Dark days 17/03/20...

Dark days 17/03/20...

Ni kwamba pesa zinatoka Bara. Kadri mapato yanavyokusanywa Bara wao wana 4.5%.
Pili, Zanzibar hawakopi ila kupitia JMT na deni hawalipi inalipa JMT ambayo ni Tanganyika
Tatu, Zanzibar haina Bajeti ya Ulinzi , mambo ya ndani, nje, hata Elimu ya Juu wanapata Bara
Nne, Bajeti ya Zanzibar inapewa ruzuku kutoka hazina Dar es Salaam
Tano, gharama za Taasisi za Muungano haziwahusu.
Sita, mapato ya Zanzibar hayavuki bahari lakini ya Tanganyika yanavuka

Kwa usawa huo wanashindwaje kufanya mambo makubwa? Jiulize kwanini inatokea sasa na si huko nyuma?
Marais waliopita hawakukubali uporaji wa rasilimali, tuna ushahidi lakini sasa shamba la bibi.
Hahahaha,nakuelewa ila mie ,nauliza tu mkusanya mapato zanzibar ni nani ? Alitokea wapi ? Nafasi yake ilikuaje huko aliko toka?
 
Asante sana Nguruvi3 kwa kiasi kikubwa umetufungua kuhusu huu muungano.
Kwa kiasi kikubwa mwalimu nyerere aliatuachia mzigo mzito unaotupa ugumu kuutua, bahati mbaya kabisa hakuacha hata mwanya mdogo wa kupenya ili kujinasua.
Nimejiuliza pia kama walifanya utafiti wa kutosha kwamba hizo faida za huo muungano zingeweza kuwa faida miaka 25, 50 na 100 ijayo, huwenda waliangalia kipindi chao tu , hawakuangalia leo yetu.

Kama maana au ufafanuzi kuhusu muungano wetu huu alioutoa Pascal Mayalla ndio hivi , tuseme tu tumeonewa vya kutosha.

Binafsi naamini ipo siku atatokea kiongozi ambaye atasema hapa imetosha.
Kwanza nianze na sentensi yako ya mwisho. Tayari kumetokea viongozi wanaoliona tatizo.
Mzee Warioba, Mzee Salim Ahmed na Mzee Butiku walikuwa wajumbe wa Tume ya Warioba iliotoa rasimu ya Katiba

Wazee hawa walikuwepo Muungano unaasisiwa, walifanya kazi na Nyerere, wameshuhudia misuko suko mingi inayohusu Muungano wakiwa Viongozi waandamizi katika serikali ya Mwalimu

Wazee hawa wakiwa na Tume ya Warioba walizunguka nchi nzima kusikiliza maoni ya Wananchi kuhusu katinba.
Moja ya mambo wanayosema yalikuwa magumu ni suala la Muungano, na walieleza kwa undani wake.

Katika hitimisho , Wazee walishauri uwepo wa Serikali tatu na kupunguza mambo ya muungano kutoka 22 hadi 7

Mambo 15 yaliyoondolewa yote yaligharamiwa na Tanganyika. 7 yaliyobaki hayakuwa na gharama za ziada

1. Katiba na mamlaka ya JMT
2. Ulinzi na Usalama wa JMT ( Gharama zisingeongezeka kwasababu jeshi linabaki lile lile la sasa )
3.Uraia na Uhamiaji ( Gharama ni zile zile za sasa )
4. Sarafu na Bank kuu (Inabaki kama ilivyo sasa )
5. Mambo ya nje (Gharama zingebaki kama ilivyo sasa)
6. Usajili wa vyama ( Kama ilivyo sasa)
7. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatakanayo na JMT

Mambo mengine yote yangebaki kuwa ya Serikali Washirika. Kusingekuwa na ongezeko la Taasisi yoyote.
Hili lingesaidia Tanganyika kupunguza mzigo wa kuendesha Muungano yenyewe.

Kwa mfano, Bunge la JMT lingekuwa na 45 kwa 25 na nchi Washirika zingegharamia Wabunge wake.

Kwasasa Tanganyika inababe gharama za Wabunge 80 wa Zanzibar wanaojadli mambo 7 yaliyoanishwa hapo juu.

Majimbo ya Zanzibar yana watu 6,000 kama mtaa mmoja wa Magomeni.
Diwani wa Kata ya Magomeni ana wapiga kura wengine zaidi ya Mbunge wa JMT kutoka Zanzibar.

Gharama za Mbunge wa Zanzibar zinatoka hazina Tanganyika. Mbunge wa Zanzibar anayechaguliwa na watu 6,000 anapewa pesa za mfuko wa Jimbo kutoka hazina Tanganyika kwenda kuendeleza Zanzibar , sawa na Mbunge wa Ubungo mwenye watu Milioni 1, au Wa Ilala au Kigamboni.

kwanini Zanzibar tugawane misaada na mikopo lakini gharama za Muungano ikiwemo pesa za majimbo ya Zanzibar zilipwe na kodi za Tanganyika?

Kwahiyo, Waasisi wa Muungano walikuwa na nia njema kwa bahati mbaya hawakuweka misingi imara
 
Binafsi sikubaliani na serikali mbili Wala tatu,nataka serikali moja ya jamuhuri ya muungano wa tz,huu usanii wa serikali mbili au tatu ndio unaleta kero za muungano,tukiwa na serikali mmoja na kukawa hakuna upendeleo Kila mtanzania atakua na haki sawa hakuna Cha huru ni mtanganyika Wala mzanzibari tunataka serikali moja ya muungano itakayo ondoa kioja kiitwacho kero za muungano!!!
Kwanza nianze na sentensi yako ya mwisho. Tayari kumetokea viongozi wanaoliona tatizo.
Mzee Warioba, Mzee Salim Ahmed na Mzee Butiku walikuwa wajumbe wa Tume ya Warioba iliotoa rasimu ya Katiba

Wazee hawa walikuwepo Muungano unaasisiwa, walifanya kazi na Nyerere, wameshuhudia misuko suko mingi inayohusu Muungano wakiwa Viongozi waandamizi katika serikali ya Mwalimu

Wazee hawa wakiwa na Tume ya Warioba walizunguka nchi nzima kusikiliza maoni ya Wananchi kuhusu katinba.
Moja ya mambo wanayosema yalikuwa magumu ni suala la Muungano, na walieleza kwa undani wake.

Katika hitimisho , Wazee walishauri uwepo wa Serikali tatu na kupunguza mambo ya muungano kutoka 22 hadi 7

Mambo 15 yaliyoondolewa yote yaligharamiwa na Tanganyika. 7 yaliyobaki hayakuwa na gharama za ziada

1. Katiba na mamlaka ya JMT
2. Ulinzi na Usalama wa JMT ( Gharama zisingeongezeka kwasababu jeshi linabaki lile lile la sasa )
3.Uraia na Uhamiaji ( Gharama ni zile zile za sasa )
4. Sarafu na Bank kuu (Inabaki kama ilivyo sasa )
5. Mambo ya nje (Gharama zingebaki kama ilivyo sasa)
6. Usajili wa vyama ( Kama ilivyo sasa)
7. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatakanayo na JMT

Mambo mengine yote yangebaki kuwa ya Serikali Washirika. Kusingekuwa na ongezeko la Taasisi yoyote.
Hili lingesaidia Tanganyika kupunguza mzigo wa kuendesha Muungano yenyewe.

Kwa mfano, Bunge la JMT lingekuwa na 45 kwa 25 na nchi Washirika zingegharamia Wabunge wake.

Kwasasa Tanganyika inababe gharama za Wabunge 80 wa Zanzibar wanaojadli mambo 7 yaliyoanishwa hapo juu.

Majimbo ya Zanzibar yana watu 6,000 kama mtaa mmoja wa Magomeni.
Diwani wa Kata ya Magomeni ana wapiga kura wengine zaidi ya Mbunge wa JMT kutoka Zanzibar.

Gharama za Mbunge wa Zanzibar zinatoka hazina Tanganyika. Mbunge wa Zanzibar anayechaguliwa na watu 6,000 anapewa pesa za mfuko wa Jimbo kutoka hazina Tanganyika kwenda kuendeleza Zanzibar , sawa na Mbunge wa Ubungo mwenye watu Milioni 1, au Wa Ilala au Kigamboni.

kwanini Zanzibar tugawane misaada na mikopo lakini gharama za Muungano ikiwemo pesa za majimbo ya Zanzibar zilipwe na kodi za Tanganyika?

Kwahiyo, Waasisi wa Muungano walikuwa na nia njema kwa bahati mbaya hawakuweka misingi imara
 
Binafsi sikubaliani na serikali mbili Wala tatu,nataka serikali moja ya jamuhuri ya muungano wa tz,huu usanii wa serikali mbili au tatu ndio unaleta kero za muungano,tukiwa na serikali mmoja na kukawa hakuna upendeleo Kila mtanzania atakua na haki sawa hakuna Cha huru ni mtanganyika Wala mzanzibari tunataka serikali moja ya muungano itakayo ondoa kioja kiitwacho kero za muungano!!!
Hapana serikali moja haitawezekana kwasababu ya Utaifa. Wazanzibar wanaona Uzanzibar ni Ubora kuliko Utanzania.
Fikiri kwamba hata sasa hivi hawautaki Utanzania, sasaunategemea nini mbele ya safari.

Tatizo la Muungano litaondoka kwa mambo mawili

1. Kura ya maoni kwa Wazanzibar ikiwa wanataka au la, kama hawataki njia nyeupe waondoke

2. Ikiwa wanataka lazima kuwe na Serikali 3. Uwepo wa Serikali ya Tanganyika utasaidia kudhibiti hujuma zinazofanywa na kuifanya Tanganyika kuwa ''cash cow' ya Zanzibar. Kwasasa Wazanzibar hawahitaji kufanya kazi!

Mfano, Rais wa JMT aliamua 21% ipewe Zanzibar. Hakuna aliyeeleza ajira hizo ni zipi na maeneo gani
Kubwa zaidi ,ikiwa kuna 21% ya ajira kwa Zanzibar huo ni msaada, na Zanzibar inawajibika kuwalipa watumishi hao

Kinyume chake, wanadai 21% na walipewa na Rais SSH lakini mzigo wa kulipa ni wa Tanganyika
Magufuli alikataa kusamehe deni la Umeme, well, ghafla Bilioni 60 zikasamehewa na mzigo akaubeba Mtanganyika

Yote yanatokea kwasababu hakuna mtetezi wa Tanganyika. Kiongozi wa JMT hawezi kuwa kiongozi wa Tanganyika

Muundo ni tatizo kubwa sana, ingawa viongozi wanakwepa ukweli, ipo siku watu watafukuzana! alisema Palamagamba
 
Ni kwamba pesa zinatoka Bara. Kadri mapato yanavyokusanywa Bara wao wana 4.5%.
Pili, Zanzibar hawakopi ila kupitia JMT na deni hawalipi inalipa JMT ambayo ni Tanganyika
Tatu, Zanzibar haina Bajeti ya Ulinzi , mambo ya ndani, nje, hata Elimu ya Juu wanapata Bara
Nne, Bajeti ya Zanzibar inapewa ruzuku kutoka hazina Dar es Salaam
Tano, gharama za Taasisi za Muungano haziwahusu.
Sita, mapato ya Zanzibar hayavuki bahari lakini ya Tanganyika yanavuka

Kwa usawa huo wanashindwaje kufanya mambo makubwa? Jiulize kwanini inatokea sasa na si huko nyuma?
Marais waliopita hawakukubali uporaji wa rasilimali, tuna ushahidi lakini sasa shamba la bibi.
Miradi lukuki inayoendelea huku Zenji, si ajabu mgao kwao umeongezwa maradufu . Charity begins at home bwana.
 
Hizi mijadala ndio ilisababisha niipende Jf enzi hizo.
Hapana serikali moja haitawezekana kwasababu ya Utaifa. Wazanzibar wanaona Uzanzibar ni Ubora kuliko Utanzania.
Fikiri kwamba hata sasa hivi hawautaki Utanzania, sasaunategemea nini mbele ya safari.

Tatizo la Muungano litaondoka kwa mambo mawili

1. Kura ya maoni kwa Wazanzibar ikiwa wanataka au la, kama hawataki njia nyeupe waondoke

2. Ikiwa wanataka lazima kuwe na Serikali 3. Uwepo wa Serikali ya Tanganyika utasaidia kudhibiti hujuma zinazofanywa na kuifanya Tanganyika kuwa ''cash cow' ya Zanzibar. Kwasasa Wazanzibar hawahitaji kufanya kazi!

Mfano, Rais wa JMT aliamua 21% ipewe Zanzibar. Hakuna aliyeeleza ajira hizo ni zipi na maeneo gani
Kubwa zaidi ,ikiwa kuna 21% ya ajira kwa Zanzibar huo ni msaada, na Zanzibar inawajibika kuwalipa watumishi hao

Kinyume chake, wanadai 21% na walipewa na Rais SSH lakini mzigo wa kulipa ni wa Tanganyika
Magufuli alikataa kusamehe deni la Umeme, well, ghafla Bilioni 60 zikasamehewa na mzigo akaubeba Mtanganyika

Yote yanatokea kwasababu hakuna mtetezi wa Tanganyika. Kiongozi wa JMT hawezi kuwa kiongozi wa Tanganyika

Muundo ni tatizo kubwa sana, ingawa viongozi wanakwepa ukweli, ipo siku watu watafukuzana! alisema Palamagamba
 
Kwanza nianze na sentensi yako ya mwisho. Tayari kumetokea viongozi wanaoliona tatizo.
Mzee Warioba, Mzee Salim Ahmed na Mzee Butiku walikuwa wajumbe wa Tume ya Warioba iliotoa rasimu ya Katiba

Wazee hawa walikuwepo Muungano unaasisiwa, walifanya kazi na Nyerere, wameshuhudia misuko suko mingi inayohusu Muungano wakiwa Viongozi waandamizi katika serikali ya Mwalimu

Wazee hawa wakiwa na Tume ya Warioba walizunguka nchi nzima kusikiliza maoni ya Wananchi kuhusu katinba.
Moja ya mambo wanayosema yalikuwa magumu ni suala la Muungano, na walieleza kwa undani wake.

Katika hitimisho , Wazee walishauri uwepo wa Serikali tatu na kupunguza mambo ya muungano kutoka 22 hadi 7

Mambo 15 yaliyoondolewa yote yaligharamiwa na Tanganyika. 7 yaliyobaki hayakuwa na gharama za ziada

1. Katiba na mamlaka ya JMT
2. Ulinzi na Usalama wa JMT ( Gharama zisingeongezeka kwasababu jeshi linabaki lile lile la sasa )
3.Uraia na Uhamiaji ( Gharama ni zile zile za sasa )
4. Sarafu na Bank kuu (Inabaki kama ilivyo sasa )
5. Mambo ya nje (Gharama zingebaki kama ilivyo sasa)
6. Usajili wa vyama ( Kama ilivyo sasa)
7. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatakanayo na JMT

Mambo mengine yote yangebaki kuwa ya Serikali Washirika. Kusingekuwa na ongezeko la Taasisi yoyote.
Hili lingesaidia Tanganyika kupunguza mzigo wa kuendesha Muungano yenyewe.

Kwa mfano, Bunge la JMT lingekuwa na 45 kwa 25 na nchi Washirika zingegharamia Wabunge wake.

Kwasasa Tanganyika inababe gharama za Wabunge 80 wa Zanzibar wanaojadli mambo 7 yaliyoanishwa hapo juu.

Majimbo ya Zanzibar yana watu 6,000 kama mtaa mmoja wa Magomeni.
Diwani wa Kata ya Magomeni ana wapiga kura wengine zaidi ya Mbunge wa JMT kutoka Zanzibar.

Gharama za Mbunge wa Zanzibar zinatoka hazina Tanganyika. Mbunge wa Zanzibar anayechaguliwa na watu 6,000 anapewa pesa za mfuko wa Jimbo kutoka hazina Tanganyika kwenda kuendeleza Zanzibar , sawa na Mbunge wa Ubungo mwenye watu Milioni 1, au Wa Ilala au Kigamboni.

kwanini Zanzibar tugawane misaada na mikopo lakini gharama za Muungano ikiwemo pesa za majimbo ya Zanzibar zilipwe na kodi za Tanganyika?

Kwahiyo, Waasisi wa Muungano walikuwa na nia njema kwa bahati mbaya hawakuweka misingi imara
Bahati mbaya hawakuweka misingi imara!
Vision yao natumaini ilikuua ni njema kabisa, na hata ukisikiliza baadhi ya hotuba za mwalimu katika engo hio unaona wazi kabisa nia na madhumuni yalikua ni mazuri na yenye maslahi mapana.

Katika chochote kinacho fanyika na mwanadamu yoyote hakikosekani error, ndio maana kila kubaliano lazima liwe na pande mbili , kwamba ikiwa hivi basi ita kuwa vile na ikiwa vile basi itakuwa hivi.

Ama waliharakisha sana kabla ya kufikiria matokeo hasi, ama walikua na mahaba sana na hio issue hawakuona side effects zake.

Makosa tunayo sisi ambao tupo kwenye uhalisia wa side effect lakini hatuna cha kufanya, tunaamini akili ya mwaka 1960 wakati sana nuru imesha tupambazukia na upeo umekua mkubwa wa kujua lipi jema na ambalo silo.
 
Hapana serikali moja haitawezekana kwasababu ya Utaifa. Wazanzibar wanaona Uzanzibar ni Ubora kuliko Utanzania.
Fikiri kwamba hata sasa hivi hawautaki Utanzania, sasaunategemea nini mbele ya safari.

Tatizo la Muungano litaondoka kwa mambo mawili

1. Kura ya maoni kwa Wazanzibar ikiwa wanataka au la, kama hawataki njia nyeupe waondoke

2. Ikiwa wanataka lazima kuwe na Serikali 3. Uwepo wa Serikali ya Tanganyika utasaidia kudhibiti hujuma zinazofanywa na kuifanya Tanganyika kuwa ''cash cow' ya Zanzibar. Kwasasa Wazanzibar hawahitaji kufanya kazi!

Mfano, Rais wa JMT aliamua 21% ipewe Zanzibar. Hakuna aliyeeleza ajira hizo ni zipi na maeneo gani
Kubwa zaidi ,ikiwa kuna 21% ya ajira kwa Zanzibar huo ni msaada, na Zanzibar inawajibika kuwalipa watumishi hao

Kinyume chake, wanadai 21% na walipewa na Rais SSH lakini mzigo wa kulipa ni wa Tanganyika
Magufuli alikataa kusamehe deni la Umeme, well, ghafla Bilioni 60 zikasamehewa na mzigo akaubeba Mtanganyika

Yote yanatokea kwasababu hakuna mtetezi wa Tanganyika. Kiongozi wa JMT hawezi kuwa kiongozi wa Tanganyika

Muundo ni tatizo kubwa sana, ingawa viongozi wanakwepa ukweli, ipo siku watu watafukuzana! alisema Palamagamba
Hawakulazimishwa kujiunga na muungano,Bali hofu Yao baada ya mapinduzi ndio iliwafanya waombe msaada wa ulinzi kutoka kwetu ndio wakaambiwa haiwezekani hadi tuungane!!

Hapo hamna namna ni kuua uzanzibari na utanganyika!!

Hatuwezi kwenda hivi,hatuwezi kwenda na ndoa nusu nusu tunataka ndoa kamili ya Tanganyika na Zanzibar!!

Inawezekana sema tuna viongozi waoga sana kufanya maamuzi magumu!!

Hilo Wala hakina mjadala atake leta fyoko anachungulia kaburi Wala hamna mjadala!!
 
Hawakulazimishwa kujiunga na muungano,Bali hofu Yao baada ya mapinduzi ndio iliwafanya waombe msaada wa ulinzi kutoka kwetu ndio wakaambiwa haiwezekani hadi tuungane!!

Hapo hamna namna ni kuua uzanzibari na utanganyika!!

Hatuwezi kwenda hivi,hatuwezi kwenda na ndoa nusu nusu tunataka ndoa kamili ya Tanganyika na Zanzibar!!

Inawezekana sema tuna viongozi waoga sana kufanya maamuzi magumu!!

Hilo Wala hakina mjadala atake leta fyoko anachungulia kaburi Wala hamna mjadala!!
Kuna habari kuwa mwenda zake alikuwa amesha set kuwa katika uongozi wake ataunganisha serikali mbili na kuwa moja, na Zanzibar ikiunganisha visiwa vya pemba, unguja na mafia itakuwa mkoa mmoja wenye wilaya 4, moja pemba, unguja wilaya mbili na ya nne mafia.
Hizi habari, amewahi kuzisema Maalim, tena hadharan. Akasema atapambana kwa hali na Mali kuhakikisha hilo halitokei,
Lakin pia habari za ndan zinasema move ilikuwa kumchukua rais wa Zanzibar kumfanya kuwa ndie mgombea urais wa 2025 ili kuwatuliza Wazanzibar. Bahati mbaya hatuko nae. Mungu ailaze roho yake mahali pema pepon.
Habari za ndan zinasema Leo lilikuwa kui neutralize kabisa, mipango ilikuwa tayar, kuhakikisha wafanyakazi wote wa serikali za miji ya zanzibar kuletwa Tanganyika na kule kupelekwa watanganyika. Wanafunzi wengi kuletwa bara na wa bara kupelekwa kule.
Bahat mbaya mwamba wa kufanya mambo makubwa hayupo.

Ni wazi kuwa aliyetunyang'anya JPM mapema alitukatili sana. Alitunyima mabadiliko makubwa sana.
 
Hawakulazimishwa kujiunga na muungano,Bali hofu Yao baada ya mapinduzi ndio iliwafanya waombe msaada wa ulinzi kutoka kwetu ndio wakaambiwa haiwezekani hadi tuungane!!

Hapo hamna namna ni kuua uzanzibari na utanganyika!!

Hatuwezi kwenda hivi,hatuwezi kwenda na ndoa nusu nusu tunataka ndoa kamili ya Tanganyika na Zanzibar!!

Inawezekana sema tuna viongozi waoga sana kufanya maamuzi magumu!!

Hilo Wala hakina mjadala atake leta fyoko anachungulia kaburi Wala hamna mjadala!!
Siamini sana kama shida ni uoga wa viongozi. Shida kubwa ni ubinafsi. Wanaona kama tutakua na serikali moja basi Wanaweza poteza nafasi ya ushawishi walio nao.

Ila kiukweli Mzanzibari/Mtanganyika wa kawaida hafaidiki kwa chochote na Mipaka hii ya kikolony.

Mawazo yangu ni kua na Serikali ya Majimbo tu kurahisisha utawala wa kila eneo
 
Kuna habari kuwa mwenda zake alikuwa amesha set kuwa katika uongozi wake ataunganisha serikali mbili na kuwa moja, na Zanzibar ikiunganisha visiwa vya pemba, unguja na mafia itakuwa mkoa mmoja wenye wilaya 4, moja pemba, unguja wilaya mbili na ya nne mafia.
Hizi habari, amewahi kuzisema Maalim, tena hadharan. Akasema atapambana kwa hali na Mali kuhakikisha hilo halitokei,
Lakin pia habari za ndan zinasema move ilikuwa kumchukua rais wa Zanzibar kumfanya kuwa ndie mgombea urais wa 2025 ili kuwatuliza Wazanzibar. Bahati mbaya hatuko nae. Mungu ailaze roho yake mahali pema pepon.
Habari za ndan zinasema Leo lilikuwa kui neutralize kabisa, mipango ilikuwa tayar, kuhakikisha wafanyakazi wote wa serikali za miji ya zanzibar kuletwa Tanganyika na kule kupelekwa watanganyika. Wanafunzi wengi kuletwa bara na wa bara kupelekwa kule.
Bahat mbaya mwamba wa kufanya mambo makubwa hayupo.

Ni wazi kuwa aliyetunyang'anya JPM mapema alitukatili sana. Alitunyima mabadiliko makubwa sana.
Kina JPM tupo wengi sana mkuu,ni fursa hatupewi coz matatizo mengi ya hii nchi yanasababishwa na kulea vitabia vya kijinga jinga kama kuwekeza mapesa mengi kwenye siasa kulipa mishahara na maposho ya mafuta na mengineyo ambayo hayana tija kabisa!!

Tukiua mapasa mengi kumwagwa kwenye siasa tutatatua nusu ya matatizo ya rushwa na ufisadi yaliyopo!!

Siasa inapaswa kuwa kazi ya kawaida sana inayofanywa na wastaafu baada ya kustaafu professional zao zenye malipo ya kueleweka na sio ifanywe na vijana wanaopoteza uanaume wao kwa kuwa machawa kiasi kwamba wanaoweza hata kuinamishwa na kushikishwa ukuta Ili wapate teuzi na ndipo tunapoelekea huko yaani mahela ya siasa yatafanya vijana wawe mashoga kivitendo coz kwa sasa machawa ni mashoga kifikra waliopoteza uanaume wao kwa kuendekeza sifa za kijinga!

Wanasiasa wanaharibu nasaba ya utanzania wetu kwa kuhonga vijana mapesa na kuwafanya kuwa machawa hadi Baadae watakua mashoga wengi sana hapa nchini!!

MAAMUZI MAGUMU

UA siasa iwe kazi ya malipo ya kawaida vijana wajikite kwenye professional zao wakasome weledi Mbali mbali waokoe taifa letu kuliko huu ujinga unaolindea na dola uliopo wa mapesa mengi kwenye siasa kiasi kwamba madokta na maprofesa wanakimbia vyuo vikuu na kuja siasani na kuacha msiba mkubwa wa kitaifa kielimu!!

UA siasa lipa fedha za kutosha kwenye professional na utaalamu wekeza kwenye tafiti za kisayansi liponye taifa na sio kuendekeza mapesa kwa wanasiasa waliopo na wastaafu kiasi kwamba huko mbeleni nusu ya bajeti ya serikali itatumika kulipa mishahara wanasiasa waliopo na waliostaafu na kusababisha msiba mkubwa kwa vitengo vingine!!!

Serikali mbili ni matumizi mabaya ya fedha za umma!!

Kifupi MI NAONA DOLA INA LINDA UJINGA MWINGI WA SIASA NA VIONGOZI BADALA YA KULINDA KADA ZENYE MASLAHI KWA TAIFA LETU YAANI AISEH HASIRA SANA MKUU!!!

WANASIASA WANALEA MACHAWA KWA MAPESA MENGI AMBAYO NI MASHOGA YA KIFIKRA NA KIVITENDO BAADAE,HUWEZI UKAWA CHAWA USIWE SHOGA HATA SIKU MOJA MKUU!LAZIMA USHOGA UTAKUNYEMELEA TU!!


Mungu ibariki Tanzania yetu tuipendayo sana!!!
 
Ni uoga tu mkuu!

UshawIishi haujawahi kumuweka mtu kwenye Dola mkuu!!

Uoga tu wa kijinga!!
Siamini sana kama shida ni uoga wa viongozi. Shida kubwa ni ubinafsi. Wanaona kama tutakua na serikali moja basi Wanaweza poteza nafasi ya ushawishi walio nao.

Ila kiukweli Mzanzibari/Mtanganyika wa kawaida hafaidiki kwa chochote na Mipaka hii ya kikolony.

Mawazo yangu ni kua na Serikali ya Majimbo tu kurahisisha utawala wa kila eneo
 
Tena sana, nimesikia akimaliza ujenzi wa barabara ya Benjamin Mkapa ya Mtoni Darajabovu, ataifumua barabara ya bububu hadi Malindi kisha Itafumuliwa ya Malindi hadi Mnazi mmoja,
Bado miradi mingine tusiyoijua,
Na ile ya Tunguu to Kizimkazi nasikia nayo inajengwa.
Ukiwasikiliza Wazanzibari baadhi yao utasikia "Samia afanye haraka amalize miradi kabla ya 2025 maana wabara hawatampa tena"
Miradi lukuki inayoendelea huku Zenji, si ajabu mgao kwao umeongezwa maradufu . Charity begins at home bwana.
 
Kuna habari kuwa mwenda zake alikuwa amesha set kuwa katika uongozi wake ataunganisha serikali mbili na kuwa moja, na Zanzibar ikiunganisha visiwa vya pemba, unguja na mafia itakuwa mkoa mmoja wenye wilaya 4, moja pemba, unguja wilaya mbili na ya nne mafia.
Hizi habari, amewahi kuzisema Maalim, tena hadharan. Akasema atapambana kwa hali na Mali kuhakikisha hilo halitokei,
Lakin pia habari za ndan zinasema move ilikuwa kumchukua rais wa Zanzibar kumfanya kuwa ndie mgombea urais wa 2025 ili kuwatuliza Wazanzibar. Bahati mbaya hatuko nae. Mungu ailaze roho yake mahali pema pepon.
Habari za ndan zinasema Leo lilikuwa kui neutralize kabisa, mipango ilikuwa tayar, kuhakikisha wafanyakazi wote wa serikali za miji ya zanzibar kuletwa Tanganyika na kule kupelekwa watanganyika. Wanafunzi wengi kuletwa bara na wa bara kupelekwa kule.
Bahat mbaya mwamba wa kufanya mambo makubwa hayupo.

Ni wazi kuwa aliyetunyang'anya JPM mapema alitukatili sana. Alitunyima mabadiliko makubwa sana.
Wazo la kuwa na serikali moja Nyerere alikuwa nalo na alisema ' Kuunda nchi moja kutaifanya Tanganyika ionekane imeimeza Zanzibar'' akiwa na maana imepoteza 'utaifa' kwasababu Tanganyika ni kubwa.

Wazo la Mwalimu lilikuwa kuchukua muda ili kutengeneza serikali ya pamoja ''Blending'

Alianza na kuunganisha vyama, halafu akaongeza mambo ya Muungano kidogo kidogo ili kufikia mahali tunakuwa nchi moja. Mkataba wa Muungano wa 1964 ulikuwa na mambo 11 , yakaongezeka hadi kufikia 22 na Wazanzibar wanasema zaidi ya 33 ukiyamnyumbulisha

Kuongezwa kwa mambo ya Muungano kuliinufaisha Zanzibar kuliko Tanganyika. Kwa mfano, Elimu ya Juu haikuwa jambo la Muungano lakini kupitia mambo 22 Wazanzibar wamenufaika sana na elimua ya Juu, Kati na hata ya sekondari hadi leo n.k. Mfano, kuna nafasi zaidi ya 1000 za mikopo ya elimu ya juu (HESLB) mahsusi kwa Zanzibar.
HESLB ni mfuko wa Tanganyika , Zanzibar wana ZHESLB. Kwa idadi ya watu milioni 1.5 hizo ni nafasi nyingi sana.
'Chukua idadi ya watu ya Mkoa wowote halafu angalia wanafunzi wangapi wanapata HESLB ukilinganisha na Zanzibar.

Zama za nyuma kabla ya mikopo, Wazanzibar walisoma Katika vyuo vya Tanganyika Bure. Angalia Safu yote ya viongozi wa Zanzibar waliopita na Waliopo, ni zao la vyuo vya Tanganyika wakiwemo wanaopinga Muungano.
Orodha ni ndefu , inatosha tu kwa mfano huo

Kwa hali ilivyo Serikali moja italeta matatizo makubwa kama yale ya UK na Scotland, Eritrea na Ethiopia, Timor Mashariki na Indonesia, Oganden na Somali, Biafra na Nigeria , Quebec na Canada, Puerto Rico na USA, Taiwani na China n.k

Kuna mambo yanayoweza kushindwa kwa kupigwa mabomu lakini Utaifa na Imani haviwezakani kabisa
Hata Mwalimu Nyerere Mwaka 1967? alisema '' Kama Zanzibar hawataki Muungano hatawapiga mabomu''

Kuna ushahidi mambo yanapofanyika kwa nia njema na uwazi hupunguza au kuondoa matatizo ya nchi zilizoungana. Mfano, Scotland walipewa kura ya maoni ikiwa wanabaki UK au wanajitoa. Kura ikasema wabaki na tangu wakati huo wenye hoja ya kuondoka wanatatizo kubwa kuihuisha

Quebec ilipewa kura ya maoni na iliamua kubaki ndani ya Canada tena kura ya maoni mara mbili.
Tangu wakati huo hoja imekuwa ngumu sana kuuibua tena.
Timor walipewa kura kama Eritrea na waliamua kuondoka na sasa wanaishi na majirani zao kwa amani.

Ni kwa muktadha huo kuna hoja kwamba Muungano haulindwi kwa bunduki au deraya za kijeshi.

muungano ni makubaliano ya pande husika. Katika Muungano mdogo hupewa haki ya kuamua, na hapa kwetu ni Zanzibar. Hivyo Zanzibar wapewe kura ya maoni kuamua ikiwa wanataka Muungano au la.

Bila kutengua kitendawili hicho hakuna muundo wa serikali wa aina yoyote utakaotoa jibu la tatizo.
 
Miradi lukuki inayoendelea huku Zenji, si ajabu mgao kwao umeongezwa maradufu . Charity begins at home bwana.
Kuna 'factor' nyingi katika hili.

1. Inawezekana Mgao umeongezeka kwasababu hatujui nini kinaendelea nyuma ya pazia.

2. Inawezekana kuna gharama hawana. Mfano, Ingia Bajeti ya SMZ unionyeshe bajeti ya Ulinzi na Usalama, Mambo ya ndani (ikiwemo Uhamiaji) , Mambo ya nje, na Taasisi za Muungano kama Bunge n.k. Hakuna

Nitakupa mfano, Uhamiaji ni suala la Muungano. Zanzibar kuna port of entry mbili tu, Unguja na Pemba
Zanzibar hawahitaji Maafisa zaidi ya 100 lakini kila mwaka wana nafasi maalumu chuo cha Uhamiji kule Tanga.
Gharama za kuwafunza ni za Tanganyika, na mishahara ya wale watakaorudi Zanzibar ni ya JMT a.k.a Tanganyika

Zanzibar wanakusanya pesa za Visa na hizo ni mali ya SMZ siyo za JMT lakini mishahara ya wakusanya kodi na vitendea kazi ni kutoka JMT au Hazina Tanganyika.

Pili, Zanzibar wanadai kkuwa matumizi ya namba za simu +255 ni ya pamoja na hivyo simu zinazopigwa au mapato ya mawasilano hasa kutoka nje yanapaswa kugawanywa. Ni hoja fair kwasababu walikuwa na code yao 259.

Tatizo linaanza pale ambapo mawasiliano yatailazimu Tanzania kulipa fedha nje, hapa atakayelipa ni JMT na si SMZ.
Hivyo wao wanafaidi tu pesa zikiingia lakini kukiwa na malipo si juu yao, kama ilivyo kwa mikopo

tatu, kupitia mamlaka ya mawasiliano TCRA Zanzibar wanapewa mgao wa matumizi ya mawasiliano. Kwa maana kwamba ukipiga simu kutoka Mtwara kwenda Musoma kuna kodi ambayo Zanzibar wanapewa. Kiasi kinahcopelekwa ni kikubwa sana katika mabilioni ukizingatia watumiaji visiwani si zaidi ya 700,000 (TCRA)

3. Pitia Bajati ya SMZ unionyeshe wapi kuna bajeti ya kulipia madeni ya mikopo. Kwa hiyo unaposikia wanapata mgao wa mikopo, kwetu ni adha kwao ni faraja kwasababu mwisho wa siku atakayelipa ni Tanganyika

4. Kuna gharama wanasamehewa. Deni la Tanesco la Bilioni 60 ambazo ni nyingi sana kwa SMZ kwa makusanyo ya Mwezi wamesamehewa. Hili ni deni na Tanesco itatafuta mahali pa kulifidia, gharama hizo atazilipa mbeba mizigo wa Buguruni , boda boda wa Ubungo au Mama Ntiilie wa Mwenge.

5. Kuna 4.5% ya pato la Tanganyika inakwenda Zanzubar kila mwezi kutoka BoT. Tanganyika na TRA wakifanya vizuri ni neema kwa upande mwingine. Jaribu kupiga hesababu za mitaani tu, 4.5% ta Trilioni moja

Unapokuwa huna matumizi kwa baadhi ya mambo, ukawa na mapato ya ziada ya kile unachopata kuna nafasi ya kufanya mambo mengi makubwa zaidi ya miradi
 
Hayo matatizo ya huko uengereza huwezi fananisha na huku!

Huku nchi mbili lakini uingereza ni visiwa vingi kuliko huku!

Serikali mbili kuwa moja ni jambo rahisi sana huku kwetu ,wazanzibari wanapaswa wakubali utaifa wao uliisha pale walipoungana na Tanganyika na uzanzibari ilitiShia pale !

Hizo nyingine ni blah blah za huruma ambazo hazina mashiko!!

Huwezi ukawa na serikali mbili katika muungano Bali serikali inakuwa moja tu baada ya muungano hakuna Cha kusema uzanzibari Wala utanganyika Wala kero za muungano Bali changamoto za kitaifa!!

Mliamua kuikuza Zanzibar baada ya muungano tatizo lipo hapo mbona watanganyika walikubali kuwa watanzania!?kwanini Zanzibar isingekubali utanzania mapema mkaendelea kulea uzanzibari!!!?


Mi nadhani watz tuache kulea hisia za moyoni za watu Bali ukweli wa kitaifa!!

Huwezi oa au kuolewa halafu eti tulee kumbukumbu zako za nyumbani kwenu,Lazima ukubaliane na ukweli kuwa uzanzibari na utanganyika ulikufa rasmi baada ya Muungano!!
Wazo la kuwa na serikali moja Nyerere alikuwa nalo na alisema ' Kuunda nchi moja kutaifanya Tanganyika ionekane imeimeza Zanzibar'' akiwa na maana imepoteza 'utaifa' kwasababu Tanganyika ni kubwa.

Wazo la Mwalimu lilikuwa kuchukua muda ili kutengeneza serikali ya pamoja ''Blending'

Alianza na kuunganisha vyama, halafu akaongeza mambo ya Muungano kidogo kidogo ili kufikia mahali tunakuwa nchi moja. Mkataba wa Muungano wa 1964 ulikuwa na mambo 11 , yakaongezeka hadi kufikia 22 na Wazanzibar wanasema zaidi ya 33 ukiyamnyumbulisha

Kuongezwa kwa mambo ya Muungano kuliinufaisha Zanzibar kuliko Tanganyika. Kwa mfano, Elimu ya Juu haikuwa jambo la Muungano lakini kupitia mambo 22 Wazanzibar wamenufaika sana na elimua ya Juu, Kati na hata ya sekondari hadi leo n.k. Mfano, kuna nafasi zaidi ya 1000 za mikopo ya elimu ya juu (HESLB) mahsusi kwa Zanzibar.
HESLB ni mfuko wa Tanganyika , Zanzibar wana ZHESLB. Kwa idadi ya watu milioni 1.5 hizo ni nafasi nyingi sana.
'Chukua idadi ya watu ya Mkoa wowote halafu angalia wanafunzi wangapi wanapata HESLB ukilinganisha na Zanzibar.

Zama za nyuma kabla ya mikopo, Wazanzibar walisoma Katika vyuo vya Tanganyika Bure. Angalia Safu yote ya viongozi wa Zanzibar waliopita na Waliopo, ni zao la vyuo vya Tanganyika wakiwemo wanaopinga Muungano.
Orodha ni ndefu , inatosha tu kwa mfano huo

Kwa hali ilivyo Serikali moja italeta matatizo makubwa kama yale ya UK na Scotland, Eritrea na Ethiopia, Timor Mashariki na Indonesia, Oganden na Somali, Biafra na Nigeria , Quebec na Canada, Puerto Rico na USA, Taiwani na China n.k

Kuna mambo yanayoweza kushindwa kwa kupigwa mabomu lakini Utaifa na Imani haviwezakani kabisa
Hata Mwalimu Nyerere Mwaka 1967? alisema '' Kama Zanzibar hawataki Muungano hatawapiga mabomu''

Kuna ushahidi mambo yanapofanyika kwa nia njema na uwazi hupunguza au kuondoa matatizo ya nchi zilizoungana. Mfano, Scotland walipewa kura ya maoni ikiwa wanabaki UK au wanajitoa. Kura ikasema wabaki na tangu wakati huo wenye hoja ya kuondoka wanatatizo kubwa kuihuisha

Quebec ilipewa kura ya maoni na iliamua kubaki ndani ya Canada tena kura ya maoni mara mbili.
Tangu wakati huo hoja imekuwa ngumu sana kuuibua tena.
Timor walipewa kura kama Eritrea na waliamua kuondoka na sasa wanaishi na majirani zao kwa amani.

Ni kwa muktadha huo kuna hoja kwamba Muungano haulindwi kwa bunduki au deraya za kijeshi.

muungano ni makubaliano ya pande husika. Katika Muungano mdogo hupewa haki ya kuamua, na hapa kwetu ni Zanzibar. Hivyo Zanzibar wapewe kura ya maoni kuamua ikiwa wanataka Muungano au la.

Bila kutengua kitendawili hicho hakuna muundo wa serikali wa aina yoyote utakaotoa jibu la tatizo.
 
Hayo matatizo ya huko uengereza huwezi fananisha na huku!
Huku nchi mbili lakini uingereza ni visiwa vingi kuliko huku!
Mbona nimekupa maeneo yote ya Dunia, Kuanzia China , middle east, Africa, Europe hadi America!
Si sahihi kusema nimengelea Uingereza peke yake.
Serikali mbili kuwa moja ni jambo rahisi sana huku kwetu ,wazanzibari wanapaswa wakubali utaifa wao uliisha pale walipoungana na Tanganyika na uzanzibari ilitiShia pale !
Ukisema wanapaswa ' hiyo ni wish' lakini uhalisia ni kwamba wao wanataka Uzanzibar wao kama Utaifa.
Kwamba ni jema au ni baya hilo kila mtu ataliangalia kwa mtazamo wake.
Ninachokuhakikishia, serikali 2 ni tatizo na hiyo moja HAIWEZEKANI! asilani
Huwezi ukawa na serikali mbili katika muungano Bali serikali inakuwa moja tu baada ya muungano hakuna Cha kusema uzanzibari Wala utanganyika Wala kero za muungano Bali changamoto za kitaifa!!
Ndivyo ingalikuwa lakini sivyo na hakuna namna ya kufanya kinyume. Nyerere alisema hilo mwaka 1967 ?
Mliamua kuikuza Zanzibar baada ya muungano tatizo lipo hapo mbona watanganyika walikubali kuwa watanzania!?kwanini Zanzibar isingekubali utanzania mapema mkaendelea kulea uzanzibari!!!?
Misingi ya Muungano haikuwa Imara! huo ndio ukweli
Mi nadhani watz tuache kulea hisia za moyoni za watu Bali ukweli wa kitaifa!!
Ni maoni yako
Huwezi oa au kuolewa halafu eti tulee kumbukumbu zako za nyumbani kwenu,Lazima ukubaliane na ukweli kuwa uzanzibari na utanganyika ulikufa rasmi baada ya Muungano!!
Lakini upo 'live' kuliko siku ulipokufa
 
Back
Top Bottom