David Kampista: DR Congo imeshuka kimpira ndiyo maana wachezaji Kama Mayele na Inonga wanaitwa Timu ya Taifa

David Kampista: DR Congo imeshuka kimpira ndiyo maana wachezaji Kama Mayele na Inonga wanaitwa Timu ya Taifa

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Kipindi cha Michezo Clouds FM cha jumapili alizungumza hayo maneno akiwa Kama mchambuzi asiyekuwa na hoja Bali kaamua kuzungumza tu ili siku iende na boss wake Kusaga amlipe mwisho wa mwezi.

Maoni yangu.
David Kampista hujui chochote kuhusu mpira (football) na hujui nini kinaangaliwa kwa mchezaji mpaka anaitwa timu ya Taifa, kusema kuwa DR Congo hawana wachezaji ni dhahiri kabisa unachambua mpira lakini huna unalolijua.

Unamuona Mayele na Inonga ni wakawaida kwa kua unachambua mpira kishabiki (Simba na Yanga), katika mpira /uchambuzi wa mpira hupaswi kuleta ushabiki usiokuwa na kichwa Wala miguu.

Saivi Clouds ina wachambuzi wa hovyo sana, mmoja wapo David Kampista.

Nawasilisha hoja.
 
Hauna hoja. Kaongea ukweli.

DRC saivi ina wachezaji wa hovyo...hadi mayele na inonga kuitwa timu ya taifa.

Hii ni fact na ni kweli...kimpira.

Tusiwe waongo wala wanafki...ligi yetu bado tupo semi proo..

DRC wana historia ya kuwa na wachezaji wengi mno wanaocheza udaransa Ligue1, Sweden huko norway na hata nchi nyingine za ulaya zenye ushindani mf. Bundesliga 1,2 na hata Serie A, B, C, etc.

Mi nadhani wakongo wengi wana kasumba ya kubadili uraia..ndio maana wengi wao wanajikataa.

Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
 
Kama ni hivyo basi Senegal ndiyo watakuwa wameshuka viwango mara dufu!

Maana wamemuita kwa mara ya pili mfululizo mchezaji kama Pape Osmane Sakho ambaye hana hata uhakika wa namba kwenye timu yake ambayo kwa misimu miwili sasa inachechemea.
 
Hivi hawa wanaojiita wachambuzi wamesomea Mpira au ujanja ujanja wa kujua kuongea mwisho wa mwezi walipwe chao?
 
Back
Top Bottom