Rose1980
JF-Expert Member
- May 10, 2010
- 5,684
- 1,305
..UPEPO WA BAHARI KWA MAJONZ UNATUPULIZA...LY TWAAGA WADOGO ZETU(asprin na rr ndo wadogo zetu)Tunaoondoka selaaa, tunayumbayumbaaa selaaa
Wanamashairi selaa,
Mimi na Teamo selaaa
Iyooyoo selaaa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
..UPEPO WA BAHARI KWA MAJONZ UNATUPULIZA...LY TWAAGA WADOGO ZETU(asprin na rr ndo wadogo zetu)Tunaoondoka selaaa, tunayumbayumbaaa selaaa
Wanamashairi selaa,
Mimi na Teamo selaaa
Iyooyoo selaaa
p fankkkkkkkkkk wap??????!!!!!!!!!sasa Miss Judi ndo aolewa sasaaaaaa
sas ndo vile mumwache sasaaaa,
sasa sio mwamsumbua sasaaaa,
Sasa sio kumPM sasaa,
sasa Judy kampata wa kumpa sasa
sasa takuwa halali na njaa sasa,
sasa hamu mepata mwisho sasa,
Sasa akitaka anagusa tu sasa
Anapewa
Anajipa
wanapeana
rahaaaaaa.....utamuuuuuuu...rahaaaa....utamuuuu
Malezi yanaanza
Makwenzi kwa watoto sasa
Ngumi kwa Miss Judy sasa
Ndoa raha na karaha
Hahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
Hapa leo masikani, ni nini mwajadilini?
Mtoto Judi jamani, sisi watutakiani?
Ndoa hiyo ya mwakani, nani yuko bahatini?
Ninakutakia heri, Ndoa uivumilie.
Ndoa uivumilie, Ni kama wenda vitani,
yakikukumba silie, yatulize kwa makini,
Ndoa uishikilie, usiyumbe asilani.
Ninakutakia heri, ndoa ni kubwa daraja.
Talaka ikikukuta, Kwa babu uje moyoni,
Babu haweki ukuta, ila tufanye sirini,
Hakika hautajuta, babu kikuweka ndani,
Kwa babu wakaribishwa, Ndoayo kisambaratika
Big Braza ODM Asprin.
Hahahahaha
Kumbe nawe uko ndani, sikujua asilani,
Kumbe kwenye hii fani, huwezi mjua nani,
Nakupatia nishani, karibu ushairini,
Nakuvulia kofia, GY nambari wani.
Da Judi nimemtakia, mafanikio ndoani
Heri nilimtakia, na furaha ya chumbani,
Mambo yakimshindia, Babu niko kwa pembeni,
Kumrithi dada Judy, Babu ana kosa gani?
babu asipirini, maumivu wayatuliza,
tena wajaa hisani, katu huwezi kuliza,
iwayo ile sirini, huko nako waliwaza,
babu nakuamini, kwa yote ulonijuza,
japo wataja talaka, hiyo kwangu hakuna,
heri nivae viraka, hiyo daima takana,
bila kufanya haraka, watu hawataachana,
babu nakuamini, kwa yote ulonijuza
ndoa kwangu sio vita, rahaye kama peponi,
na vita vinaposita, wajeshi cheko usoni,
bali ndoa kisita, chozi tele machoni
babu nakuamini, kwa yote ulonijuza
Hebu tema mate chini, dada Judi nakwambia,
Talaka ziko mfukoni, mwa mumeo nakwambia,
Ukileta kisirani, talaka akutupia,
Omba kwa Mungu mapema, kabla hayajakufika,
talaka kikutupia, angalizo nilikupa
kwa babuyo kimbilia, kawaida sina pupa,
Mikononi takutia, raha zote nitakupa,
Babuyo niko tayari, kukutulizia shida.
Nita kuweka chumbani, udi ntakununulia,
Pafyumu ya arabuni, chumbani takuwekea,
Ntakugandisha moyoni, njia hautapotea,
Babuyo niko tayari, talaka ukipatiwa.
Hahahahahahahahahhahahahahhah
Kumrithi dada Judy, babu anakosa gani?
Eti mlio weledi, swali hili swali gani
Nimeamua nirudi, nielewe kiundani
Maana babu bepari, Judy uwe makini
Atajifanya kukagua, matiti kwa kuanzia
Bila wewe kutambua, kumbe babu avizia
Mwishowe wastukia, bepari keshajilia
Judy babu ukimpatia, na mimi ntanyatia
1.
Kila niwapo salani, naomba mola nichunge,
Nipatetinga ndoani, upendo wako nipunge,
Niishi kama peponi, dunia isinizonge,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
2.
Butege aliuliza, kwa vipi ningali misi,
Hoja yake kakuza, wangu huu si halisi,
Hata bila kuuliza, yeye kajipa makisi,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge.
3.
Kweli wengi nimeepa, wachumba pia washenga,
Walokuwa na za epa, wote walipigwa chenga,
Walonukia vikwapa, kwa wao huo mpunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
4.
Walianza praimari, nikiwa bado kichanga,
Enzi zile sekondari, wengi walijiunga,
Chuo hakika hatari, kama vya hari vimbunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
5.
Kutunza bikira kazi, katika hii dunia,
Wengi waruka wazazi, kwa zao mbaya tabia,
Ya siri sasa ya wazi, wapi bikira tunzia,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
6.
Namshukuru Manani, himeni yangu salama,
Hadi huko mwakani, haitotiwa alama,
Wala siweki sokoni, yake wangu kujinoma,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
7.
Maisha yetu mabinti, kweli yataka hesabu,
Ili kupata pointi, liwe sahihi jawabu,
Ukihaha nazo senti, tachacha kama ulabu,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
8.
Miaka inapopaa, nawe wapaswa jipanga,
Ni nani wa kukufaa, lazima kichwa kugonga,
Japo awe msambaa, tabibu au mchunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
9.
Mimi yangu tayari, ndoa ni hapo mwakani,
mlio nayo mahari, sasa leteni ukweni,
hima leteni habari, ya ndoa ilo makini,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
10.
Nawaaga mabachala, nao wenye masitazi,
wapweke na makapela, usingo hakika kazi,
hata ukiwa na hela, hazikwishi jinamizi
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
judith best angu,naomba uwe wifi angu
nakukaribisha uje kwetu,uongeze idadi yetu
uwe mama wa wanetu,hilo kwetu tashukuru.
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
tumezaliwa watatu,mimi na kaka zangu,
wamenipa kazi tatu,kuwachagulia wa kudumu
asiwe sistaduu,wala wa kupiga vibomu
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
sifa za nimpendae,wa kuja kua wifi angu
awe na dini yake,inayomwabudu mungu
asiwe na dunia yake,inayopenda majungu
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
kama ubeti wa tano,sifa zake zimo
njoo kwa maringo,hadi kwa mzee timo
tutachinja majogoo,kukukaribisha nditto
nakuomba judith uje kabla ya dedilaini.
kaka zangu mapacha,wote mahendisamu,
wanafanya kazi moja,makazi darisalamu
wakisafiri wiki moja,kurudi haraka muhimu
nakuomba judit uje kabla ya dedilaini
mimi si wifi mtata,nimefunzwa mila zetu
wifi angu tampenda,uwe kama ndugu yetu
mana sina hata dada,wewe takua best angu.
nakuomba judit,uje kabla ya dedilaini.
Hapa leo masikani, ni nini mwajadilini?
Mtoto Judi jamani, sisi watutakiani?
Ndoa hiyo ya mwakani, nani yuko bahatini?
Ninakutakia heri, Ndoa uivumilie.
Ndoa uivumilie, Ni kama wenda vitani,
yakikukumba silie, yatulize kwa makini,
Ndoa uishikilie, usiyumbe asilani.
Ninakutakia heri, ndoa ni kubwa daraja.
Talaka ikikukuta, Kwa babu uje moyoni,
Babu haweki ukuta, ila tufanye sirini,
Hakika hautajuta, babu kikuweka ndani,
Kwa babu wakaribishwa, Ndoayo kisambaratika
Big Braza ODM Asprin.
judith best angu,naomba uwe wifi angu
nakukaribisha uje kwetu,uongeze idadi yetu
uwe mama wa wanetu,hilo kwetu tashukuru.
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
tumezaliwa watatu,mimi na kaka zangu,
wamenipa kazi tatu,kuwachagulia wa kudumu
asiwe sistaduu,wala wa kupiga vibomu
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
sifa za nimpendae,wa kuja kua wifi angu
awe na dini yake,inayomwabudu mungu
asiwe na dunia yake,inayopenda majungu
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
kama ubeti wa tano,sifa zake zimo
njoo kwa maringo,hadi kwa mzee timo
tutachinja majogoo,kukukaribisha nditto
nakuomba judith uje kabla ya dedilaini.
kaka zangu mapacha,wote mahendisamu,
wanafanya kazi moja,makazi darisalamu
wakisafiri wiki moja,kurudi haraka muhimu
nakuomba judit uje kabla ya dedilaini
mimi si wifi mtata,nimefunzwa mila zetu
wifi angu tampenda,uwe kama ndugu yetu
mana sina hata dada,wewe takua best angu.
nakuomba judit,uje kabla ya dedilaini.
judith best angu,naomba uwe wifi angu
nakukaribisha uje kwetu,uongeze idadi yetu
uwe mama wa wanetu,hilo kwetu tashukuru.
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
tumezaliwa watatu,mimi na kaka zangu,
wamenipa kazi tatu,kuwachagulia wa kudumu
asiwe sistaduu,wala wa kupiga vibomu
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
sifa za nimpendae,wa kuja kua wifi angu
awe na dini yake,inayomwabudu mungu
asiwe na dunia yake,inayopenda majungu
nakuomba judith,uje kabla ya dedilaini.
kama ubeti wa tano,sifa zake zimo
njoo kwa maringo,hadi kwa mzee timo
tutachinja majogoo,kukukaribisha nditto
nakuomba judith uje kabla ya dedilaini.
kaka zangu mapacha,wote mahendisamu,
wanafanya kazi moja,makazi darisalamu
wakisafiri wiki moja,kurudi haraka muhimu
nakuomba judit uje kabla ya dedilaini
mimi si wifi mtata,nimefunzwa mila zetu
wifi angu tampenda,uwe kama ndugu yetu
mana sina hata dada,wewe takua best angu.
nakuomba judit,uje kabla ya dedilaini.
haloooo haloooooooooooooo!!!!!!!!....haloooooooo ya babuuuu....kulea WAJUKUUU!!!!!!!!
birungi nakujilia, kicheko mefungulia,
ombilo nafikiria, kakazo wasaidia,
kama tamthilia, akili yanigomea,
mimi bado kuijua, mbeleko ya kubebea
kakazo wako wawili, mie mdada mmoja,
yangu dhaifu misuli, yatosha mume mmoja,
katu sidhani bahili, wote takuwa kioja,
mimi bado kuijua, mbeleko ya kubebea
hakika u mkarimu, kwenu wanikaribisha,
mie sinayo laumu, upendo menionesha,
wahidi hata karamu, wifiyo mkaribisha,
mimi bado kuijua, mbeleko ya kubebea
huo ubeti wa tano, hakika yote yakini,
lau upate maono, hima taleta kidani,
utamaliza vinono, Judi kumleta ndani,
mimi bado kuijua, mbeleko ya kubebea
sasa nakupa shauri, kama mmoja ni radhi,
huyo alete mahari, pia apime maradhi,
nae mwenyewe akiri, kama ataka nihodhi
mimi bado kuijua, mbeleko ya kubebea
Na wewe Jeneresheni, uzibe waniwekea?
Mwenzio niko kazini, mbona unanibania,
Naitimiza zangu fani, wewe waniharibia?
Undugu undugu gani, Nguguyo wambania?
Wengine mechakachua, shangazi mmewaita,
Kisa kuniharibia, Au mnataka vita?
Wengine nakuachia, Da Judi hutampata,
Undugu undugu gani, Nguguyo wambania?
Miss all the bets.
Mh kwenye vina kati na mwisho cmooooooooo!
Ila kuna beti ya majibu mstarri wa mwisho nahisi umechanganya beti ya tisa badala ya beti ya sits! Nimehisi tu, kama haina makosa bac cjaielewa.
Na wewe Jeneresheni, uzibe waniwekea?
Mwenzio niko kazini, mbona unanibania,
Naitimiza zangu fani, wewe waniharibia?
Undugu undugu gani, Nguguyo wambania?
Wengine mechakachua, shangazi mmewaita,
Kisa kuniharibia, Au mnataka vita?
Wengine nakuachia, Da Judi hutampata,
Undugu undugu gani, Nguguyo wambania?