September 2017
Nairobi, Kenya
David Opati Etale azungumzia uanajeshi wake Uingereza : Dira ya wiki
Mchezaji mpira wa kandanda nchini Kenya kwa jina David Opati Etale baada ya kuona mpira wa kulipwa haulipi Kenya akaamua kuacha soka na kujiunga jeshi la Uingereza. Alichezea timu kubwa za kandanda Kenya kama Tusker FC, Kenya Commercial Bank n.k
Alijunga Jeshi hilo la Uingereza akiwa na umri wa miaka 21 baada ya kuomba nafasi ya uaskari kupitia intaneti na kukubaliwa kwa vile Kenya ni nchi mojawapo ya Jumuiya ya Madola (Commonwealth). Baada ya mafunzo ya awali ya miezi sita ktk Jeshi La Uingereza huko ulaya alipelekwa nchi za Iraq na Afghanistan kutumikia jeshi la Uingereza.
Source: KTN news Kenya
Bahati Mbaya wakati akiwa huko Afghanistan gari lao la deraya lilikanyaga bomu la kutega ardhini na kupata kilema cha kupoteza mguu mmoja hospitalini Uingereza. Kabla ya kupoteza mguu wake, juhudi kubwa zilifanywa katika hospitali za Uingereza kwa kufanyiwa operesheni 8 mpaka 12 kujaribu kuokoa mguu wake lakini madaktari baadaye walimwambia inabidi mguu ukatwe kuokoa maisha yake.
Kwa Hivi sasa David Opati Etale anafanya kazi ya kuwapa matumaini wale wote waliopitia changamoto zinazowafanya kukata tama ya maisha. Maana David Opati Etale baada ya kuona mengi katika uwanja wa vita nchini Iraq na Afghanistan na pia kupoteza mguu wake mmoja alikata tamaa ya maisha akataka kujidhuru PTSD (Post-Traumatic Stress Disorder in Military veterans).
Pia anafanya kampeni ya uelewa nchini Kenya wa jinsi ya kuwahudumia askari wote wenye matatizo ya afya ya ubongo (PTSD) baada ya kukabiliana na mambo ya kuogofya walipokuwa uwanja wa vita kama Somalia na Sudan ya Kusini.
Matatizo ya kukata tamaa ya maisha huwapata pia vijana wa kizazi kipya kutokana na mitandao ya kijamii kupitia intaneti na hivyo David Opati Etale anasisitiza vijana wapatiwe sapoti wanapoonyesha dalili za kukata tamaa ya kuishi.
Nairobi, Kenya
David Opati Etale azungumzia uanajeshi wake Uingereza : Dira ya wiki
Mchezaji mpira wa kandanda nchini Kenya kwa jina David Opati Etale baada ya kuona mpira wa kulipwa haulipi Kenya akaamua kuacha soka na kujiunga jeshi la Uingereza. Alichezea timu kubwa za kandanda Kenya kama Tusker FC, Kenya Commercial Bank n.k
Alijunga Jeshi hilo la Uingereza akiwa na umri wa miaka 21 baada ya kuomba nafasi ya uaskari kupitia intaneti na kukubaliwa kwa vile Kenya ni nchi mojawapo ya Jumuiya ya Madola (Commonwealth). Baada ya mafunzo ya awali ya miezi sita ktk Jeshi La Uingereza huko ulaya alipelekwa nchi za Iraq na Afghanistan kutumikia jeshi la Uingereza.
Source: KTN news Kenya
Bahati Mbaya wakati akiwa huko Afghanistan gari lao la deraya lilikanyaga bomu la kutega ardhini na kupata kilema cha kupoteza mguu mmoja hospitalini Uingereza. Kabla ya kupoteza mguu wake, juhudi kubwa zilifanywa katika hospitali za Uingereza kwa kufanyiwa operesheni 8 mpaka 12 kujaribu kuokoa mguu wake lakini madaktari baadaye walimwambia inabidi mguu ukatwe kuokoa maisha yake.
Kwa Hivi sasa David Opati Etale anafanya kazi ya kuwapa matumaini wale wote waliopitia changamoto zinazowafanya kukata tama ya maisha. Maana David Opati Etale baada ya kuona mengi katika uwanja wa vita nchini Iraq na Afghanistan na pia kupoteza mguu wake mmoja alikata tamaa ya maisha akataka kujidhuru PTSD (Post-Traumatic Stress Disorder in Military veterans).
Pia anafanya kampeni ya uelewa nchini Kenya wa jinsi ya kuwahudumia askari wote wenye matatizo ya afya ya ubongo (PTSD) baada ya kukabiliana na mambo ya kuogofya walipokuwa uwanja wa vita kama Somalia na Sudan ya Kusini.
Matatizo ya kukata tamaa ya maisha huwapata pia vijana wa kizazi kipya kutokana na mitandao ya kijamii kupitia intaneti na hivyo David Opati Etale anasisitiza vijana wapatiwe sapoti wanapoonyesha dalili za kukata tamaa ya kuishi.