Deconstructing Lowassa

Deconstructing Lowassa

Kwa taarifa, sijamsafisha Lowassa kwa alichotuhumiwa au nilichokisema. Nimeainisha baadhi ya vitu vya kiutendaji ambavyo alivifanya pamoja na bugudha niliyokuwa nayo ya kuona alichokuwa akikifanya ni batili kabisa.
Naona ili tuwe salama mbele ya safari, tuandae viongozi wengine waadilifu. Huyu bwana watu wanavyomuchukulia itakuwa ngumu sana kuwa kiongozi tena TZ.Tunao watu wenye uwezo wa kuongoza. Tuanze kuachana sasa na haya majina yasiobadilika toka enzi zile na hakuna lolote linalofanyika
 
Lowasa atarudi madarakani muda si mrefu na anategemewa kuchukua uraisi hapo baadaye.

Kumbukeni Mwalimu Nyerere aliwakataa Kikwete na Lowasa kugombea nafasi hizo kubwa. Hawa jamaa kwa pamoja waliamua kung'ang'ania na kusaidiana kwa hali na mali hadi wakapata nafasi hizo kwa makubaliano ya kuachiana kiti cha uraisi. Hivyo Lowasa anajua kabisa kwamba ni lazima arudi madarakani haraka kadri iwezekanavyo ili iwe rahisi kwake kuwa raisi wa Tanzania.

Alichokuwa anafanya Lowasa katika nafasi ya uwaziri mkuu ni kukusanya pesa kwa kila namna ambazo zingemsaidia katika kampeni yake ya kwenda ikulu. Huo mradi wa Richmond ilikuwa ni moja kati ya njia za kukusanya pesa. Alikuwa ana mipango kabambe kabisa ya kuuza Bandari ili kukusanya pesa za kampeni.

Pamoja na makelele yetu yote bado Lowasa atarudi serikalini na kuchukua madaraka makubwa katika nchi hii.

Tanzania inamilikiwa na watu wachache sana na Lowasa ni moja kati yao.

Ni kweli pamoja na mapungufu yake mengi, mpende au mchukie Lowasaa ni political strategist mzuri na hapo hapo ni king maker wa hali ya juu. Wakati wa awamu ya Mkapa kipindi cha kwanza Lowassa alikuwa nje ya serikali na inasemekana alianza kuwa mwiba kwa Mkapa kwa vile alikuwa na nafasi tele alianza kuzunguka nchi nzima huko na huko akifanya kampeini za chini chini kuijiandaa na uchaguzi 2005. Mkapa alishauiriwa kumpa uwaziri ili kumpuguza makali lakini kama tulivyoona 2005 Lowasaa na kundi lake la mtandao waliibuka kidedea.

Analosema kidatu kuhusu mkakati wa kutafuta pesa za 2015 kupitia Richmond/Dowans ni kweli kabisa ndio maana wahasimu wa Lowassa kisiasa piga ua hawawezi kuruhusu Dowans kuuza mitambo yake hapo nchini. Wakati fulani Mwakyembe alifikia hatua ya kusema ni heri nchi iingie gizani kuliko kununua mitambo ya Dowans. Wanujua pesa itakayopatikana malengo yake ni nini.

Lowassa kama alivyosema Mzee Butiku juzi juzi bado anautamani urais na bado hajawahi kuvunja kambi lake toka 1995. Imagine! Richmond kama alivyosema swaiba wake JK ilikuwa ni ajali ya kisiasa hivyo kwa vyoyote vile lazima makovu yake yaponywe na kufutika kabisa ili kumueka pazuri EL katika patashika ya 2015. Binafis sioni wa kumdhibiti EL ila nguvu ya umma.
 
What kind of question is this? That you are at all able to entertain this kind of idea shows how seriously you must be underestimating the intelligence of ordinary Tanzanian people. Stop peddling this kind of nonsense and get real!

intelligence ipi takataka tupu.we kalale huko huna unachoongea hapa.mngekuwa na hiyo intelligence mngekuwa mnapigwa michanga ya macho daily
 
Kwa taarifa, sijamsafisha Lowassa kwa alichotuhumiwa au nilichokisema. Nimeainisha baadhi ya vitu vya kiutendaji ambavyo alivifanya pamoja na bugudha niliyokuwa nayo ya kuona alichokuwa akikifanya ni batili kabisa.


Sawa sawa Mchungaji,huenda hiyo bugudha ya wakati ule ilikuwa uncalled for? ndicho ninachojaribu kutafakari..kiutendaji I mean....huenda ingefaa zaidi, pamoja na tuhuma zake, tuendelee naye?
 
SHERIA / KANUNI NA TARATIBU ZILIZOVUNJWA

1. UVUNJAJI WA SHERIA MAMA YA NCHI - KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 1977
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (kama ilivyofanyiwa mabadiliko) Mbunge yeyote anatakiwa kula kiapo cha uaminifu cha kulinda na kuihifadhi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria nyingine zote za nchi . Ibara ya 68 ya Katiba hii inasema wazi kabisa kuwa ``Kila Mbunge atatakiwa kuapishwa katika kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika uchaguzi wa Spika........
Hivyo Mbunge akiapa kulinda sheria za nchi alafu Mbunge huyo akavunja sheria hizo kwa ufisadi , mtu huyo anafaa kuitwa fisadi kama umegushi vyeti vya taaluma.

Katika hili , Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inamtaka Waziri kula kiapo cha uaminifu na kulinda sheria za nchi ; hivyo Waziri yeyote anayevunja sheria za nchi kwa kugushi taaluma inampasa kujiuzulu nafasi ya uwaziri. Katika Ibara 56 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatamka wazi kuwa `` Waziri hatashika madaraka yake ila awe ameapa kwanza mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na pia kiapo kingine chochote kinachousika na utendaji wa kazi yake kitakachokuwa kwa mjibu wa sheria iliyotungwa na Bunge ``




2. UVUNJAJI WA SHERIA YA VYUO VIKUU YA MWAKA 2005.
Sheria ya Vyuo Vikuu ya mwaka 2005 yaani The Universities Act, 2005 katika sehemu 58 inasema dhahiri kuwa `` Mtu yeyote atakayefanya kosa lolote au tendo lolote ambalo ni kinyume cha sheria hii , ikiwa hakuna adhabu maalum ambayo imeelezewa katika sehemu yoyote ataadhibiwa kwa kufungwa kifungo kisichozidi miezi sita au kulipa faini ya shilingi 1,500,000 au vyote kwa pamoja.
Hivyo Mheshimiwa Mbunge au Waziri akiwa amegushi sifa za taaluma anakuwa amavunja sheria hiyo na hivyo anapaswa kujiuzulu kwa sababu si msafi tena.

3. UVUNJAJI WA SHERIA YA MAKOSA YA JINAI SURA 16 (KAMA ILIVYOFANYIWA MABADILIKO MWAKA 2002)
Sheria ya Makosa ya Jinai Sura 16 iko wazi kuhusu kosa na adhabu kwa mtu akigushi sifa za taaluma , cheti au document yoyote . Katika sehemu ya 333 Sheria hii inaanzisha kosa hilo na kuelezea adhabu yake.


4. SABABU ZA KUPINGA UFISADI WA TAALUMA.
Katika zama hizi, kila kitu kinaenda kisomi, usomi au taaluma inatumika au inamgusa kila Mtanzania katika maisha ya kila siku popote alipo.
Kwa ufupi, Kama ni mwanafunzi wa shule ya msingi au sekondari anastahili kufundishwa na mwalimu aliyefuzu ualimu. Ili mwanafunzi aitimu akiwa na maarifa ni lazima afundishwe na mtu ambaye akugushi cheti cha ualimu vinginevyo mwanafunzi atamaliza darasa la saba akiwa hajui kusoma wala kuandika
Mgonjwa ili apate tiba inayoendana na maradhi yake anastahili tabibu aliye fuzu mafunzo ya utabibu au udaktari. Kama daktari amegushi vyeti kuna uwezekano wa mgonjwa kumfanyiwa oparesheni ya kichwa badala ya mguu na mguu badala ya kichwa.
Kama mhasibu amegushi cheti kunaowezekano wa mhasibu huyo kukosea hesabu na kuliingizia taifa hasara ya mabilioni ya fedha.
Mhandisi au msanifu wa majengo kama amegushi cheti kuna uwezekano mkubwa kufanya ukandarasi na kujenga jengo likaangukia waliomo ndani wapita njia.
Vivyo hivyo mwanasheria aliyegushi cheti na kulitumikia taifa kama Mheshimiwa Hakimu au Jaji kuna uwezeko wa hakimu au Jaji huyu kukosea sheria kwa sababu ana uwelewa kidogo kuhusu sheria hizo ; hivyo haki za watu kupotea na baadaye mtuhumiwa kufungwa bila hatia au jambazi kuachiwa huru kutokana na kugushi wa vyeti aliofanya Mheshimiwa Hakimu husika.
Hivyo , kwa mifano hiyo michache sana, sisi Watanzania tuna haki na sababu ya kupinga ufisadi wa taaluma kwa nguvu zote kwa ajili ya sisi wenye na uzao wetu ujao.

Katika Toleo hili la kwanza mafisadi wa taaluma ni kama ifatavyo.
MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI
clip_image002.jpg


Ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi.
Mbunge wa Ismani kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI ni Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam.
Amekuwa Mbunge wa Ismani kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi tangu mwaka 1995 hadi leo.
Amekuwa Naibu wa Waziri wa Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Vijana tangu 1995 hadi 2000.
Amekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera) tangu 2000 hadi 2005.
Amekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba mwaka 1994 hadi 1995.
Amekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.
Ni fisadi taaluma kwa sababu amegushi sifa za taaluma kuwa ni msomi mwenye Shahada au Digrii ya Maswala ya Kimataifa na Diplomasia yaani Bachelor of Art (International Studies and Diplomacy ) wakati elimu yake ni darasa la saba na ualimu wa shule msingi. Hajawahi kuingia darasa lolote la digrii wala kufanya mtihani wowote wa digrii wala kusoma digrii yoyote, wakati wowote, katika maisha yake yote na mahali popote duniani.
Mwaka 2002 , MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI akiwa anawakilisha Tanzania nchini Namibia katika mkutano wa wabunge wa Jumuiya ya Madola , aliwasilisha taarifa za kifisadi kuhusu taaluma yake kwa kudanganya kuwa yeye ni msomi mwenye digrii ya uzamili katika maswala ya biashara na uongozi yaani Masters of Busainess Administration.
Taarifa za kweli ni kwamba baada ya kumaliza elimu ya msingi na kuishia darasa la Saba B , mwaka 1975 MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI alienda kusomea ualimu wa shule za msingi katika Chuo cha Ualimu- Tabora
Mwaka 1980 kwa siku chache alienda Iringa kujifunza maswala ya usalama wa taifa
Mwaka 1985 alienda Moscow -Urusi kujifunza Siasa kwa miezi michache
Katika taarifa hizo MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI hajawahi kusomea Digrii hiyo ya Maswala ya Kimataifa na Diplomasia yaani Bachelor of Art (International Studies and Diplomacy ) na Digrii ya uzamili - Masters in Business Administration (MBA). Katika fani yeye ni mwalimu wa shule ya msingi na ana cheti cha ualimu.
Kwa kutumia taarifa za uongo kuhusu elimu yake ameweza kuaminiwa na kupata nafasi za kisiasa. Kwa mfano taarifa zilizoko katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI ni msomi mwenye Digrii hiyo ya Maswala ya Kimataifa na Diplomasia. Pia amemdanganya Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu taaluma yake , katika taarifa zilizoko katika Document za Mheshimiwa Spika zinaonyesha MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI ni msomi kiasi hicho aliyeboboe katika maswala ya kimataifa na diplomasia wakati ni wizi mtupu .
Mwaka 2005 aliwagiribu wananchi wa Ismani kwa kusema kuwa yeye ni msomi kiasi hicho na hivyo kuwa na sifa ya ziada ambayo ilimfanya apate Ubunge kwa mteremko
Mwaka huu alipohimia Dar Es Salaam kama Mkuu wa Mkoa pia akaendeleza tabia ya kifisadi taaluma na kudai kuwa ni msomi mwenye Digrii hiyo ya Maswala ya Kimataifa na Diplomasia .
MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI kama amegushi sifa za taaluma kiasi hicho , basi amekosa sifa za ubora za kuwa Mkuu wa Mkoa - Dar es Salaam kwa sababu siyo muadilifu tena .
Amepoteza sifa za kuwa katika Kamati ya Usalama Mkoa wa Dar Es Salaam.
Amepoteza sifa za kuwa Mbunge wa Ismani.
Lakini aendelee kuwa mwanachama na mjumbe wa kamati za Chama Cha Mapinduzi kwa sababu Chama Cha Mapinduzi na ufisadi ni vitu mapacha.
MHESHIMIWA DOKTA KONGORO MAHANGA
clip_image004.jpg
MHESHIMIWA DOKTA KONGORO MAHANGA ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi
Mbunge wa Ukonga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
Ni Naibu Waziri wa Wizara ya Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana ya tangu mwaka 2008 hadi leo
MHESHIMIWA DOKTA KONGORO MAHANGA amekuwa mbunge wa Ukonga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi tangu mwaka 2000 hadi leo
Amekuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu tangu 2006 hadi 12 / 5 / 2008
MHESHIMIWA DOKTA KONGORO MAHANGA ni fisadi taaluma kwa sababu amegushi sifa za taaluma kuwa ana Digrii ya Uzamivu yaani Ph.D. wakati hajawahi kusoma digrii hiyo wakati wowote na mahali popote duniani.
Ni kweli kuwa MHESHIMIWA DOKTA KONGORO MAHANGA, mwaka 1977 hadi 1983 alisomea Uhasibu (NBAA (T)) na kupata Diploma (CPA )
Mwaka 1978 aliudhuria Mafunzo ya Kodi/Ushuru kwa mwaka mmoja katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha- IFM
Mwaka 1997 hadi 1998 alisomea Shahaada ya Uzamili (Masters Degree) katika Chuo cha Strathclyde - Uingereza

Mwaka 1998, MHESHIMIWA MAKONGORO MAHANGA akiwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala katika Shirika la Nyumba la Taifa - NHC aliwasilisha taarifa za kughushi sifa zake za taaluma na kujiita msomi kiwango cha Dokta au Daktari wa Falsafa wakati akijua kuwa U-Dokta wake ni sawa na U-Dokta wa Dokta Remmy Ongalla

Mwaka 2000 aliwasilisha taarifa kifisadi kwa Mheshimiwa Spika wa wakati huo kuwa yeye ni msomi kiwango cha Ph.D.Pia amefanya ufisadi wa taalumu mwaka 2005 kwa kujinadi kwa wapiga kura wa Jimbo la Ukonga na kuwadanganya kuwa yeye ni msomi mwenye Digrii ya Uzamivu yaani Ph.D. wakati taarifa hizo ni za kifisadi na uongo .
Taarifa zilizoko hadi sasa katika Wizara ya Maendeleo ya Miundo Mbinu zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA MAKONGORO MAHANGA mwaka 2006 , akiwa Naibu wa Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Miundo mbinu aliwasilisha taarifa za kifisadi kuhusu taaluma yake na kudanganya kuwa yeye ni msomi mwenye Digrii ya Uzamivu yaani Ph.D.
Tarehe 12 / 5 / 2008 aliwakilisha taarifa za kugushi taaluma kwenye, kama Naibu Waziri wa Wizara ya Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana kuwa yeye ni msomi mwenye Digrii ya Uzamivu yaani Ph.D. Hadi sasa, taarifa zilizoko kwenye Wizara ya Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA MAKONGORO MAHANGA anaendeleza ufisadi huo wa kujipachika sifa za taaluma hiyo ambazo hana .
Mwaka 2006 MHESHIMIWA MAKONGORO MAHANGA akiwa Mbunge wa Jimbo la Ukonga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi aliwakilisha taarifa za kifisadi kuwa yeye ni msomi mwenye shahada au digrii ya Uzumivu yaani Doctor of Philosophy, Ph.D kwenye ofisi ya Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taarifa zilizoko mezani kwa Mheshimiwa Spika na ambayo Mheshimiwa Spika anazo zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA MAKONGORO MAHANGA ni msomi mwenye Digrii ya Uzumivu yaani Doctor of Philosophy, Ph.D. Wakati hajawahi kuipata na aliyo nayo ni ya kugushi
MHESHIMIWA VICTOR MWAMBALASWA
clip_image006.jpg






MHESHIMIWA VICTOR MWAMBALASA ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi
Ni Mbunge wa Lupa – Mbeya kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
Amekuwa Mkurugenzi wa Miradi katika Kiwanda cha Sigara
MHESHIMIWA VICTOR MWAMBALASA ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Kodi yaani Tanzania Revenue Authority - TRA
MHESHIMIWA VICTOR MWAMBALASA ni fisadi taalum kwa sababu amegushi sifa za taaluma kwamba ana Digrii ya Uzamili yaani Biashara na Utawala yaani Masters of Bussiness Administration MBA wakati hajawahi kusoma digrii hiyo.
MHESHIMIWA VICTOR MWAMBALASA alisoma katika Shule ya Msingi Chalangwa kati ya mwaka 1962 hadi 1968 . Alimaliza kidato cha nne 1972 katika shule ya Sekondari ya Kantalamba .
Na mwaka 1974 alihitimu kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Mkwawa – Iringa.
Mwaka 1979 alipapta Digrii ya kuotesha mimea yaani BSc.(Statistics & Botany) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam
Amefanya ufisadi wa taaluma kwa kumdanganya Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taarifa katika Ofisi ya Mh Spika na ambayo Mheshimiwa Spika anazo zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA VICTOR MWAMBALASWA ni msomi mwenye Digrii ya Uzamili katika maswala ya Biashara na Utawala yaani Masters of Business Administration- MBA
Katika taarifa zilizoko katika ofisi za TRA, MHESHIMIWA VICTOR MWAMBALASWA, kama Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Kodi yaani Tanzania Revenue Authority - TRA , zinaonyesha kuwa ni mtaalamu wa maswala ya Biashara na Utawala kwa kuwa na masters degree wakati ni wizi mtupu , yaani sifa hizo za elimu hajawahi kuzipata






























MHESHIMIWA DOKTA MARY NAGU
clip_image008.jpg
MHESHIMIWA MARY NAGU ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi
Mbunge wa Hanang kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
Ni Waziri wa Wizara ya Viwanda , Biashara na Masoko tangu 13/ 2008 hadi leo
MHESHIMIWA MARY NAGU amekuwa Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba mwaka 2006 hadi 2008

MHESHIMIWA MARY NAGU ni fisadi taaluma kwa sababu amegushi sifa za taaluma na kujiwasilisha kwamba ana Digrii ya Udaktari wa Falisafa yaani Doctor of Philosophy wakati hajawahi kusomea udaktari wowote wakati wowote na mahali popote, yeye amesoma na kuishia digrii ya pili yaani Masters Digree . Kwa kutumia digrii hiyo ya kujipa ameweza kuaminiwa na kupewa nafasi za kisiasa na kiutawala wakati ni ufisadi mtupu . Katika maisha yake hajawahi kusomea udaktari wa aina yoyote .
Katika taaluma , MHESHIMIWA MARY NAGU alisoma Shule ya Msingi ya Katesh – Endasak kati ya mwaka 1960 – 1963 , mwaka 1964- 1966 alisoma katika Shule ya Msingi Nangwa na alipata elimu ya kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Weruweru kati ya mwaka 1967- 1970 . Alisoma kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Kilakala kati ya mwaka 1971 hadi 1972 ,
Mwaka 1973 alijiunga na Chuo Kikuu Dar es Salaam - UDSM , na mwaka 1976 alipata Shahada ya Kwanza katika Uchumi .Pia mwaka 1984 alipata Shahada ya Uzamiri katika Uchumi. Hajawahi kusomea udaktari wowote ule .




MHESHIMIWA OMAR SHAABAN KWAANGW`.
clip_image010.jpg

Ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi
Mbunge wa Babati Mashariki kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
Amekuwa Mbunge Babati Mashariki kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi tangu mwaka1995
Ni mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge - Uduma za Jamii
Ni fisadi taalum kwa sababu amegushi sifa za taaluma, kwamba ana digrii ya ualimu yaani Bachelor of Art with Education (B A (Ed)) na kutumia taaluma hiyo kupata nafasi za kisiasa wakati digrii hiyo hana na hajawahi kusoma digrrii yoyote , wakati wowote na mahali popote duniani .
Ukweli ni kwamba MHESHIMIWA OMAR SHAABAN KWAANG alisomea katika Shule ya Msingi ya Maisaka 1961 hadi 1965 na mwaka 1966 hadi 1968 alisomea katika Shule ya Msingi ya Gendi. Alipata elimu ya kidato cha nne 1972 katika Shule ya Sekondari ya Ilboru iliyoko Arusha .
Mwaka 1973 hadi 1975 aliudhuria mafunzo ya kilimo katika Chuo cha Kilimo Ukiruguru kilichopo Misungwi - Mwanza na kupata cheti cha kilimo .
Mwaka 1975 mpaka1978 aliudhuria mafunzo ya ualimu katika Chuo cha Ualimu Mpwapwa – Dodoma na hivyo kufuzu kuwa mwalimu wa Shule za Sekondari
MHESHIMIWA OMAR KWAANG` akiwa amesoma hadi kuishia hapo, mwaka 2004 akiwa Mbunge wa Babati Mashariki kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi aliwakilisha taarifa za kugushi na za kifisadi kuhusu taaluma yake ,kwenye ofisi ya Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taarifa katika Ofisi ya Mheshimiwa Spika zinaonyesha kuwa mwaka 2004, MHESHIMIWA OMAR SHAABAN KWAANG aliwasilisha taarifa za kifisadi kuwa ni msomi mwenye Digrii ya Ualimu yaani Bachelor of Art with Education (B A (Ed)) wakati ni uongo
Isitoshe, tarehe 3/1 / 2006 MHESHIMIWA OMAR SHAABAN KWAANG alirudia ufisadi wa taaluma kwa kuwasilisha taarifa za kugushi taaluma katika ofisi za Mheshimiwa Spika kwamba yeye ni msomi kiasi hicho . Amemdanganya Mheshimiwa Spika kuwa yeye ni msomi mwenye degrii hiyo. Kwa mjibu wa documents zilizoko katika ofisi ya Mheshimiwa Spika na ambazo Mheshimiwa Spika anazo, zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA OMAR SHAABAN KWAANG ni msomi wa kiwango hicho , wakati hajawahii kupata digrii ya aina yoyote katika maisha yake
Na mwaka 2005 alikuwa amejinadi kwa wapiga kura wa Babati Mashariki kwa kudai kuwa ni msomi mwenye elimu kiasi hicho na kujipatia kura kwa kuwadanganya wananchi kwa kutumia sifa ya elimu kama ziada .
MHESHIMIWA DOKTA EMMANUEL NCHIMBI
clip_image012.jpg
clip_image014.jpg
MHESHIMIWA DOKTA EMMANUEL NCHIMBI ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi.
Mbunge wa Songea Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
Ni Naibu Waziri Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
MHESHIMIWA DOKTA EMMANUEL NCHIMBI Amekuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Amekuwa Mweyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi.
MHESHIMIWA DOKTA EMMANUEL NCHIMBI ni fisadi taaluma kwa sababu amegushi sifa za taaluma na kujifanya kuwa ana Digrii ya Uzamivu yaani Ph.D. Hivyo kujipa sifa za udaktari wakati udaktari wake ni sawa na wa waganga wa kienyeji, ni udaktari wa kugushi, ni wa kifisadi na wakujipachika. Udaktari wake ni sawa U-Profesa wa Profesa Maji Marefu
Kuhusu taaluma yake , alisoma katika Shule ya Msingi Oysterbay mwaka 1980 - 1986
MHESHIMIWA DOKTA EMMANUEL NCHIMBI alisoma kidato cha kwanza na pili mwaka 1987 mpaka 1988 katika
Seminari ya Uru iliyoko Kilimanjaro na alimaliza kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Sangu.
Alipata elimu ya kidato cha sita 1993 katika Shule ya Sekondari ya Forest Hill.
Mwaka 1997 alipata Stashada Utawala kutoka katika Taasisi ya Maendeleo na Utawala - Mzumbe (IDM - Mzumbe).
Alipata shahada ya Uzumili kutoka katika Chuo Kikuu Mzumbe mwaka 2003.
Katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya wa Bunda taarifa zinaonyesha kuwa Mwaka 2004 MHESHIMIWA EMMANUEL NCHIMBI akiwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda aliamka na kujipa digrii ya udaktari wa Falisafa yaani Ph.D. (Management).

Kwenye Wizara ya Habari , Utamaduni na Michezo , MHESHIMIWA EMMANUEL NCHIMBI akiwa ni Naibu Waziri , tarehe 2 / 1 / 2006 alidanganya Wizara kwa kujitambulisha kuwa yeye ni Mwanazuoni mwenye udaktari wa falisafa yaan PhD
MHESHIMIWA DOKTA EMMANUEL NCHIMBI Kama Naibu Waziri , alipohamia katika Wizara ya Kazi , Ajira na Maendeleo ya Vijana aliendeleza ufisadi wake wa taaluma na alidanganya Wizara kwa kujitambulisha kuwa yeye ni Daktari wa falisafa yaan PhD
Tarehe 13/ 2 / 2008 alipohamia katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa aliendeleza ufisadi wa taaluma kwa kudai kuwa yeye msomi mwenye Digrii ya udaktari wakati ni wizi mtupu . Ameifisidi Ofisi ya Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumpatia taarifa za kugushi taaluma yake. Nukuu kwenye Documents za Mheshimiwa Spika zinaonyesha MHESHIMIWA DOKTA EMMANUEL NCHIMBI ni dokta wakati hajawahi kusomea udaktari wowote katika maisha yake na udaktari wake ni sawa na DECI
Kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu – Kitengo cha TAMISEMI kuna habari kuwa MHESHIMIWA EMMANUEL NCHIMBI , Mwaka 2004 aliidanganya Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa yeye ni daktari wa falisafa
Katika Uchaguzi wa ubunge mwaka 2005 MHESHIMIWA EMMANUEL NCHIMBI , aliwagiribu wananchi wa Songea Mjini kwa kuwadanganya kuwa yeye ni msomi mwenye digrii ya udaktari wakati hajawahi kusoma digrii yoyote ya Udaktari . Ufisadi huu wa taaluma ulimfanya ashinde ubunge kwa kishindo.
MHESHIMIWA DOKTA RAPHAEL CHEGENI
clip_image016.jpg

MHESHIMIWA DOKTA RAPHAEL CHEGENI ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi.
Mbunge wa Busega kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
Amekuwa Mbunge wa Busega kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi tangu mwaka 2001 hadi leo.
MHESHIMIWA DOKTA RAPHAEL CHEGENI ni mjumbe wa Chama Cha Wabunge yaani Parliamentary Global for Action - PGA tangu 2004 mpaka leo.
Ni mwakilishi wa Afrika Mashariki katika Mtandao wa Wabunge katika maswala ya Benki ya Dunia yaani Parliamentary Network of the World Bank, East Africa Chapter Representative tangu 2003 mpaka leo.
MHESHIMIWA DOKTA RAPHAEL CHEGENI ni mjumbe wa Bodi ya Kidunia ya Chama Cha Wabunge Duniani katika Kuzuia na Kupokonya Silaha za Nyuklia yaani Parliamentarians for Nuclear Non-proliferation and Disarmament (PNND) tangu 2002 mpaka leo.
Amekuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Wabunge Eneo la Maziwa Makuu katika Kuleta Amani yaani General Secretary -The Great Lakes Region Parliamentary Forum , Amani Forum 2001 – 2005.
Ni mwenyekiti wa Shirika lisilo la Kiserikali la The Community Development and Relief Agency (CODRA)la Mkoani Mwanza tangu 2001 hadi leo.
Ni mkurugenzi wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umma la Consolidated Holding Corporation -CHC ( zamani ikijulikana kama NBC Holding Corporation).
MHESHIMIWA DOKTA RAPHAEL CHEGENI ni fisadi taaluma kwa sababu amegushi sifa za taaluma na kujiwasilisha kwamba ana Digrii ya Uzamivu yaani Ph.D. Na hivyo kujifanya Dokta wakati hajawahi kusoma digrii yoyote ya Udaktari au Uzamivu , wakati wowote na mahali popote duniani na vyeti alivyonavyo kuhusu elimu hiyo nivya kugushi
Katika nyazifa zilizotajwa hapo juu, MHESHIMIWA DOKTA RAPHAEL CHEGENI amewadanganya wahusika kuwa yeye ni DOKTARI wa Falisafa , na kutumia uongo huo akaweza kujipatia nafasi za kazi na uwakilishi katika Jumuiya za Kimataifa.
Kuhusu taaluma yake ni kwamba mwaka 1972 hadi 1978 alipata elimu ya Msingi katika Shule ya Msingi Mkula iliyoko Magu – Mwanza.
Alipata elimu ya sekondari katika Seminari ya Nyegezi - Mwanza kati ya mwaka 1979 – 1982. Pia alisoma kidato cha tano na sita katika Seminari hiyo kati ya mwaka 1983 hadi 1985.
MHESHIMIWA RAPHAEL CHEGENI alisoma uhasibu katika Bodi ya Uhasibu hapa Dar Es Salaam kati ya mwaka 1986 mpaka 1990 na mwaka 1995 alienda Uholanzi katika Chuo cha Laiden na kusomea stashahada ya Juu (Post Graduate Dipoloma ) katika usimamizi wa fedha . Mwaka 1996 hadi mwaka 1997 alikuwa Uingereza kuchukua shahada ya pili ( Maters in Finance ) katika usimamizi wa fedha.
Kwa kuwa MHESHIMIWA RAPHAEL CHEGENI ni mwakilishi wa Afrika Mashariki katika Mtandao wa Wabunge katika maswala ya Benki ya Dunia yaani Parliamentary Network of the World Bank, East Africa Chapter Representative mwaka 2003 aliwasilisha taarifa za ufisadi kuhusu taaluma yake kuwa ana digrii ya Uzamivu ya PhD.
Kama mjumbe wa Bodi ya Kidunia ya Chama Cha Wabunge Duniani katika Kuzuia na Kupokonya Siraha za Nyuklia yaani Parliamentarians for Nuclear Non-proliferation and Disarmament (PNND) mwaka 200X alidanganya na kuifisadi taasisi hiyo kuwa yeyeni msomi mwenye digrii ya Uzamivu ya PhD.
Na baadaye kama Katibu Mkuu wa Chama Cha Wabunge Eneo la Maziwa Makuu katika kuleta amani yaani General Secretary -The Great Lakes Region Parliamentary Forum , Amani Forum, MHESHIMIWA RAPHAEL CHEGENI mwaka 2004 alifanya ufisadi wa taaluma kwa kuidanganya Taasisi hiyo kuwa ana digrii ya Uzamivu ya PhD .
Isitoshe mwaka 2003 aliwasilisha taarifa za kifisadi kwenye ofisi za Mhe Spika wa wakati huo kuwa yeye ni msomi mwenye digrii ya Uzamivu ya PhD.
Mwaka 2006, kutokana taarifa zilizoko katika ofisi ya Mhe. Spika , MHESHIMIWA RAPHAEL MASUNGA CHEGENI aliwakilisha taarifa za kifisadi kuwa yeye ni msomi mwenye digrii ya Uzumivu yaani Doctor of Philosophy, Ph.D kwenye ofisi ya Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taarifa zilizoko mezani kwa Mhe Spika na ambayo Mhe. Spika anazo zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA RAPHAEL CHEGENI ni msomi mwenye Digrii ya Uzumivu yaani Doctor of Philosophy, Ph.D. Kitu ambacho ni uongo, ufisadi na ulaghai.
Katika Shirika la Umma la Consolidated Holding Corporation -CHC ( zamani ikijulikana kama NBC Holding Corporation) MHESHIMIWA RAPHAEL MASUNGA CHEGENI aliwakilisha taarifa za kifisadi kuwa yeye ni msomi mwenye digrii ya Uzumivu yaani Doctor of Philosophy, Ph.D wakati hajawahi kusomea udaktari wa aina yoyote.
Tena amefanya ufisadi wa taaluma kwa kudanganya Shirika lisilo la kiserikali la The Community Development and Relief Agency (CODRA) kuwa yeye ni Daktari wa Falisafa na kupata sifa ya ziada na kuaminiwa kupewa uwenyekiti wa Shirika hilo.



MHESHIMIWA DOKTA DAVID MATHAYO
clip_image018.jpg






Ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi.
MHESHIMIWA DOKTA DAVID MATHAYO ni Mbunge wa Same Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi tangu 2005.
Ni Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.
MHESHIMIWA DOKTA DAVID MATHAYO amekuwa Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko.
MHESHIMIWA DOKTA DAVID MATHAYO ni fisadi wa taaluma kwa sababu amegushi sifa za taaluma kwamba ana Stashahada ya Juu katika Maswala ya Mausiano ya Kimataifa ( Post Graduate Diploma in International Relations )wakati hajawahi kusoma stashahada ua Diploma hiyo wakati wowote na mahali popote .
MHESHIMIWA DOKTA DAVID MATHAYO alisoma katika Shule ya Msingi Marindi kati ya mwaka 1978 mpaka 1984 , alimaliza elimu ya kidato cha nne mwaka 1988 katika Shule ya Sekondaeri Galanos na mwaka 1991 na alimaliza kidato sita katika Shule ya Sekondari ya Tosamaganga .
Baada ya hapo alisomea katika Chuo Kikuu cha Sokoine na kupata udaktari wa mifugo ikiwa ni mwaka 1997
Baadaye alisomea katika Chuo Kikuu cha Free States Africa ya Kusini na kupata PhD (Agriculture)



MHESHIMIWA MUSTAFA MKULO
clip_image020.jpg
clip_image022.jpg





MHESHIMIWA MUSTAFA MKULO ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi.
Mbunge wa Kilosa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
Ni Waziri wa Mipango na Fedha tangu mwaka 2008 hadi leo
MHESHIMIWA MUSTAFA MKULO amekuwa Naibu Waziri wa Fedha mwaka 2006 hadi 2008.
Amekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa NSSF kati ya mwaka 1987 mpaka mwaka 2000.
Amekuwa Mkurugenzi wa Operesheni katika Shirika la Maendeleo la Taifa.
Amekuwa Mkurugenzi wa Mipango na Fedha katika Shirika la Maendeleo la Taifa.
Amekuwa Msajiri wa Hazina - Wizara ya Fedha.
MHESHIMIWA MUSTAFA MKULO ni fisadi taaluma kwa sababu amegushi sifa za taaluma kwamba ana Digrii ya Uzamili yaani yaani Masters of Business Administration wakati hajawahi kusoma digrii hiyo wakati wowote na mahali popote duniani.
Ni kweli kuwa MHESHIMIWA MUSTAFA MKULO alisoma Shule ya Msingi Rudewa kati ya mwaka 1956 mpaka 1960 na mwaka 1961 mpaka 1964 alisoma katika shule ya msingi Zombo na kumaliza Middle School 1965 mpaka 1968 alisomea elimu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Pugu.

Mwaka 1971 mpaka 1973 alisomea Nairobi na kupata cheti cha ACCA yaani Association of Chartered Certified Accountants.
Mwaka 1975 mpaka 1977 alienda London na kusomea Uhasibu - ACCA (Association of Chartered Certified Accountants)
Mwaka 1982 alisoma katika Bodi ya Uhasibu na kupata Cheti yaani CPA.

Amefanya ufisadi wa taaluma kwa kudanganya kuwa yeye ni msomi mwenye shahada au digrii uzamili katika maswala Biashara na Utawala yaani Masters of Bussiness Administration MBA.

Kwa taarifa zilizopo katika Wizara ya Fedha zinaonyesha kuwa 3/1/2006 akiwa Naibu Waziri wa Fedha aliwasilisha taarifa za kifisadi kwa kugushi sifa za taalum kwamba yeye ni msomi mwenye digrii ya uzamili katika maswala ya Biashara na Utawala yaani Masters of Business Administration MBA.

Na katika taarifa zilizopo katika Wizara ya Mipango na Fedha na Uchumi zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA MKULO amendeleza ufisadi wa taaluma kwa kudai kuwa ni msomi mwenye digrii hiyo ya Uzamili katika maswala Biashara na Utawala hadi leo.

Pia amefanya ufisadi wa taaluma kwa kujipatia sifa za taalum kwa kumdanganya Mh. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwenye ofisi ya Mheshimiwa Spika taarifa ambayo Mh Spika anazo zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA MUSTAFA MKULO ni msomi mwenye Digrii ya Uzamili katika maswala ya Biashara na Utawala yaani Masters of Business Administration - MBA wakati hajawahi kuisomea katika maisha yake.

Mwaka 2005 aliwadanganya wananchi wa Kilosa , ili wampe kura, kuwa ni msomi mwenye elimu kiwango hicho. Ni hicho kigezo cha ziada kilicho mfanya apate ushindi katika uchaguzi wa mwaka 2005.


MHESHIMIWA DOKTA DIODORUS KAMALA
clip_image024.jpg

Ni mwanachama Chama Cha Mapinduzi
Mbunge wa Nkenge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
MHESHIMIWA DOKTA DIODORUS KAMALA ni Waziri wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki tangu 2008 hadi leo.
Amekuwa Mbunge wa Nkenge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi tangu mwaka 2000 hadi leo.
Amekuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki tangu 2006 hadi 2008
MHESHIMIWA DOKTA DIODORUS KAMALA ni fisadi taaluma kwa sababu amegushi sifa za taaluma kwamba ana Digrii ya Uzamivu yaani Ph.D wakati hajawahi kusoma digrii hiyo, wakati wowote na mahali popote duniani .
Kwa taarifa zilizopo ni kwamba MHESHIMIWA DIODORUS KAMALA kati ya mwaka 1978 hadi 1982 alisomea katika Shule ya Msingi Mugana B iliyoko katika kata ya Muguna Bukoba vijijini.
Na mwaka 1982 hadi 1984 alisomea katika Shule ya Msingi Rumuli iliyoko Kata ya Kashai - Bukoba Mjini.
Mwaka 1988 alihitimu kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Bukoba na mwaka 1991 aliitimu kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Ihungo iliyoko Kata ya Nshambya katika Wilaya ya Bukoba.
Kati ya mwaka 1992 hadi 1995 alisoma IDM–Mzumbe na kupata Stashada ya Mipango ya Kiuchumi.
Mwaka 1996 mpaka 1997 alisomea shahada ya Uzamili kwenye maswala ya mifumo ya kiutawala katika Chuo Kikuu cha Lincoln kilichopo Uingereza.
Baadaye, mwaka 1997 hadi1998 alisomea Shahada ya Uzamili kwenye maswala ya maendeleo ya kilimo na fedha yaani Agricaltural Development and Rural Finance kutoka Chuo kikuu cha Humberside Bradford cha Uingereza.
Kwa taarifa zilizopo ni kwamba MHESHIMIWA DIODORUS KAMALA hajawahi kusomea shahaada au digrii ya Uzumivu yaani Doctor of Philosophy, PhD.
Digrii ya Uzumivu amejivika na kuitumia kupata nafasi za kazi na kisiasa. Hivyo MHESHIMIWA DIODORUS KAMALA ni fisadi elimu.

Mwaka 2004 MHESHIMIWA DIODORUS KAMALA akiwa Mbunge wa Nkenge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi aliwakilisha taarifa za kifisadi kuwa yeye ni msomi mwenye shahaada au digrii ya Uzumivu yaani Doctor of Philosophy, Ph.D kwenye ofisi ya Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taarifa katika mafaili ya Mheshimiwa Spika zinaonyesha kuwa MHESHIMIWA DIODORUS KAMALA ni msomi mwenye Digrii ya Uzumivu yaani Doctor of Philosophy, Ph.D wakati ni uongo .Sifa hizo za taaluma ni za kugushi , kifasadi , uwongo na wizi mtupu .

Kwa tabia yake ya ufisadi wa taaluma , mwaka 2005 alijiwasilisha kwa wapiga kura wa Nkege kuwa yeye ni mwanazuoni aliyebobea hadi kiwango cha Ph.D. hivyo akaaminiwa na kuchaguliwa kugombea ubunge bila kupingwa na mgombea kutoka katika chama chochote cha siasa katika Jimbo la Nkenge .

Tena taarifa zilizoko katika Wizara ya Ushirkiano wa Afrika Mashariki , MHESHIMIWA DIODORUS KAMALA akiwa Naibu Waziri wa Wizara ya Ushirkiano wa Afrika Mashariki mwaka 2006 aliwasilisha taarifa za kifisadi kwenye Wizara hiyo kuwa yeye ni mwanazuoni mwenye Ph.D.
Tarehe 15 / 2 / 2008, MHESHIMIWA DIODORUS KAMALA akiwa Waziri wa Wizara ya Ushirkiano wa Afrika Mashariki aliendelea kuwasilisha taarifa za kifisadi kwenye Wizara hiyo kuhusu taaluma yake kuwa yeye ni mwanazuoni mwenye Ph.D.
Pia MHESHIMIWA DIODORUS KAMALA alidanganya Baraza la Vijana la Afrika Mashariki kwa kudai kuwa yeye ni daktari wa falisafa wakati hajawahi kusomea udaktari wa aina yoyote. .

MWISHO WA TOLEO LA KWANZA LA MAFISADI WA ELIMU.

I AM READY FOR ANY CHALLENGE.
 

MWISHO WA TOLEO LA KWANZA LA MAFISADI WA ELIMU.

I AM READY FOR ANY CHALLENGE.

Join Date: Tue Oct 2009
Posts: 8
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0

Mmaringo, naona hii topic yako umeileta kusikohusika. Pia karibu JF naona wewe ni mgeni, jaribu kujifunza humu kwenye mambo ya kupost, JF law kabla.
 
Ninachoweza sema kwa hili ni kwamba ili tupate tanzania yenye maamuzi ya msingi na kwa maslahi ya nchi, wananchi wenyewe ndo wenye nguvu ya kuamua hilo, lakini nasikitika kwamba wananchi hatujajua nguvu tulionayo katika kufanikisha hili. Ubinafsi, usaliti na tamaa ya kupenda njia za mkato zinasababisha watu wawe warahisi kurubuniwa na kuweka kando haki na heshima zao.
Watu wataendelea kufanya watakavyo hadi hapo uvumilivu utakapowashinda wananchi na matokeo yake siyaoni kama ni mazuri.
 
Back
Top Bottom