DOKEZO Daraja la Mbwemkuru-Lindi linamaliza malori na watu, Serikali fanyeni jambo

DOKEZO Daraja la Mbwemkuru-Lindi linamaliza malori na watu, Serikali fanyeni jambo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Shift

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2014
Posts
1,087
Reaction score
2,195
Mimi sio mwandishi mzuri ila kwa kweli inasikitisha sana nimepita mara kadhaa daraja hili lililopo mkoani Lindi barabara kuu ya Dar-Lindi, linamaliza ndugu zetu wa malori.

Ukitokea Lindi ni km 70, kuna mteremko sio mkali sana ila una kona kidogo, chini ya mteremko huo ndio kuna daraja ambalo liliathiriwa na mvua na hivyo magari kupita kwenye mchepuko. Kwa kipindi chote hicho cha miezi 5 hivi kuna malori kadhaa yamepata ajali mbaya sana.

Kuna alama mbili tu, yaani vibao vidogo vya 30km/hr vilivyochorwa kwa mkono na ambavyo vimewekwa kwa mti mfupi sana kiasi kwamba haviko visible, dereva akishuka na lory ghafla anakutana na mchepuko hivyo hulazimika kutupa gari motni ama sehemu nyingine na hivyo kusababisha ajali.

Mwezi wa sita nilishuhudia ajali kwa macho yangu ambapo lori lilidumbukia mtoni likiwa limebeba sulphur, ni watu wangapi walikunywa maji yenye sulphur? Ni madhara kiasi gani yamepatikana? Hakuna ila pia gari lile lilikua liligonge basi la baraka kwa nyuma na hivyo madhara yake yangekua makubwa zaidi.

Leo tena nimekuta ajali ya lory lingine (la nne hili sasa kama sio la tano) hapo hapo liliwa limeng'oka engine, tairi yaani limekua vipande tupu. Kuna siku atakuja kutumbukia kiongozi huenda ndio tutajenga.

Picha chini ni lorry ambalo ajali yake ingelimaliza Basi la Baraka kwa Nyuma hivyo dereva kuamua kuingia huko majini, hapo liko chini zaidi ya mita 25-30 kutoka juu na hiyo ni sulphur.

1721756349829.jpeg

Screenshot 2024-07-31 112339.jpg

Screenshot 2024-07-31 112304.jpg
Pia soma ~ Serikali yasaini mikataba Ujenzi wa madaraja 13 yaliyoathiriwa na mvua - Lindi, Tsh. Bilioni 140 kutumika
 
Kujenga daraja mbali sana, mbwemkuru panataka kuwa well posted ili madereva wachukue tahadhari kabla hawajafika kwenye diversion.
Ni kutojali tu. Kuna kipande baada ya wami hapo wakati wa ujenzi wa daraja waliweka diversion. Pale pamoja na vibao usiku alikuwa anakaa mtu na tochi. Kuna usiku mmoja nakumbuka nimejiachia huyo mwenye tochi ndio alinushtua kwa kuflash la sivyo ningepita na barrier na mapipa ya zege.
 
Afadhali mashimo, enzi hakuna barabara ya kueleweka siku mbili kukaa hiyo kipande ilikua kawaida tu.
Badala mpande gari mnajikuta njia nzima mnaibeba gari toka kwenye tope.
Miaka hiyo tulipata shida Sana nakumbuka mwaka 1995 nilisafiri Kwa siku 5 kutoka DAR- MASASI, kipindi kile tunavuka pale rufiji
 
Kujenga daraja mbali sana, mbwemkuru panataka kuwa well posted ili madereva wachukue tahadhari kabla hawajafika kwenye diversion.
Wala si mbali, kwa nchi yenye viongozi serious na wanajua maana ya uongozi basi pale daraja tayari lishajengwa, tena fasta
 
Hii njia kiufupi imeoza hakuna njia huku.
Hii mikoa ya kusini ni kama ndio wapo 1999 ikiwa dar na mikoa mingine ipo 2024.

Cement inatoka dangote lakin njia ya kuja dar haieleweki

Njia ya kuunga unga tu haina muelekeo hata kidogo.
 
Duh nakumbuka mara ya mwisho kupita huko kama 2013 njia ilikuwa tamu hio na haina magari kabisa.
subutuuuu ina mashimbo na madaraja kama sita hivi yamesombwa na maji, nazungumzia madaraja sio kalavati, madaraja yaliyojengwa kwa mabilioni.
 
Back
Top Bottom