Dawa za usingizi zinafanyaje kazi?

M45

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2015
Posts
1,110
Reaction score
1,462
Habari,

Mimi ni Kijana 25years .

Nina tatizo la kukosa usingizi takribani miaka mitatu sasa, Ninalala mapema saa nne usiku lakini usingizi nakuja kuupata saa kumi au saa tisa, hali ambayo inanifanya nisinzie nikiwa kazini kwani kazi inanihitaji.

Katika kuuliza tatizo nikapata jamaa yangu na kunieleza kuwa kuna dawa za usingizi zipi madukani.

Aina mojawapo ni (Valium)(Zolpidem)

Je hizi dawa zinafanya kazi baada ya muda gani?

Je inaruhusiwa kutumia na maziwa au pombe?

Asante!
 
Pole sana. Ngoja waje wataalamu
 
Kukosa usingizi ni ugonjwa unaofahamika Kama insomnia, ugonjwa huu hautibiki kwa dawa. Ukiutibu kwa dawa Kama hizo Valium na piriton, utajikuta unakuwa teja.
Ninakushauri hivi kwa sababu niliwahi kusumbuliwa na tatizo hilo baada ya kumaliza kidato cha sits msuli PCM. Niliwahi kudhania halitaisha lakini baadaye liliisha.
Usitumie dawa yeyote, usijegeuka teja bure.
 


Lakin Mkuu hizo dawa kwani ni za kulevya?
 
Invisible Naomba umsaidie huyu kija kuupeleka uzi wake JF Doctor's.
 
Last edited by a moderator:
Inatakiwa kwanza ufahamu chanzo cha tatizo kwanza ndio utafute tiba. Je kwa upande wako ni nini chanzo cha tatizo? Uoga, stress au ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…