DC Kilolo asema wanaoshabikia Timu za nje kuwekwa ndani kwa kokosa uzalendo

Matamko matamko kila aina! sasa hapa anaanzaje?
 
Safi sana Mkuu wa wilaya, anza na washabiki wa Iringa wanaoshabikia Simba na Yanga badala ya Lipuli ya mkoani kwao. Ukitaka kula haramu kula tembo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria gani halali ya nchi inakuwa imevunjwa na hao mashabiki wa timu ya nje badala ya ndani? Kama timu ya nje inapiga total football kuliko ya ndani kwa nini nisiishangilie? Atawapataje wale watakaokuwa wana-watch nyumbani kuptia luninga au kusikiliza redioni? Au kosa ni hadharani tu? Baada ya kusweka ndani, na watu kutokwenda uwanjani, atakuja na wasiokwenda uwanjani kuswekwa ndani.
 
Mashallah
 
Uzalendo wa nchi inapokuja swala la vyama vya siasa na haki zao sijui unahamia wapi! Sasa kama Yanga wamefungwa mchana na lipuli ambayo ndo kamepanda hivi unawaambiaje wakawashangilie mnyama Simba jioni anayecheza mechi za kimataifa

Nyie Angalieni haki kwanza hayo mnayoyahubiri kwenye utekelezaji zero yatakuja tu
 
Huyu mmama analazimisha kuingilia mioyo ya mashabiki. Hatari sana, itabidi waongeze majengo ya mahabusu maana idadi hiyo itakuwa ni balaa.
 
Ukiisoma hiyo habari lazima ufurahie kama si kucheka
 
Hivi huko wilayani kwake shida za wananchi zimeisha?
 
MaDC wa matukio ndo hawa ukifuatilia wilaya anayoiongoza ina matatizo debe zima.ujinga ni mzigo
 
yani mimi niache kuishabikia Zamalek eti nikaishabikie Yanga utakuwa uwendawazimu huo, kwani mmeona wapi uzalendo unalazimishwa
 
Labda na yeye ni chixi maana mpangaji mkuu pale magogoni alisema yeye ni kicha a.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…