DAWASA Kibaha wanabambikia watu bili za maji, mamlaka waangalie kuna kitu huku

DAWASA Kibaha wanabambikia watu bili za maji, mamlaka waangalie kuna kitu huku

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Kuna huu mchongo ambao unaendelea Kibaha japo kuna washkaji zangu nilizungumza nao wanadai kuwa siyo Kibaha peke yake bali maeneo mengi.

Inadaiwa kuwa wana mchezo wa kubambikia watu bili za maji.

Inashangaza kidogo kwa kuwa malipo unalipia online, waoa wanafaidikaje hapo au ni uzembe wao tu?

Kuna ndugu yangu mita yake ya maji imeharibika na ameshaenda mara kadhaa kuripoti lakini hawaendi kuibadilisha, kisha ikifika mwisho wa mwezi wanabuni bili wanakutumia.

Kuna mama mmoja naye nilimkuta palepale ofisini kwao Maili Moja analalamika kuwa kuna siku bili ilikuja zaidi ya elfu 60 kwa mwezi wakati bili yake huwa haizidi buku 15 kwa mwezi.

Wakamwambia mama fuatilia labda mabomba yako au system yako ya maji ina shida, bi mkubwa akakomaa hakufanya kitu anasema akalipa kishingo upande na hakurekebisha popote na matumizi yake ni yaleyale, mwezi uliofuata wakatuma bili buku 15 ileile ya mwanzo.

Mimi mwenyewe mita yangu imeharibika ina mwaka sasa, haisomi lakini kila mwezi jamaa wanakuja eti kusoma mita na bili natumiwa, nikumuuliza unasomaje hizo namba ananijibu niendi ofisini kwao ndiyo wana majibu.

Wazee hoo kitu ipoje huo kwenu?
 
Ni kweli tupu mkuu.

Kwanza Mita wanakadiria mara nyingi hawasomi.

Huku kwetu walikuja na mfumo wa kutubadilishia mita za zamani na kuweka mpya..
Sababu ya kuweka Mita mpya hazijulikani,

Kumbe zote zilikuwa ni mbinu ya kutaka kutuchoma wanainchi na kitu chenye incha Kali shingoni.

Baada ya zoezi lile la kubadilishiwa Mita ,,
Mwisho wa mwezi waliongeza deni kwa baadhi ya watu Kati ya sh 35000 na sh 40000 kwenye ACC ya Mita mpya...
Mimi ni mmoja wapo.

Vilio na mayowe yalisikika kutoka kwa wanainchi .
Lakini Dawasa hawakujali ,
mwisho walikuja kusitisha huduma ya maji bila huruma..
 
Wanabambikia sana watu madeni yasiyokuwa na macho wala miguu
 
Ukiwa hauna maarifa ya Kitu flani,matokeo yake ni kuongea vitu visivyokuwa na uhakika.

Shida yetu wabongo huwa tunapenda kusapoti vitu pasipo kuwa na Evidence.

Tunalishana Elimu ya Matango pori pasipo utafiti.

Dawasa huwa wanatoa Taarifa kuwa tar 20 zoezi la Usomaji meter huwa linaanza,inatakiwa mtu usome na msoma Meter atakapofika kwenye hizo tar. Kama No haujaziona kwanini usiende ofisi zao ukiwa umeipigia picha meter YAKO kama ushahidi?

Lakini kingine umeesema huyo mama walimbambikia tsh 60000 baadae ikarudi kuwa kawaida tsh 15000.

Je, ulimfuatilia kuwa hakufanya marekebisho palipokuwa na Changamoto?

Mimi ninaamini tuliomo humu ni Great thinkers,basi tuwe wadadavuaji wa vitu kabla hatujaanza kudoubt.

Cha Mwisho,Nyumba nyingi zinazotumia mfumo wa maji ndani,maji hutumika sana tofauti na anaechota maji kwa nje.

Jizoeshe kuikagua mifumo YAKO mara kwa mara ili kudhibiti leakege
 
Lakini kingine umeesema huyo mama walimbambikia tsh 60000 baadae ikarudi kuwa kawaida tsh 15000. Je ulimfuatilia kuwa hakufanya marekebisho palipokuwa na Changamoto???
Huyu wakuwa naye makini.

Ameandika alimkuta ofisini maili moja analalamika ina maana mwezi uliofuata alimuona tena palepale ofisini au walibadilishana namba ili kupeana taarifa? 🙆
 
Huyu wakuwa naye makini.
Ameandika alimkuta ofisini maili moja analalamika ina maana mwezi uliofuata alimuona tena palepale ofisini au walibadilishana namba ili kupeana taarifa? 🙆
Shangaa nawewe ,wanalishana sumu za Uongo tu
 
Kuna huu mchongo ambao unaendelea Kibaha japo kuna washkaji zangu nilizungumza nao wanadai kuwa siyo Kibaha peke yake bali maeneo mengi.

Inadaiwa kuwa wana mchezo wa kubambikia watu bili za maji.

Inashangaza kidogo kwa kuwa malipo unalipia online, waoa wanafaidikaje hapo au ni uzembe wao tu?

Kuna ndugu yangu mita yake ya maji imeharibika na ameshaenda mara kadhaa kuripoti lakini hawaendi kuibadilisha, kisha ikifika mwisho wa mwezi wanabuni bili wanakutumia.

Kuna mama mmoja naye nilimkuta palepale ofisini kwao Maili Moja analalamika kuwa kuna siku bili ilikuja zaidi ya elfu 60 kwa mwezi wakati bili yake huwa haizidi buku 15 kwa mwezi.

Wakamwambia mama fuatilia labda mabomba yako au system yako ya maji ina shida, bi mkubwa akakomaa hakufanya kitu anasema akalipa kishingo upande na hakurekebisha popote na matumizi yake ni yaleyale, mwezi uliofuata wakatuma bili buku 15 ileile ya mwanzo.

Mimi mwenyewe mita yangu imeharibika ina mwaka sasa, haisomi lakini kila mwezi jamaa wanakuja eti kusoma mita na bili natumiwa, nikumuuliza unasomaje hizo namba ananijibu niendi ofisini kwao ndiyo wana majibu.

Wazee hoo kitu ipoje huo kwenu?
Nimeshuhudia diversion zikifanyika usiku uko kibaha, mabomba yanachepushwa.

Hivyo pengine wao wako sahihi ila wizi wa maji ndio chanzo.
 
Kuna huu mchongo ambao unaendelea Kibaha japo kuna washkaji zangu nilizungumza nao wanadai kuwa siyo Kibaha peke yake bali maeneo mengi.

Inadaiwa kuwa wana mchezo wa kubambikia watu bili za maji.

Inashangaza kidogo kwa kuwa malipo unalipia online, waoa wanafaidikaje hapo au ni uzembe wao tu?

Kuna ndugu yangu mita yake ya maji imeharibika na ameshaenda mara kadhaa kuripoti lakini hawaendi kuibadilisha, kisha ikifika mwisho wa mwezi wanabuni bili wanakutumia.

Kuna mama mmoja naye nilimkuta palepale ofisini kwao Maili Moja analalamika kuwa kuna siku bili ilikuja zaidi ya elfu 60 kwa mwezi wakati bili yake huwa haizidi buku 15 kwa mwezi.

Wakamwambia mama fuatilia labda mabomba yako au system yako ya maji ina shida, bi mkubwa akakomaa hakufanya kitu anasema akalipa kishingo upande na hakurekebisha popote na matumizi yake ni yaleyale, mwezi uliofuata wakatuma bili buku 15 ileile ya mwanzo.

Mimi mwenyewe mita yangu imeharibika ina mwaka sasa, haisomi lakini kila mwezi jamaa wanakuja eti kusoma mita na bili natumiwa, nikumuuliza unasomaje hizo namba ananijibu niendi ofisini kwao ndiyo wana majibu.

Wazee hoo kitu ipoje huo kwenu?
Watolee taarifa kwa Mh. Juma Aweso huwa hana masikhara na watu wanaotaka kumharibia, atawatimua wote!

kuanzia meneja na wasoma mita wake
 
Ukiwa hauna maarifa ya Kitu flani,matokeo yake ni kuongea vitu visivyokuwa na uhakika.
Shida yetu wabongo huwa tunapenda kusapoti vitu pasipo kuwa na Evidence. Tunalishana Elimu ya Matango pori pasipo utafiti.

Dawasa huwa wanatoa Taarifa kuwa tar 20 zoezi la Usomaji meter huwa linaanza,inatakiwa mtu usome na msoma Meter atakapofika kwenye hizo tar. Kama No haujaziona kwanini usiende ofisi zao ukiwa umeipigia picha meter YAKO kama ushahidi???
Lakini kingine umeesema huyo mama walimbambikia tsh 60000 baadae ikarudi kuwa kawaida tsh 15000. Je ulimfuatilia kuwa hakufanya marekebisho palipokuwa na Changamoto???
Mimi ninaamini tuliomo humu ni Great thinkers,basi tuwe wadadavuaji wa vitu kabla hatujaanza kudoubt.
Cha Mwisho,Nyumba nyingi zinazotumia mfumo wa maji ndani,maji hutumika sana tofauti na anaechota maji kwa nje. Jizoeshe kuikagua mifumo YAKO mara kwa mara ili kudhibiti leakege
Kwamba unatufundisha kusoma Mita?
Au hatujuwi tulisemalo?

Mimi nilikuwa nadaiwa deni 385000.
Ni deni ambalo lilikuja nikiwa sipo inchini.

Waliokuwapo walikuwa hawafatilii bili za maji.

Niliporudi nikaamua kufatilia kwa karibu chanzo cha lile deni kuwa kubwa.

Niliweka utaratibu wa kulipa kila mwezi 60000.

Nikawa napunguza deni na huku nafatilia matumizi ya maji kwa kila unit.

Kila nikilipa napata sms balance ya deni liliilobakia.

Siku deni limebaki 8000 Tu..

The next month's napata sms ya kudaiwa 43000.

Naambiwa Nina deni la mwanzo 35000 ..
Najiuliza hili deni 35000 limetoka wapi wakati tangu mwanzo nimepewa deni la 385000 .?

Nikagunduwa hata lile deni la mwanzo 385000 limekuwa kubwa sababu ya kutokuwa na mfatiliaji..

Dawasa ni kwl wanabambika watu madeni..

Na hata bills wanasoma tofauti au hawasomi bali wanakadiria.
 
Ukiwa hauna maarifa ya Kitu flani,matokeo yake ni kuongea vitu visivyokuwa na uhakika.
Shida yetu wabongo huwa tunapenda kusapoti vitu pasipo kuwa na Evidence. Tunalishana Elimu ya Matango pori pasipo utafiti.

Dawasa huwa wanatoa Taarifa kuwa tar 20 zoezi la Usomaji meter huwa linaanza,inatakiwa mtu usome na msoma Meter atakapofika kwenye hizo tar. Kama No haujaziona kwanini usiende ofisi zao ukiwa umeipigia picha meter YAKO kama ushahidi???
Lakini kingine umeesema huyo mama walimbambikia tsh 60000 baadae ikarudi kuwa kawaida tsh 15000. Je ulimfuatilia kuwa hakufanya marekebisho palipokuwa na Changamoto???
Mimi ninaamini tuliomo humu ni Great thinkers,basi tuwe wadadavuaji wa vitu kabla hatujaanza kudoubt.
Cha Mwisho,Nyumba nyingi zinazotumia mfumo wa maji ndani,maji hutumika sana tofauti na anaechota maji kwa nje. Jizoeshe kuikagua mifumo YAKO mara kwa mara ili kudhibiti leakege
Mita zao saa ingine mbovu,sisi hapa tunapokaa maji huwa tunapandisha juu ya matank lakini baada ya siku siku mbili maji ya meisha Lita 10000,wao kutwa walikuwa wanangangania kuwa Kuna sehemu maji yanavuja,pamoja na kuchunguza na wao hatujaona wapi panavuja,kumbe limita lao wenyewe libovu linarudisha maji,mean mfano juu Kuna maji,harafu Yale ya dawasco online yakakatika,yajuu yanarudi kwenye mfumo wa dawasco,tiligundua juzi wenyewe,wao walishachemka,tukafunga return valve,ndo pona yetu
 
Kuna huu mchongo ambao unaendelea Kibaha japo kuna washkaji zangu nilizungumza nao wanadai kuwa siyo Kibaha peke yake bali maeneo mengi.

Inadaiwa kuwa wana mchezo wa kubambikia watu bili za maji.

Inashangaza kidogo kwa kuwa malipo unalipia online, waoa wanafaidikaje hapo au ni uzembe wao tu?

Kuna ndugu yangu mita yake ya maji imeharibika na ameshaenda mara kadhaa kuripoti lakini hawaendi kuibadilisha, kisha ikifika mwisho wa mwezi wanabuni bili wanakutumia.

Kuna mama mmoja naye nilimkuta palepale ofisini kwao Maili Moja analalamika kuwa kuna siku bili ilikuja zaidi ya elfu 60 kwa mwezi wakati bili yake huwa haizidi buku 15 kwa mwezi.

Wakamwambia mama fuatilia labda mabomba yako au system yako ya maji ina shida, bi mkubwa akakomaa hakufanya kitu anasema akalipa kishingo upande na hakurekebisha popote na matumizi yake ni yaleyale, mwezi uliofuata wakatuma bili buku 15 ileile ya mwanzo.

Mimi mwenyewe mita yangu imeharibika ina mwaka sasa, haisomi lakini kila mwezi jamaa wanakuja eti kusoma mita na bili natumiwa, nikumuuliza unasomaje hizo namba ananijibu niendi ofisini kwao ndiyo wana majibu.

Wazee hoo kitu ipoje huo kwenu?
Jamani mwenzenu bili imekuja laki 5 kwa mwezi sijalipia miezi 2 asaivi bili imefika milion moja na laki tano, nikienda kulalamika wananiambia lipia kwa aawamu , naombeni ushauri nifanyeje.
 
Kumbe kweli, itakuwa kuna kamchezo wanafanya, haiwezekani iwe hivi kirahisi rahisi tu chalii
Yani mie mwanzoni bili ilikua inakuja elfu 50 nikakubaliana na hali sema asaivi wameniletea bili laki 5 kwa mwezi yani sielewi kabisa, ukienda wanakuambia tunakuachia ulipe kwa awamu
 
Yani mie mwanzoni bili ilikua inakuja elfu 50 nikakubaliana na hali sema asaivi wameniletea bili laki 5 kwa mwezi yani sielewi kabisa, ukienda wanakuambia tunakuachia ulipe kwa awamu
Hao ni wezi kabisa, kuna haja ya kuwaripoti kwenye mamlaka husika. Haiwezekani mtu apewe bill ya Tshs 500,000/= kwa mwezi kwa matumizi tu kawaida ya nyumbani. Au Sister una mashamba unafanya kilimo cha umwagiliaji?
 
Back
Top Bottom