Dau la Miquissone lipo juu licha ya yeye kukubali

DullyJr

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2011
Posts
13,983
Reaction score
11,857
Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Msumbiji Luis Jose Miquissone amekubali kurejea Simba SC, ili kuendelea kulinda kiwango chake katika kipindi hiki ambacho ametolewa kwa mkopo akitokea kwa Mabingwa wa zamani wa Afrika Al Ahly.

“Dau la Shilingi Milioni 600 ni kubwa kwetu kulitoa kwa mchezaji mmoja na badala yake uongozi umepanga kuachana naye, licha ya yeye mwenyewe kukubali kurejea tena kwetu.”

“Kiasi hicho cha fedha ni kikubwa kama klabu hatuna uwezo wa kumpa na badala yake tutaangalia mchezaji mwingine wa aina yake tutakayemsajili katika Dirisha Dogo.”

“Tunaheshimu kiwango cha Luis. lakini ukubwa wa dau hilo la fedha limetufanya tuachane naye na kuangalia mchezaji mwingine wa aina yake tutakayemsajili.”

“Tunafahamu na kuheshimu kiwango bora cha Luis, lakini kama klabu hatupo tayari kumpatia kiasi hicho cha fedha cha Shilingi Milioni 600.” amesema Try Again

 
600M kwa Club giant wa Africa ni pesa ya nyanya
Ingekuwa ndo anakuja kwa mara ya kwanza hapo sawa ila mchezaji simba ndo wamemuuza halafu wamnunue tena kwa dau kubwa hzo hesabu za wapi sasa simba akitoa hizo million 600 itakuwa amepata faida gani kwenye Dili la miquisoni au ndio kufurahisha mashabiki lakini club inajaa madeni.
 
Lobi wanzuki naye mlishindwa kumlipa 400m, kwa hiyo uwezo wa simba ni hawa akina joji mpole wa 10m?
 
Hio sio sababu kama kiwango kimepanda dau lazima liongezeke refer Pogba, Lukaku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…