DC Jokate Mwegelo: Taa za kisasa kuwekwa eneo la nje mkabala na uwanja wa Benjamin Mkapa (Temeke)

DC Jokate Mwegelo: Taa za kisasa kuwekwa eneo la nje mkabala na uwanja wa Benjamin Mkapa (Temeke)

Solar 300,000
Battery 250,000
Wiring 50,000
Post, nuts etc 250,000
Kokoto na Mchanga 50,000
Cement 2bags Sh. 40,000
Kuchimba shimo sh. 10,000
Ufundi kwa jumla sh. 100,000
Jumla Sh. 1,050,000

Tena hapo nimepiga hesabu za juu kabisa maana serikali sasa hivi inaendesha miradi kwa force account hivyo wananunua materials then wanamwajiri fundi.

Huyo meneja wa TARURA aache ujinga

Nilisikia betri zinakaa mbili. Moja ni 500,000×2=1,000,000

Ni maneno ya vijiweni sijui kama yana ukweli.
 
Ufundi?

material zingine?

vibarua?
Injinia soma hiyo
Solar 300,000
Battery 250,000
Wiring 50,000
Post, nuts etc 250,000
Kokoto na Mchanga 50,000
Cement 2bags Sh. 40,000
Kuchimba shimo sh. 10,000
Ufundi kwa jumla sh. 100,000
Jumla Sh. 1,050,000

Tena hapo nimepiga hesabu za juu kabisa maana serikali sasa hivi inaendesha miradi kwa force account hivyo wananunua materials then wanamwajiri fundi.

Huyo meneja wa TARURA aache ujinga
 
DC JOKATE MWEGELO: TAA ZA KISASA KUWEKWA ENEO LA NJE MKABALA NA UWANJA WA BENJAMIN MKAPA TEMEKE.

MKUU wa Wilaya ya Temeke, Mhe Jokate Mwegelo ametanabaisha dhamira yake ya kubadilisha taswira ya muonekano wa eneo la mbele ya Ofisi DC iliyopo maeneo ya uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na wanahabari mara baada ya kukutana na Maafisa wa TARURA, wa Manispaa wakiongozwa na mkurugenzi wa Manispaa Mh. Jokate alisema eneo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya linatazamana na uwanja wa Benjamin Mkapa na kwamba hukutanisha maelfu ya Watanzania na watu wa mataifa mbalimbali, hivyo ni vyema taswira yake ikaendana na hadhi hiyo.

"Eneo hili lina taswira ya Kitaifa na Kimataifa kwa kuwa hutumika katika michezo na dhifa mbalimbali za kiinchi, hivyo ni lazima linafanane na hadhi hiyo", alisema.

Alisema ana taarifa za uhalifu nyakati za usiku ambapo eneo hilo kwa kukosa taa huwa na kiza kinene, kinachopelekea wepesi wa vitendo viovu kufanyika.

"Mimi ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa wilaya ya Temeke haitaleta afya hata kidogo uhalifu kufanyika eneo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kwa Temeke usalama ni moja ya kipaumbele chetu" Alisema Mhe. Mwegelo.

Meneja wa TARURA ambaye pia ni mratibu wa uendelezaji Jiji la Dar es Salaam, amesema kuwa zoezi la ukarabati na uwekaji wa taa 32 katika eneo hilo la barabara lenye urefu wa kilometa 1.3 litagharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 102 na litakamilika baada ya majuma mawili mara baada ya taratibu nyingine kukamilika.

Naye Diwani wa kata ya Miburani, Mhe.Juma Mkenga amemshukuru Mkuu wa wilaya Jokate kwa kutambua umuhimu wa eneo hilo na kwamba uwekaji wa taa hizo kwa kiasi kikubwa utapunguza matukio ya uhalifu na kulipa heshma eneo la uwanja wa Taifa.

Kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamikia eneo hilo hasa kwa kukithiri kwa vitendo vya kiuhalifu kama uporaji hasa nyakati za usiku. Lakini mheshimiwa Jokate amedhamiria kukomesha uovu huo na kuwa historia.

Wananchi wanahitaji maendeleo mbinu za kurejesha hela mifukoni muonekano wa ofisi hauna maana yote kwa nchi maskini kama Tz, huyu bint anapenda starehe anashindwa kufahamu anatakiwa kuwa field muda mwingi sio kukaa ofisini na kusuka suka miguu kwenye viti vya kuzunguka na AC.,

Ofisi ya mkuu wa Wilaya inatosha meza 1 na kiti cha mbao kimoja na vyengine 3 ata vya plastic ili ikitokezea akiwa ofisini akipata mgeni asikae chini inatosha kabisa.

Yeye anataka akae ofisini kama nyumbani kwake. taa nje zinawaka ndani AC zinapiga kelele
 
Na hiki ndio kipaumbele ?, Taswira ?

Ingekuwa bora kwanza angebuni namna ya kupata hizo chenji sio kuchukua zilizopo, nina uhakika ana lobbying power kubwa
 
Jokate Mungu amsaidie nahisi kama mzigo aliyopewa ni mzito kuliko umri wake

Maana mabingwa wa kutafuna miradi ya maendeleo wapo temeke asipo kuwa makini watamjaza upepo ili waendelee kupiga



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taa zenye mwanga mkali zinaenda hadi shilingi milioni mbili na zaidi, inategemea wameainisha taa zenye nguvu kiasi gani!
 
lakini tumeambiwa wanarekebisha uchumi kwanza na kuvutia uwekezaji labda pengine wawekezaji wakishakuja hapo baadae ndo gharama inaweza ikapungua
 
Yuko vizuri kichwani!
Hamna kitu hapo! Wilaya za TZ unaweza ukaanza na kupamba eneo la ofisi? Temeke ina matatizo ya shule utadhani siyo mjini. Mpaka leo shule za msingi watoto wanapitia madirishani na sakafu za vumbi. Ni vi mtu vinavyosifiwa kwa mengine tu!
 
Halafu hizo taa baada ya wiki 2 ni mwendo wa hii inawaka,ile haiwaki,hii inasinzia sinzia,nyingine imeegemea kushoto,nyingine imeegemea kulia...
 
Back
Top Bottom