Dark wealth, dark path, is the only way to rich

Dark wealth, dark path, is the only way to rich

Tafuta taratibu utapata, njia ya giza ina utajiri lakini umejaa mateso, mahangaiko na taabu tupu.

Nje utaonekana kama una nuru lakini moyoni kunawaka moto.

Wazazi/walezi wako hawakuwa wajinga kuacha kukutoa kafara ili wawe matajiri.
Kuna kipindi kuna mtaalamu fulani alikuja kutoka bush akaja town kufanya mambo, basi akafanya mambo yake akawa anataka kumaliza jamaa mmoja akamfuata tukiwa pamoja na mimi nikasikia akamwambia anataka kua tajiri kwa namna yoyote sijui walifanya nini ila ulipita mwaka mmoja tu jamaa akawa tajiri kweli ila utajiri wa hivi ni mbaya kuna kitu unaambiwa ufanye km kutekeleza damu yako iwe inaishi kwa mateso sehemu yaan unatia mimba kisha mtoto humuangalii tangu akiwa mtoto ukimrudia tu utajiri unayeyuka na masharti mengine magumu kuna vitu jamaa alikua anavifanya kisa tu apate utajiri na vyote ni giza tupu
 

Kijana soma Biblia​

Kumbu Kumbu la Torati 8:18​


Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
We naye elimu yako ya kuunga unga haijakusaidia..embu soma vizur huo mstari wako .."akupaye nguvu"
Mtu anayekupa nguvu ndio mwenye milki za utajiri na mali za dunia ?
 
Kijana Soma Biblia....! Utajiri wa Mungu ni Utajiri wa amani na furaha

FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA.

Shalom Taifa la Mungu....

Kilichonifanya niandike hii mada ni kisa hiki....

Siku moja nilikuwa soko fulani maarufu. Nikaingia dukani kwa mfanyabiashara mmoja nikanunua vitu....tukapiga stori mbili tatu akaniambia..." hizi hela na utajiri ni vya shetani kwani hata biblia inaonyesha sehemu ambayo shetani alimwambia Yesu " nisujudie nikupe utajiri "....Mathayo 4:8-9.

Mimi nikamjibu biblia Takatifu inasema FEDHA na dhahabu ni MALI YA BWANA. Hagai 2:8.

Nikamwambia tena biblia Takatifu inasema Ulimwengu na vyote viujazavyo ni MALI YA BWANA. Zaburi 24:1-2;
1 Kor 10:26.

Ikisemwa ni Mali ya Bwana....maana yake mmiliki halali wa fedha na dhahabu ( utajiri) ni Bwana/ Mungu ( na warithi wake)......

Sasa toka wakati huo nikapata maswali mengi sana...baadhi ni haya...

1. Biblia inatuambia Mungu aliumba mbingu na nchi. Mwanzo 1:1....Je, inawezekanaje huyo aliyeumba mbingu na dunia ASHINDWE kuwapa aliowaumba utajiri? .....

Nikapata neno hili...Kumb 8:18...inasema UTAMKUMBUKA BWANA MUNGU WAKO MAANA NDIYE AKUPAYE NGUVU ZA KUPATA UTAJIRI. Kwahiyo nikajua sababu mojawapo ya umasikini ni KUMSAHAU MUNGU.

2. Najua kuwa shetani hajaumba kitu. Wala hamiliki chochote. Tena biblia inasema yeye ni malaika aliyeasi akafukuzwa mbinguni.( Isaya 14:12-14.)
....sasa anatoa wapi mali za kuwapa watu wanaomwabudu?

Nikapata neno hili
SHETANI NI MWIZI ..
Yohana 10:10
Tena SHETANI NI MUONGO na ni baba wa uongo na asili yake ni uongo. Yohana 8:44

**Hivi ulishawahi kukutana na MWANAUME maeneo ya stendi ya basi anaonekana amechoka kwa ulevi halafu amebeba HERENI za GOLD kama gramu 3@ halafu anakuambia nipe elfu 30 nikuuzie? Ukimuuliza za nani anakujibu.."ZANGU".....

*Utajiuliza wewe mwanaume hereni za kike zako?-uongo

*Utajiuliza mbona huyu mtu haonekani ana uwezo wa kumiliki duka la sonara? Mbona anauza mkononi tena pair moja?--mwizi

*Utajiuliza mbona thamani ya hizi hereni; bei yake na mazingira anayouzia yana
walakini ?- utapata jibu kwamba huyu ni mwizi ama hizi hereni sio gold anataka Kunitapeli

Sasa huyo ndio shetani alivyo. Hajaumba kitu na wote tunajua hilo...hamiliki kitu wote tunajua; lakini anaaminisha wengine kwamba atawapa UTAJIRI KWA NJIA RAHISI......MUONGO; MWIZI; TAPELI....

**Asiye mmiliki wa kitu hawezi kukupa kitu. Kama sina nguo natembea uchi....maana yake hata nguo ya kukugawia wewe sina pia....."U CAN'T GIVE WHAT YOU DON'T HAVE "

Kama wote tunajua shetani hana mali lakini anagawa mali basi tuwe na UHAKIKA kwamba AMEIBA MAHALI...sababu yeye ni MWIZI...na kwa sababu sio chake kihalali anagawa kihasara hasara bila kufuata utaratibu wa mwenye mali....nia yake ni KUKUTAPELI....

Biblia inatuambia nia ya mwizi ni kuiba ; kuua na kuharibu;Yohana 10:10.

Kwa hiyo ukienda kwa shetani kwa sababu yoyote ile iwayo..... nia yake ya ndani ni KUKUIBIA, KUKUHARIBIA na KUKUUA hata kama kwa nje unajiona unapata mali na cheo.....huo ndio utapeli wa shetani.

Tapeli ni mwizi anayejificha kwenye Sura nzuri isiyoonyesha nia mbaya ya ndani kwa urahisi....Ukifanya kazi/ biashara naye mwanzoni unaeza ukaona mafanikio; ukamuamini, lakini mwishoni LAZIMA akulize vibaya.

**Biblia inatuamuru KUMWABUDU MUNGU PEKE YAKE.....Mathayo 4:10,
Kutoka 3,5; kumbukumbu 5:7,9a.

**Tena biblia inatukataza kuwaendea WAGANGA/ MAKUHANI WA SHETANI ili kufanya ibada kwa shetani kwa sababu yoyote ile iwayo.
Walawi 19:31, Kumb 18:10-12.

**Ila siku hizi imekuwa kawaida kabisa kuona MATANGAZO ya UGANGA yakisomeka.....njoo kwa MGANGA XX upate...
-pete ya utajiri/ bahati
-pesa za majini
-mafanikio kazini
-zindiko la kuvuta wateja kwenye biashara.....

***NA KWA SABABU HIYO.....
watu wengi hata WAKRISTO wanaamini Kuwa HUWEZI KUTAJIRIKA BILA KUABUDU SHETANI....

***Ndio maana imekuwa shida- mtu akifanikiwa sana katika jambo lake anahisiwa amejiunga na waabudu shetani...

***Tena imekuwa shida zaidi kwamba watu wengi hata WAKRISTO wanaabudu shetani kwa namna mbali mbali ili tu wapate mali na vyeo.

***Hivi kweli Mungu anaweza kukuumba wewe na ulimwengu wote ashindwe kukupa mali ambazo ni yeye pia kaziumba?

***Hivi kweli ni akili gani inayotumika ya kwenda kuomba mali kwa asiye na mali yoyote ile?

**Ama hatuamini lile neno linalosema kwamba sisi ni wana wa Mungu (kama Yesu) na ni warithi pamoja naye? Rumi 8:16-17. Maana yake sisi ni wamiliki / warithi halali wa mali za Mungu.

Ama tuna mashaka na uwezo wa Yesu wa kutupatia mahitaji yetu katika huo utajiri alionao?
Hebu soma hapa uone:Wafilipi 4:19.

**Hii tabia ya Wakristo kusema kwamba kila mafanikio ni ya kishetani na au kwenda kuomba mali kwa shetani ....NI TANGAZO KWAMBA YESU HAWEZI KUTAJIRISHA WAKRISTO....kwa hiyo tunamdhalilisha Yesu na nguvu zake.

**Tunawahalalishia wengine waendelee kuabudu miungu mingine inayoweza kuwapa mahitaji.

Yaani sisi Wakristo ndio tunakuwa wapotoshaji wakubwa wa imani ya kikristo na uweza wa Mungu.

Tuyachunge sana maneno yetu. Kwa Kuwa hatujui kwa hakika SIRI za mafanikio ya mtu ni vizuri KUNYAMAZA.

Zaidi sana TUSIFUNGE UWEZA WA MUNGU KWENYE MIPAKA YA AKILI ZETU. Maana hakuna neno gumu lolote asiloliweza. Kwa Mungu yote yanawezekana.

Mungu atubariki; TUBADILISHE MTAZAMO wetu juu ya Mungu na uweza wake.
Kisha The Devil akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia."

Akamfukuza..ila ajabu ni kwamba hakumpinga kauli yake kwamba mali na utajiri ni vya kwake.
 
Jipige kifua, bisha sana, toka jasho sana, kua atheist, kua mlokole hadi ukiomba unapiga kichwa kwenye ukuta, vyovyote ila ukweli ndio huo

To be rich, ufalme wa giza, ndio njia pekee ya kuweza kupata utajiri na mali za dunia hii na kama wasemavyo, money is power.

Kama uongo waulize wanaojaza crusade za maombi kisingizio cha mkesha, wafanyabiashara wakubwa, wote hao dark kingdom ndio back up yao.

And am ready to ascend to that kingdom.

"Kisha The Devil akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia."

Akamfukuza..ila ajabu ni kwamba hakumpinga kauli yake kwamba mali na utajiri ni vya kwake.
wewe ndio ibilisi mwenyewe, shindwa pepo
 
Unadanganya tu watu, tafuta mtaji, fungua biashara inayoeleweka, na unayoielewa, isimamie pata hela.
Hela wekeza kwenye madili haya. The more the money , the more the profit.
Hamna cha shetani, njia pekee ya utajirii ni more transactions.
Tupo sisi tulianza na laki nne mtaji na return ya 210,000 kwa mwezi biashara uchwara kabisa za mitaani.
Sahvi tunapigania deals kubwa zaidi. One deal profit kubwa tu. Unasema uchawi. Fck you.
Acheni kuandika ujinga humu. Mitandaoni.
 
Tafuta taratibu utapata, njia ya giza ina utajiri lakini umejaa mateso, mahangaiko na taabu tupu.

Nje utaonekana kama una nuru lakini moyoni kunawaka moto.

Wazazi/walezi wako hawakuwa wajinga kuacha kukutoa kafara ili wawe matajiri.
Shida iko Hivi! Ndo maana wengi wanaenda shortcut wakidhani watafanikiwa maisha yao yote. Utajiri wa shetani una gharama za makafara ya kuua na utajiri ule huwa ni wa muda maana ni Kiini macho.

Wengi wanakimbia kumwomba Mungu utajiri sababu Utajiri wa Mungu sio wa kila mtu anaweza. Mungu ili aweze kukupa utajiri Lazima akupitishe kwenye Hekima zake( Ili dhahabu ing'ae lazima ipite kwenye Moto). Kwahiyo Wengi hiyo hawataki.
Mungu hataki akikupa utajiri uanze kuutapanya mwisho wa siku huna hata mia. Mungu anataka akikupa utajiri unakua ni Baraka kwa vizazi vyako vyote.

Watu wanaenda shortcut sababu wa ukipitishwa kwenye hekima za Mungu lazima ujitambue kua wewe ni nani na ni wapi unakoelekea/Maono yake.

Yeye shetani anagawa tu hata sahizi ukiitaji unaibuka tajiri. Utajiri wa Mungu Una mchakato sana.Ila ukibarikiwa unakua ni utajiri wa vizazi na vizazi.
 
Kuna kipindi kuna mtaalamu fulani alikuja kutoka bush akaja town kufanya mambo, basi akafanya mambo yake akawa anataka kumaliza jamaa mmoja akamfuata akamwambia anataka kua tajiri kwa namna yoyote sijui walifanya nini ila ulipita mwaka mmoja tu jamaa akawa tajiri kweli
Utajiri kwa njia za giza ni kweli unapatikana, lakini hauna utulivu wala furaha ya kutosha ndani yake.

Mwanzoni utafurahia, lakini Shetani akianza kukaza nati, hakika hakuna rangi utaacha kuiona.
 
Shida iko Hivi! Ndo maana wengi wanaenda shortcut wakidhani watafanikiwa maisha yao yote. Utajiri wa shetani una gharama za makafara ya kuua na utajiri ule huwa ni wa muda maana ni Kiini macho.

Wengi wanakimbia kumwomba Mungu utajiri sababu Utajiri wa Mungu sio wa kila mtu anaweza. Mungu ili aweze kukupa utajiri Lazima akupitishe kwenye Hekima zake( Ili dhahabu ing'ae lazima ipite kwenye Moto). Kwahiyo Wengi hiyo hawataki.
Mungu hataki akikupa utajiri uanze kuutapanya mwisho wa siku huna hata mia. Mungu anataka akikupa utajiri unakua ni Baraka kwa vizazi vyako vyote.

Watu wanaenda shortcut sababu wa ukipitishwa kwenye hekima za Mungu lazima ujitambue kua wewe ni nani na ni wapi unakoelekea/Maono yake.

Yeye shetani anagawa tu hata sahizi ukiitaji unaibuka tajiri. Utajiri wa Mungu Una mchakato sana.Ila ukibarikiwa unakua ni utajiri wa vizazi na vizazi.
Umenifungua macho
 
Kisha The Devil akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia."

Akamfukuza..ila ajabu ni kwamba hakumpinga kauli yake kwamba mali na utajiri ni vya kwake.
Yesu ni mwana wa Mungu! Alikua anajua fika kuwa shetani ana mjaribu maana hana huwezo huo wa kumpa utajiri.
Utajiri wa shetani ni Kiini macho huwa ni utajiri wa Muda fulani tu.
 
Unadanganya tu watu, tafuta mtaji, fungua biashara inayoeleweka, na unayoielewa, isimamie pata hela.
Hela wekeza kwenye madili haya. The more the money , the more the profit.
Hamna cha shetani, njia pekee ya utajirii ni more transactions.
Tupo sisi tulianza na laki nne mtaji na return ya 210,000 kwa mwezi biashara uchwara kabisa za mitaani.
Sahvi tunapigania deals kubwa zaidi. One deal profit kubwa tu. Unasema uchawi. Fck you.
Acheni kuandika ujinga humu. Mitandaoni.
Wewe bado fukara unatukana ovyo mitandaoni unatukana usiowajua ..unautajir gani wewe fukara bado una muda wa kuja kutukana usiowajua humu , wewe endelea na biashara za walalahoi hizo unapata vimilioni ukitukana watu ndio unajiona tajiri fala wewe huna hela wewe nahujui lolote
 
Aiseeh.. hatari sana! Kwahiyo mambi ya mwilini tukampigie magoti shetani???

Mungu hayuko hivo!
Unaujua utajiri?🤔
Achana na pesa za kubadilisha mboga hizo utapata ila kua tajiri sahau
Mungu atakupa utajiri wa rohoni na ghala lako halitokaukiwa chakula wala maji.

Luka 16:13, Yesu alisema juu ya "ukwasi" (neno la Kiaramu kwa "utajiri"): "Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana, ama atamchukia huyu na kumpenda huyu, ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali."
 
Yesu ni mwana wa Mungu! Alikua anajua fika kuwa shetani ana mjaribu maana hana huwezo huo wa kumpa utajiri.
Utajiri wa shetani ni Kiini macho huwa ni utajiri wa Muda fulani tu.
Kisha The Devil akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia."

Akamfukuza..ila ajabu ni kwamba hakumpinga kauli yake kwamba mali na utajiri ni vya kwake.
 
Kuna kipindi kuna mtaalamu fulani alikuja kutoka bush akaja town kufanya mambo, basi akafanya mambo yake akawa anataka kumaliza jamaa mmoja akamfuata tukiwa pamoja na mimi nikasikia akamwambia anataka kua tajiri kwa namna yoyote sijui walifanya nini ila ulipita mwaka mmoja tu jamaa akawa tajiri kweli ila utajiri wa hivi ni mbaya kuna kitu unaambiwa ufanye km kutekeleza damu yako iwe inaishi kwa mateso sehemu yaan unatia mimba kisha mtoto humuangalii tangu akiwa mtoto ukimrudia tu utajiri unayeyuka na masharti mengine magumu kuna vitu jamaa alikua anavifanya kisa tu apate utajiri na vyote ni giza tupu
Ndo maana tunamwambia jamaa hapo utajiri wa shetani ni kiini Macho wenyewe hao waliomfanyia huo utajiri hawautaki hata ishi yao sio ya kufurahia.
Utajiri huo ukiyeyuka kama hutasikia jamaa Kafa au kawa kichaa nimekaa pale. Asipojisalimisha kwa Yesu ndo habari yake kwisha
 
Back
Top Bottom