Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu CCM Ni Kama Maji usipoyanywa utayaoga Tu,Huwezi ukazikwepa kuzisikia habari za CCM,huwezi ukajipa upofu wa kutokuona ukubwa na mizizi ya cccm hapa nchini,huwezi ukazuia habari za CCM na ukafanikiwa,huwezi ukaishinda CCM katika medani za kisiasa,huwezi ukaibomoa CCM hata kwa nyundo,huwezi ukaisambaratisha CCM kwa mdomo wako au fedha zako au mikono yako,huwezi ukaiteka CCM na kuifanya Kama Mali yako,huwezi ukaiteka CCM na kuiweka mfukoni mwako na ikakaa na kutosha Wala huwezi ukaihifadhi CCM katika begi lako.
CCM Ni kubwa ,Ni kubwa kuliko mtu mwingine yeyote,Ni kubwa kuliko mtu binafsi,Ni kubwa kuliko jina la mtu binafsi,CCM ni Taasisi,Taasisi iliyo imara ,nguvu na ushupavu wa kiuongozi, mizizi ya CCM Ni mirefu mikubwa ,mipana na iliyokwenda mbali sana,. Hakuna taasisis au eneo ambako hutaikuta CCM na Wana CCM,kila mahali lazima uikute CCM,lazima uione CCM,lazima uone sauti,ishara na matawi ya CCM, Ni CCM kila mahali ,Ni ccm kila eneo,Ni CCM kila uendako lazima uikute CCM na kukutana na nguvu ya CCM.
Huwezi ukaitisha Wala kuiyumbisha Wala kuikoromea CCM,.Hakuna mtu mwenye uwezo huo ,hayupo na Wala bado hajazaliwa.ukiondoka CCM kwa mbwembwe utarudi CCM kwa magoti na majuto ya kuondoka. Hakuna anayeweza kuondoka ndani ya CCM na akaiishi kwa amani uhamishoni,lazima aikumbuke CCM maana ndani ya CCM Kuna demokrasia ya kutosha na upendo wa kutosha
Hakuna ubaguzi Wala kubaguana ndani ya CCM,Hakuna udini Wala ukabila Wala ukanda ndani ya CCM,bali ndani ya CCM Kuna watu wa Dini zote,makabila yote na Kanda zote na wote wanaishi kwa amani upendo ushirikiano na mshikamano. Ndani ya CCM yeyote anaweza kuwa kiongozi wa ngazi yoyote Ile bila kujari familia aliyotokea kiuchumi. Ndani ya CCM wanachama wote Wana nafasi sawa,
Kinachokubeba kiuongozi na kuwa kiongozi ndani ya CCM ni Sera zako,sifa zako kiuongozi katika kumudu majukumu ya uongozi, kukubalika kwako na ushawishi wako kwa wanachama wenzako na mengine Kama hayo. Ndani ya CCM mfuko wako wa fedha siyo tiketi ya kupewa uongozi maana unaweza ukatoa fedha na ukanyimwa Kura.
Hakika vyama vingine Barani Afrika vina kila sababu ya kujifunza demokrasia Iliyopo Ndani ya CCM katika kuendesha mambo yake na kushughulikia migogoro ya wanachama wake. Vyama vya upinzani viache kujiendesha Kama vikundi vya watu binafsi kwa maslahi ya familia zao,visijiendshe Kama miradi ya kujipatia vipato binafsi,vsiwe Kama vitega uchumi vya watu kwa maslahi Binafsi.
Hakuna wakuitoa CCM madarakani,Hakuna chama Wala mtu mwenye ubavu huo,hayupo na Wala hajazaliwa bado. Hakuna chama chenye Sera na ajenda zenye kugusa maisha ya watanzania Kama ilivyo kwa CCM,ndio maana vyama vingine vinapuuzwa na kudharaulika Sana, huku CCM ikiendelea kukubalika na kuungwa mkono na mamillion ya watanzania kutokana na umadhubuti na ushupavu wake kiuongozi na kimfumo ulio imara na Thabiti.
Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa , kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627
CCM Ni kubwa ,Ni kubwa kuliko mtu mwingine yeyote,Ni kubwa kuliko mtu binafsi,Ni kubwa kuliko jina la mtu binafsi,CCM ni Taasisi,Taasisi iliyo imara ,nguvu na ushupavu wa kiuongozi, mizizi ya CCM Ni mirefu mikubwa ,mipana na iliyokwenda mbali sana,. Hakuna taasisis au eneo ambako hutaikuta CCM na Wana CCM,kila mahali lazima uikute CCM,lazima uione CCM,lazima uone sauti,ishara na matawi ya CCM, Ni CCM kila mahali ,Ni ccm kila eneo,Ni CCM kila uendako lazima uikute CCM na kukutana na nguvu ya CCM.
Huwezi ukaitisha Wala kuiyumbisha Wala kuikoromea CCM,.Hakuna mtu mwenye uwezo huo ,hayupo na Wala bado hajazaliwa.ukiondoka CCM kwa mbwembwe utarudi CCM kwa magoti na majuto ya kuondoka. Hakuna anayeweza kuondoka ndani ya CCM na akaiishi kwa amani uhamishoni,lazima aikumbuke CCM maana ndani ya CCM Kuna demokrasia ya kutosha na upendo wa kutosha
Hakuna ubaguzi Wala kubaguana ndani ya CCM,Hakuna udini Wala ukabila Wala ukanda ndani ya CCM,bali ndani ya CCM Kuna watu wa Dini zote,makabila yote na Kanda zote na wote wanaishi kwa amani upendo ushirikiano na mshikamano. Ndani ya CCM yeyote anaweza kuwa kiongozi wa ngazi yoyote Ile bila kujari familia aliyotokea kiuchumi. Ndani ya CCM wanachama wote Wana nafasi sawa,
Kinachokubeba kiuongozi na kuwa kiongozi ndani ya CCM ni Sera zako,sifa zako kiuongozi katika kumudu majukumu ya uongozi, kukubalika kwako na ushawishi wako kwa wanachama wenzako na mengine Kama hayo. Ndani ya CCM mfuko wako wa fedha siyo tiketi ya kupewa uongozi maana unaweza ukatoa fedha na ukanyimwa Kura.
Hakika vyama vingine Barani Afrika vina kila sababu ya kujifunza demokrasia Iliyopo Ndani ya CCM katika kuendesha mambo yake na kushughulikia migogoro ya wanachama wake. Vyama vya upinzani viache kujiendesha Kama vikundi vya watu binafsi kwa maslahi ya familia zao,visijiendshe Kama miradi ya kujipatia vipato binafsi,vsiwe Kama vitega uchumi vya watu kwa maslahi Binafsi.
Hakuna wakuitoa CCM madarakani,Hakuna chama Wala mtu mwenye ubavu huo,hayupo na Wala hajazaliwa bado. Hakuna chama chenye Sera na ajenda zenye kugusa maisha ya watanzania Kama ilivyo kwa CCM,ndio maana vyama vingine vinapuuzwa na kudharaulika Sana, huku CCM ikiendelea kukubalika na kuungwa mkono na mamillion ya watanzania kutokana na umadhubuti na ushupavu wake kiuongozi na kimfumo ulio imara na Thabiti.
Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa , kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627