Demokrasia iliyopo ndani ya CCM ni mfano wa kuigwa kwa vyama vyote Barani Afrika, hakuna wa kukiondoa madarakani

Demokrasia iliyopo ndani ya CCM ni mfano wa kuigwa kwa vyama vyote Barani Afrika, hakuna wa kukiondoa madarakani

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu CCM Ni Kama Maji usipoyanywa utayaoga Tu,Huwezi ukazikwepa kuzisikia habari za CCM,huwezi ukajipa upofu wa kutokuona ukubwa na mizizi ya cccm hapa nchini,huwezi ukazuia habari za CCM na ukafanikiwa,huwezi ukaishinda CCM katika medani za kisiasa,huwezi ukaibomoa CCM hata kwa nyundo,huwezi ukaisambaratisha CCM kwa mdomo wako au fedha zako au mikono yako,huwezi ukaiteka CCM na kuifanya Kama Mali yako,huwezi ukaiteka CCM na kuiweka mfukoni mwako na ikakaa na kutosha Wala huwezi ukaihifadhi CCM katika begi lako.

CCM Ni kubwa ,Ni kubwa kuliko mtu mwingine yeyote,Ni kubwa kuliko mtu binafsi,Ni kubwa kuliko jina la mtu binafsi,CCM ni Taasisi,Taasisi iliyo imara ,nguvu na ushupavu wa kiuongozi, mizizi ya CCM Ni mirefu mikubwa ,mipana na iliyokwenda mbali sana,. Hakuna taasisis au eneo ambako hutaikuta CCM na Wana CCM,kila mahali lazima uikute CCM,lazima uione CCM,lazima uone sauti,ishara na matawi ya CCM, Ni CCM kila mahali ,Ni ccm kila eneo,Ni CCM kila uendako lazima uikute CCM na kukutana na nguvu ya CCM.

Huwezi ukaitisha Wala kuiyumbisha Wala kuikoromea CCM,.Hakuna mtu mwenye uwezo huo ,hayupo na Wala bado hajazaliwa.ukiondoka CCM kwa mbwembwe utarudi CCM kwa magoti na majuto ya kuondoka. Hakuna anayeweza kuondoka ndani ya CCM na akaiishi kwa amani uhamishoni,lazima aikumbuke CCM maana ndani ya CCM Kuna demokrasia ya kutosha na upendo wa kutosha

Hakuna ubaguzi Wala kubaguana ndani ya CCM,Hakuna udini Wala ukabila Wala ukanda ndani ya CCM,bali ndani ya CCM Kuna watu wa Dini zote,makabila yote na Kanda zote na wote wanaishi kwa amani upendo ushirikiano na mshikamano. Ndani ya CCM yeyote anaweza kuwa kiongozi wa ngazi yoyote Ile bila kujari familia aliyotokea kiuchumi. Ndani ya CCM wanachama wote Wana nafasi sawa,

Kinachokubeba kiuongozi na kuwa kiongozi ndani ya CCM ni Sera zako,sifa zako kiuongozi katika kumudu majukumu ya uongozi, kukubalika kwako na ushawishi wako kwa wanachama wenzako na mengine Kama hayo. Ndani ya CCM mfuko wako wa fedha siyo tiketi ya kupewa uongozi maana unaweza ukatoa fedha na ukanyimwa Kura.

Hakika vyama vingine Barani Afrika vina kila sababu ya kujifunza demokrasia Iliyopo Ndani ya CCM katika kuendesha mambo yake na kushughulikia migogoro ya wanachama wake. Vyama vya upinzani viache kujiendesha Kama vikundi vya watu binafsi kwa maslahi ya familia zao,visijiendshe Kama miradi ya kujipatia vipato binafsi,vsiwe Kama vitega uchumi vya watu kwa maslahi Binafsi.

Hakuna wakuitoa CCM madarakani,Hakuna chama Wala mtu mwenye ubavu huo,hayupo na Wala hajazaliwa bado. Hakuna chama chenye Sera na ajenda zenye kugusa maisha ya watanzania Kama ilivyo kwa CCM,ndio maana vyama vingine vinapuuzwa na kudharaulika Sana, huku CCM ikiendelea kukubalika na kuungwa mkono na mamillion ya watanzania kutokana na umadhubuti na ushupavu wake kiuongozi na kimfumo ulio imara na Thabiti.

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa , kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627
 
Hoja inajibiwa na hoja iliyo bora zaidi, kujiamini kote huko kwa ccm, woga wao upo wapi kuhusu tume huru ya uchaguzi ili tupate uchaguzi huru?,why vyombo vya dola havifanyi kazi kutegemeana na viapo vyao?

Sio kazi ya Tiss kuwachagulia viongozi ccm, kazi ya tiss ni kuhakikisha nchi yetu ipo salama, wewe unaona ni vema police kumwagwa Dodoma kulinda kikao cha ccm na hawafanyi hivyo kwa vyama vingine, hivi kabisa deep in your heart unaona uchaguzi wa 2020 ulikua wa haki?

Hii nchi sio ya CCM ni ya watanzania wote wenye itikadi tofauti, vyama vingine virus usiwe navyo kufanya shughuli zake kwa uhuru
 
Hoja inajibiwa na hoja iliyo bora zaidi, kujiamini kote huko kwa ccm, woga wao upo wapi kuhusu tume huru ya uchaguzi ili tupate uchaguzi huru?,why vyombo vya dola havifanyi kazi kutegemeana na viapo vyao?,sio kazi ya Tiss kuwachagulia viongozi ccm, kazi ya tiss ni kuhakikisha nchi yetu ipo salama, wewe unaona ni vema police kumwagwa Dodoma kulinda kikao cha ccm na hawafanyi hivyo kwa vyama vingine, hivi kabisa deep in your heart unaona uchaguzi wa 2020 ulikua wa haki?,hii nchi sio ya ccm ni ya watanzania wote wenye itikadi tofauti, vyama vingine virus usiwe navyo kufanya shughuli zake kwa uhuru
Kazi ya polisi Ni kulinda usalama,kwa hiyo hata wewe na chama chenu mkiwa na vikao toeni Taarifa polisi kuomba ulinzi na mtapewa bila shida yoyote ile
 
Mleta mada sidhani kama unajua kilnachoendelea ndani ya ccm!
CCM hakuna demokrasia unayofikiria wewe!
Jiulize ni nani wanaohesabu zile kura ndani ya vyumba vya kuhesabia kura kule ukumbini!
Kumbuka hata kuchukua fomu ni kwa maelekezo ya 'mkuu' na sio kwa uhuru!
Kumbuka hata "safu" imeshapangwa tayari tena kwa majina na kura!
 
Mleta mada sidhani kama unajua kilnachoendelea ndani ya ccm!
CCM hakuna demokrasia unayofikiria wewe!
Jiulize ni nani wanaohesabu zile kura ndani ya vyumba vya kuhesabia kura kule ukumbini!
Kumbuka hata kuchukua fomu ni kwa maelekezo ya 'mkuu' na sio kwa uhuru!
Kumbuka hata "safu" imeshapangwa tayari tena kwa majina na kura!
Ulishawahi kugombea uongozi ndani ya CCM? Uliona mfumo uliotumika kuhesabu kura za maoni za ubunge ndani ya CCM mwaka 2020? Hukuona uhesabuji ulikuwa wa wazi na kila mtu alilidhika? Hata huu Naamini utakuwa wa wazi na kila mtu atapata kura kulingana na ushawishi wake kwa wajumbe
 
Ulishawahi kugombea uongozi ndani ya CCM? Uliona mfumo uliotumika kuhesabu kura za maoni za ubunge ndani ya CCM mwaka 2020? Hukuona uhesabuji ulikuwa wa wazi na kila mtu alilidhika? Hata huu Naamini utakuwa wa wazi na kila mtu atapata kura kulingana na ushawishi wake kwa wajumbe
Unahangaika nae wa nini huyo? Jitu linaonekana wazi ni kichwa maji
 
Mwenyekiti hana mgombea mwenza ndo demokrasia[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kama unaona unaweza kushindana naye nenda kachukue fomu ushindane Naye uone atakavyokuburuza mpaka uishiwe pumzi,wanaccm Tumeona Mama Dr Samia suluhu Hassani anafaa Kuendelea kutuongoza na kututumikia katika nafasi ya uenyekiti katika miaka mitano mingine
 
Unahangaika nae wa nini huyo? Jitu linaonekana wazi ni kichwa maji
Mie nina akili na ni mchambuzi mzuri sana wa mambo tofauti na wewe!
Hata ulichoandika unaonyesha zaidi ya matusi huna upeo wowote kichwani nakuhakikishia!
Kama unabisha tubishane kwa hoja na uhalisia kama utaweza!
 
Lukas fanya kazi halali hapo hata moyo wako unakusuta uzalendo sio kuimba mapambio na kuwinda teuzi ili kulinda njaa yako huna uzalendo wowote zaidi ya uroho unaokusumbua
Mimi Ni mkulima na hata hapa nimetokea shambani,
 
Back
Top Bottom