DC Sima na mwendelezo wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi, sasa ni zamu ya Rukoma, Kibirizi na Kikomelo

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera Mhe. Erasto Sima anaendelea na ziara yake iliyoanza wiki hii ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi ambapo kesho ziara inaendelea. Kesho Jumatatu Juni 10, 2024 ni Kata ya Rukoma na Kibirizi na Jumanne Kikomelo. Wananchi wote mnakaribishwa. Bukoba Kazi Inaendelea ya kushughulika na masuala ya wananchi.
 
Channel IPI? Au yeye Hana yale Makamera?
 
Sima ni mtu na nusu huyu jamaa
 
DC tafadhali ndugu, kutatua kero siyo sifa. Kwann utatue kero? Wewe kama rais wa kipande cha nchi (ktk hiyo wilaya), unapaswa kuweka mifumo ya kutokuzalisha kero.

Ninapoona kiongozi anatatua kero tena mbele ya kamera namchukulia kama mtafuta kiki tu. DC usiingie kwenye mtego huo, fanya kazi zako bila kiki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…