Dauda: VAR itawekwa kwa miundombinu ipi?

Dauda: VAR itawekwa kwa miundombinu ipi?

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Kwangu nadhani ili Tanzania tuweze kupiga hatua, VAR ni kitu cha baadaye sana. Kwanza inabidi tuwekeze kwenye kuendeleza kiwanda chetu cha michezo kabla ya masuala mengine ambayo yanaweza kufanyika baadaye sana.

Ni wazo zuri kufunga VAR lakini kwangu wazo zuri zaidi kwa sasa ni kuwekeza kwenye miundombinu ya michezo kama nchi. Ni ngumu kwenda na vitu vyote kwa wakati mmoja, lazima kuwe na vipaumbele kwenye uwekezaji.

Tutengeneze kwanza mifumo ya kuendeleza soka la vijana, kwa maana ya kuwa na ‘proper academies’ na kupata wataam waliobobea kwenye eneo hilo sio kuwa na vituo vya kulelea watoto.

Ni viwanja vingapi Tanzania vina miundombinu rafiki ya kufungwa teknolojia ya VAR? Kama timu bado zinacheza mechi za Ligi Kuu kwenye viwanja vilivyojaa maji bado tunahitaji VAR kuwa kipaumbele kwa sasa?

Mataifa ambayo yanatumia VAR tayari yamepiga hatua kubwa kwenye maeneo mengine, tukubaliane kama nchi kwamba kuna mambo mengi ya kufanya kabla ya kufikiria kutumia VAR baada ya kupata usumbufu unaotokana na makosa ya waamuzi.

My Take
Fikiria huyu ndio waziri wa fedha anayemshauri Rais masuala ya fedha na uchumi. Hawa ndio walituletea tozo bila tafiti,leo wanataka kuleta VAR bila wiwanja. Utopolo ni utopolo tu
 
Kwani Tiefuefu inafikiria habari za VAR au kuna kitu sielewi?
 
Kwani Tiefuefu inafikiria habari za VAR au kuna kitu sielewi?
Screenshot_20220207-155815_Chrome.jpg


Haya ni maamuzi baada ya Uto kupata sare
 
Mnaogopa VAR nini acha walete tutaweka hivyo hivyo ili muache michongo yenu .

Mmeanza kuping kwa kuwa mtapigwa sana maana ninyi ni wazee wa michongo

Sent from my Nokia C1 using JamiiForums mobile app
Sio kuogopa VAR. Hoja ni vipaumbele.Unajua bei ya VAR? Halafu utaweka kwenye viwanja gani? Hizo VAR ni za umma au za CCM?
 
Sio kuogopa VAR. Hoja ni vipaumbele.Unajua bei ya VAR? Halafu utaweka kwenye viwanja gani? Hizo VAR ni za umma au za CCM?
ama wabongo waibe zile computer naonaga zinachora Ile mistari ya offside wakauze bure....😃🙌

Naunga mkono hoja yako mkuu ...viwanja tu Kwa kuanzia ni tatizo .. na hakuna mpira wa miguu bila kiwanja ... Tuanzie kuweka hapa ..kwenye miundombinu.
 
Sio kuogopa VAR. Hoja ni vipaumbele.Unajua bei ya VAR? Halafu utaweka kwenye viwanja gani? Hizo VAR ni za umma au za CCM?
Mkuu mimi nadhani sio lazima tuige kama wazungu VAR wanazotumia wao. Bali kwa upande wetu tuangalie namna rahisi ya kuondoa hizi sintofahamu zinazotokea uwanjani kwa kuweka miundo mbinu rahisi. Azam ndio mrusha matangazo rasmi wa ligi kuu bara, anauwezo wa kuweka tv moja pembeni ya pitch na kwavile gari lao la matangazo lipo uwanjani kurusha mechi live ni rahisi kwa refarii kwenda kwenye tv iliyowekwa pembeni ya uwanja kuangalia tukio kwa ufasaha ili ajiridhishe. Kinachotakiwa uwanjani ni tv moja+ dish na azam+ king'amuzi cha Azam. Pia Azam waongeze camera ili tukio liwe linaweza kuhukumiwa kwa kuangalia angle mbali mbali
 
Kwangu nadhani ili Tanzania tuweze kupiga hatua, VAR ni kitu cha baadaye sana. Kwanza inabidi tuwekeze kwenye kuendeleza kiwanda chetu cha michezo kabla ya masuala mengine ambayo yanaweza kufanyika baadaye sana.

Ni wazo zuri kufunga VAR lakini kwangu wazo zuri zaidi kwa sasa ni kuwekeza kwenye miundombinu ya michezo kama nchi. Ni ngumu kwenda na vitu vyote kwa wakati mmoja, lazima kuwe na vipaumbele kwenye uwekezaji.

Tutengeneze kwanza mifumo ya kuendeleza soka la vijana, kwa maana ya kuwa na ‘proper academies’ na kupata wataam waliobobea kwenye eneo hilo sio kuwa na vituo vya kulelea watoto.

Ni viwanja vingapi Tanzania vina miundombinu rafiki ya kufungwa teknolojia ya VAR? Kama timu bado zinacheza mechi za Ligi Kuu kwenye viwanja vilivyojaa maji bado tunahitaji VAR kuwa kipaumbele kwa sasa?

Mataifa ambayo yanatumia VAR tayari yamepiga hatua kubwa kwenye maeneo mengine, tukubaliane kama nchi kwamba kuna mambo mengi ya kufanya kabla ya kufikiria kutumia VAR baada ya kupata usumbufu unaotokana na makosa ya waamuzi.

My Take
Fikiria huyu ndio waziri wa fedha anayemshauri Rais masuala ya fedha na uchumi. Hawa ndio walituletea tozo bila tafiti,leo wanataka kuleta VAR bila wiwanja. Utopolo ni utopolo tu
Screenshot_20220207-165514_Lite.jpg
 
Mnaogopa VAR nini acha walete tutaweka hivyo hivyo ili muache michongo yenu .

Mmeanza kuping kwa kuwa mtapigwa sana maana ninyi ni wazee wa michongo

Sent from my Nokia C1 using JamiiForums mobile app
Posho za marefa tu zinawashinda mtaweza kuendesha huo mfumo wa VAR?Anzeni kwanza na vitu vya msingi kama viwanja na sio kuchezea kwenye mbunga/majaruba.
 
Var bongo inaweza wekwa tatizo atakaye kaa pale kwenye hizo computer za var utakuta ni mwijaku! hapo utasema tuna var?
 
Mkuu mimi nadhani sio lazima tuige kama wazungu VAR wanazotumia wao. Bali kwa upande wetu tuangalie namna rahisi ya kuondoa hizi sintofahamu zinazotokea uwanjani kwa kuweka miundo mbinu rahisi. Azam ndio mrusha matangazo rasmi wa ligi kuu bara, anauwezo wa kuweka tv moja pembeni ya pitch na kwavile gari lao la matangazo lipo uwanjani kurusha mechi live ni rahisi kwa refarii kwenda kwenye tv iliyowekwa pembeni ya uwanja kuangalia tukio kwa ufasaha ili ajiridhishe. Kinachotakiwa uwanjani ni tv moja+ dish na azam+ king'amuzi cha Azam. Pia Azam waongeze camera ili tukio liwe linaweza kuhukumiwa kwa kuangalia angle mbali mbali
Umewaza kama mimi,AVR ni replay tu ya tukio,tuanze na zile mechi zinazorekodiwa na azam,hakuna gharama kama watu wanavyodhani zaidi ya Tv screen moja tu
 
Viwanja vibovu mfano pale manungu ukaweke VAR si vichekesho hivi

Azam mrusha matangazo habadiliki sijui uwanjani ana Camera tatu tu. Anashindwa kuweka Camera za juu tuone pitch kwa ukubwa wake kama ulaya, pia Camera za offside hakuna, replays majanga....kiufupi anakula tu pesa za ving'amuzi ila urushaji wake wa matangazo ya mpira upo local sana.
 
Viwanja vibovu mfano pale manungu ukaweke VAR si vichekesho hivi

Azam mrusha matangazo habadiliki sijui uwanjani ana Camera tatu tu. Anashindwa kuweka Camera za juu tuone pitch kwa ukubwa wake kama ulaya, pia Camera za offside hakuna, replays majanga....kiufupi anakula tu pesa za ving'amuzi ila urushaji wake wa matangazo ya mpira upo local sana.
Lkn at least replay ingepunguza utata kama penalty ya Simba vs prison, Namungo vs Yanga, offside ya jana ya Kagere
 
Kwangu nadhani ili Tanzania tuweze kupiga hatua, VAR ni kitu cha baadaye sana. Kwanza inabidi tuwekeze kwenye kuendeleza kiwanda chetu cha michezo kabla ya masuala mengine ambayo yanaweza kufanyika baadaye sana.

Ni wazo zuri kufunga VAR lakini kwangu wazo zuri zaidi kwa sasa ni kuwekeza kwenye miundombinu ya michezo kama nchi. Ni ngumu kwenda na vitu vyote kwa wakati mmoja, lazima kuwe na vipaumbele kwenye uwekezaji.

Tutengeneze kwanza mifumo ya kuendeleza soka la vijana, kwa maana ya kuwa na ‘proper academies’ na kupata wataam waliobobea kwenye eneo hilo sio kuwa na vituo vya kulelea watoto.

Ni viwanja vingapi Tanzania vina miundombinu rafiki ya kufungwa teknolojia ya VAR? Kama timu bado zinacheza mechi za Ligi Kuu kwenye viwanja vilivyojaa maji bado tunahitaji VAR kuwa kipaumbele kwa sasa?

Mataifa ambayo yanatumia VAR tayari yamepiga hatua kubwa kwenye maeneo mengine, tukubaliane kama nchi kwamba kuna mambo mengi ya kufanya kabla ya kufikiria kutumia VAR baada ya kupata usumbufu unaotokana na makosa ya waamuzi.

My Take
Fikiria huyu ndio waziri wa fedha anayemshauri Rais masuala ya fedha na uchumi. Hawa ndio walituletea tozo bila tafiti,leo wanataka kuleta VAR bila wiwanja. Utopolo ni utopolo tu
ufike kipindii watu tupanuke kiakilii VAR TZ bado sanaa!
kwa akili ya kawaida tuu na mpira wa simba na yanga huu VAR kwa michuano ipiii??
 
Back
Top Bottom