Mparee2
JF-Expert Member
- Sep 2, 2012
- 3,092
- 5,386
Kuna daraja lenye urefu wa kama meta 50 hivi ambalo limejengwa ndani yamaji (yaani wamemimina maji yapite juu). Huo mto Mara ni mkubwa sana ambapo ndio watalii hufurika kuona Nyumbu wakivuka (crossing). Changamoto ya daraja ni kuwa , maji yakiongezeka kidogo, daraja huwa halionekani na hivyo kuvuka hapo ni Kwenda kwa bahati nasibu.
Ajali kadhaa zimekuwa zikitokea hapo na hata wiki iliyopita gari la wageni (watalii) lilianguka hapo bahati nzuri watalii walitoka salama
Utatuzi wake;
Kuweka nguzo kwenye kingo za daraja kila urefu wa kama meta 8hivi ili madereva waone kingo za daraja na pengine ziwekwe mark mahala ambapo maji yakifika sio salama kwa gari kupita
Mara nyingine napata wasiwasi na hawa wakandarasi wetu kwani daraja limekarabatiwa hivi karibuni japo tatizo KUBWA KABISA ambalo niweka alama za kuonesha Kingo za daraja wakati maji yameongezeka halikufanyiwa kazi!
Ajali kadhaa zimekuwa zikitokea hapo na hata wiki iliyopita gari la wageni (watalii) lilianguka hapo bahati nzuri watalii walitoka salama
Utatuzi wake;
Kuweka nguzo kwenye kingo za daraja kila urefu wa kama meta 8hivi ili madereva waone kingo za daraja na pengine ziwekwe mark mahala ambapo maji yakifika sio salama kwa gari kupita
Mara nyingine napata wasiwasi na hawa wakandarasi wetu kwani daraja limekarabatiwa hivi karibuni japo tatizo KUBWA KABISA ambalo niweka alama za kuonesha Kingo za daraja wakati maji yameongezeka halikufanyiwa kazi!