DART inasuasua, tatizo linaanzia serikalini, Ubia wa WORLD BANK na Wachina uangaliwe

DART inasuasua, tatizo linaanzia serikalini, Ubia wa WORLD BANK na Wachina uangaliwe

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
1741247185216.png

Nimemsikia Waziri wa Ujenzi, Abdalla Ulega akigombana na Makandarasi wa kichina wanaotekeleza miradi kadhaa ya DART(Dar es salaam Rapid Bus Trasnport), inayohusu ujenzi wa barabara za mwendo kasi wa mavbasi jijini Dar es salaam.
Bahati mbaya kwamba waziri Ulega ameyarithi matatizo yaliyokuwepo nyuma.
Waziri aliyemtangulia alisaini miradi mingi ya DART jijini, bila kuwa na strategic execution plan.

Miradi hiyo kama ifuatavyo:
-Airport-KAMATA/JAMHURI RD
-Bibi Titi rd
-Azikiwe rd
-Alihassan Mwinyi Rd-Morocco
-Morocco-Mwenge
-Ubungo-Mwenge
-Kimara -Mwenge
-Mwenge-Tegeta
-Tegeta-Boko

Hiyo ni miradi tisa(9), na yote inafanyika kwa wakati mmoja.
Hili kwa jiji la Dar es salaam inashangaza , ukifikiria msongamano wa magari na ufinyu wa njia za mchepuko(Diversions)
Kulikuwa na ulazima gani kuifanya miradi hii kwa pamoja,.
Hilo anaweza kujibu Waziri Mbarawa, inaelekeea kuna kitu nyuma ya pazia hapa.
Halafu utekelezaji wa miradi ya miji yote hufanyika kwa kiwango kikubwa usiku.
Sasa hawa wenzetu wa kampuni za kichina, hawafanyi kazi mchana wala usiku.

Kwenye picha ni Bibi Titi rd, wafanyakazi hapo wanabarizi tu, hakuna kinachoendelea

Hapa somo lazima liwepo.
Mbaya zaidi miradi karibu yote ya WORLD BANK ni wachina wanapewa.
Wachina wanajulikana kwa kuhonga ili kupata miradi, na WORLD BANK nao si malaika, tunajua wako corrupt.
Serikali iwasikilize wadau wake.
 
Kumbe pesa ni ya World Bank, lakini ukisoma Habari wachina wanasema hiyo pesa wametoa wao. Kumbe waongo eh
WORLD BANK na wachina wana ubia usio na uwazi.
Serikali yetu ni kama imewekwa mtu kati, na wachina wanafanya wapendavyo.
Hivyo nilimhurumia waziri Ulega alipong'aka, lakini sijui kama anna la zaidi.
 
wachina bwana wanaanza kujenga barabara saa mbili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni wanatoka hadi kesho tena, Jomamosi/Jumapili na sikukuu wanashinda nyumbani. Na si ajabu kwa jua la Dar lilivyo kali nao wanatafuta kivuli cha kujifunika mchana
 
eti Barabara ya Kimara bado ina uafadhali, ila Mwendokasi Karume ishapasuka
Ukienda Mbagala ndo usiseme
 
Mradi unaendeshwa kiutapeli
Kwa kifupi wtz wote tushapigwa d la tk hapo

Ova
 
Wachina wanajulikana kwa kuhonga ili kupata miradi
Ulishawahi kupata tender ya mradi wowote wa serikali?

Kuanzia halmashauri mpaka serikali kuu ili wakupe lazima engineers au watu wa procurement wa serikalini kuna percent wataitaka kutoka kwako

Heading uliandika vizuri sana kwamba "tatizo linaanzia serikalini" hapo mwishoni ukaja kujichanganya
 
Mtikila RIP aliwahi kusema Apedomia inatusumbua! We still apes brothers
 
kipindi hiki cha jua kali ndio muda mzuri wa kupiga kazi..lakini wao wamechimba mashimo tu barabarani na mvua zinazokuja sijui patakuwa na hali gani.!
 


Ulishawahi kupata tender ya mradi wowote wa serikali?

Kuanzia halmashauri mpaka serikali kuu ili wakupe lazima engineers au watu wa procurement wa serikalini kuna percent wataitaka kutoka kwako

Heading uliandika vizuri sana kwamba "tatizo linaanzia serikalini" hapo mwishoni ukaja kujichanganya
Paragraph ya 2 , imenisikitisha sn
 
Mmetifuatifua Barabara kila mahala na kuleta mifoleni isiyo na msingi barabarani huko halafu leo mnakuja na ngonjera sizizoelewaka.

Tulipaswa kujenga moja na kumaliza then tunaamiw nyingine.

Ile ya Tazara to Airport ni kipande kifupi sana ambacho kinaweza kufanyika week moja, hata hicho cha ubungo mawasiliano to mwenye nacho ni week moja tu unamaliza.

Kila siku tunawaambia CCM boresheni mifumo ya Elimu na muwajengee watu wenu uwezo ili hizi kazi wazifanye wenyewe MNALETA SIASA SIASA.
Ukiwa na engineers wa highways, Civil, structural na Mechanical wenye uwezo na competency ukawapa uwezo na vifaa hizi kazi zingefanywa na wakandarasi wa ndani Kwa bei nafuu saana.

Tunawaambia pia muanze haraka uchimbaji wa IRON ORE pale Liganga na Mchuchuma ili tuzarishe chuma chetu wenyewe na kupunguza gharama za kuimport chuma, gharama za haya maujenzi zingeenda chini sana na tungekuwa tunayafanya wenyewe kila kukicha.

Ili uweze kujenga miundo mbinu Kwa haraka haraka na Taifa likakimbia kwenye uwanja huo unapaswa kuwa na watu wako mwenyewe wenye uwezo wakuyafanya hayo na mitambo ( hapo tunazungumzia enough skilled workforce) au huwa na hela za kutosha kupitia resources zako ulete 1st class construction companies zitakazokujengea kwa time frame ndogo na quality kubwa ( GCC wanatumia hii style).

Ni ngumu Sana jambo lolote chini ya CCM kufanikiwa maana wenyewe wanachowaza ni chama kuendelea kubaki madarakani na watu waendelee kuwa wajinga.
 
Ukiachana ua suala Mkandarasi - Wachina hao upande mwingine uko hivi:
1. Kuhusu 'Bei' halisi ya mradi
2. Gharama kiuchumi zitokanazo na kuchelewesha mradi

Kwa hiyo 'twaliwa kotekote' ingawa hapo namba moja inasemekana 'mgao' lazima huwepo. Kama ndo hali halisi kwenye miradi, SHIDA NI KUBWA MNO!! Kihivyo ni 'rushwa'. Inatia huzuni! Nani anajali haya ukiondoa mimi na wewe utakaekereka na kukumbushwa hayo kama ni kweli?
 
Sijausoma uzi kabisa zaidi ya heading BUT ni mwehu, mwendawazimu na mtu ambaye hana akili kabisa ndio anaweza kuelewa why mradi wa UDART unakufa. Sijausoma uzi cause jambo hili la mwendo kasi linaudhi sana. Wateja wapo wa kutosha kabisa, biashara haina ushindani, mamlaka za serikali hazikusumbui halafu bado una fail? Hata kama huna UBONGO kabisa kichwani bado huwezi kushindwa kuendesha biashara ile, kukosa uzalendo na kutoitazama kesho ya Tanzania ndio kunaumiza haya mambo
 
View attachment 3260970
Nimemsikia Waziri wa Ujenzi, Abdalla Ulega akigombana na Makandarasi wa kichina wanaotekeleza miradi kadhaa ya DART(Dar es salaam Rapid Trasport), inayohusu ujenzi wa barabara za mwendo kasi wa mavbasi jijini Dar es salaam.
Bahati mbaya kwamba waziri Ulega ameyarithi matatizo yaliyokuwepo nyuma.
Waziri aliyemtangulia alisaini miradi mingi ya DART jijini, bila kuwa na strategic execution plan.

Miradi hiyo kama ifuatavyo:
-Airport-KAMATA/JAMHURI RD
-Bibi Titi rd
-Azikiwe rd
-Alihassan Mwinyi Rd-Morocco
-Morocco-Mwenge
-Ubungo-Mwenge
-Kimara -Mwenge
-Mwenge-Tegeta
-Tegeta-Boko

Hiyo ni miradi tisa(9), na yote inafanyika kwa wakati mmoja.
Hili kwa jiji la Dar es salaam inashangaza , ukifikiria msongamano wa magari na ufinyu wa njia za mchepuko(Diversions)
Kulikuwa na ulazima gani kuifanya miradi hii kwa pamoja,.
Hilo anaweza kujibu Waziri Mbarawa, inaelekeea kuna kitu nyuma ya pazia hapa.
Halafu utekelezaji wa miradi ya miji yote hufanyika kwa kiwango kikubwa usiku.
Sasa hawa wenzetu wa kampuni za kichina, hawafanyi kazi mchana wala usiku.

Kwenye picha ni Bibi Titi rd, wafanyakazi hapo wanabarizi tu, hakuna kinachoendelea

Hapa somo lazima liwepo.
Mbaya zaidi miradi karibu yote ya WORLD BANK ni wachina wanapewa.
Wachina wanajulikana kwa kuhonga ili kupata miradi, na WORLD BANK nao si malaika, tunajua wako corrupt.
Serikali iwasikilize wadau wake.
Sasa kama wanachukuliwa kwenda kwenye mikutano ya chama, mnataka wajenge saa ngapi???
 

Attachments

  • 20250306_140427.jpg
    20250306_140427.jpg
    103.7 KB · Views: 1
Back
Top Bottom