Dassault Rafale: Ndege ya Jeshi la Anga la Ufaransa

Dassault Rafale: Ndege ya Jeshi la Anga la Ufaransa

Mwl.RCT

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2013
Posts
14,624
Reaction score
20,666
1691304787344.gif

Dassault Rafale
ni ndege ya kivita ya Ufaransa yenye uwezo wa kufanya kazi katika anga, ardhi, na baharini. Iliundwa na kampuni ya Dassault Aviation na ilianza kutumika mnamo mwaka 1986. Ni ndege ya kwanza ya Ufaransa ya kizazi kipya na ina sifa kubwa kwa utendaji wake.

Ndege hii ina silaha za kisasa, kama makombora, mabomu, na mizinga. Ina mfumo wa elektroniki wa juu, ikiwa ni pamoja na radar na mifumo ya kudhibiti elektroniki. Inaweza kugundua na kushambulia malengo ya adui kwa haraka na ufanisi. Pia ina mfumo wa kujilinda dhidi ya silaha za adui.

1691305409791.gif

Dassault Rafale inalinda usalama wa Ufaransa katika mazingira mbalimbali. Inafanya ulinzi wa anga, upelelezi, na operesheni za kimataifa. Ina uwezo mkubwa wa mashambulizi na ulinzi na inaweza kukabiliana na adui yeyote.

Ndege hii pia imetambuliwa kimataifa na imeuzwa kwa nchi nyingine duniani. Imethibitisha uwezo wake katika vita na imekuwa chombo muhimu katika usalama wa kimataifa.

==

F-35 inaondoa maana ukiondoa stealth. Kila kitu kwenye fighter hiyo kinategemea stealth capabilities. Ina weapons integration ndogo kuliko Rafale sababu sio ndege ya kufanya kazi kubwa za mara kwa mara bali kazi ngumu na za uchache.
Ina datalink & communication nzuri na electronic warfare nzuri, ina variant nzuri zaidi kwa aircraft carrier.

Rafale naiona nzuri zaidi ya Typhoon.
1. Rafale ina carrier based variant ambayo India wamenunua mwaka jana or juzi. Typhoon haina uwezo huo (moja ya sababu Ufaransa ilijitoa kwenye hiyo programu na kwenda yenyewe na Rafale)

2. Rafale ni system ya nchi moja, unahitaji kuwa na mahusiano mazuri na Ufaransa tu ili uinunue. Typhoon mpaka Ujerumani, Uingereza, Italy na Spain wakubali maana consortium inawahusu wote waliichangia. Kununua silaha ni geopolitics nyingi na kuna sintofahamu kubwa mbelen, Iran walinunua F-14 Tomcats hawapewi support tangu mapinduzi ya Shah, Ukraine wana Soviet weapons nyingi wanapata shida components ziko Russia, Russia wana melivita ambazo ziliundwa shipyards za Ukraine na wana powerplants za helicopter walikuwa wanachukua components Ukraine. Kuhusisha silaha yako kwa nchi nyingi ni hatari zaidi kuliko nchi moja.

3. Rafale naona ina performance nzuri na overall capabilities nzuri zaidi ingawa zinashindana vikali na Typhoon. Kwenye tender Rafale Iiko more likely kushinda kama vitu vingine viko constant.
Tatizo lake ni bei yake kubwa sababu mgawanyo wa cost of production ni kwa Ufaransa tu, ila Typhoon waligawana nchi nne. Hata MBT ya Ufaransa ile Lecrerc ni bei ghali sana kuliko vifaru vyote vya NATO ila haimaanishi ndio kina uwezo mkubwa kuzidi vingine.
 
Drone ambazo waliiba tekmolojia kwa Muamerika baada ya kutungua ile drone iliyo kua ina fanya Surveillance Iran..
Nilijua wame kuja na kipya kumbe wanasubiri wamagharibi wa buni wao wafanye kuiba teknolojia kama michina
Nyie mliiga kipi ambacho mmekitengeneza kwenu zaidi ya kuagiza kila siku hadi stik za meno kiazi wewe
 

Dassault Rafale
ni ndege ya kivita ya Ufaransa yenye uwezo wa kufanya kazi katika anga, ardhi, na baharini. Iliundwa na kampuni ya Dassault Aviation na ilianza kutumika mnamo mwaka 1986. Ni ndege ya kwanza ya Ufaransa ya kizazi kipya na ina sifa kubwa kwa utendaji wake.

Ndege hii ina silaha za kisasa, kama makombora, mabomu, na mizinga. Ina mfumo wa elektroniki wa juu, ikiwa ni pamoja na radar na mifumo ya kudhibiti elektroniki. Inaweza kugundua na kushambulia malengo ya adui kwa haraka na ufanisi. Pia ina mfumo wa kujilinda dhidi ya silaha za adui.


Dassault Rafale inalinda usalama wa Ufaransa katika mazingira mbalimbali. Inafanya ulinzi wa anga, upelelezi, na operesheni za kimataifa. Ina uwezo mkubwa wa mashambulizi na ulinzi na inaweza kukabiliana na adui yeyote.

Ndege hii pia imetambuliwa kimataifa na imeuzwa kwa nchi nyingine duniani. Imethibitisha uwezo wake katika vita na imekuwa chombo muhimu katika usalama wa kimataifa.
Hii ni bora kuliko F-35 ukitoa 'stealth' ?....au ni kama tu Eurofighter typhoon ?

T14 Armata
 
Ndo maana mimi naikubali iran yenyewe inawekeza kwenye drone tu
Sababu Iran haina uwezo wa kuwekeza kwenye 4th generation fighters ndio maana mpaka leo inatumia F-14 Tomcats kutoka Marekani.

Iran wako kwenye development ya 3rd generation fighter inaitwa Qaher na wako na development ya advanced trainer ya Kowsar. Hizi mbili ni copy za F-5 za Marekani ambazo Iran iliuziwa miaka ya 60 kama sio 70 na bado inazitumia.
Ni vigumu nchi kuanza kwenye generation fulani wakati haina hata na uzoefu na generations mbili zilizopita.

Iran ingepata msaada wa Russia kama ingenunua Su-35 ila mpaka sasa hawajatangaza deal kusainiwa. Na kinachochelewesha ni Iran kutaka technology transfer/licence production ambayo hii lazima iambatane na baadhi ya assembly ya hizo kufanyika Iran. Assembling ingeweza kukubalika sababu hata India anafanya assembly ya Su-30MKI kwake ila tech transfer ni ngumu, na inategemea unataka transfer kiasi gani. Labda Warusi wakijitahidi sana watoe licence production ila hakuna nchi iliwahi pewa technology ya fighter jet na Urusi, hata China haijawahi.
 
Back
Top Bottom