Dar: Wakazi wa Nyumba za NSSF Kigamboni, watolewa kwa Mabavu

Dar: Wakazi wa Nyumba za NSSF Kigamboni, watolewa kwa Mabavu

Kabla hujarukia sababu zako, jaribu kufika eneo la tukio kupata ukweli.

Kuna tatizo kubwa sana kwenye hii NSSF tangu enzi za Dau kuhhsu zile nyumba pale.

Ukweli ni kwamba, wale wamepangishwa kwa kodi inayozidi Tshs milion 1 kwa mwezi na wanapaswa kuilipa NSSF milioni tatu kila baada ya miezi mitatu, ikifika kuanzia milioni 120 na kuendelea ndo unapewa nyumba yako.

Nyumba yenyewe hata kwa Tshs 300,000 kwa mwezi haipangishiki labda kwa bei ya juu ya Tshs 200,000 kwa mwezi.

Nimejaribu kukuelezea uhalisia ambao Bodi ya NSSF inajutahidi kuuficha kwa gharama kubwa na kuidanganya mamlaka ya juu nchini.
Option ni kurudisha tu hizo nyumba, mimi nina nyumba ya kuishi ila nilivutiwa kuchukuwa moja kule kwenye mradi wa Pspf wa Buyuni Chanika, nyumba niliyochukuwa ni category three ya million 74 kwa miaka 15.

Nilitowa deposit ya million 5 nikamuweka mtu akae baada ya mwaka mmoja ndio vikaanza kuja vikokotoo na nilivyopiga hesabu kwa miaka 15 maana yake unawalipa million 100 na kitu, na hapo ndio wakafosi kila mwezi tulipe laki sita au zaidi, kumbuka kipindi hicho tayari Magufuli ameshaharibu uchumi wa nchi tukapewa demand note na dalali wao nikaona isiwe tabu nikarudisha na aliyeiomba kuingia tukafanya makubaliano akanilipa gharama zangu za grill nikairudisha nyumba niliona hapa natafuta stress bure.

Ila taarifa nilizonazo bei ya hizo nyumba zimeshushwa baada ya Jenister Mhagama kufanya vikao vingi na wakazi, tatizo kubwa la miradi ya nyumba ni ya kifisadi na kuover rate, ukiwa na kiwanja chako million 40 unajenga nyumba ya kisasa kabisa.

Kingine hizo nyumba kabla ya watu kuingia hawawapi elimu ya kutosha maana wengi kwa ufahamu wangu naona kipengele cha kulipa kila mwezi hawakijui wameaminishwa deni lilipwe ndani ya miaka ya mkataba na si lazima kila mwezi utowe pesa, shida iko hapo kwa kipato cha Mtanzania wa kawaida aachane na hizi nyumba za miradi hazipo kwa ajiri ya kusaidia Watanzania ni za upigaji tu kwenye vitengo vya investment, hao National housing wenye jukumu lao ndio mafisadi namba moja wapangaji wao wa mijini sasa hivi wanauza flat zao wanachukuwa upangaji watu wapya wenye msuli wa kulipa kodi mpya za NHC.
 
Kabla hujarukia sababu zako, jaribu kufika eneo la tukio kupata ukweli.

Kuna tatizo kubwa sana kwenye hii NSSF tangu enzi za Dau kuhhsu zile nyumba pale.

Ukweli ni kwamba, wale wamepangishwa kwa kodi inayozidi Tshs milion 1 kwa mwezi na wanapaswa kuilipa NSSF milioni tatu kila baada ya miezi mitatu, ikifika kuanzia milioni 120 na kuendelea ndo unapewa nyumba yako.

Nyumba yenyewe hata kwa Tshs 300,000 kwa mwezi haipangishiki labda kwa bei ya juu ya Tshs 200,000 kwa mwezi.

Nimejaribu kukuelezea uhalisia ambao Bodi ya NSSF inajutahidi kuuficha kwa gharama kubwa na kuidanganya mamlaka ya juu nchini.

dubu
Pamoja na Yote Ningependa Uthibitisho Kuwa ni Kweli Wametolewa Na Je Ni Kweli Iwe Wanadaiwa Au Hawadaiwi Na Je Ni Kweli Hakuna Notice au Remove Oder? Ikiwa ni Hivyo Hakuna Uhalali wa Kuwaondoa Kwa Nguvu,
Hata kama Wanadaiwa

Kilichofanyika Itakuwa Ni BATILI
 


MADAI

Taarifa zinadai kuwa Wakazi 23 wa NSSF wametolewa vyombo vyao nje Mtaa wa Changanyikeni, Kata ya Toangoma Mkoani Dar es Salaam. Inasemekana kuwa hakuna removal order na kuna kesi mahakamani.

Aidha inadaiwa kuwa Watu wameharibiwa vitu vyao na wengine kuumizwa. Zoezi limefanywa na YONO Auction Mart.

Video hii iliyowekwa hapa inahusianishwa na tukio hilo

1660289936221.png
 
Back
Top Bottom