu kweli,mungu hana mshirika na apangiwiNajaribu kuwaza tu
Hivi ikafika mwakani na mange akafa ama akadhurika
Faida yake nini,
Sifa zitamuendea Mungu ama shehe, ama uchawi?
Ni wapi alipochanganya dini na siasa?! Umeshaambiwa, ile picha ambayo watu walikuwa wanatandika ubwabwa ilikuwa ni msibani... kuna Sheikh kafariki K,nyama na Sheikh Mkuu alikuwa pale. Jama wa CCM walipomuona, wakaenda kumjulia khali.Kwa hiyo yeye alianza zamani kuchanganya siasa na dini! Hapa kinachokera ni kwa nini awatuhumu wenzie (kina Bagonza ) wakati yeye ni mdau mkubwa wa kuchanganya?? Angepiga kimya kama alijua kuwa si msafi katika hili na hakuna ambaye angejali!
Sawa nafasi aliyonayo ni kubwa sana lakini kaamua kuidhalikisha kwa sababu ya njaa na tamaa ya mali ndo maana kaamua kuitumbukiza siasa katika kipawa chake ili tu afurahie maisha ya duniani huku akihubiri wenzie wasiangaikie msisha ya duniani(UNAFIKI)Kuwa katika position kama yake sio kitu cha mchezo mchezo tu
Maana ingekuwa ni rahisi hata wewe ungekuwa hapo
Lakini ana kipawa ambacho Mwenye Enzi Mungu anemtunuku!
Ndiyo maana kwenye Biblia Takatifu Mfalme Daudi hakuthubutu kumwuua Mfalme Sauli, tena alimwita mpakwa mafuta wa Mola, akamwambia Mwenye Enzi Mungu pekee ndiyo atakaye kuhukumu!
Hivi viti wanavyo kalia wakuu wa dini sio vya mchezo, ni watu wanao shika roho za watu yaani ni IMANI!
Tuwe wasngalifu sana kwenye maswala haya!
Tusiwafanye wakakunja roho zao!
Kweli nawaambia mwisho wake huwa sio mzuri hata!
Huyu Jamaa angekuwa na uwezo huo angeua watu wengi sana kumbe ni tapeli tu, eti nitaishitaki JF kwa kutoa habari hiyo
Mkuu hapa ndio Shehk anasema alikuwa kwenye msiba...???Oh! Kumbe Mange...!! Yaani kwavile Mange kasema ndo basi tena unashindwa kutumia uelewa wako mwenyewe kupima?!
Kwanza nini maana ya kuchanganya dini na siasa?! Huyo Sheikh alikuwa anaongea mambo ya siasa msikitini hadi useme anachanganya dini na siasa?!
Isitoshe, picha ambayo uliisema wewe ni hii hapa:
View attachment 691081
Hapo juu unaona maelezo yanasema " Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu Akimkarisbisha Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam"
Hivi sasa Mbunge wa Temeke ni Abbas Mtemvu?!
Maelezo zaidi ya hiyo picha yanasema:
Kumbe kulikuwa na Mkutano Mkuu wa Jimbo la Temeke... lakini kwa kuwa mnameza kila mnacholishwa na Mange, mkakubali tu kwamba alikuwa kwenye kampeni za Ubunge Kinondoni!!!
Lakini mbaya zaidi, ni wakati Mbunge wa Temeke ni Abbas Mtemvu ambae hakurudi tena bungeni kwenye uchaguzi wa 2015. Kumbe kwa maana nyingine, mmelishwa matango pori kwa kuwekewa picha za zamani!!!
Picha zingine za hilo tukio ni hii hapa:
View attachment 691083
View attachment 691086
Na hili usidhani kwamba ni photoshop, tukio zima lipo hapa!
Au ni picha zipi hizo unazosema kwamba alikuwa anachanganya dini na siasa?!
Huo ni Mkutano wa CCM Temeke mwaka 2014 na yeye alienda pale kama Mgeni Mwalikwa! Na ulikuwa ni mkutano wa ndani wa kuchagua viongozi wa Jambo!!Mkuu hapa ndio Shehk anasema alikuwa kwenye msiba...???
Me naona ni kama mkutano wa chama...,au ni macho yangu..???
Hebu Shehk atueleze vizuri maana kwa pembeni naona kiboa kimeandikwa Albino Cultural.........