DC Makonda 'amekiri' kuwa lilikuwa ni suala la kinidhamu, alikosea

DC Makonda 'amekiri' kuwa lilikuwa ni suala la kinidhamu, alikosea

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Mkuu HAMY-D, ameweka video ya sakata la kuswekwa ndani kwa Watendaji wa Ardhi wa Kinondoni kwa amri ya Mkuu wa Wilaya hiyo,Mhe. Paul Makonda. Nimeitazama na kuisikiliza kwa makini sana video hiyo inayodaiwa ndiyo ufafanuzi wa kilichotokea. Swali hapa ni: Watendaji hao walitenda mmakosa ya aina gani? Katika utumishi wa umma kuna makosa ya aina mbili. Aina ya kwanza ni makosa ya jinai. Haya huweza kutendwa na watumishi wa umma na kupelekea wao kukamatwa nakushtakiwa na Jamhuri mahakamani.

Makosa ya jinai ni kama kuiba, kuua, kubaka,kulawiti, kunajisi, kujihusisha na kusafirisha na matumizi ya madawa ya kulevya na kadhalika. Aina ya pili ya makosa yanayoweza kutendwa na watumishi wa umma ni makosa ya kinidhamu. Makosa haya ni yale yanayohusika moja kwa moja na utendaji wa kazi wa mhusika. Makosa haya yanaainishwa chini ya Sheria za Kazi za Tanzania hasa Kanuni za Utendaji Bora, Tangazo la Serikali Nambari 64 la mwaka 2007. Makosa haya ni pamoja na utoro kazini, uzembe, kutotii mamlaka, ufanyaji kazi usioridhisha, upotevu wa mali ya mwajiri au mteja, uharibifu wa mali na kadhalika.

Kwa mujibu wa DC Makonda, Watendaji wa Ardhi walichelewa sehemu ya utatuzi wa mgogoro wa ardhi. DC Makonda amesema kuwa walikubaliana wote (yeye na Watendaji hao) kukutana sehemu ya tukio saa mbili asubuhi. Wao walifika saa tano asubuhi. Kwakuwa Watendaji hao, kimamlaka, wako chini ya Mkuu wa Wilaya na kwakuwa Watendaji hao walipokubaliana ni kama walipokea amri ya kiongozi wao, walipaswa kufika kabla au katika muda uliopangwa. Kuchelewa kwao ni kosa. Kosa husika hapo ni kutotii mamlaka. Hili ni kosa la kinidhamu, na si la kijinai. Hatua za kinidhamu ndizo zilizopaswa kuchukuliwa.

Hatua hizo ni pamoja na kusimamishwa kazi na hata kuachishwa kazi pale ambapo taratibu za kinidhamu zitafanyika na wao kukutwa na hatia ya kutenda makosa hayo ya kinidhamu. Kwa jana, DC Makonda alipaswa kuwatimua Watendaji hao na si kuwasweka rumande. Nimalizie kwa kusema kuwa,mamlaka ya Mkuu wa Wilaya kuamuru kukamatwa kwa mtu anayetenda kosa au anayedhamiria kutenda kosa au anayehatarisha amani na utulivu yanahusu makosa ya jinai tu. Sheria inayotoa mamlaka hayo ni Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997 chini ya kifungu cha 15 chenye vifungu vidogo 1 hadi 9. Kifungu kizima cha 15 kinahusu makosa ya jinai kwakuwa anayewekwa kizuizini anapaswa kushtakiwa mahakamani (kwa kufikishwa mbele ya Hakimu ndani ya saa 48). Kifungu cha 15 (3) kinasomeka kwa kumaanisha hivyo. Ni hiki:

(3) A person arrested under
the powers conferred by this
section shall, as soon as
Practicable, and in any case
within not more than forty-eight
hours, after he is taken into
custody, be taken before a
magistrate empowered to deal with
the case by the law for the time
being in force in relation to the
institution and prosecution of
criminal proceedings.

Kuna angalizo la kisheria, chini ya kifungu kidogo cha 9 cha kifungu hicho cha 15 cha Sheria tajwa. Angalizo lenyewe ni hili:

(9) Where a District Commissioner exercises the
power conferred on him by this section in abuse of
the authority of his office, then he, as well as any other
Person involved in procuring the District Commissioner
to exercise the power in abuse of authority, is
guilty of an offence and may be proceeded against m
accordance with section 96 of the Penal Code.

Ni hayo tu. Tukubaliane kuwa, DC Makonda alikosea kufanya alivyofanya kwakuwa makosa ya Watendaji hao ni makosa ya kinidhamu na si jinai.
 
Last edited by a moderator:
Acheni watu wanyooshwe! Ikibidi itangazwe hali ya Hatari ( state of emergence) sheria zote zinakuwa pending. Serkal ya kucheka na watumish wazembe imemaliza muda wake
 
Acheni watu wanyooshwe! Ikibidi itangazwe hali ya Hatari ( state of emergence) sheria zote zinakuwa pending. Serkal ya kucheka na watumish wazembe imemaliza muda wake

Mkuu, kuwa makini na lugha yako
 
leo watakua wamewahi zaidi ya hata ya wananchi kwenye eneo husika la mgogoro.
 
Kipi bora kufukuzwa, kusimamishwa kazi au kuadhibiwa kwa kulala mahabusu kwa masaa?
 
Mkuu, kuwa makini na lugha yako

Serikal ya kucheka cheka na Watumishi wa Umma imemaliza muda wake 5 Nov. 2015. Ccm imechukiwa kwa sababu ya Watumish wa Umma washenzi lazima wanyooshwe! Hizo nchi tunazozitumia kama Mfano watu wana nidhamu ya utendaji kazi, leo Sourthern of Sahara sifa kubwa ya watanzania ni kuchelewa kufika kwenye Vikao.
 
Kadhalika kama zipi?
Hapo juu umesema kuhusu kufukuzwa kazi.
Hivi ni mkurugenzi au mkuu wa wilaya ndo mwenye kufukuza mtumishi?

Mkuu, kuna adhabu kulingana na uzito wa kosa. Ndiyo maana ya kadhalika. Uyumwike?
 
Acheni watu wanyooshwe! Ikibidi itangazwe hali ya Hatari ( state of emergence) sheria zote zinakuwa pending. Serkal ya kucheka na watumish wazembe imemaliza muda wake

mnaoshabikia hili suala ni ambao hamna kazi na hamjui sheria za kazi. endeleeni kusambaza CV labda mtabahatika kujua haya mambo! you are merely a poor minded voter mwenye shida kuu na kutumaini kuokolewa na JPM, jiokoe mwenyewe!
 
Sheria na ziheshimiwe. Makonda haheshimu sheria. Alimpiga mzee Warioba.
 
Mkuu, kuna adhabu kulingana na uzito wa kosa. Ndiyo maana ya kadhalika. Uyumwike?

Niyumwike.
Sheria ni kizungumkuti.
Ndo maana nauliza sheria ingefuatwa ,si ingekua mbaya zaidi?

Wewe ungependekeza adhabu gani kwa hao maafisa?
 
Niyumwike.
Sheria ni kizungumkuti.
Ndo maana nauliza sheria ingefuatwa ,si ingekua mbaya zaidi?

Wewe ungependekeza adhabu gani kwa hao maafisa?

Ingetegemea na utetezi wao na makosa yao. Wangeweza kuonywa au kufukuzwa. Kama hakukuwa na sababu nzito za kuchelewa kwao, na baada ya vikao vya kinidhamu kwa mujibu wa sheria, hao watumishi walipaswa kuachishwa kazi
 
mnaoshabikia hili suala ni ambao hamna kazi na hamjui sheria za kazi. endeleeni kusambaza CV labda mtabahatika kujua haya mambo! you are merely a poor minded voter mwenye shida kuu na kutumaini kuokolewa na JPM, jiokoe mwenyewe!

Poor minded ni mtu yeyote anaetumia sheria na taratibu za kazi kama kinga dhidi ya uzembe na matumizi mabaya ya Ofisi. Wewe unaejua sheria za kazi inakuaje unapanga ratiba ya kikao wewe mwenyewe halafu DC anafika kwa wakati halafu wewe mtumishi mwenye kujua "sheria na taratibu" unafika kwa kuchelewa kwa saa3 i.e kutoka saa mbili asbh unafika saa 5 asbh halafu unajitapa unajua sheria za kazi. Visingizio vya kufiwa, foleni, kuuguliwa vipo kwa watumish wa Umma peke yake? Mfanyakazi wa Stanbic Bank anawahi kila siku ofisin posta, mfanyakazi wa ofisi ya Umma nae anachelewa kila siku ofisini posta lakin wote wanaishi mtaa mmoja kimara jee huko barabarani kuna folen za watumish wa Umma na wengine tofauti? Msipojinyoosha mtanyooshwa this time!
 
mnaoshabikia hili suala ni ambao hamna kazi na hamjui sheria za kazi. endeleeni kusambaza CV labda mtabahatika kujua haya mambo! you are merely a poor minded voter mwenye shida kuu na kutumaini kuokolewa na JPM, jiokoe mwenyewe!

Mkuu idoyo ..ww ni kilaza sana.kwanza kudharau wasio na kaz ...inaonyesha ulivyolimbuken wa kutumikishwa kazi za watu.....sasa tufanye zifuatwe taratibu ungefurahi wangefujuzw? kazi?? watumishi walio wengi(sio wote wa serikali)ni wazembe kuliko maelezo....wanyooshwe tu
 
Back
Top Bottom