Hapa leo masikani, ni nini mwajadilini?
Mtoto Judi jamani, sisi watutakiani?
Ndoa hiyo ya mwakani, nani yuko bahatini?
Ninakutakia heri, Ndoa uivumilie.
Ndoa uivumilie, Ni kama wenda vitani,
yakikukumba silie, yatulize kwa makini,
Ndoa uishikilie, usiyumbe asilani.
Ninakutakia heri, ndoa ni kubwa daraja.
Talaka ikikukuta, Kwa babu uje moyoni,
Babu haweki ukuta, ila tufanye sirini,
Hakika hautajuta, babu kikuweka ndani,
Kwa babu wakaribishwa, Ndoayo kisambaratika
Big Braza ODM Asprin.
shairi uloandika , limenipa tabasamu
tena nimefurahika, ewe ulo mkarimu
daima utasifika , kwa yako tele nidhamu
uwe wake malaika, awe wako hensamu
mengi ulioandika, yamenigusa moyoni
sifa zisizo mipaka, umenipa klorokwini
na hina ukazipaka,nashukuru kwa kunithamini
nimepokea hakika, hizo zako shukrani
natamani ningekesha, shairi kukutungia
jinsi ulivyonikosha , nashindwa kuongezea
hofu nisije chemsha, yana tabu mazowea
vina vyako vyanitisha, hakika vimetulia
hiyo siku ikifika, twaomba kuhudhuria
kama utatualika, mpunga kuja jilia
Mungu alietukuka, akupe njema afia
ufurahi na kuruka, chumbani ukiingia.
mkuu lile sredi la nguli la bongo fleva liko wapi? lilikuwa linasaidia sana kutolea ma stress. hehehyoooo....
yooooo...!one two one two MAKROFONI TEST!yoooo
yooo....!
Hapa leo masikani, ni nini mwajadilini?
Mtoto Judi jamani, sisi watutakiani?
Ndoa hiyo ya mwakani, nani yuko bahatini?
Ninakutakia heri, Ndoa uivumilie.
Ndoa uivumilie, Ni kama wenda vitani,
yakikukumba silie, yatulize kwa makini,
Ndoa uishikilie, usiyumbe asilani.
Ninakutakia heri, ndoa ni kubwa daraja.
Talaka ikikukuta, Kwa babu uje moyoni,
Babu haweki ukuta, ila tufanye sirini,
Hakika hautajuta, babu kikuweka ndani,
Kwa babu wakaribishwa, Ndoayo kisambaratika
Big Braza ODM Asprin.
ngoja waje wajuzi, himeni watakujuza,
mie labda wa juzi, kwa mengi ninawakwaza,
hata na wewe mzazi, washindwa japo kuwaza,
himeni i kama vazi, chanwapo hiyo huliza,
umewaita malenga, kwa dogo hilo jawabu,
ungeuliza wakunga, wasingeipata tabu,
hao wako wadunga, japo wengine vibabu
himeni i kama vazi, chanwapo hiyo huliza,
washituka kujinoma, hali wajua vitamu,
wataka iwepo noma, japo ile maalumu,
kimoja hiyo hukoma, ndipo yasemwa nitamu,
himeni i kama vazi, chanwapo hiyo huliza,
hahahaaha home boy kumbe na wewe umo? lolBabu wewe mtata, Judi wamtakya nini
Mwenyewe kaishapata,laazizi wa ubani
Na deadline kaweka, haitozidi mwakani
Judi babu ukimpa, na mimi pia ntataka
Babu wewe mtata, Judi wamtakya nini
Mwenyewe kaishapata,laazizi wa ubani
Na deadline kaweka, haitozidi mwakani
Judi babu ukimpa, na mimi pia ntataka
hahahaaha home boy kumbe na wewe umo? lol
ni mimi tu nimebaki...
Jieleleze jieleze, jeileze jeilezee, jieleze jieleze jieleze, najielezaaaaaa babaaaaaaa
Mimi apa mimi apa, jina languuu jiiiiiwaiiiiiii
kinywaji changu ni valuu, kaunta yangu ni ya juu
Najelezezaaaaa baabaaaaaaa
na mimi haaapaaa ni teaaamoo,mfaluumeee wa amaaaniiJieleleze jieleze, jeileze jeilezee, jieleze jieleze jieleze, najielezaaaaaa babaaaaaaa
Mimi apa mimi apa, jina languuu jiiiiiwaiiiiiii
kinywaji changu ni valuu, kaunta yangu ni ya juu
Najelezezaaaaa baabaaaaaaa
Tunaoondoka selaaa, tunayumbayumbaaa selaaahehehehe!
NAOMBA NIMSINDIKIZE KOLOKWINI KWA WOMBO....''wana ngonjeera jama twaondoookaa,wana ngonjeeraa jama twaondoookaaaa!upepoooooo bahariiiniiiiiiii MAWIMBI YANA TUPEPERUSSHAAAAA''
SHUUUULEEEEE NAAAIIPEENDAAAAA SHUUUULEEEEE AAAAAAH!shuuulee naaipeendaa shuleeee aaaaah
kiiunoo chaangu chembambaaaa chakuvaliiaaa mkaaandaaa shuleeeee aaaaaah