Dar yakusanya Tsh. Trilioni 13 kati ya 16.5 zilizokusanywa na TRA. Ni aibu kwa Tanzania kutegemea 80% ya Mapato kutoka Mkoa mmoja

Hata USA pamoja na utajiri wao mkubwa GDP yao almost 35% inatoka California, Texas na NY states zingine 47 wanachangia 65% tu ni kawaida na sababu zipo kwanini.
Hapo 35% unazungumzia state tatu! Huwezi kulinganisha na huku kwetu 80% tunazungumzia mkoa mmoja tena wenye eneo dogo la ardhi kuchukua kuzalisha mapato 80%!
 
Sasa Dar si wanayo bandari kuu wewe kayumba? Unadhani hizo trilioni 13 ni za Mbagala au Mburahati???
 
Sasa Dar si wanayo bandari kuu wewe kayumba? Unadhani hizo trilioni 13 ni za Mbagala au Mburahati???
Hii sio mada ya watu wenye akili ndogo kama wewe.

Mkoa wowote ambao uko kando ya Bahari unaweza kuwa na Bandari kuu,punguza ujinga
 
Hapo 35% unazungumzia state tatu! Huwezi kulinganisha na huku kwetu 80% tunazungumzia mkoa mmoja tena wenye eneo dogo la ardhi kuchukua kuzalisha mapato 80%!
Yes 3 lakini states kule kama nchi tu zinajitegemea kwa kiasi kikubwa, California tu ni kama nusu ya Tanzania, yaani California ukiziunga mara mbili kama Tanzania yote. Huku Dar ilipendelewa miaka yote toka tunapata uhuru kwingine kuliachwa sana hivi sasa ndio kidogo miji mingine inajitutumua. Sasa state moja kama California kuchangia 14% ni kitu kikubwa sana. State 3 35% na zingine 47 ndio 65% ni kama kila state 1% tu ni tofauti kubwa sana.
 
Hakuna kitu cha kulaumu hapo , ndio maana utafutaji wa Dar ukitumia akili ni rahisi kupata pesa. Vitu vingi vya kustimulate uchumi viko Dar huu ni ukweli mchungu
Upo sawa lakini endapo limetokea janga moto au tetemeko kwisha habari tutayumba kidogo mwandishi nimemuelewa kuwa serikali ijaribu kusambaza miundombi rafiki ya ukuzaji uchumi katika mikoa mingine zaidi ili kuweka usawa ikitokea Jiji Moja limepigwa tukio Bado majiji mengine yana ishi Mfano RUSSIA KAWEKEZA Africa kusini Nishat ya nuclear, Niger, Burkina Faso Syria pakiwaka sehemu Moja kwingine safi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…