DC Godwin Gondwe awapigia magoti Wananchi Munkhola akisisitiza waondoke hifadhi ya Msitu

DC Godwin Gondwe awapigia magoti Wananchi Munkhola akisisitiza waondoke hifadhi ya Msitu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mkuu wa Wilaya ya Singida Godwin Gondwe, amewapigia magoti Wananchi wa Vijiji vya Msikiii na Munkhola katika Wilaya hiyo ikiwa ni msisitizo wa kuwaomba waondoke katika eneo walilovamia la hifadhi ya Msitu wa Munkhola ambalo limeanza kupata mmomonyoko wa ardhi unaoweza kusababisha madhara kama yaliyotokea Hanang, Manyara.

Hatua hii imekuja baada ya Wananchi wa Kijiji cha Msikii na Munkhola kuvamia eneo hilo na kujimilikisha kinyume na utaratibu wa sheria na kufanya shuhuli zao na kusababisha mmomonyoko wa ardhi katika kijiji cha Munkhola ambapo nyumba zaidi ya 150 zimeharibika kutokana na chemchem inayotoka katika hifadhi hiyo.

Aidha, DC Gondwe ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Singida ndani ya siku 14iwe imetoa nakala kwa Wavamizi kuondoka katika eneo hilo na atakayekaidi agizo hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao "kuharibu hifadhi ni ubinafsi, mvua mtapata wapi? hapo chini kijiji kitakwisha, yalitokea Hanang ndio hayo mnataka yatokee hapa achenii"
 
Hivyo vijiji vipo kata gani? Bila shaka ni Singida DC na sio Singida MC, Msikii na Munkhola
 
Sina mengi ya kuandika picha inajieleza.
 

Attachments

  • 20250113_160458.jpg
    20250113_160458.jpg
    390 KB · Views: 2
Mkt wa Kamati ya Usalama anapigia magoti wananchi mbele ya KU yake nadhani si sawa. Jambo walilofanya wananchi linahatarisha usalama wa watu hivyo ni hatua za haraka kuchukuliwa yeye ni mkt wa KU na ana vyombo vya kutosha. Kuna mbinu nyingi za kutumia kufanikisha hicho anachopigia magoti. Ameiga ya viongozi wa kisiasa kupiga magoti akina Jenista Mhagama. Wale ni political figures wanatafuta umaarufu na wanaomba zaidi kwa ajili ya wananchi wao. Yeye ni mtawala na msimamizi wa serikali Wilayani, ni maoni yangu kuwa hajawaza vyema kwenye hili.
 
Waondoke kisheria na si kuombwa wala kulazimishwa

Tusipojifunza kutii sheria na taratibu tutangeneza Taifa la hovyo sana. Kama kuna kitu kinanikera na najiuliza imekuwaje, ni hii tabia ya magari ya umma kupita barabarani bila kujari sheria na taratibu.
Taa nyekundu zinawaka halafu wao wanajiona kama haziwahusu, hata kama watasababisha ajari. Ukiona wananchi wanafanya hivyo, ina maana wamejifunza sehemu nyingine kuwa sherai na taratibu sio lazima zifuatwe.
But, kwa ajiri ya usalama na ustawi wetu wenyewe, tunajitengenezea mambo magumu
 
Back
Top Bottom