dawa ya unene

dawa ya unene

Pamoja na wadau kusema wembamba sana (size 8) ni sawa tu na kuwa tukubali tu jinsi tulivyo ama wembamba ni urembo, mambo sivyo yalivyo. Binadamu kisaikolojia huwa na wakati anakuwa na udadisi juu ya jinsi watu wanavyomchukulia kimwonekano, kijamii, kifedha (angalau kwa baadhi ya nilivyotaja) n.k. Hiyo ndiyo saikolojia ya kila binadamu. Na jamii imetengeneza "urembo" na "kupendeza" kwa namna "ilivyovumishwa" hadi ikakubalika. Ni kweli kuwa majini (with some exception)/mashetani/mapepo/wachawi hudhaniwa kuwa na sura mbaya (sura mbaya ni ipi?). Waweza kukandamiza uso wako kutoka mashavuni kuelekea mbele na ukafanikiwa kumtisha mtoto mdogo hadi akalia (sura mbaya!!). Dr Remmy, Jangala na Masudi Ally (kama sijakosea jina) walishiriki katika mashindano ya sura mbaya na inakubalika kuwa wana sura mbaya (vigezo ni vipi?) Nachomaanisha hapa ni kuwa jamii imetengeneza "standards" fulani kuhusu mwonekano.

Hii inamaanisha hata dada yetu aliyeanzisha thread hii anaangukia katika vipimo hivi hivi vilivyowekwa (hata kama viko unfair). Hivyo naamini mtu mwenye umbo la wastani (inavyoaminika ni wastani) hupendeza machoni na ni rahisi kupata nguo zinazomtosha vizuri (nguo nyingi zinazotengezwa huwa na size ya kati).

USHAURI WANGU

  1. Naunga mkono ushauri uliotolewa katika post namba 18 ya Mayassa hapo juu
  2. Jitahidi kupata mavazi unaoendana nayo na kama ukiweza "shonesha" ili upate vipimo vyako. Epuka mavazi yenye mistari inayokwenda chini au yenye kitambaa laini sana. Viatu vyenye visigino virefu humfanya mwembamba aonekane mwembamba sana
  3. Usitilie maanani "sana" mpango wa kunenepa. Wakati mwingine unene huja kutokana na umri.
  4. Wembamba sana si mzuri. Hata hivyo bora kuwa mwembamba sana kuliko mnene sana.
  5. Hata usipoongezeka, jiulize marafiki zako wanaendelea kukupenda? Mumeo? Kazini? Mwanao? Comments zipo tu.
  6. Wakati mwingine tukubali kutofikia viwango fulani vya jamii kwa kuwa hatujafikia na hatutafikia. Najiuliza walemavu wa macho wanajisikiaje!!! Hawatazami mpira, Masanja mkandamizaji, Jukwaa la wakubwa etc. lakini wanajifunza kukubali ukweli.
  7. Kitendo cha kujua kompyuta kwa Afrika yetu hii, Kitendo cha kuwa JF memba kinakufanya uwe juu, HIVYO UKO JUU NOELLA (Umezaliwa wakti wa Xmas?)
Adios.
 
Salamu wote wanaJF

Mimi ni mama wa mtoto mmoja,nina tatizo la umbile langu yani ni mwembamba ninavaa size 8.kwa kweli huwa nikijiangalia hata sipendezewi na umbo langu,nimekuwa nikila ovyo ili ninenepe lakini wapi..nimekula mpaka cerelac na uji vya mtoto lakini wapi.

sasa nimesikia kuna dawa za kuongeza unene.nahitaji ushauri wenu kwa hili tafadhali.
kuna yeyote aliyewahi kunywa hizo dawa,je zina side effects gani?
au kama kuna njia mbadala naomba ushauri.hata nikivaa nguo sipendezi.
jibu lako
Kula mara tano kwa siku, yaani msosi hevi.. utaona matokeo yake. Asubuhi chai na vitumbua au chapati 2, saa tano tano pata uji wa ulezi, mchana pata ugali/wali na nyama au samaki tena ule sahani imejaa. Saa 10 piga chai maandazi, na saa 2 usiku ule wali wa kushiba. Fanya hivyo kwa miezi 3 tu utapata matokeo.
 
unene utakuja tu. Subiri ufikie miaka ya 30 huko ndio utajua maana ya kunenepa.
 
Mumeo wa kaskazini nini? Mimi nimeolewa huko kaskazini kila nikijifungua napewa mitori na mauji ya ulezi ninenepe nisiwatie aibu,nikakataa,sasa nina watoto wa3 bado portable wenyewe wananikubali sasa wanadai umbo langu zuri sionyeshi kama nimezaa. Jikubali ulivyo na kuna siku utamshukuru MUNGU kwa kukujaalia hilo umbo.
 
Pamoja na wadau kusema wembamba sana (size 8) ni sawa tu na kuwa tukubali tu jinsi tulivyo ama wembamba ni urembo, mambo sivyo yalivyo. Binadamu kisaikolojia huwa na wakati anakuwa na udadisi juu ya jinsi watu wanavyomchukulia kimwonekano, kijamii, kifedha (angalau kwa baadhi ya nilivyotaja) n.k. Hiyo ndiyo saikolojia ya kila binadamu. Na jamii imetengeneza "urembo" na "kupendeza" kwa namna "ilivyovumishwa" hadi ikakubalika. Ni kweli kuwa majini (with some exception)/mashetani/mapepo/wachawi hudhaniwa kuwa na sura mbaya (sura mbaya ni ipi?). Waweza kukandamiza uso wako kutoka mashavuni kuelekea mbele na ukafanikiwa kumtisha mtoto mdogo hadi akalia (sura mbaya!!). Dr Remmy, Jangala na Masudi Ally (kama sijakosea jina) walishiriki katika mashindano ya sura mbaya na inakubalika kuwa wana sura mbaya (vigezo ni vipi?) Nachomaanisha hapa ni kuwa jamii imetengeneza "standards" fulani kuhusu mwonekano.

Hii inamaanisha hata dada yetu aliyeanzisha thread hii anaangukia katika vipimo hivi hivi vilivyowekwa (hata kama viko unfair). Hivyo naamini mtu mwenye umbo la wastani (inavyoaminika ni wastani) hupendeza machoni na ni rahisi kupata nguo zinazomtosha vizuri (nguo nyingi zinazotengezwa huwa na size ya kati).

USHAURI WANGU

  1. Naunga mkono ushauri uliotolewa katika post namba 18 ya Mayassa hapo juu
  2. Jitahidi kupata mavazi unaoendana nayo na kama ukiweza "shonesha" ili upate vipimo vyako. Epuka mavazi yenye mistari inayokwenda chini au yenye kitambaa laini sana. Viatu vyenye visigino virefu humfanya mwembamba aonekane mwembamba sana
  3. Usitilie maanani "sana" mpango wa kunenepa. Wakati mwingine unene huja kutokana na umri.
  4. Wembamba sana si mzuri. Hata hivyo bora kuwa mwembamba sana kuliko mnene sana.
  5. Hata usipoongezeka, jiulize marafiki zako wanaendelea kukupenda? Mumeo? Kazini? Mwanao? Comments zipo tu.
  6. Wakati mwingine tukubali kutofikia viwango fulani vya jamii kwa kuwa hatujafikia na hatutafikia. Najiuliza walemavu wa macho wanajisikiaje!!! Hawatazami mpira, Masanja mkandamizaji, Jukwaa la wakubwa etc. lakini wanajifunza kukubali ukweli.
  7. Kitendo cha kujua kompyuta kwa Afrika yetu hii, Kitendo cha kuwa JF memba kinakufanya uwe juu, HIVYO UKO JUU NOELLA (Umezaliwa wakti wa Xmas?)
Adios.

3D asante sana kwa ushauri wako uliosimama
nitaachana na mawazo ya dawa
ila duh!huo ushauri wa mayassa sidhani kama nitauweza,kula sana siwezi
Ubarikiwe
BTW yes nimezaliwa siku ya xmas
 
Mumeo wa kaskazini nini? Mimi nimeolewa huko kaskazini kila nikijifungua napewa mitori na mauji ya ulezi ninenepe nisiwatie aibu,nikakataa,sasa nina watoto wa3 bado portable wenyewe wananikubali sasa wanadai umbo langu zuri sionyeshi kama nimezaa. Jikubali ulivyo na kuna siku utamshukuru MUNGU kwa kukujaalia hilo umbo.

Haswaa Ennie umepatia
ila cha kushangaza alikuwa anapenda wembamba, sasa gafla anasema mi mwembamba sana
hiyo mitori ndo sikuila kabisa nilikataa
 
3D asante sana kwa ushauri wako uliosimama
nitaachana na mawazo ya dawa
ila duh!huo ushauri wa mayassa sidhani kama nitauweza,kula sana siwezi
Ubarikiwe
BTW yes nimezaliwa siku ya xmas

Kama kula sana huwezi basi sahau unene. Manake unene huletwa na njia mbili either genetics au kula sana.
 
Unene haufahi kabisa.....hatausiufikirie.....unene unaandamwa na magonjwa kibao.nenda siku moja gym utakuta watu wanavyoteseka kuondoa....
 
my dear noella, ridhika na umbo lako mbona ni zuri tuu
mimi nina umbo nadhani naelekea size 6 nini hiyo yako 8 na niko poa tu wala sijali
nina mtoto wa mwaka mmoja niligain kidogo tu nilivyokuwa mjamzito na mitori nilikunywa
mimi wananiita kining'oning'o lakini sijali ila nikivaa napendeza
tafuta vijiguo vidogo vinavyoendana na mwili wako na utapendeza mrembo
jiamini amini wewe u mzuri na unavutia achana na madawa utakuwa boonge ukumbuke mwili wako mdogo
mimi hata sijawahi kutamani kuwa mnene kwa jinsi navyoona watu wamejaa gym

pia unaweza kufanya mazoezi to increase ur hips and butts kama unataka
kuna yale yanaitwa SQUATS na mengine LUNGES yanasaidia kupanua misuli ya mapaja, hips na butts
ndo mazoezi wanayofanya kina Beyonce na JLO mpaka wakawa na mashepu yale..

pia kama unataka kuongezeka kidogo jaribu kula ndizi mbivu kutwa mara tatu, maziwa (whole milk)
na banana milk shake pia zinasaidia kuongeza weight within 2 weeks utajiona mwenye tofauti
all the best mdada
 
Salamu wote wanaJF

Mimi ni mama wa mtoto mmoja,nina tatizo la umbile langu yani ni mwembamba ninavaa size 8.kwa kweli huwa nikijiangalia hata sipendezewi na umbo langu,nimekuwa nikila ovyo ili ninenepe lakini wapi..nimekula mpaka cerelac na uji vya mtoto lakini wapi.

sasa nimesikia kuna dawa za kuongeza unene.nahitaji ushauri wenu kwa hili tafadhali.
kuna yeyote aliyewahi kunywa hizo dawa,je zina side effects gani?
au kama kuna njia mbadala naomba ushauri.hata nikivaa nguo sipendezi.

believe me huo wembamba wako ndio mzuri,ukiwa mnene utahangaika mbaya,kwanza utakuwa mzito,na cyo mwepesi kama ukiwa mwembamaba,pili ukiwa mnene inamaana mafuta yamejaa mwilini,hii itakusababishia kutoka jasho kwa wingi,yaani tuseme hata utembee kidogo tu utaanza kutoka jacho

Kumbuka mafuta huwa pia yanahifadhiwa kwenye moyo,ndiyo maana watu wa nene huwa wanapata pressure,for real sister be proud of your body!!!!!
 
Mie kabla ya kukushauri ningependa kujuA baadhi ya vitu ili nifanye evaluation ya kitaalam- kusema size 8 tu haitoshi.
Nahitaji kujua umri, urefu na uzito wako kwa sasa.
 
Mie kabla ya kukushauri ningependa kujuA baadhi ya vitu ili nifanye evaluation ya kitaalam- kusema size 8 tu haitoshi.
Nahitaji kujua umri, urefu na uzito wako kwa sasa.

Outlier,
mimi umri wangu ni miaka 33, urefu ni 152cm na uzito ni 54kg
nasubiri ushauri wako wa kitaalam.
thnx
 
I see, kwa urefu wako na umri uzito wako ni mzuri kabisa- ni kitaalam kuongezeka uzito itakusababisha uwe overweight na overweight ina uhusiano na matatizo Kibao Kama kisukari, magonjwa ya Moyo na cancer.
BMI yako, Indicator ya weight for height ni 23.4 na normal ni 18-25!
Hao wanaokuulizauliza kuhusu mwili wako wanakutafutia stress za bure!
Na Mara nyingi with age, uzito pia unaongezeka, hivyo usishangae in 5 years waweza kuwa mnene Zaidi ya sasa.
Ushauri, maintain uzito wako wa sasa!
Na range ya uzito unaotakiwa kuwa nao ni 42Kg to 58Kg!
Asante.
 
My dia Noella, mimi ni mwembamba na sipendi kuwa mnene na nachukia mtu akiniambia nimenenepa...na napenda sana nimwonapo mdada yupo bado portable while ameshazaa..Nitafanya kila njia nijimantain nikizaa....Wala usiwaze.Wewe ni mzuri.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Back
Top Bottom