Darasa la ujenzi la Madrassatul Abraar latunukiwa Tuzo ya ubunifu wa ujenzi kutoka Shirika la Uingereza

Ana mahaba ndindinsi huyo bibi wa calgary Canada.
Ingawa sijaelewa maana ya hilo neno, kazi iendelee.

Kati ya blocks zetu zinazookoa sana gharama na muda wa ujenzi ni hizo floor slabs.


Your browser is not able to display this video.
 
Hata hivyo hayo ni mapenzi yenu... turudi mezani... enhe mwauzaje hizo blocks?
Hahahahaha, mahaba niue.

Moja kwa Shillingi 1,000 tu.

Ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu.
 
Licha ya darasa la vifaa vya ujenzi na ujenzi, hapa Abraar Education Cntre pia tuna madarasa ya Qur'an, English (lugha), Arabic (lugha), Computer (IT).

Pia madarasa ya kutoa uzoefu wa kazi kwa vitendo kama vile "office practices", "book Keeping for beginners", (Store Keeping and procurement).

Madarasa yetu yanayohusisha kazi yapo kimtindo wa "apprenticeship" yaaani kujifundisha kazi kwa vitendo na mwanafunzi alie kwenye mpango wetu huu analipwa posho ya chakula na anapatiwa sehemu ya kulala (boarding and lodging) kwa muda.

Na hivi tulivyo tunaandaa mpango wa kipekee wa mafunzo yote hayo kwa mtindo wa weekend au retreat.

Yeyote ataependa kufahamu zaidi atume whatsapp 0625249605 kwa maelezo zaidi.
Linakua na ukubwa gani? Kwahiyo wapachika bila cement? Mafundi wanayawezea?
Size ni around 10x20x40 centimeters.

Yanabandikwa yenyewe tu bila cement, kama paving blocks. Fundi yeyote hata fundi "maiko" anayaweza vizuri sana.

Yanaokoa sana muda, gharama za ufundi wa zege na za zege lenyewe.
 
Nilikuwa nataka kujua mnatumia njia gani ktk ujenzi wa ghorofa upande wa kumwaga zege, yaani mnamwaga zege au Kuna blocks mnaweka?

Sent from my TECNO KD7 using JamiiForums mobile app
 
Nilikuwa nataka kujua mnatumia njia gani ktk ujenzi wa ghorofa upande wa kumwaga zege, yaani mnamwaga zege au Kuna blocks mnaweka?

Sent from my TECNO KD7 using JamiiForums mobile app
Kuna precast roof slabs tunaweka halafu tunamwaga zege la inchi mbili (2" only).

Zinaokoa sana gharama ya bati, mbao za bati, gypsum boards na mbazo zake, zote hazihitajiki tena, na unapata nafasi kubwa sana juu ambayo ingefunikwa na bati. Jionee chini hapa.
Your browser is not able to display this video.
 
Hongereni sanaa. ustaadhi akili hii kubwa inaonesha wewe ni muislam ulioelimika
 
Ahsante, lkn bado sijaelewa vizuri, kwanini mnaweka zege (2inches) ilhali kuna precast slabs kama ulivyosema? Ufafanuzi tafadhali na picha zaidi kama inawezekana.

Sent from my TECNO KD7 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…