Elections 2010 DC Igunga ni mkristo mkatoliki; Kwanini hajasema kitu?

Mkuu wangu yaani unasema huyu mama aje na kusema ukwlei kuwa yeye ni Muislaam au sio Muislaam?.. Yeye kisha timiza alichokitaka na zengwe ndio hilo halafu hakuna mahala popote mama huyu alidai yeye ni Muislaam hivyo Bakwata ndio walikurupuka kutokana na kile walicholishwa na washabiki wa kisiasa. Hii kitu imetengenezwa tunapoteza muda na pumzi zetu bure kwa ujinga wa hawa viongozi wa Bakwata. Chadema did nothing wrong isipokuwa wapo wahusika na kesi iko mahakamani...
 
acha kupotosha watu ndoa za mseto zinafungwa na makanisa mengi,kama umekubali kuolewa na mkristo hulazimishwi kubatizwa hiyo ni hiyari yako.

 

Kweli kupenda huondoa macho..kumvua mwanamke nguo zake za stara siyo tatizo?

Kulikuwa na haja gani ya kumvuta mama yule..kihuni vile..hakukuwa na na njia ya kistaarabu kumuondoa hapo?

Kulikuwa hakuna wanachadema wanawake wa kwenda kumuondoa "muhalifu huyo kama wasemavyo?

Millions of questions can asked..ultimately chadema wamedhalilisha alama za dini tena kwa chuki...yet chuki zaidi hata kusema soory it was fans not chama wamekataa the inceidence tells all.
 

Kwa jinsi ninavyomfahamu mimi Mkandara ni mtu mwenye upeo mkubwa sana na ni mtu anaeufahamu vema uislamu, huna uwezo wow6te wa kufanya Argument na Mkandara kwa sababu yeye ana fikra huru na wewe uko hapa kutimiza maelekezo unayopewa na mabwana zako. Nyinyi ndio mnaoudhalisha uislamu kwa kukubali kutumiwa na ccm kama kondomu. Muda huu nilidhani Bakwata itakuwa imeshaandika plopozo ya kuomba MoU lakini badala yake wanajiingiza kwenye siasa uchwara na mazuzu kama wewe unaunga mkono. Wale al shabaab wametoa zawadi ya bunduki na mabomu kwa washindi wa kusoma koran tukufu, je haya ndio mafundisho ya uislamu? Labda tuanze na hili huenda kuna kitu sikijui katika uislamu.
 
Sasa umetoka kwenye kumtetea mwanamke muislam na kumtetea 'mwanamke'. BAKWATA walikuwa wapi kutoa tamko alipokamatwa mbunge mwanamke wa CUF na kutupwa rumande na wanaume? au walikuwa wapi wakati mchumba wa Dr Slaa alipopigwa vibaya na FFU?
Yaani pamoja na kuumbuka kote huko bado mnaing'ang'ania CHADEMA wakati kesi iko mahakamani? Inaelekea mkuu wewe ni mmoja wa hao mashehe uchwara.....!
 

Propozo propozo!.
Bakwata zamani walikuwa hawaelewi,sasa ndio wanungana na wenzao kupitia matukio kama haya ya hijabu.
Hizo unazosema zipo nyingi tu lakini za waislamu huwa zinapuuzwa ndio maana sasa muda umefika ama zitekelezwe au na za kikristo zivunjwe ndipo tutakwenda salama usalimini.
 

Kutumiwa na CCM kwa malengo ya kisiasa ni kudhalilika!!!! Ni kama utumwa fulani, maana mtu kanunuliwa na atafanya yote kwa ajili ya master wake naye anabaki pale pale kimaendeleo, kifikra na kiuchumi.

Kataeni utumwa.
 
Sweke kwa ujinga wako juu ya uislamu unalazimisha waislamu kutetea vitu unavyoona wewe ni sawa na hijabu kama vile mchumba wa dkt Slaa na mwanamke aliyewekwa na wanaume rumande.Hivyo vitu uzito wake unahitaji kupimwa kutokana na vitu kadhaa ndani ya uislamu,yaani kutafutiwa fatwa.Hili la hijabu ni aya ya Qur'an iliyo wazi.
 

Nioneshe aya ya koran inayosema mtoto atakaeshinda mashindano ya kusoma koran basi zawadi yake ni bunduki na mabomu!
 
katoliki,zipo ndoa za mseto.Mi ninaye ndugu yangu kafunga ndoa na mke muislam.inaruhuriwa,
 
katoliki,zipo ndoa za mseto.Mi ninaye ndugu yangu kafunga ndoa na mke muislam.inaruhuriwa,
sawa zipo! lakini huyo mama ni mhudhuriaji tu mzuri wa kanisa....! kwani ameshaonekana msikitini?
 
hii ni aibu ya chama ya cha magamba pamoja na bakwata na wale wa suruali fupi na wengine wote waliotoa matamko yao
 
Kama ni kweli wale masheik walioshindwa kutambua tofauti kati ya hijab na ushungi wataswali msikiti gani? Watakuwa na uhalali gani wa kutoa mafundisho ya dini ya kiislam? tusubiri muda mengi yanaweza kufumuka na nahofia aibu ya karne!
hii ndio tatzo la kuropoka kwa viongozi wa Dini wasiojua ukweli-HII INAONYESHA JINSI GANI VIONGOZI WA DINI WANAWALISHA "SUMU" WAUMINI WAO.
ni muda muafaka sasa kwa kila muumini kutafakari mambo yanayosemwa na kiongozi wake kuliko ku-react kama kichaa
 
Aibu iliyoje hii?,in case kama kweli ni mkatoliki basi Muumba wetu anajukumu zito siku ya hukumu.
 

Yeye kama si Muislam alitakiwa afike aseme yeye si Muislam. Kama yeye ni Muislam hana haja ya kwenda kwenye vyombo vya umma kujieleza kuwa yeye ni Muislam, kwa sababu tutataka afanye hivyo kwa faida ya nani? Kama haki yake ya kutetewa kama Muislam tayari ameshaipata. Kwangu inanishangaza kweli kweli kuwa tunataka "mama huyu adai kuwa yeye ni Muislam". Afanye hivyo ili iweje?

Besides hatujui kuwa alizungumza na Bakwata kabla au la. Kwa mujibu wa Video iliyowekwa hapo juu, Bakwata wanazungumzia kuwa aliambiwa "unajifanya Hajat....." kabla ya kuvuliwa mtandio wake. Tuamini kuwa Bakwata imeongeza chumvi, wanachadema hawakumwambia hivyo, lakini kuna elements zinazoonyesha kuwa walijiridhisha kuwa ni Muislam au wamemuona akitekeleza dini yake zaidi ya kuvaa huo mtandio (Usikute pengine ni Hajat kweli).

Chadema did wrong, awe huyo mama ni Muislam au la (Naamini ni Muislam hadi pale vyombo vya habari vitakaposema vyenginevyo, na sio propaganda za JF zisizoombwa ushahidi zinazoletwa na wana Chadema). Kumvua mtu nguo yake anayoamini kuwa ni stara kwake ni kosa. Iwe nguo hiyo ni Mtandio, Blouse, skirt au nyengineyo yoyote. Kilichotokea ni udhalilishaji wa wazi kwa mwanamke. Hatukemei sasa kwa vile aliyefanyiwa ni CCM lakini itatu cost baadae kukiacha chama cha siasa kuchukua sheria mkononi zinazoambatana na udhalilishaji.
 
hahahaa!!.....Muungano wa BAKWATA na wenzao wepi??? na kiunganishi ndio discussion ya HIJAB?...........aseeee!!

.Again, malalamiko, whats your problem dudes??

Several times kama sio wewe basi ndugu wengine, wamekuwa wakisisitiza kuwa ili kuwa na usalama, lazima hizo unazoziita MOU za kikristo zifutwe.
This makes me think..........mmmh!!! what will you do?? side with CCM? burn down churches or mission schools and health facilities that WE ALL get service from??

Acheni kujichanganya bana!!!! tulieni mfanye mambo yenye akili.
 
<br><br>Tulia mama, unatumia nguvu nyingi sana.<br>Ok, kwahiyo tusema kweli mtandio umevuliwa katika purukushani za kumkamata na kumtoa asifanye kikao, kama picha zinavyoonyesha.<br>Je, unavyosema amenyanyaswa, na unavyosema chama cha siasa ndio kimemnyanyasa huyo mama, unatupilia mbali sababu za yeye kukamatwa?<br><br>Pili, unajua nguvu za namna hii zilikuwa zinahitajika sana wakati askari wa jiji walipokuwa wanawakamata akina mama na dada zetu kama kuku, wakiwabeba mzobe mzobe kuwapandisha kwenye malori, wakiwachania kaniki zao na kuwaacha watupu, HAMKUWEPO, kwa nini??kwasababu hawakuigusa dini wala itikadi zenu???. Au kwasababu they were SOME random women??<br><br>
 
Penye purukashani lolote laweza kutokea. Nini Mtandio kuvuliwa hata Suruali waweza kuvuliwa. Si unajua tena likitokea kwa mama ni story nyingine. Tuache mahakama wahukumu wenyewe hii story imekosa mvuto.
 
Igunga kuna VUMBI na UPEPO mkali ambao ulipeperusha hata SHATI la Bwana Rage hadi kuonyesha Bastola yake hadharani. Huenda mama Kimario naye alificha nywele zake kwa Mtandio ili kukwepa Vumbi na UPEPO siku hiyo. Bahati mbaya ukatokea Ugomvi Kitambaa Mtandio ukamvuka akiwa amebebwa na Vijana. Ili kuwafanya CHADEMA wabaya lazima waseme ile ni HiJabu amevuliwa.
 
Ndugu, mimi nipo karibu na hiyo familia, nimesikitishwa sana na upotoshaji unaoendelea kwenye thread hii! Ukweli ni kuwa bi Fatma amezaliwa muislam, na kweli pia aliolewa na mkristo Kimaryo . MUHIMU HAPA KU-NOTE NI KUWA BI FATMA SI MKRISTO kwa dini na PIA WAMETENGANA NA HUYO MUME WAKE KITAMBO SASA, na hiyo imempa fursa ya kumrejea MOLA wake! Wale washambulizi wa CHADEMA walifanya hivyo wakijua kuwa ni muislamu, angekuwa dada yao wakikatoliki wasingethubutu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…