Deal Done: Harry Maguire atua rasmi Manchester United

Deal Done: Harry Maguire atua rasmi Manchester United

Napoli walikataa. Man u hawakuwa na jinsi
Man united wangemchukua coulibaly wa napol ndo angewazima watu mdomo yule ndo beki kisiki kwelkwel kaka ila huyo Maguire Hana tofauti kubwa na kina mustafi,Phil jones,Smalling na ungechanganya na Hilo dau yaani hapo man u kapigwa kweupe.
 
Hatimaye Manchester United na Leicester City wamekubaliana dau la Pauni 80 milioni kwa beki wa kati Harry Maguire.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kufanyiwa vipimo pale Manchester United wikiendi hii.
Anakuwa mchezaji wa tatu kusainiwa katika klabu ya Manchester United katika dirisha hili, wengine wakiwa ni Aaron Wan-Bissaka na Daniel James ambao walitua wakitokea Crystal Palace na Swansea kwa mfuatano huo.
Tangu amejiunga na Leicester City akitokea Hull City mwaka 2017, Maguire amecheza mechi 69.
Usajili huo unamaanisha kwamba Maguire amekuwa beki ghali zaidi duniani akipiku kiasi cha Pauni 75 milioni ambacho Liverpool waliilipa Southampton ili kumnasa Virgil van Dijk Januari, 2018.
United walikuwa wakimtafuta Maguire kwa muda mrefu lakini walishindwa kumnasa miezi 12 iliyopita hiyo ni kwa kuwa mchezaji huyo alikuwa na dau kubwa zaidi wakati Man United walikuwa tayari kutoa Pauni 70 milioni.
Hahhahhahahha

khaa kuna mtu alipata na nguvu ya kumuandikia #HarryMagwaya sredi 😅😅😅🙉
 
Back
Top Bottom