Intelligence Justice
JF-Expert Member
- Oct 23, 2020
- 3,443
- 4,006
Wana Jukwaa nguli,
Gari limeshindwa kuvuka mto kwenda kanaani baada ya daraja kukatika kwa maji ya mvua iliyonyesha ghafla. Dereva anageuza gari kurejea Misri ambako uhuru na starehe zote zipo. Abiria ndani ya gari wanahoji tunaenda wapi? Dereva na konda wanajibu si mmedai mtakula wapi, nawapeleka mahali salama penye kila kitu na mfuko wenu tu.
Baada ya kukaribia ufukwe wa bahari mfu, baadhi ya abiria wanashuka na kuanza kupiga kelele ambazo hazikusikilizwa.
Baada ya gari kuwasili ufukweni mwa bahari mfu dereva anashuka kwanza akiwa amebeba mfano wa fimbo nyeusi ya mpingo na kuyagusa maji akitarajia yatagawanyika apite kurejea Misri, lakini cha ajabu fimbo inaonesha kama bua la mhindi mkavu, inakatika bila kuyashitua maji anasubiri kupewa upenyo avuke bila mafanikio. Abiria walifanya nini baada ya tukio hilo?
Abiria walivishwa barakoa na kuandaliwa kupata chanjo ili kuzimua mizimu lakini kuwazuia wasinene chochote mpaka watakapofanikiwa kupewa kibali cha kuvuka. Kila mmoja anaanza kutoa laana za kila aina kuanzia wazazi hadi walezi-mwisho wake ni upi?
Gari limeshindwa kuvuka mto kwenda kanaani baada ya daraja kukatika kwa maji ya mvua iliyonyesha ghafla. Dereva anageuza gari kurejea Misri ambako uhuru na starehe zote zipo. Abiria ndani ya gari wanahoji tunaenda wapi? Dereva na konda wanajibu si mmedai mtakula wapi, nawapeleka mahali salama penye kila kitu na mfuko wenu tu.
Baada ya kukaribia ufukwe wa bahari mfu, baadhi ya abiria wanashuka na kuanza kupiga kelele ambazo hazikusikilizwa.
Baada ya gari kuwasili ufukweni mwa bahari mfu dereva anashuka kwanza akiwa amebeba mfano wa fimbo nyeusi ya mpingo na kuyagusa maji akitarajia yatagawanyika apite kurejea Misri, lakini cha ajabu fimbo inaonesha kama bua la mhindi mkavu, inakatika bila kuyashitua maji anasubiri kupewa upenyo avuke bila mafanikio. Abiria walifanya nini baada ya tukio hilo?
Abiria walivishwa barakoa na kuandaliwa kupata chanjo ili kuzimua mizimu lakini kuwazuia wasinene chochote mpaka watakapofanikiwa kupewa kibali cha kuvuka. Kila mmoja anaanza kutoa laana za kila aina kuanzia wazazi hadi walezi-mwisho wake ni upi?