Dar: Watu watatu wakamatwa kwa tuhuma za Mauaji ya Mtendaji wa Serikali za Mtaa

Dar: Watu watatu wakamatwa kwa tuhuma za Mauaji ya Mtendaji wa Serikali za Mtaa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Dar es salaam, 12, Oktoba, 2021
KUKAMATWA KWA WATU WATATU KWA TUHUMA ZA MAUJAJI YA MTENDAJI WA SERIKALI YA MTAA.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya afisa mtemtendaji wa Serikali ya mtaa wa Mbezi Msumi aliyefahamika kwa jina la Kelvin Costa Mowo (38), Mkazi wa Bunju, Afisa mtendaji wa Msumi.

Majina ya watuhumiwa hao yanahifadhiwa kwa saababu za kiupelelezi.

Tukio hili limetokea tarehe 11/10/2021 saa 11:54 asubuhi huko eneo la Msumi Mbezi wilaya ya Ubungo katika ofisi za Serikali ya mtaa, ambapo marehemu akiwa ofisini kwake anaskiliza mgogoro wa ardhi.

Ghafla watu wapatao wanne waliingia ofisini na mmoja wao akatoa panga na kumshambulia mtendaji huyo kitendo kilichopelekea kupata majeraha makubwa na baadae akapoteza maisha wakati akikimbizwa hospitalini, watu watatu wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo wanahojiwa kwa kina na watafikishwa mahakamani haraka iwezekanavyo.

MULIRO J. MULIRO- ACP

KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM, DAR ES SALAAM

 
Polisi bhana! wakiamua kufanya kazi zao kwa weredi, hufikia hitimisho ndani ya dakika sifuri tu . Na wakiamua kujitoa ufahamu, huwa wanajitoa kweli kweli mpaka unawashangaa.
Sawa ila nani anaamini hao washukiwa kuwa ni wao au wamekamata wasiohusika

USSR
 
Polisi bhana! wakiamua kufanya kazi zao kwa weredi, hufikia hitimisho ndani ya dakika sifuri tu . Na wakiamua kujitoa ufahamu, huwa wanajitoa kweli kweli mpaka unawashangaa.
... kushambuliwa kwa Tundu Lissu hadi leo mwaka wa 4 hakuna hata mmoja aliyeshukiwa pamoja na eneo lile kujaa vifaa vyote vya usalama including CCTV cameras 24/7x365!
 
... kushambuliwa kwa Tundu Lissu hadi leo mwaka wa 4 hakuna hata mmoja aliyeshukiwa pamoja na eneo lile kujaa vifaa vyote vya usalama including CCTV cameras 24/7x365!
hahahaha ukitaka kuona Kamanda Zerro kapanic zungumzia swala la waliompiga risasi Tundu Lissu utaona atavyochachawa na kutoa visababu uchwara!
 
Sasa mtuhumiwa si mmoja tu hapo, aliyetoa panga au? Hao wengine ni mashahidi tu.
 
DAH MTU KAUWAWA KATIKATI YA KUNDI LA WATU AKISIKILIZA MGOGORO WA ARDHI NA WALIOKUWEPO WASIFANYE VYOKO.

POLENI WAFIWA
 
Hasira hasara....machungu Mara mbili. Kumpoteza mtoto na jela. Pengine chanzo ni uzinzi na usaliti wa mmojwapo wa wazazi.

R.I.P mtoto, umekufa bila hatia.
 
Back
Top Bottom