Dar yakusanya Tsh. Trilioni 13 kati ya 16.5 zilizokusanywa na TRA. Ni aibu kwa Tanzania kutegemea 80% ya Mapato kutoka Mkoa mmoja

Takwimu hizi pia zituongoze, tunaishi wapi, tunafungua biashara wapi, sasa kakae sehemu hata haina mzunguko wa fedha
Uko sawa Kwa maana hiyo ila mzunguko wa hela Dar haujajileta Bali umetengenezwa na Serikali na ndio maana tunailamu kutengeneza mzunguko wa hela Kwa Nchi kutegemea Mkoa mmja Kwa 80%.
 
Cha ajabu nini hapo? Dar wanakusanya sababu ndio bidhaa zinaingia lakini wanunuzi ni Tanzania nzima kila kinachopita hapo walaji ni Tanzania nzima kwa hiyo ni makusanyo ya Tanzania nzima sababu Dar hawazalishi kitu ni huduma tu zi kibiashara,
 
Cha ajabu nini hapo? Dar wanakusanya sababu ndio bidhaa zinaingia lakini wanunuzi ni Tanzania nzima kila kinachopita hapo walaji ni Tanzania nzima kwa hiyo ni makusanyo ya Tanzania nzima sababu Dar hawazalishi kitu ni huduma tu zi kibiashara,
Kama huoni Cha ajabu uku huna akili na mada imekuzidi uwezo.
 
Uko sawa Kwa maana hiyo ila mzunguko wa hela Dar haujajileta Bali umetengenezwa na Serikali na ndio maana tunailamu kutengeneza mzunguko wa hela Kwa Nchi kutegemea Mkoa mmja Kwa 80%.
Kweli kabisa, nadhani pia kunahitajika mkakati maalum wa ku-boost utalii kanda ya ziwa, na kuweka uwekezaji wa kimkakati.
 
Hii takwimu ina walakini aeleze vizuri makusanyo ya mikoa mingine yanaingia chungu kipi.
Kwa takwimu hizo ina maana Dsm pekee kwa mwezi inachangia Tillion 2.5+ kwa mwezi
 
Kweli kabisa, nadhani pia kunahitajika mkakati maalum wa ku-boost utalii kanda ya ziwa, na kuweka uwekezaji wa kimkakati.
Hayo hawawezi kutokea kama watu wanaona ni sawa Kwa status quo iliyopo Hadi waje watu wenye akili tofauti.

Lazima Majiji Makuu ya Kanda yatumike kama vitovu vya Uchumi kwenye Mikoa iliyo jirani and so Huduma zote kama zilizopo Dar zilitamkwa zipatikane Kila Kanda.

Ukisema Muhimbili ni Hospital ya Taifa basi inatakiwa kuwa na hospital Zenye Hadi ya Taifa kwenye Kanda zote 7,this should be done across sectors.

Tungekuwa na Kumbi kubwa za mikutano huko Mwanza haingewwzekana Kila mkutano kufanyika Dar na Arusha kidogo.
 
Hii takwimu ina walakini aeleze vizuri makusanyo ya mikoa mingine yanaingia chungu kipi.
Kwa takwimu hizo ina maana Dsm pekee kwa mwezi inachangia Tillion 2.5+ kwa mwezi
Chingu kipi kiaje? Taarifa Iko wazi hapo nini hujaelewa?
 
Hata USA pamoja na utajiri wao mkubwa GDP yao almost 35% inatoka California, Texas na NY states zingine 47 wanachangia 65% tu ni kawaida na sababu zipo kwanini.
 

Hii ndio post yako ya kwanza nayoiona imejaa ukweli. Umesema jambo la maana sana na sio kwamba unamtukana wala kumuone mtu.
Lazima TRA wajipange kuongezea wigo wa mapato. Kila mkoa wana ofisi na vitendea kazi kibao. Kwanini msako mkali uwe mkoa mmoja tu?
 
Kama huoni Cha ajabu uku huna akili na mada imekuzidi uwezo.
Sasa wewe mwenye akili ulitegemea mkoa wa Mara uwe kama Dar? TRA wanakusanya kodi bandarini bidhaa zote za Tanzania zinapita bandarini na zinalipiwa kodi pale sasa unataka iweje, Iringa wawe kama Dar? Sasa wewe mwenye akili tuambie tatizo ni nini?
 
Kama huoni Cha ajabu uku huna akili na mada imekuzidi uwezo.
Mafuta ya nchi nzima yanalipiwa kodi Dar bandarini nchi nzima unadhani kitu kidogo hicho. Containers zote zinalipiwa Dar hayo mafuta yakipita hapo na bidhaa mikoani hazilipiwi kitu zinapita tu. Bado unashangaa
 
Sasa wewe mwenye akili ulitegemea mkoa wa Mara uwe kama Dar? TRA wanakusanya kodi bandarini bidhaa zote za Tanzania zinapita bandarini na zinalipiwa kodi pale sasa unataka iweje, Iringa wawe kama Dar? Sasa wewe mwenye akili tuambie tatizo ni nini?
Unaelewa maana ya even distribution of resources?

Kwani inashindikana nini Mkoa wa Mara kuwa kama Dar kimapato? Kuna ulazima gani wa bidhaa za Mkoa wa mara kwenda Dar wakati zinaweza pita port ya Dar na Musoma port kuwa modernized?

Kama mada imekuzidia uwezo pisha.
 
Mafuta ya nchi nzima yanalipiwa kodi Dar bandarini nchi nzima unadhani kitu kidogo hicho. Containers zote zinalipiwa Dar hayo mafuta yakipita hapo na bidhaa mikoani hazilipiwi kitu zinapita tu. Bado unashangaa
This is the kind of nonsense am talking about,and you people you view it as okay,ubongo wa kuku na unfortunately watu wengi wa hivi ndio wako huko kwenye vitengo vya maamuzi ya kimkakati.
 
Sasa unaongelea sera hapa sio uhalisia, ziko sababu nyingi meli zinakuja Dar kwanza ni bandari kubwa na iko equipped na pia wafanya biashara walioshinda tender wako Dar. Wewe ukiagiza container lako utashusha Mara? kwanza meli gani itakushushia Mara sababu gharama zitakuwa kubwa ikiwa Tanga tu na Mtwara ni shida. Kama unaleta hoja za kisera hiyo ni mjadala mwingine hapa ni wewe unayeshangaa Dar kukusanya 80% ndio nauliza unashangaa nini?
 
Cha ajabu nini hapo? Dar wanakusanya sababu ndio bidhaa zinaingia lakini wanunuzi ni Tanzania nzima kila kinachopita hapo walaji ni Tanzania nzima kwa hiyo ni makusanyo ya Tanzania nzima sababu Dar hawazalishi kitu ni huduma tu zi kibiashara,
Mfano mzuri pia ni mitandao ya simu! Collection zote zinafanyika Dar es Salaam!
 
TRA hawawezi ongeza mapato sehemu ambayo hayo mapato hamna, unataka wakabe na kubambikia kodi watu?

Kwa mfano unataka waende Nachingwea kuongeza mapato, wayatoe wapi kama sio viduka vya mangi vinavyolipa elfu kumi kama kodi.

Hapa wajibu ni wa serikali kuu kutengeneza vyanzo vya mapato mikoani. Kujenga viwanda sio kila kiwanda Dar, kujenga plants za kuzalisha kama Mtwara wanatakiwa wawe wanabangua korosho zote na kuzipaki zikauzwe nje kama finished product, sio kwenye magunia kupeleka ajira za viwandani nje uko Vietnam na India. Pia korosho zote zipite bandari ya Mtwara.

Tanga kujengwe viwanda zaidi hasa vya matunda, mazao ya mbao, mazao ya baharini.
Mwanza wanastahili airport kubwa zaidi ya iliyopo.
Morogoro wanahitaji viwanda vingi sana vya mazao ya kilimo.

Makampuni yanayofanya shughuli mkoa fulani sharti yawe na makao makuu mkoa ule au ukanda ule. Tungeona kampuni za madini kanda ya ziwa zinakuwa na HQ Mwanza, sio Dar. Kama Tanga Cement ilivyo na HQ Tanga.

Ingekuwa marufuku kujenga chuo cha serikali chochote Dar. Vya binafsi na umma vilivyopo vinapitiliza idadi.

Kuna mengi ya kufanya makubwa na madogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…