Dark days 17/03/20...

Dark days 17/03/20...

Kuna habari kuwa mwenda zake alikuwa amesha set kuwa katika uongozi wake ataunganisha serikali mbili na kuwa moja, na Zanzibar ikiunganisha visiwa vya pemba, unguja na mafia itakuwa mkoa mmoja wenye wilaya 4, moja pemba, unguja wilaya mbili na ya nne mafia.
Hizi habari, amewahi kuzisema Maalim, tena hadharan. Akasema atapambana kwa hali na Mali kuhakikisha hilo halitokei,
Lakin pia habari za ndan zinasema move ilikuwa kumchukua rais wa Zanzibar kumfanya kuwa ndie mgombea urais wa 2025 ili kuwatuliza Wazanzibar. Bahati mbaya hatuko nae. Mungu ailaze roho yake mahali pema pepon.
Habari za ndan zinasema Leo lilikuwa kui neutralize kabisa, mipango ilikuwa tayar, kuhakikisha wafanyakazi wote wa serikali za miji ya zanzibar kuletwa Tanganyika na kule kupelekwa watanganyika. Wanafunzi wengi kuletwa bara na wa bara kupelekwa kule.
Bahat mbaya mwamba wa kufanya mambo makubwa hayupo.

Ni wazi kuwa aliyetunyang'anya JPM mapema alitukatili sana. Alitunyima mabadiliko makubwa sana.
Amini nakuambia hiyo move itakuja kutimia siku moja!

Hatupo mbali kabisa kufikia maamuzi hayo ni swala la muda tu,mawazo ya JPM ndio framework ya siasa zijazo huko mbeleni!!!
 
....moja HAIWEZEKANI! asilani
Moja inawezekana kabisa kama watanganyika na Wazanzibari na hasa Wazanzibari watakubaliana. Na wakawa na Nia ya dhati ya kuimarisha Pan-Africanism.

Tatizo Kuna "elites" kadhaa nadhani katika pande zote mbili za Muungano wanaonufaika na set up hii ya Muungano. Na kwa kweli siamini kama Mzanzibar wa kawaida/ raia wa kawaida anachukia kuungana na mtanganyika kutengeneza Serikali moja, kama yupo kweli basi huyo atakuwa ni " kada wa elite " ( tunajua kada wa mtu ni chawa).

Binafsi, na sisitiza kumaliza kero za Muungano ni ama kuwa na serikali mbili/ nchi huru mbili zinazojitegemea kwa Kila kitu yaani Tanganyika na Zanzibar ama serikali Moja ya Muungano wa hizi nchi mbili.

Sikubaliani na Muungano wa serikali Tatu kwa sababu kutaongeza gharama kwa raia. Na kutaendeleza kero za Muungano.

Tukiwa na serikali moja hakutakuwa na malalamiko ya kwa nini wanafunzi wa Zanzibar wanachukua mkopo HESLB na kadhalika na kadhalika. Vivo hivyo tukiwa na serikali mbili/ nchi huru mbili hambazo hazihusiani katika uendeshaji wake hakutakuwa na kero za Muungano.

Hakuna kinachoshindikana chini ya Jua. Tukubali kufuta KERO za Muungano moja kwa moja na asilani tusiongeze kero za Muungano kwa kutengeneza Serikali Tatu.
====
yoga utusamehe lengo la uzi limebadilishwa siyo fictional thread Tena ambayo inatumia codes. Lakini, nadhani baada ya kuahidi kuleta uzi mwingine (huu umetelekezwa) acha tuendelee kuelimishana kupitia hapa.

Kumradhi yoga .
 
Moja inawezekana kabisa kama watanganyika na Wazanzibari na hasa Wazanzibari watakubaliana. Na wakawa na Nia ya dhati ya kuimarisha Pan-Africanism.
Haiwezekani! , Wazanzibar hawataki kujitambulisha kwa Utanzania kwasababu Uzanzibar ni Bora kwao

Kuna 'egoism' kwamba Wazanzibar ni Watu muhimu sana na wanahitaji 'special treatment' katika Muungano.
Hiyo mentality wanayo na huwezi kuiondoa.

Kuna tatizo jingine, Zanzibar ni wamoja kukiwa na Tanganyika. Wakiwa wenyewe kuna wanaoamini mapinduzi ni haramu na hutawasikia hata wakitamka. Kundi hili linaamini katika Zanzibar ya nyakati hizo na lina 'theory' kwamba mapinduzi yameletwa na Tanganyika

Kuna Mapinduzi daima, wanaamini katika mapinduzi , hawa wapo tayari kwa Serikali moja na ndio hasa wanaotaka Serikali mbili kwa hofu kwamba Usultan utarudi. Unamkumbuka Mbunge Kassim alisema nini Bungeni? Serikali moja haiwezekani! na kwangu mimi ni wazo baya sana kuliko kuunja Muungano
Binafsi, na sisitiza kumaliza kero za Muungano ni ama kuwa na serikali mbili/ nchi huru mbili zinazojitegemea kwa Kila kitu yaani Tanganyika na Zanzibar ama serikali Moja ya Muungano wa hizi nchi mbili.
Hapa una maana kuvunja Muungano. Huwezi kuwa na nchi mbili bila kitu common.
Kama unahitaji kiunganisho, ni serikali ya JMT na hapo tayari una Serikali 3
Sikubaliani na Muungano wa serikali Tatu kwa sababu kutaongeza gharama kwa raia. Na kutaendeleza kero za Muungano.
Hili ni jambo linalohitaji mjadala, nashukuru sana umelileta. Kwa hili tumalize upotoshaji wa either side
Naomba unionyeshe ni wapi, kwa namna gani Serikali tatu itaongeza gharama.
Tukiwa na serikali moja hakutakuwa na malalamiko ya kwa nini wanafunzi wa Zanzibar wanachukua mkopo HESLB na kadhalika na kadhalika. Vivo hivyo tukiwa na serikali mbili/ nchi huru mbili hambazo hazihusiani katika uendeshaji wake hakutakuwa na kero za Muungano.
Serikali moja haiwezekani si kwasababu ya Tanganyika ni kwasababu ya Zanzibar.
Hakuna kinachoshindikana chini ya Jua. Tukubali kufuata KERO za Muungano moja kwa moja na asilani tusiongeze kero za Muungano kwa kutengeneza Serikali Tatu.

Hakuna kero za Muungano, kuna malalamiko ya Wazanzibar. Malamaiko yamejikita katika kutaka kupewa na si kuwajibika. Huwezi kudai kero ya ajira halafu ukapewa 21% kisha ukakimbia kuwalipa mishahara. Hiyo si kero

Wanadai mapato ya Visa yabaki Zanzibar, mishahara ya Uhamiaji itoke Tanganyika. Hiyo si kero
Wanataka mikopo ya nje wapate mgao Maalumu, halafu hawalipi mikopo hiyo. hiyo si kero
Wanataka kutumia umeme hawataki kulipa. Hiyo si kero
Wanapougua wanakuja Wizara ya Afya Tanganyika ili wakatibiwe India. Hiyo si kero
Wanataka bidhaa ziingie kutoka Zanzibar wasikokusanya kodi. Hiyo si kero

Orodha ni ndefu, naomba unitajie kinachoitwa kero moja genuine tuaijadili hapa

Mwisho, naomba utushawishi Watanganyika kwamba tunahitaji Muungano

 
Naomba unionyeshe ni wapi, kwa namna gani Serikali tatu itaongeza gharama.
Asante sana, Mkuu, kwa kuendelea kutoa Elimu juu ya masuala haya ya Muungano.

Umeniuliza swali ni kwa namna gani serikali Tatu zitaongeza gharama. Kuongezeka kwa gharama kwa raia Kuna jidhihirisha katika rasimu ya katiba mpya iliyoandaliwa na "Tume ya Katiba" iliyoongozwa na Mheshimiwa Jaji Warioba. Ukweli, gharama nilizosema zilikuwa zime"kokotolewa" kutoka kwenye rasimu hiyo ya Katiba.

Katika rasimu hiyo, hasa SURA YA SITA inayooelezea muundo wa Muungano utaona kabisa, kuwa Jamhuri ya Muungano itagharamiwa na raia hawa hawa wa nchi Mbili, pia wananchi hawa hawa watagharamia serikali za nchi zao. Tena katika sura hii, raia hawa hawa watalazimika kutengeneza katiba mpya nyingine za nchi zao!!! Kwa hiyo, kwenye katiba Yao watakuwa na "Rais wao" atakayelipwa mshahara na masulufu mengine na raia hawa hawa! Kifupi, raia hawa hawa watawalipa mshahara Marais wa wawili. Huo ni mfano mmoja tu wa kuongeza gharama (watanganyika wameishazoea hili nadhani)!

Pia kuhusu, Serikali Tatu kuongeza kero za Muungano (ambazo unasema ni Bora tuziite Malalamiko ya Muungano). Hili linajionyesha wazi kwenye sura hii ya SITA ya rasimu ya katiba mpya, sura ya SABA na kipengele cha Mambo ya Muungano (tafadhali yasome Tena uone kama kweli Yale yanaondoa malalamiko kwa Wazanzibari) yaliyotajwa ibara ya 63 na kuambatanishwa mwishoni mwa rasimu hiyo ya katiba mpya.

Yaani itakuwa ni vurugu badala ya Malalamiko, maana Kuna mambo mengi ambayo yana mkanganyiko hayako wazi ambayo yataleta mgongano!

Mfano, ni Ibara ya 65 na ibara ndogo zake nne ambayo inahusu mahusiano ya Nchi mshirika wa Muungano na jumuiya za kikanda na kadhalika. Yaani ibara ndogo ya nne ya ibara hii ya 65 inaelekeza Bunge ndilo litatunga Sheria ya namna Bora ya utekelezaji wa Ibara hii.

Sasa kama nchi mshirika kupitia Bunge lake ( maana watatunga katiba Yao na watakuwa na Bunge lao) itakuja na sheria tata kuhusu jambo hili itakuwaje! Maana ibara ndogo ya 3 ya ibara hii ya 65 inasema mshirika "anaweza" (siyo lazima) kumshirikisha Serikali ya Muungano juu ya Nia yake yakuwa na mshirika wa kikanda nakadhalika!!!!

Na katika kuweka sawa utata huu utakapojitokeza huko mbeleni gharama zote atabebeshwa raia hawa hawa wa nchi hizi mbili kwa kuunda matume na task forces!!!

Vipo vipengele vingi kwa kweli katika muundo wa Muungano wa serikali Tatu mbali na kuongeza gharama kwa raia lakini pia vitasababisha kero/malalamiko ya Muungano kuwa vurugu na kuhatarisha Amani na tengamano wa Raia. Tuepuke Muundo wa serikali Tatu.

Mkuu, nadhani nimejitahidi kujibu swali lako! Asubuhi njema.
 
Haiwezekani! , Wazanzibar hawataki kujitambulisha kwa Utanzania kwasababu Uzanzibar ni Bora kwao

Kuna 'egoism' kwamba Wazanzibar ni Watu muhimu sana na wanahitaji 'special treatment' katika Muungano.
Hiyo mentality wanayo na huwezi kuiondoa.

Kuna tatizo jingine, Zanzibar ni wamoja kukiwa na Tanganyika. Wakiwa wenyewe kuna wanaoamini mapinduzi ni haramu na hutawasikia hata wakitamka. Kundi hili linaamini katika Zanzibar ya nyakati hizo na lina 'theory' kwamba mapinduzi yameletwa na Tanganyika

Kuna Mapinduzi daima, wanaamini katika mapinduzi , hawa wapo tayari kwa Serikali moja na ndio hasa wanaotaka Serikali mbili kwa hofu kwamba Usultan utarudi. Unamkumbuka Mbunge Kassim alisema nini Bungeni? Serikali moja haiwezekani! na kwangu mimi ni wazo baya sana kuliko kuunja Muungano

Hapa una maana kuvunja Muungano. Huwezi kuwa na nchi mbili bila kitu common.
Kama unahitaji kiunganisho, ni serikali ya JMT na hapo tayari una Serikali 3

Hili ni jambo linalohitaji mjadala, nashukuru sana umelileta. Kwa hili tumalize upotoshaji wa either side
Naomba unionyeshe ni wapi, kwa namna gani Serikali tatu itaongeza gharama.

Serikali moja haiwezekani si kwasababu ya Tanganyika ni kwasababu ya Zanzibar.


Hakuna kero za Muungano, kuna malalamiko ya Wazanzibar. Malamaiko yamejikita katika kutaka kupewa na si kuwajibika. Huwezi kudai kero ya ajira halafu ukapewa 21% kisha ukakimbia kuwalipa mishahara. Hiyo si kero

Wanadai mapato ya Visa yabaki Zanzibar, mishahara ya Uhamiaji itoke Tanganyika. Hiyo si kero
Wanataka mikopo ya nje wapate mgao Maalumu, halafu hawalipi mikopo hiyo. hiyo si kero
Wanataka kutumia umeme hawataki kulipa. Hiyo si kero
Wanapougua wanakuja Wizara ya Afya Tanganyika ili wakatibiwe India. Hiyo si kero
Wanataka bidhaa ziingie kutoka Zanzibar wasikokusanya kodi. Hiyo si kero

Orodha ni ndefu, naomba unitajie kinachoitwa kero moja genuine tuaijadili hapa

Mwisho, naomba utushawishi Watanganyika kwamba tunahitaji Muungano
Hao jamaa ni nyoro nyoro!Cha msingi ni kuhakikisha wanaanza kutumia ipasavyo misuli Yao kupata riziki!!


Serikali inalea hisia zao,kazi ya serikali sio kulea hisia za MTU Bali kilichobora ambacho ni utaifa wa Tanzania!!
 
Kina JPM tupo wengi sana mkuu,ni fursa hatupewi coz matatizo mengi ya hii nchi yanasababishwa na kulea vitabia vya kijinga jinga kama kuwekeza mapesa mengi kwenye siasa kulipa mishahara na maposho ya mafuta na mengineyo ambayo hayana tija kabisa!!

Tukiua mapasa mengi kumwagwa kwenye siasa tutatatua nusu ya matatizo ya rushwa na ufisadi yaliyopo!!

Siasa inapaswa kuwa kazi ya kawaida sana inayofanywa na wastaafu baada ya kustaafu professional zao zenye malipo ya kueleweka na sio ifanywe na vijana wanaopoteza uanaume wao kwa kuwa machawa kiasi kwamba wanaoweza hata kuinamishwa na kushikishwa ukuta Ili wapate teuzi na ndipo tunapoelekea huko yaani mahela ya siasa yatafanya vijana wawe mashoga kivitendo coz kwa sasa machawa ni mashoga kifikra waliopoteza uanaume wao kwa kuendekeza sifa za kijinga!

Wanasiasa wanaharibu nasaba ya utanzania wetu kwa kuhonga vijana mapesa na kuwafanya kuwa machawa hadi Baadae watakua mashoga wengi sana hapa nchini!!

MAAMUZI MAGUMU

UA siasa iwe kazi ya malipo ya kawaida vijana wajikite kwenye professional zao wakasome weledi Mbali mbali waokoe taifa letu kuliko huu ujinga unaolindea na dola uliopo wa mapesa mengi kwenye siasa kiasi kwamba madokta na maprofesa wanakimbia vyuo vikuu na kuja siasani na kuacha msiba mkubwa wa kitaifa kielimu!!

UA siasa lipa fedha za kutosha kwenye professional na utaalamu wekeza kwenye tafiti za kisayansi liponye taifa na sio kuendekeza mapesa kwa wanasiasa waliopo na wastaafu kiasi kwamba huko mbeleni nusu ya bajeti ya serikali itatumika kulipa mishahara wanasiasa waliopo na waliostaafu na kusababisha msiba mkubwa kwa vitengo vingine!!!

Serikali mbili ni matumizi mabaya ya fedha za umma!!

Kifupi MI NAONA DOLA INA LINDA UJINGA MWINGI WA SIASA NA VIONGOZI BADALA YA KULINDA KADA ZENYE MASLAHI KWA TAIFA LETU YAANI AISEH HASIRA SANA MKUU!!!

WANASIASA WANALEA MACHAWA KWA MAPESA MENGI AMBAYO NI MASHOGA YA KIFIKRA NA KIVITENDO BAADAE,HUWEZI UKAWA CHAWA USIWE SHOGA HATA SIKU MOJA MKUU!LAZIMA USHOGA UTAKUNYEMELEA TU!!


Mungu ibariki Tanzania yetu tuipendayo sana!!!
Hapo kwenye siasa nipo pamoja na wewe ..Siasa imefanya Vijana kuondoa confidence na ubunifu wao, wamegeuka ma changudoa wa siasa...Imeua kabisa taifa hili...Siasa ifanywe na watu ambao wameshatumikia taifa na sasa wanafanya back stoping isiwe profession. Maana mtu mwenye kuamua vizuri ni lazima awe experienced na awe mature ..Watoto hawa wanaoenda kwenye siasa wanawaza V8 tu na kupiga basi!
 
Hoja ya Serikali tatu kuwa na gharama ni hisia za watu wasiotaka Serikali 3 kwa kupotosha Umma

Nimekuuliza na bandiko hapo chini hujaweza kuanisha kwa uyakinifu wapi gharama zitaongezeka.

Kwamba gharama zinazongezeka kwa Raia wa nchi mbili si kweli.

Kwasasa gharama amezibeba Raia wa Tanganyika pekee kwa jina la JMT

Kwa mfano, kuna Wabunge 393 akiwemo AG. Kati yao, 80+ wanatoka Zanzibar gharama zao zinabebwa na Tanganyika kwa jina la JMT ikiwemo kuwapa fedha za Tanganyika kwa mfuko wa jimbo wa Zanzibar!
Pesa za mfuko wa jimbo ni za Tanganyika kwa jina la JMT

Rasimu ya Warioba inasema kutakuwa na Wabunge 50 kutoka Tanganyika na 20 kutoka Zanzibar na Rais atateuwa 5 kutoka kundi la Walemavu kwa jumla ya 75 ( Rasimu ya Warioba Sura ya Tisa 113 (a )(b)

Idadi ya Wabunge 75 ni ndogo sana ukilinganisha na Wabunge 80 pekee kutoka Zanzibar leo hii.

Gharama za Bunge la serikali 3 ni kidogo zaidi kuliko gharama za Wabunge 80 wa JMT kwa sasa.
Watu hawaoni gharama hizi kwasababu zinalipwa na Tanganyika kutoka Hazina.

Pili, nchi Washirika zitaamua idadi ya Wabunge kutokana na Uchumi.. Kwa mfano, Baraza la Wawakilishi lina Wajumbe 50, la kushangaza Wabunge wa JMT kutoka Zanzibar ni 80+.

Ikiwa utaiambia SMZ kulipia Wabunge 80 haitakubali kwasababu BLW linalipia 50, kwavile wanalipiwa na Tanganyika hata wakija 300 hakuna anayejali kwasababu gharama kazibeba Mtanganyika.
Niambie gharama zitaongezeka wapi ?

Nije kwenye hoja zako
Katika rasimu hiyo, hasa SURA YA SITA inayooelezea muundo wa Muungano utaona kabisa, kuwa Jamhuri ya Muungano itagharamiwa na raia hawa hawa wa nchi Mbili, pia wananchi hawa hawa watagharamia serikali za nchi zao.
Kwa muundo wa Serikali mbili Raia wa Tanganyika amebeba jukumu la kuendesha Muungano kwa Gharama.

Raia wa Zanzibar hawana gharama za kuendesha Muungano. Unaposema Raia wa nchi mbili si kweli.

Ikiwa ni kweli unachosema , tuonyeshe Zanzibar inachangia nini katika muundo wa sasa wa Muungano

Tena katika sura hii, raia hawa hawa watalazimika kutengeneza katiba mpya nyingine za nchi zao!!! Kwa hiyo, kwenye katiba Yao watakuwa na "Rais wao" atakayelipwa mshahara na masulufu mengine na raia hawa hawa! Kifupi, raia hawa hawa watawalipa mshahara Marais wa wawili. Huo ni mfano mmoja tu wa kuongeza gharama (watanganyika wameishazoea hili nadhani)!
Kwasasa ndivyo ilivyo, kwamba kila cha JMT kunahusu Tanganyika kwasababu Zanzibar wana Serikali yao.

Waziri Mkuu wa Tanzania si ndiye 'Rais wa Tanganyika kwasasa'. Tena ana Naibu Waziri mkuu mbona huoni hiyo ni gharama. Zanzibar wana admistrative structure yao. Hivyo hakuna kinachoongezeka hata senti tano.

Nitajie Taasisi moja ya Umma hata ulinzi na Usalama ambayo haina mbadala Zanzibar. Moja tu!
Pia kuhusu, Serikali Tatu kuongeza kero za Muungano (ambazo unasema ni Bora tuziite Malalamiko ya Muungano). Hili linajionyesha wazi kwenye sura hii ya SITA ya rasimu ya katiba mpya, sura ya SABA na kipengele cha Mambo ya Muungano (tafadhali yasome Tena uone kama kweli Yale yanaondoa malalamiko kwa Wazanzibari) yaliyotajwa ibara ya 63 na kuambatanishwa mwishoni mwa rasimu hiyo ya katiba mpya.
Rasimu imeorodhesha mambo 7 tu., nimeyaweka. Nionyeshe jambo moja tu ambalo Zanzibar watalalamika

Mambo 7 hayana gharama kwasababu hata sasa yapo na gharama zitabebwa na Tanganyika na hata sasa yanabebwa na Tanganyika. Zanzibar wanalalamika nini?

Orodhesha jambo moja unalodhani litakuwa kero, moja tu
Yaani itakuwa ni vurugu badala ya Malalamiko, maana Kuna mambo mengi ambayo yana mkanganyiko hayako wazi ambayo yataleta mgongano!
Yaorodheshe hapa usiseme kwa ujumla. Taja moja tu at minimum
Mfano, ni Ibara ya 65 na ibara ndogo zake nne ambayo inahusu mahusiano ya Nchi mshirika wa Muungano na jumuiya za kikanda na kadhalika. Yaani ibara ndogo ya nne ya ibara hii ya 65 inaelekeza Bunge ndilo litatunga Sheria ya namna Bora ya utekelezaji wa Ibara hii.
Yes na kuna Wabunge 50/20 plus 5 kutoka kila upande. Hata sasa hivi kinachoitwa Tume ya kumaliza kero ndiyo itakayokuwa sekretariet. Rejea rasimu 117(1) madaraka ya kutunga sheria
Sasa kama nchi mshirika kupitia Bunge lake ( maana watatunga katiba Yao na watakuwa na Bunge lao) itakuja na sheria tata kuhusu jambo hili itakuwaje! Maana ibara ndogo ya 3 ya ibara hii ya 65 inasema mshirika "anaweza" (siyo lazima) kumshirikisha Serikali ya Muungano juu ya Nia yake yakuwa na mshirika wa kikanda nakadhalika!!!!
Kuna Sekretariati ya kuratibu mambo ya nchi Washirika. Kuna sheria zimeanishwa katika rasimu zitakazokuwa chini ya Bunge la JMT. Kuna madaraka ya Rais wa JMT na yameanishwa. n.k.
Na katika kuweka sawa utata huu utakapojitokeza huko mbeleni gharama zote atabebeshwa raia hawa hawa wa nchi hizi mbili kwa kuunda matume na task forces!!!
Unaposema Raia wa nchi mbili unapotosha. Hakuna , narudia tena HAKUNA Raia wa Zanzibar anayebeba gharama hata senti tano ya kuendesha Muungano. Kwasasa gharama zote zinabebwa na Tanganyika 100%

Narudia tena, tuonyeshe mchango wa Raia wa Zanzibar kwa muundo wa sasa kabla ya Serikali 3.
Vipo vipengele vingi kwa kweli katika muundo wa Muungano wa serikali Tatu mbali na kuongeza gharama kwa raia lakini pia vitasababisha kero/malalamiko ya Muungano kuwa vurugu na kuhatarisha Amani na tengamano wa Raia. Tuepuke Muundo wa serikali Tatu.Mkuu, nadhani nimejitahidi kujibu swali lako! Asubuhi njema.
Hakuna kipengele kinachoongeza gharama ndiyo maana hujaweza kutaja idara, taasisi, Wizara itakayoongeza gharma. Tukijadili hili nina uwezo wa kukuonyesha kwamba hakuna hata senti tano itakayoongezeka

Kinachotokea kwa serikali 3 ni kupunguza gharama kwa Tanganyika.

Kwamba Zanzibar itawajibika kwa mambo yake na Raia wake na Tanganyika pia.
Kwasasa Tanganyika imejibeba na kubeba mzigo wa ziada wa Zanzibar isiyo na mchangi wowote kiuchumi

Suala la gharama za Serikali 3 linapotoshwa kwasababu kuna mambo mengi tunajifanya hatuyaoni

1. Mafao ya viongozi Wastaafu kuanzia Marais, Makamu wa Rais na Mawaziri Wakuu na ma- Spika wa Bunge ambazo ni kubwa sana na analipia Raia wa Tanganyika. Mbona hatuoni hili

Gharama za malipo ya Wastaafu hawa kwa mwaka ni kubwa kuliko gharama za Wizara ndogo ya JMT

2. Tunawezaje kupata pesa za kulipa Wake wa wastaafu halafu tunadai serikali 3 inagharma . Yaani tunalipa wanandoa lakini hatuoni hizi ni gharama. Kuna Wake wa Wastaafu wangapi.

3. Tunapoteza pesa (CAG) kwa matrilioni hatuoni kama ni gharama anazobeba Raia

Kusema serikali 3 ina gharama si KWELI, kwa muundo wa sasa bado tuna serikali 3 zilizojificha ndani ya 2.
Serikali ya JMT ni ya Tanganyika pamoja na ya Muungano halafu tuna SMZ.
Kuzitengenisha kutasaidia kupunguza gharama kwa Tanganyika arguably Zanzibar itabaidi walipe gharama

Kwanini watu wanaogopa serikali 3? Ni kwamba itafunua utegemezi wa Zanzibar. Itaondoa free ride ya Zanzibar katika ku abuse Muungano kwa jina la JMT.

Jibu la Kweli ni Kura ya maoni kwa Zanzibar, wakitaka tuwe na 3 ili wawajibike, wakikataa njia nyeupe

Mwisho, naomba unishawishi kwanini na kwa faida gani Mtanganyika anahitaji Muungano na kubebea gharama kubwa peke yake.
 
Mwisho, naomba unishawishi kwanini na kwa faida gani Mtanganyika anahitaji Muungano na kubebea gharama kubwa peke yake.
Asante sana, Mkuu. Na kwa kweli mwenye masikio na asikie.

Nitachelewa kidogo kuja kujibu hoja zako lengo kuwapa wasomaji wa uzi huu kutafakari kwa kina hoja ulizoweka hapa jukwaani nao watoe maoni.

Kwa mara nyingine nakushukuru sana.
 
Ni kwamba pesa zinatoka Bara. Kadri mapato yanavyokusanywa Bara wao wana 4.5%.
Pili, Zanzibar hawakopi ila kupitia JMT na deni hawalipi inalipa JMT ambayo ni Tanganyika
Tatu, Zanzibar haina Bajeti ya Ulinzi , mambo ya ndani, nje, hata Elimu ya Juu wanapata Bara
Nne, Bajeti ya Zanzibar inapewa ruzuku kutoka hazina Dar es Salaam
Tano, gharama za Taasisi za Muungano haziwahusu.
Sita, mapato ya Zanzibar hayavuki bahari lakini ya Tanganyika yanavuka

Kwa usawa huo wanashindwaje kufanya mambo makubwa? Jiulize kwanini inatokea sasa na si huko nyuma?
Marais waliopita hawakukubali uporaji wa rasilimali, tuna ushahidi lakini sasa shamba la bibi.
Dah? Kwasasa mkono umekuwa mrefu acha wajikune sehem zilizokuwa zinawasha!
 
Kanuni ya mkopo ni anayelipa ni aliyekopa, hivyo mikopo ya JMT Zanzibar anapatiwa 4.5% na halipi, analipa aliyekopa!.

Ila kuna mikopo Zanzibar anakopa kwa udhamini wa JMT, hii ni Zanzibar wenyewe wanalipa, ila ikitokea Zanzibar akashindwa kulipa, atakayedaiwa ni mdhamini!.

Kuna madeni kibao tunawalipia na hatuna tatizo!. Vipi wenzangu unaona shida yoyote kumlipia deni mkeo?.

P
😆😆😆 Mke tena?
 
Mkuu Nguruvi3, it's very unfortunately tangu tumeungana, hakuna any civic education or public information program to educate the public about the union, hivyo kuna wengi hawaujui muungano wetu ukiwemo wewe, hivyo najitolea kukuelimisha ili pia kuwaelimisha na wengine.
1. Muungano wetu ni very unique muungano duniani, miungano yote ni ama ni muungano wa union, ama ni muungano wa federation lakini muungano wetu ni both union and federation at the same time.
2. Kimataifa muungano wetu ni muungano wa union wa nchi mbili kuungana na kuunda nchi moja ya JMT ambayo ndio dola yenye sovereignty, yenye rais mmoja wa JMT, yenye serikali moja ya JMT, yenye Bunge moja la JMT, Mahakama moja ya Rufani ya JMT, sarafu moja ya JMT, Benki Kuu moja ya JMT, na uraia mmoja wa JMT.
3. Kwa vile tuna uraia mmoja wa JMT, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari bali kuna mtu mmoja tuu, Mtanzania mwenye haki zote za Utanzania. Hivyo Kila Mzanzibari ni Mtanzania ana haki zote za Utanzania ikiwemo kumiliki ardhi, ajira, elimu, kuishi popote, kufanya kazi popote na kuteuliwa kushika madaraka kwenye wadhifa wowote!.
4. Kimataifa Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT hivyo JMT ndio nchi inawajibika kuhudumia Zanzibar kwa kila kitu.
5. Muungano wetu ni kama ndoa kuna mume amechumbia, amelipa mahari, ameoa, amekabidhiwa mke, hivyo ni wajibu wa mume kumtunza mkewe kwa kila kitu, hivyo serikali ya JMT inaihudumia Zanzibar kwa kila kitu!.
6. Kitaifa muungano wetu ni federation ya nchi mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar yenye utawala wake wa ndani.
7. Hivyo ndani ya Tanzania, muungano wetu ni wa nchi mbili za Tanzania na Zanzibar, zenye serikali mbili, ya JMT na SMZ , zenye marais wawili, rais wa JMT na rais wa Zanzibar, zenye mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, lenye Mahakama mbili, Mahakama Kuu ya JMT na Mahakama Kuu ya Zanzibar, yenye ardhi mbili, ardhi ya JMT na ardhi ya Zanzibar, yenye mipaka miwili, mipaka ya Tanzania Bara na mipaka ya Zanzibar, yenye uraia wa aina mbili, uraia wa JMT na Ukaazi wa Zanzibar.
8. Wenye haki Tanzania ni Watanzania wote, ila wenye haki Zanzibar ni Watanzania ambao ni Wakaazi wa Zanzibar pekee!.
9. Hivyo kila Mtanzania ana haki zote za Utanzania wakiwemo Watanzania wote ambao ni Wakaazi wa Zanzibar
10. Wenye haki Zanzibar ni Wazanzibari Wakaazi pekee.

Sii kweli kuwa wanapata 4.5% ya GDP ya Tanzania, Zanzibar are entitled 4.5% ya fedha zote za mikopo na misaada ya kimataifa only. Fedha hizi ni entitled!.
Mimi nilimuoa sweetheart wangu wa chuo, mimi nikaajiriwa RTD yeye Guardian. 1995 nikaacha kazi RTD na kujiunga DTV, nikamuachisha kazi wife na kukubali kumlipa mshahara wake wote aliokuwa analipwa as her entitlement. Muungano wetu ni kama ndoa, kwenye wanandoa wawili hawa kuna mmoja ambaye ni mume ana sovereignty na ni dola na kuna mwingine ni mke hana sovereignty, hada dola hivyo ni jukumu la mume kuhudumia mkewe. Huduma za mke kutoka kwa mumewe sio favours ni stahiki ni haki yake kwasababu Zanzibar imepoteza sovereignty haiwezi kukopa kimataifa na sio nchi, hivyo JMT ina wajibu kuhudumia!.

Refer No. 3 ya uraia, Mbarawa ni Mtanzania ana haki zote za Utanzania kama Mtanzania mwingine yeyote, na KM wake the same.
Shaka ni kama Mbarawa ana haki zote za Utanzania kama Mtanzania mwingine yeyote ikiwemo kuteuliwa kwenye nafasi yoyote.
Wazanzibari hawapewi ardhi bali wanamiliki ardhi kwa haki ya Utanzania wao kama Mtanzania mwingine yeyote, ila Mtanzania hawezi kumiliki ardhi Zanzibar bali ni Wanzanzibari wakaazi pekee!. Watanzania wote wakiruhusiwa kumiliki ardhi, Watanzania watavamia vile visiwa vitazama!.

Referring to No. 3 again, wabunge wa Zanzibar ndani ya Bunge la JMT wana haki zote za Utanzania na wanajadili chochote!.

Sio sababu za kipuuzi, wana sababu za msingi sana.
Naamini wewe una wazazi, una ndugu na una mke, how much do you spend kwa wazazi na ndugu zako compared to mkeo?. Muungano wetu ni kama ndoa, Zanzibar ni mwanandoa, Simiyu ni mwana ndugu!.

Zanzibar ndio wana sheria ya kura ya maoni, sisi Tanzania Bara, hatuna ila pia hoja kama hii niliwahi kushauri humu Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja
Kwa vile nimeandika sana humu kuhusu muungano, bandiko hili nitalisambaza kwenye baadhi ya post hizo ili uzitumie kama post darasa ujifunze zaidi kuhusu muungano, tena tumshukuru sana Samia, ndie aliyetoa uhuru huu "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza
Natumaini nimekusaidia sana kukuelimisha kuhusu huu muungano wetu adhimu.

Pasco.
Karibu katika baadhi ya Rejea Zangu kuhusu huu Muungano wetu adhimu.
-
-
-
-
-
Brother Pascal Mayalla kama Zanzibar ni mke kwa Tanganyika na Simiyu ni miongoni mwa watoto, hivi ndoa ikija kuvunjika kwa mke huyu huyu mume atakuwa na faida?
Kwa sababu mke aliyeolewa anapewa maendeleo akiwa kwao wala si kwenye himaya ya mume, ndoa ikivunjika mume si itakuwa imekula kwake gharama zoooote alizotumia kwa mke huyu Zanzibar?
 
Safi sana, kwa maneno mengine lazima tuwe na demarcation . Mzee Warioba alisema wazi mambo 7 tu, mengine kila mtu kivyake. Katika mambo 7 mambo 3 tu ndiyo yenye gharama na hizo lazima zichangiwe

Nje, ya Muungano lazima Zanzibar itakuwa na jeshi. Tufanye kwamba watakuwa na Batalion moja (1000) wala siyo brigade, na siyo kama bara. Piga hesababu za kuendesha jeshi la Batalioni moja kwa uchumi wa Zanzibar.
Kwa maana kwamba ni lazima Zanzibar ichangie hata kama ni kwa hesabu za udogo wake

Vivyo hivyo kwa Polisi na Usalama wa Taifa. Nje ya Muungano lazima Zanzibar wawe nazo na hivyo wanalazimika kuchangia na si kupata free ride kama ilivyo sasa

Watanganyika wanasema kwamba tunatumia rasilimali nyingi Zanzibar kuliko kuelekeza maendeo yenye kuchangia pato la Taifa. Zanzibar wanakusanya kodi na wana uchumi wao , waachwe, lakini wasidai kisicho chao kama haki.

Mfano, wanasema Bandari na gesi si jambo la Muungano. Wakati huo huo wanataka 4.5% ya mapato ya Bandari, gesi na madini ikiwemo kodi za mishahara ya Watanganyika. Huu ni ukupe usio na kichwa wala miguu

Zanzibar katika Muungano imegeuka kuwa zigo, kwasababu hatuoni mchango wao zaidi ya kulalama , kudai na kila kelele ambazo kimsingi tumezibomoa isiipokuwa moja '' ni nchi ya kwanza kuwa na TV' ya rangi'' ingawa walioangalia ni Sultan na wake zake. Leo watu wanajisaidia baharini hiyo TV iliwasaidia nini

Tunasema hivi kwasababu muda mrefu waliaminisha dunia wanaibiwa na wanaonewa na Tanganyika.
JK aliwaruhusu waende kukopa wenye, mbona hawaendi. Ni kwasababu hawana uwezo wa kulipa

Bajeti yao ni Trilioni 2.7 sawa na JWT, makusanyo ni bilioni 200 kwa mwezi.
Wazanzibar wanadhulumu Tanesco vipi wanaweza kuzungumza na IMF au WB.

Hiyo miradi mnayoiona na fedha za kukopa au kuchotwa kutoka hazina Tanganyika.

Jibu ni rahisi, kura ya maoni, hawataki hewala! njia nyeupe
Mkuu Nguruvi3 kwamba mapato ya Zanzibar bilioni 200 ni kwa mwaka au?
 
Mkuu Nguruvi3 kwamba mapato ya Zanzibar bilioni 200 ni kwa mwaka au?
Kiasi hicho si halisia ni kikubwa sana ukilinganisha na uhalisi. Kilikuwa kwa ''mjadala'' Uhalisia ni huu hapa

Kwa taarifa ya ZRA ya 02 April 2023, kaika kipindi cha miezi 9 (July 2022- March 2023) mamlaka ilikusanya 449 Bilioni chini ya lengo la 460 Bilioni. Yaani makusanyo yalikuwa Tsh 54 Bilioni kwa mwezi

Tufanye kwamba kiasi cha 54 Bilioni kitaongezeka na kuwa Bilioni 80 kwasababu zozote zile.
Kwa mwaka ni sawa na Bilioni 960. Hiyo ni baada ya ku-inflate figure. Bajeti halisi ni hii hapa chini

Bajeti ya Zanzibar kwa mujibu wa Waziri wa fedha wa Zanzibar, ni Tsh 2.8 Trilioni. Kati ya hizo 1.3T ni matumizi ya kawaida na 1.5 ni kwa maendeleo. Matumizi ya kawaida ni kulipa mishahara ambapo hakuna gharama za ulinzi na usalama, mambo ya ndani, nje, Wizara za Muungano na taasisi zake. Hizo ni kwa mambo ya SMZ

Kwa maneno mengine hata kama watakusanya 1 Trilioni, bado kuna upungufu wa 1.8 Trilioni.
Hizi wanazipata kutoka wapi?

Usisahau kuwa kuna 4.5% wanapaa kutoka Tanganyika kila mwezi.
Ikiwa Tanganyika watakusanya 1 Trilioni kwa mwezi Zanzibar wanapata Bilioni 40 karibia sawa na makusanyo yao.

Pia kumbuka, Bajeti ya 2.8T inakaribiana na Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Usalama ambayo ni 2.T

Kituko ni pale wanataka kuwe na account ya pamoja ya fedha. Rais Mwinyi kawaambia ukweli Desemba 11 2022 kwamba account ya pamoja itabidi Ichangiwe na Zanzibar pia. Sasa wana kipi cha kuchangia ?
 
Haiwezekani! , Wazanzibar hawataki kujitambulisha kwa Utanzania kwasababu Uzanzibar ni Bora kwao

Kuna 'egoism' kwamba Wazanzibar ni Watu muhimu sana na wanahitaji 'special treatment' katika Muungano.
Hiyo mentality wanayo na huwezi kuiondoa.

Kuna tatizo jingine, Zanzibar ni wamoja kukiwa na Tanganyika. Wakiwa wenyewe kuna wanaoamini mapinduzi ni haramu na hutawasikia hata wakitamka. Kundi hili linaamini katika Zanzibar ya nyakati hizo na lina 'theory' kwamba mapinduzi yameletwa na Tanganyika

Kuna Mapinduzi daima, wanaamini katika mapinduzi , hawa wapo tayari kwa Serikali moja na ndio hasa wanaotaka Serikali mbili kwa hofu kwamba Usultan utarudi. Unamkumbuka Mbunge Kassim alisema nini Bungeni? Serikali moja haiwezekani! na kwangu mimi ni wazo baya sana kuliko kuunja Muungano

Hapa una maana kuvunja Muungano. Huwezi kuwa na nchi mbili bila kitu common.
Kama unahitaji kiunganisho, ni serikali ya JMT na hapo tayari una Serikali 3

Hili ni jambo linalohitaji mjadala, nashukuru sana umelileta. Kwa hili tumalize upotoshaji wa either side
Naomba unionyeshe ni wapi, kwa namna gani Serikali tatu itaongeza gharama.

Serikali moja haiwezekani si kwasababu ya Tanganyika ni kwasababu ya Zanzibar.


Hakuna kero za Muungano, kuna malalamiko ya Wazanzibar. Malamaiko yamejikita katika kutaka kupewa na si kuwajibika. Huwezi kudai kero ya ajira halafu ukapewa 21% kisha ukakimbia kuwalipa mishahara. Hiyo si kero

Wanadai mapato ya Visa yabaki Zanzibar, mishahara ya Uhamiaji itoke Tanganyika. Hiyo si kero
Wanataka mikopo ya nje wapate mgao Maalumu, halafu hawalipi mikopo hiyo. hiyo si kero
Wanataka kutumia umeme hawataki kulipa. Hiyo si kero
Wanapougua wanakuja Wizara ya Afya Tanganyika ili wakatibiwe India. Hiyo si kero
Wanataka bidhaa ziingie kutoka Zanzibar wasikokusanya kodi. Hiyo si kero

Orodha ni ndefu, naomba unitajie kinachoitwa kero moja genuine tuaijadili hapa

Mwisho, naomba utushawishi Watanganyika kwamba tunahitaji Muungano
Kuna tatizo jingine, Zanzibar ni wamoja kukiwa na Tanganyika. Wakiwa wenyewe kuna wanaoamini mapinduzi ni haramu na hutawasikia hata wakitamka. Kundi hili linaamini katika Zanzibar ya nyakati hizo na lina 'theory' kwamba mapinduzi yameletwa na Tanganyika

Kuna Mapinduzi daima, wanaamini katika mapinduzi , hawa wapo tayari kwa Serikali moja na ndio hasa wanaotaka Serikali mbili kwa hofu kwamba Usultan utarudi. Unamkumbuka Mbunge Kassim alisema nini Bungeni? Serikali moja haiwezekani! na kwangu mimi ni wazo baya sana kuliko kuunja Muungano
Nguruvi3 ni kweli usemayo, Watu Waunguja wanaupenda muungano kuliko watu wa Pemba.
Ikubaliwe kura ya maoni wanaotaka muungano au hawautaki, kama wameshinda wenye kuukataa njia nyeupe, Kisiwa cha Unguja kama watataka kuendelea na muungano kuwe sasa na makubaliano mapya, ya serikali moja au tatu.
Na hivi gharama za kuihudumia Zanzibar na gharama za kulinda mipaka ya baharini ipi gharama kubwa?? Nguruvi3 , Brother Pascal Mayalla
 
Back
Top Bottom