Dawa ya Kupunguza Hasira

Inabidi ajitambue mwenyewe kuwa ana hasira na aelewe kuwa ni shida kuwa nayo na hapo atajifunza kujicontrol!
 

Sasa akijifunza karate si ataua kabisa? Hauwezi kutoa hayo mafunzo hapa? Hili tatizo la hasira ni la watu wengi sana. Jinis ya kuweza kucontrol hasira haswa kwa wale ambao wana hasira za haraka haraka au huwa wepesi kuchukizwa na mambo hata madogo madogo.:twitch:
 
Duuu hiki ni kilema kinachosumbua wengi, nimesoma post zote sijaona dawa iliyotajwa, wengine wanazidisha hasira manake mtu anakwambia anahitaji katiba mpya si anataka uendelee kukasirika.

Haya aende Muhimbili sa ngapi sasa, ukimwambia nenda huko si atakasirika pia? Hakuna madaktari hapa watuambie vizuri?

Au ndo linatibiwa kwa maombi zaidi, sasa kama hapendi kuombewa ukimwambia tunakuombea si atakasirika pia??
 
Ebu mwambie avute bangi, inatuliza watu wenye hasira, try it
 
Humu kuna waganga wa kienyeji wengi sana..ati anywe au aoge maji ya baridi..really?

Hasira kila mtu anayo cha msingi ni kuwa na self-control and to know when to stop. Hakuna binadamu asiye na hasira...kama huna hasira jichunguze, huenda sio binadamu.
 
Mwambie akiwa hasira ajifungie ndani alie weee hadi hasira ziishe na pia anywe maji kama wadau wengine walivyosema.

Pili kama amekasirishwa anaweza kutafuta jambo lolote linalomfurahisha akalifanya kwa muda huo. Mfano akasikiliza miziki anayoipenda au akacheza game.

Tatu ambayo huwa mimi naifanya; mtu akinikasirisha sana huwa siongei nae kwa muda huo. Hata kama atataka kuniomba msamaha sikubali hadi hasira zangu ziishe. Mwambie ajaribu kumuepuka mtu aliyemkasirisha maana akiongea anaweza akaongea lugha chafu au anaweza akampiga na kusababisha balaa zaidi.
 
Mwenzio ana hasira hata akiona glass mbele yake anaivunjia ukutani. Hayo maji atakunywaje sasa.

Umeamka salama dearest? dawa ni kumuomba mungu tu tena ukimaanisha mambo mengine ni laana tunazorithi kutoka kwa mababu/bibi zetu na hiyo laana inaendele kizazi hadi kizazi so yanahitajika maombi ya nguvu kuivunja hiyo laana na taratibu utaona unabadilika na mwisho unakua huna hasira kabisa. Ila inachukua muda kidogo mungu hachelewi wala hawahi
 
zikimpanda akimbilie chumban fasta na sdemuw ake...
 

Mwambie dawa ya hayo yote ni kuokoka hakuna lingine hasira zote zitakwisha na atashangaa mabadiliko makubwa atakayopata.
 
Ajitahidi kuji control wenye hasira wanakuwa na maisha mafupi sana
 
Ndugu wanajamvi nahisi huwa nina matatizo ya kupatwa na hasira mara kwa mara hata tu kwa mtu akiniudhi kidogo. Tafadhalini naombeni mnipatie dawa ya kupunguza na kutoa hasira.
 
Anger is a normal, healthy emotion, but when chronic, explosive anger spirals out of control, it can have serious consequences for your relationships, your health, and your state of mind.

Kama unahitaji namna bora ya kudhibiti hasira hiyo naweza kukusaidia ila kondoa na kupunguza hasira tusubiri wadau wengine
 
Jitahidi kuchukulia kila kitu simple tu...ukiona kitu au ukisikia jambo lolote usiseme au usiulize au usifuatilie nyamazia tu, baadae ndo ufuatilie lakini ni kama tu kina umuhimu kwamba usipofuatilia kuna athari za wazi zitatokea.
 
Jaribu kufanya mazoezi na angalia vyakula unavyokula,punguza mafuta na kula mbogamboga, jaribu kupima pressure na kiwango cha mafuta kwenye damu yako(cholesterol)
 
Namna bora ya kudhibiti hasira

1. Tafuta chanzo cha hasira
Ni mambo gani yanakufanya kuwa na hasira? Ukishayajua tafuta namna ya kupata suluhisho la mambo hayo.

2.Epuka watu,maeneo, na mambo yanakufanya kupandwa na hasira
Pengine ni kwenye ushabiki wa mpira au labda ni kwenye majadiliano ya kisiasa, epuka mambo hayo.Si lazima ubishane kuhusu siasa au mpira,tafuta jambo lingine

3. Jifunze namna ya kudhibiti hisia zako
Hisia zinapaswa kuwa chini ya uwezo wako wa kuamua, si lazima kwa kuwa unahisi hasira basi ufanye mambo kwa hasira. Kwa kifupi tumia kichwa na sio fikara

4. Angalia/Tafuta namna bora za kutoa hisia za hasira
Wengi tumeshindwa hapa, si lazima ukiwa na hasira utoe matusi au maneno mabaya. Hamna haja ya kutaka kupigana au kutoa maneno ya kashfa,eleza kilichokuudhi bila kutumia hasira. '' When communicated respectfully and channeled effectively, anger can be a tremendous source of energy and inspiration for change.''

4. Jichunguze....
Jifanyie tathmini, je hasira zako zimetatua tatizo lolote? Je hasira inakufanya kuwa mtu bora mbele ya famlia yako, mke,mume na watoto.

Umeharibu urafiki mara ngapi kwa sababu ya hasira?

KIla la kheri mdau...
 
hasira iliyopitiliza ni tatizo. hata hivyo; kuna magonjwa mengi sana ya kisaikolojia ambayo mojawapo ya dalili zake ni hasira ambayo mtu anashindwa kuicontrol. kwa dalili hizo mbili tu ulizotoa sio rahisi kukuambia tatizo lake. baadhi tu ya matatizo yanayoweza kua na dalili hizo mbili ni Sonona na PTSD. ushauri ni kuwa aonane na wataalamu wa saikolojia tiba (clinical Psychologists) au Psychotherapist watamsaidia.

kwa maelezo zaidi unaweza kulike Facebook page yetu psychological support and mental health awareness
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…