BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kupambana na Kudhibiti Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo amesoma ripoti ya Operesheni iliyofanywa na mamlaka hiyo kuanzia Machi 25, 2023 hadi Juni 19, 2023 ikiwa ni takribani miezi miwili na wiki tatu ambapo amefafanua mambo mbalimbali kuhusu uhalifu wa dawa za kulevya
Lyimo amesema katika Operesheni yao kwa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Kilimanjaro na Arusha wamekamata watuhumiwa 109 wakiwa na dawa mbalimbali baadhi ni Heroin Kg 200.5, Heroin kete 3,878, Cocaine kete 138 ikiwemo Bangi kavu iliyotayari kisafirishwa nje gunia 978, bangi mbichi gunia gunia 5, 465, bangi iliyosindikwa (Skanka) kilo 1.5 huku ikiteketekeza eka 1093 za mashamba ya bangi.
Amesema kuwa kiasi cha Heroin kilichokamatwa kingeweza kutumiwa na kuathiri watu milioni 4.815, wakati ambapo baadhi ya watuhumiwa wamefikishwa Mahakamani wakati wowote taratibu za kisheria zitakapokamilikia.
Mamlaka hiyo imewatahadharisha Wanawake wanaojiingiza kwenye mahusiano na Wanaume raia wa kigeni ambao wamekuwa wakiwapangia nyumba na kuwahudumia bila kujua shughuli halisi wanazofanya.
Amesema baadhi ya raia hao wanaanzisha uhusiano na Wanawake zaidi ya mmoja na kuficha dawa za kulevya kwenye nyumba za wenza wao hao wakati wao wakiishi kwingine na inapotokea Wanawake hao wanapokamatwa kwa kujihusisha na biashara hiyo haramu huwakana.
“Kutokana na udhibiti kuwa mkubwa, Wafanyabiashara wa Dawa za Kulevya wameendelea kubuni mbinu mpya za usafirishaji ili kukwepa kukamatwa.
“Mamlaka imebaini mbinu hizo na kuchukua hatua, mbinu mojawapo inayotumika ni Raia wa kigeni mmoja kuanzisha mahusiano ya kimapenzi na Wanake wa Kitanzania zaidi ya mmoja na kuficha Dawa za Kulevya kwenye makazi ya Wanawake hao huku wao wakipanga nyumba tofauti na wanakoishi Wapenzi wao.
“Hali hii husababisha Wanawake wa Kitanzania kuingia kwenye matatizo makubwa ya kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria huku Wanaume wakiwakana Wanawake hao, Mamlaka imejipanga kikamilifu kupambana na biashara ya dawa za kulevya hivyo wanaojihusisha au wenye mpango wa kujihusisha na biashara hiyo waache mara moja au wajisalimishe wenyewe kabla hawajafikiwa na mkono wa sheria.
“Wananchi wanapaswa pia kuwa makini na mizigo wanayopewa kubeba au kuhifadhi pasipo kujua ndani yake kuna nini, Wanawake wanatakiwa kuwa makini zaidi kwani katika baadhi ya matukio wamekuwa wakitumiwa na Wapenzi wao hasa Raia wa kigeni kusafirisha na kupokea mizigo wasiyoijua na wakati mwingine mizigo hiyo huwa na dawa za kulevya na hivyo hujikuta matatani.”
Amesisitiza kuwa mamlaka imejipanga kukabiliana na wanaojihusisha na biashara hiyo ya kihalifu.
MAKUBALIANO NA TAKUKURU
Ameongeza kuwa “Katika kuendelea kukabiliana na wahalifu mbalimbali tumeingia makubaliano na TAKUKURU kutumia klabu zao zilizoanzishw akwenye shule na vyuo kutoa elumu ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya.
RAIS SAMIA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO
“Mwezi Juni kila mwaka, Tanzania huungana na mataifa mengine Duniani katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupinga Dawa za Kulevya Duniani kwa lengo likiwa kuongeza uelewa wa jamii na kuhamasisha kushiriki katika mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya Duniani.
Mwaka huu Maadhimisho hayo yatafanyika KitaifaJuni 23 hadi 25 Jijini Arusha kwenye Uwanja wa Sheik Amri Abeid yakiambatana na maonesho ya shughuli mbalimbali za udhibiti wa Dawa za Kulevya zinazofanywa na mamlaka na wadau wake na utoaji elimu wa
Mgeni rasmi siku ya kilele Juni 25, 2023 anatarajiwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan, kauli mbiu ikiwa ni “Tuzingatie Utu na Kuboresha Huduma za Kinga na Tiba”.
Lyimo amesema katika Operesheni yao kwa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Kilimanjaro na Arusha wamekamata watuhumiwa 109 wakiwa na dawa mbalimbali baadhi ni Heroin Kg 200.5, Heroin kete 3,878, Cocaine kete 138 ikiwemo Bangi kavu iliyotayari kisafirishwa nje gunia 978, bangi mbichi gunia gunia 5, 465, bangi iliyosindikwa (Skanka) kilo 1.5 huku ikiteketekeza eka 1093 za mashamba ya bangi.
Amesema kuwa kiasi cha Heroin kilichokamatwa kingeweza kutumiwa na kuathiri watu milioni 4.815, wakati ambapo baadhi ya watuhumiwa wamefikishwa Mahakamani wakati wowote taratibu za kisheria zitakapokamilikia.
Mamlaka hiyo imewatahadharisha Wanawake wanaojiingiza kwenye mahusiano na Wanaume raia wa kigeni ambao wamekuwa wakiwapangia nyumba na kuwahudumia bila kujua shughuli halisi wanazofanya.
Amesema baadhi ya raia hao wanaanzisha uhusiano na Wanawake zaidi ya mmoja na kuficha dawa za kulevya kwenye nyumba za wenza wao hao wakati wao wakiishi kwingine na inapotokea Wanawake hao wanapokamatwa kwa kujihusisha na biashara hiyo haramu huwakana.
“Kutokana na udhibiti kuwa mkubwa, Wafanyabiashara wa Dawa za Kulevya wameendelea kubuni mbinu mpya za usafirishaji ili kukwepa kukamatwa.
“Mamlaka imebaini mbinu hizo na kuchukua hatua, mbinu mojawapo inayotumika ni Raia wa kigeni mmoja kuanzisha mahusiano ya kimapenzi na Wanake wa Kitanzania zaidi ya mmoja na kuficha Dawa za Kulevya kwenye makazi ya Wanawake hao huku wao wakipanga nyumba tofauti na wanakoishi Wapenzi wao.
“Hali hii husababisha Wanawake wa Kitanzania kuingia kwenye matatizo makubwa ya kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria huku Wanaume wakiwakana Wanawake hao, Mamlaka imejipanga kikamilifu kupambana na biashara ya dawa za kulevya hivyo wanaojihusisha au wenye mpango wa kujihusisha na biashara hiyo waache mara moja au wajisalimishe wenyewe kabla hawajafikiwa na mkono wa sheria.
“Wananchi wanapaswa pia kuwa makini na mizigo wanayopewa kubeba au kuhifadhi pasipo kujua ndani yake kuna nini, Wanawake wanatakiwa kuwa makini zaidi kwani katika baadhi ya matukio wamekuwa wakitumiwa na Wapenzi wao hasa Raia wa kigeni kusafirisha na kupokea mizigo wasiyoijua na wakati mwingine mizigo hiyo huwa na dawa za kulevya na hivyo hujikuta matatani.”
Amesisitiza kuwa mamlaka imejipanga kukabiliana na wanaojihusisha na biashara hiyo ya kihalifu.
MAKUBALIANO NA TAKUKURU
Ameongeza kuwa “Katika kuendelea kukabiliana na wahalifu mbalimbali tumeingia makubaliano na TAKUKURU kutumia klabu zao zilizoanzishw akwenye shule na vyuo kutoa elumu ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya.
RAIS SAMIA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO
“Mwezi Juni kila mwaka, Tanzania huungana na mataifa mengine Duniani katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupinga Dawa za Kulevya Duniani kwa lengo likiwa kuongeza uelewa wa jamii na kuhamasisha kushiriki katika mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya Duniani.
Mwaka huu Maadhimisho hayo yatafanyika KitaifaJuni 23 hadi 25 Jijini Arusha kwenye Uwanja wa Sheik Amri Abeid yakiambatana na maonesho ya shughuli mbalimbali za udhibiti wa Dawa za Kulevya zinazofanywa na mamlaka na wadau wake na utoaji elimu wa
Mgeni rasmi siku ya kilele Juni 25, 2023 anatarajiwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan, kauli mbiu ikiwa ni “Tuzingatie Utu na Kuboresha Huduma za Kinga na Tiba”.