Mdakuzi
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,294
- 6,872
Hivi kwanini una justify tweet ya davido? Unaamini hawezi kukuponda we mtanzania au?
Hukumbuki p-square walivyokuja bongo wakasema eti hawamjui diamond wala hawajawahi msikia. Wakati Obama "the world's president" alivyokuja bongo alimtaja hasheem thabit ambaye ata NBA hafanyi vizuri, just Because ya ustaarabu na kuthamini mchango wa watanzania.
Mimi sio fun wa diamond, but niko hapa kutetea utanzania, siwezi kusema its ok. Wakati najua mtu anajaribu kutudharau.
Sasa we ndugu yangu kama unajaribu kujustify na kutetea ata kwenye kudharauriwa its you (kisa tz nchi ya amani) huu ni upuuzi.
Davido na wenzake wote walilenga kupondea mshindi wa big brother from TZ. Usijustify ujinga.
Angalia insta na tweet zingine za davido, kijana always ana mdomo mchafu wa kujisikia, hana ata ustaarabu. Sijui wewe unatetea nini.
Mkuu, mbona suala la Obama & Hasheem, na P Square & Nassib ni vitu viwili tofauti, kiasi kwamba nashangaa kwanini umevitumia kwa pamoja kama vile ni vitu vinavyofanana. Kwa kuwa tupo kwenye jukwaa lenye members kama laki mbili hivi, ngoja nitumie muda mfupi kujaribu kuwekana sawa.
Suala la Obama na Hasheem, ilikuwa rahisi kwa Obama kukiri kumtambua Hasheem, kwanza anaishi kwenye nchi yake na anayoiongoza. Pili, Obama ni shabiki wa NBA na kwa Marekani karibu kila mchezaji wa NBA ni super star, isitoshe Hasheem ni mmoja wa wachezaji wawili wa kikapu aliyefanya vizuri kwenye Draft ya kuingia NBA.
Ni Tanzania tu ndio tunaomchukulia poa Hasheem, lakini kwa Marekani jamaa anapewa heshima kubwa tu, ukipata nafasi ya kuwa Marekani na ukakutana naye kwenye mijumuiko ya watu kama vile Night Clubs au kwenye viwanja vya NBA na sehemu nyingine zinazofanana nazo.
Kuhusu P Square na Nassib, ikumbukwe kwamba wakati P Square wanakuja nchini wimbo wa Number One Remix wa Nassib alioimba na Davido ulikuwa bado haujatoka, na ndio wimbo ambao kwa kiasi kikubwa ulimtangaza Nassib kwa Nigeria na Africa, hivyo wala haishangazi kusema kuwa hakuwa akimjua.
Kama unakumbuka Nassib alipata nafasi ya kuhudhuria kwenye harusi yao wakati akiwa Nigeria kwa ajili ya kurekodi video ya Number One Remix, na kwa wakati huo Nassib alikuwa akijuana zaidi na akina Iyanya na Davido pekee. Sidhani kama mchonga vinyago wa Tanzania anamjua kila mchonga vinyago wa Nigeria.
Kuhusu kufahamiana, hata Luke Shaw wa Man United alipokuwa akizungumzia na Frank Lampard wa Man City aliweka wazi kuwa hamjui Tonny Adams.
Ova