Daz Baba "Awa Kichaa"

BashiriOnline

Senior Member
Joined
Nov 5, 2012
Posts
127
Reaction score
44
Habari kutoka kwa chanzo cha uhakika zinadai
kuwa msanii wa zamani wa kundi Daz Nundaz
na hitmaker wa ‘Figure Namba 8′ Daz Baba
amechanganyikiwa kutokana na hivi karibuni
kuonekana akifanya vitendo ambavyo havilingani
na mtu mwenye akili timamu.

Chanzo hicho kimesema Daz alionekana maeneo
ya Morogoro akiwa katika hali iliyowatia mashaka
ndugu, mashabiki wa muziki pamoja na wasanii
wenzake.

Rafiki wa karibu na Daz Baba amemwambia
mwandishi wetu jana akiwa mkoani Morogoro
kuwa hali ya msanii huyo ni mbaya na ana dalili
zote za mtu ambaye ni Kichaa na amekuwa
mtu wakuzunguka barabarani huku akifanya
matukio ya ajabu.

“Hivi juzi juzi Daz alienda nyumbani kwa Afande
usiku, akapiga kelele sana, Afande akaamka na
kumkuta Daz akiwa mchafu na akiongea maneno
ambayo hayaeleweki, baadaye alitaka kumfanyia
tendo baya kwa mfanyakazi wa kike wa Afande
lakini hakufanikiwa, ila watu wakajua kweli Daz
hayuko sawa,” alisema.

Baada ya taarifa hiyo mwandishi wetu alimtafuta
Afande Sele, ndipo alipothibitisha kutokea kwa
tukio hilo nakusema ameshampatia taarifa dada
yake Daz wa Dar es salaam.
“Kweli hali ya Daz ni mbaya sana nimejaribu
kumuweka sawa lakini nimeshindwa labda
wakamfanyie matambiko ya kwao kwasababu
baba na mama yake walifariki na walikuwa
hawaelewani labda kuna matatizo ya kifamilia.”
alisema Afande.
 
Kwani kuna jingine jipya zaidi,Ya mibangi na mi cocaine wanayoibwia,hafu wanajifanya hajaaga kwao 'aende akafanyiwe tambiko'.SASA tambiko na Bangi wapi na wapi?
 
Chezea mihadarati wewe...methardone inamuhusu sana. Inasikitisha
 
kama sembe na bangi alikuwa anatumia inawezekana ndo amezidisha doz
 
Kichaa kimempanga Jery,
baada ya kuvuta mneri
wengi walidhani karogwa na jiran
kumbe mibangi imempanda kichwani.....
 
Ni mmoja wa wasanii wa kwanza kabisa kubwia sembe,loo pole yake.
 
naona katka makala yako unataja na mwandshi wetu lakni mwisho hujatoa source? huyo mwandshi ni nani?
 
Wavuta Bangi kwa kuteteana! badala ashauri mwenzake apelekwe mirembe, anasema akafanyiwe tambiko!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…