Mataga watakataa🤣Basi tumuache samia atawale hadi atakapokufa baada ya hapo abdul atawale hadi atakapokufa baada ya hapo aingie mtoto abdul nadhani tutapata maendeleo kuliko marekani yenye demokrasia si ndio ndugu zangu??
We kapige kwanza mswaki
Nchi za Afrika hatuna demokrasia yenyewe tunaigiza inshort viongozi wa afrika hawataki democrasia ile yenyewe bali hii ya maigizo
Korea zote ziliendeshwa kidikteta. Moja ikawa tajiri nyingine bado. Hiyo iliyokuwa tajiri ikaamua kuwa na demokrasia. Sina mfumo ninaotaka, ninachotaka ni tukae chini na kutafuta mfumo utakaoweza kuteletea maendeleo.Haueleweki unataka mfumo gani ufalme? Hizo nchi ni ndogo sana jaribu kutuletea ufalme hapa kama utaweza!
Kwa hizo nchi tajiri za demokrasia zilizaliwa tajiri ? Mfumo mzuri ndiyo umewapa huo utajiri hata nchi za Europe hazikuwa na demokrasia.
Kuna Korea mbili tuambie ipi tajiri yenye demokrasia au isiyo nayo?
Kutokuwa na demokrasia si guarantee ya kuendelea, ila kuwa na demokrasia ni guarantee ya kutoendelea.Mbona Africa hakuna demokrasia na umasikini bado tunaongoza??
Naunga mkono asilimia mia Ccm DaimaDEMOKRASIA NA NCHI MASIKINI
Leo nakuja tena na hii mada.
Kwanza ijulikane kuwa hakuna nchi masikini imewahi endelea ikIwa chini ya demokrasia. Ukifutilia historia utaona kuwa hakuna nchi imewahi kutoka kwenye umaskini ikiwa inaongozwa kidemokrasia. Nchi zote zilizofanikiwa kutoka kwenye umaskini zimeongozwa kidikteta au kifalme.
Demokrasia ni anasa ya matajiri. Nchi masikini ikiingia kwenye demokrasia inajichimbia kaburi. Kwanza sababu ni kuwa ni gharama kubwa sana kuendesha nchi ya kidemokrasia. Nchi ya kidemokrasia ina walaji wengi sana. Msomi mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya udikteta na demokrasia ni idadi ya watu unaotakiwa kuwaridhisha ili uendelee kushika madaraka. Idadi hiyo ni kubwa sana kwenye demokrasia. Wanaridhishwa kwa kupewa vyeo vingi vilivyoundwa kwa ajili yao. Na mzigo wote wa kuwalipa na kuwagharamia unaangukia nchi ambayo ni maskini.
Serikali ya kidemokrasia haiwezi kuja na sera za maendeleo ambazo zitawataka wananchi wafunge mikanda. Kuna wakati ili nchi iendelee ni lazima watu wafunge mikanda. Mfano nchi inaweza kusema hatutaagiza ngano ila tutahakikisha tunazalisha wenyewe kiasi cha kututosha. Kwenye nchi ya kifalme au kidikteta hilo linaweza kufanyika na baada ya muda nchi ikajitosheleza kwa ngano. Kwenye nchi ya kidemokrasia ngano ikiadimika wiki tu watu watangia barabarani na kuiangusha serikali. Wapinzani watapiga kelele za ajabu. Rais mwenye maono wa Liberia aliangushwa kwa namna hii na nchi ikachukuliwa na watu wazembe kama Samuel Doe. Ukisema tukuze textile industry yetu hivyo tulinde soko letu watu watazama barabarani na kukunyofoa madarakani. Waliotuletea demokrasia walijua vema wanachokifanya.
Kwenye nchi ya kidemokrasia ajenda kuu ya mtawala ni namna ya kubaki madarakani. Maamuzi yake yote yanazingatia kutimizwa kwa ajenda hii, hata kama yapo kinyume na maslahi ya nchi. Mfalme au dikteta anakuwa yupo imara madarakani. Anaweza kuwaza namna ya kukuza uchumi na hivyo kujiongezea kipato.
Nchi kama S Korea, Singapore, Malaysia na Shelisheli zimeweza kutoka kwenye umaskini kupitia madikteta.
Nchi kama UAE, KSA na Brunei zimeweza kufanya vizuri chini ya Ufame.
Bado hakuna nchi ya kidemokrasia iliyojitoa kwenye umaskini. Kila aina ya utawala ina mapungufu yake lakini demokrasia ni mfumo wa hovyo zaidi.
Habari kubwa kwenye nchi za kidemokrasia si za maendeleo, bali habari kuhusu michakato ya kidemokrasia.
DEMOKRASIA NA NCHI ZILIZOENDELEA
Nchi iliyoendelea na inayofuata demokrasia lazima itarudi kwenye umaskini. Nchi ya kidemokrasia iliyoendelea lazima itageuka ya kisocialist. Yaani wananchi wake watakuwa wanadai huduma kutoka kwa serikali kila leo hadi serikali itashindwa kuhudumia. Wananchi watataka afya bure. Mwanasiasa atakaye waahidi hilo wanamchagua. Kesho watadai elimu bure, kesho kutwa mishahara mikubwa, ruzuku wakulima nk nk. Nchi hizi zinajikuta zina matumizi makubwa kuliko mapato. Na wakati huo huo wanachi wakiwachagua wanasiasa wanaowaahidi kodi ndogo. Mwisho zinajikuta zina madeni wasiyoyaweza na deficit(nakisi) kwenye bajeti. Kaangalie nchi zinazodaiwa madeni ya kutisha, utakuta nchi za kidemokrasia zilizoendelea hasa ndizo zinaongoza kwa madeni, wala si nchi maskini zinazotangazwa kila leo. US deni lake ni asilimia 90 ya GDP yake. UK ni kama asilimia 250 wakati China ni kama 13%.
Hili la nchi kushindwa kumudu gharama limetokea kwa Argentina na nchi nyingi zilizoendelea zinaenda muelekeo huo.
Wafanyakazi wa nchi zilizoendelea na zinazofuata demokrasia wanaunda unions, na kudai mishahara mikubwa, benefits na haki nyingi. Matokeo yake gharama za uzalishaji zinakuwa kubwa na nchi kushindwa kushindana na bidhaa za kutoka mataifa mengine kama China. Matokeo yake viwanda vinafunga.
Gharama za kujenga miundombinu kwenye nchi za kidemokrasia ni kubwa sana. China imeziacha mbali sana nchi za magharibi kwenye suala la treni ziendazo kasi. Sababu kubwa ni mchakato mgumu na gharama kubwa za kufanya hivyo kwenye nchi za kidemokrasia. Kwenye nchi za kidemokrasia ukitaka kujenga kitu utakutana na red tapes za maana. Kila kikundi kitatoa sauti zao. Wenye ardhi watagoma reli isipite kwenye mapori yao au watadai fidia za ajabu na kukupeleka mahakamani juu.
Wengi wape lakini wakati mwingine wengi hukosea vibaya sana. Suala la Brexit ni mfano wa hili. Watu wengi walipiga kura UK ijiondoe EU. Leo hii baada ya athari kubwa za Brexit waingereza wengi wanajuta na kusema kuwa suala la Brexit halikuwa sawa. Mambo ya kitaalamu hayapaswi kuendeshwa kidemokrasia.
Demokrasia haifai kwa nchi maskini. Tukae chini tutafute mfumo mwingine.
Ofcourse democarcy ina work well kwenye jamii ambazo tayari ni developed, organized, na zime staarabika.Naunga mkono title ya mada hii. Demkkrasia inafaa kwa mataifa yaliyoendelea tayari. Lakini kwetu sisi ni upotezaji wa rasilimali muda, fedha na nguvukazi
Kwa nini Korea Kusini ambayo imekuwa na utawawa wa kidemokrasia kwa kipindi kirefu cha zaidi ya nusu karne imekuwa tajiri na yenye maendeleo makubwa sana kuliko Korea Kaskazini ambayo imekuwa na utawala wa kidikteta karne zote/maisha yake yote mpaka sasa??Korea zote ziliendeshwa kidikteta. Moja ikawa tajiri nyingine bado. Hiyo iliyokuwa tajiri ikaamua kuwa na demokrasia. Sina mfumo ninaotaka, ninachotaka ni tukae chini na kutafuta mfumo utakaoweza kuteletea maendeleo.
Udikteta umefanya kazi nzuri Africa kuliko demokrasia. Nchi kama Shelisheli, Libya na Misri ni mfano wa nchi chache zilizofanya vizuri chini ya Udikteta. Kwa miaka zaidi ya 30 "kelele za kudai demokrasia" na demokrasia yenyewe haijafanya chochote kuitoa Africa kwenye umaskini...Udikteta umeshindwa kuleta maendeleo Afrika, ndio maana kumekuwepo na kelele za kudai demokrasia.
Nchi kama South Africa tunaweza kusema ina demokrasia iliyokomaa vizuri kwa miaka 30. Kilichotokea ni demokrasia hiyo kuharibu maendeleo yaliyopatikana enzi za apartheid.Kwa asilimia kubwa Africa haina demokrasia na bado inaongoza kwa umaskini na maendeleo duni.
Kutokuwepo kwa demokrasia siyo guarantee ya kuendelea, ila uwepo wa demokrasia ni guarantee ya kutoendelea.Hoja ya mleta uzi ni mfu. Africa hakuna democracy na hakuna maendeleo either.
Kutokuwepo kwa demokrasia siyo guarantee ya kuendelea, ila uwepo wa demokrasia ni guarantee ya kutoendelea.
NK ilikuwa bora kuliko SK balaah lilianza miaka mwisho wa miaka ya 80s na anguko la Soviet liliizika NK ukichanganya na vikwazo vingi alivyonavyo ndio balaah linazidi.Korea zote ziliendeshwa kidikteta. Moja ikawa tajiri nyingine bado. Hiyo iliyokuwa tajiri ikaamua kuwa na demokrasia. Sina mfumo ninaotaka, ninachotaka ni tukae chini na kutafuta mfumo utakaoweza kuteletea maendeleo.
Maendeleo ya Korea kusini yanesababishwa na udikteta wa kijeshi chini ya sheria za kijeshi kwa muda mrefu juzi tu hapa Yoon Suk Yeol alitaka kuwarudisha kule walipo pazoea tuachane na hayo.Kwa nini Korea Kusini ambayo imekuwa na utawawa wa kidemokrasia kwa kipindi kirefu cha zaidi ya nusu karne imekuwa tajiri na yenye maendeleo makubwa sana kuliko Korea Kaskazini ambayo imekuwa na utawala wa kidikteta karne zote/maisha yake yote mpaka sasa??
Korea Kaskazini hakuna maendeleo zaidi ya kutengeneza mabomu, muda mrefu tu wamekuwa wakipewa msaada wa chakula na Korea Kusini, Japan, China na Marekani. Korea Kaskazini ni tegemezi wa China.Maendeleo ya Korea kusini yanesababishwa na udikteta wa kijeshi chini ya sheria za kijeshi kwa muda mrefu juzi tu hapa Yoon Suk Yeol alitaka kuwarudisha kule walipo pazoea tuachane na hayo.
Ila Korea zote mbili maendeleo yake yamebebwa na udikteta kwa asilimia kubwa utofauti uliopo ni kati ya SK na NK ni katika vita baridi baada ya Eastern bloc kuanguka baada ya anguko la Usoviet kilicho fuatia ni anguko la NK pia toka miaka ya 80s wakati upande wa pili SK haikuathirika na anguko hilo kwa sababu haikuwa upande huo.
Baada ya hapo ni vikwazo vilifuatia kwa NK mpaka leo hivyo haishangazi SK kuwa bora kuliko NK
Unafafanisha nchi inayokabiliwa na rundo la vikwazo baada ya kuanguka kwa usoviet na hizo nchi ulizotaja upo serious kweli ?Korea Kaskazini hakuna maendeleo zaidi ya kutengeneza mabomu, muda mrefu tu wamekuwa wakipewa msaada wa chakula na Korea Kusini, Japan, China na Marekani. Korea Kaskazini ni tegemezi wa China.
Kwa nini Poland, Hungary, Romania, Bulgaria, Czech na Ukraine zilizokuwa chini ya USSR zimeweza kupata maendeleo makubwa katika demokrasia baada ya kuanguka usovieti(USSR) huku Korea Kaskazini ikashindwa kupata maendeleo chini ya udikteta wa familia ya Kim??
Chukua Pakistan, Nepal, Myanmar(Burma) na Cambodia.Unafafanisha nchi inayokabiliwa na rundo la vikwazo baada ya kuanguka kwa usoviet na hizo nchi ulizotaja upo serious kweli ?
Halafu ?Chukua Pakistan na Cambodia
Zote zimekuwa zinatawaliwa kidikteta kwa zaidi ya karne ila bado ni masikini wa kutupwa.Halafu ?