DC Moshi, James Kaji: Ningekuwa na mamlaka, ningetimua wote waliokosa kushiriki maadhimisho ya Uhuru

DC Moshi, James Kaji: Ningekuwa na mamlaka, ningetimua wote waliokosa kushiriki maadhimisho ya Uhuru

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, James Kaji, amesema hatawavumilia watumishi wazembe na kuagiza majina ya waliokwepa kushiriki maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika yawasilishwe kwake mara moja ili wachukuliwe hatua.

Kaji ametoa onyo hilo leo Jumatatu, Desemba 9, 2024, wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Mashujaa, Manispaa ya Moshi, yakitanguliwa na shughuli za usafi katika makaburi ya Karanga.

Amesema uzembe wa baadhi ya watumishi wa umma unakwamisha juhudi za maendeleo zinazofanywa na Serikali na kuahidi kuchukua hatua kali dhidi yao.

"Watumishi wengi hawawajibiki mpaka wasukumwe au kushikiwa fimbo. Nchi hii ni yetu sote, sitavumilia uzembe huu. Wapo watu mitaani wanazunguka na vyeti hawana kazi, ninyi mmepata nafasi msichezee nafasi hizi. Nitachukua hatua kali kwa wote waliokwepa kushiriki maadhimisho haya kwa kuwa hiyo ni dharau," amesema Kaji.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Mwajuma Nasombe, amesema kwa kushirikiana na wadau, wamefanya usafi katika makaburi ya Karanga, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha usafi wa mji.
 
James Kaji anajipendekeza kutoka cheo kile hadi DC ......hajiongezi kuwa anapwaya ? Angetulia tuuuuu....kukaa kimya ni .busara kubwaaa sanaaa
Ni wazee ambao jua lipo magharibi wanakurupuka tu alikuaga ni mpishi wa hoteli gani kwani mkuu?
 
Hakuna eneo lisilo na mwenyewe. Laweza kuwa ni la mtu binafsi, kampuni, jiji, manispaa, halmashauri, kanisa ama msikiti.

Hii tabia ya kuwasomba wananchi wakafanye kazi katika maeneo yasiyowahusu wakati ushuru na tozo zinakusanywa sio sawa.

Parking ushuru, stand ushuru, sokoni ushuru. Hizi mamlaka zinashindwa nini kuwalipa watu kufanya usafi katika maeneo husika?

Pia iwe kila mwananchi afanye usafi katika eneo lake.
 
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, James Kaji, amesema hatawavumilia watumishi wazembe na kuagiza majina ya waliokwepa kushiriki maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika yawasilishwe kwake mara moja ili wachukuliwe hatua.

Kaji ametoa onyo hilo leo Jumatatu, Desemba 9, 2024, wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Mashujaa, Manispaa ya Moshi, yakitanguliwa na shughuli za usafi katika makaburi ya Karanga.

Amesema uzembe wa baadhi ya watumishi wa umma unakwamisha juhudi za maendeleo zinazofanywa na Serikali na kuahidi kuchukua hatua kali dhidi yao.

"Watumishi wengi hawawajibiki mpaka wasukumwe au kushikiwa fimbo. Nchi hii ni yetu sote, sitavumilia uzembe huu. Wapo watu mitaani wanazunguka na vyeti hawana kazi, ninyi mmepata nafasi msichezee nafasi hizi. Nitachukua hatua kali kwa wote waliokwepa kushiriki maadhimisho haya kwa kuwa hiyo ni dharau," amesema Kaji.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Mwajuma Nasombe, amesema kwa kushirikiana na wadau, wamefanya usafi katika makaburi ya Karanga, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha usafi wa mji.
Viazi kama hivi sijui wanavipataga wapi hadi vinapewa madaraka
 
Hahaha nasubiri suti ya kitenge cha SSH nikahudhurie sherehe za Uhuru wa visiwani Zanzibar.
 
Uhuru? Uhuru gani kama watu wanatekwa na kuteswa na kuuawa ovyo na hakuna kauli au hatua inayochukuliwa.
SISI NI MAITI ZINAZOTEMBEA
 
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, James Kaji, amesema hatawavumilia watumishi wazembe na kuagiza majina ya waliokwepa kushiriki maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika yawasilishwe kwake mara moja ili wachukuliwe hatua.

Kaji ametoa onyo hilo leo Jumatatu, Desemba 9, 2024, wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Mashujaa, Manispaa ya Moshi, yakitanguliwa na shughuli za usafi katika makaburi ya Karanga.

Amesema uzembe wa baadhi ya watumishi wa umma unakwamisha juhudi za maendeleo zinazofanywa na Serikali na kuahidi kuchukua hatua kali dhidi yao.

"Watumishi wengi hawawajibiki mpaka wasukumwe au kushikiwa fimbo. Nchi hii ni yetu sote, sitavumilia uzembe huu. Wapo watu mitaani wanazunguka na vyeti hawana kazi, ninyi mmepata nafasi msichezee nafasi hizi. Nitachukua hatua kali kwa wote waliokwepa kushiriki maadhimisho haya kwa kuwa hiyo ni dharau," amesema Kaji.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Mwajuma Nasombe, amesema kwa kushirikiana na wadau, wamefanya usafi katika makaburi ya Karanga, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha usafi wa mji.
watu wote waliokuwa wameajiriwa idara ya TISS, huwa wanajiona miungu watu sana,
 
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, James Kaji, amesema hatawavumilia watumishi wazembe na kuagiza majina ya waliokwepa kushiriki maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika yawasilishwe kwake mara moja ili wachukuliwe hatua.

Kaji ametoa onyo hilo leo Jumatatu, Desemba 9, 2024, wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Mashujaa, Manispaa ya Moshi, yakitanguliwa na shughuli za usafi katika makaburi ya Karanga.

Amesema uzembe wa baadhi ya watumishi wa umma unakwamisha juhudi za maendeleo zinazofanywa na Serikali na kuahidi kuchukua hatua kali dhidi yao.

"Watumishi wengi hawawajibiki mpaka wasukumwe au kushikiwa fimbo. Nchi hii ni yetu sote, sitavumilia uzembe huu. Wapo watu mitaani wanazunguka na vyeti hawana kazi, ninyi mmepata nafasi msichezee nafasi hizi. Nitachukua hatua kali kwa wote waliokwepa kushiriki maadhimisho haya kwa kuwa hiyo ni dharau," amesema Kaji.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Mwajuma Nasombe, amesema kwa kushirikiana na wadau, wamefanya usafi katika makaburi ya Karanga, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha usafi wa mji.
Uyu kwa kauli hizi kwa watumishi astahili ata dakika 10 kuwa ofisini , Hajui ata maana ya uhuru, kila mtu anahaki kuazimisha sherehe tajwa kwa matakwa yake ,ulipatika uhuru ili watu wawe huru, sasa analeta ujinga gani wa kupangia watumishi cha kufanya . Hawa upataje nafasi kama izi?
 
Back
Top Bottom