Demokrasia ni adui wa maendeleo

Demokrasia ni adui wa maendeleo

Zote zimekuwa zinatawaliwa kidikteta kwa zaidi ya karne ila bado ni masikini wa kutupwa.
Kwa nini hazijapata maendeleo??
Hizo ndizo North Korea na South Korea kwa ulicho kiandika ?

By the way sipo hapa kutetea udikteta kwa namna yoyote ile.
 
DEMOKRASIA NA NCHI MASIKINI

Leo nakuja tena na hii mada.
Kwanza ijulikane kuwa hakuna nchi masikini imewahi endelea ikIwa chini ya demokrasia. Ukifutilia historia utaona kuwa hakuna nchi imewahi kutoka kwenye umaskini ikiwa inaongozwa kidemokrasia. Nchi zote zilizofanikiwa kutoka kwenye umaskini zimeongozwa kidikteta au kifalme.

Demokrasia ni anasa ya matajiri. Nchi masikini ikiingia kwenye demokrasia inajichimbia kaburi. Kwanza sababu ni kuwa ni gharama kubwa sana kuendesha nchi ya kidemokrasia. Nchi ya kidemokrasia ina walaji wengi sana. Msomi mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya udikteta na demokrasia ni idadi ya watu unaotakiwa kuwaridhisha ili uendelee kushika madaraka. Idadi hiyo ni kubwa sana kwenye demokrasia. Wanaridhishwa kwa kupewa vyeo vingi vilivyoundwa kwa ajili yao. Na mzigo wote wa kuwalipa na kuwagharamia unaangukia nchi ambayo ni maskini.

Serikali ya kidemokrasia haiwezi kuja na sera za maendeleo ambazo zitawataka wananchi wafunge mikanda. Kuna wakati ili nchi iendelee ni lazima watu wafunge mikanda. Mfano nchi inaweza kusema hatutaagiza ngano ila tutahakikisha tunazalisha wenyewe kiasi cha kututosha. Kwenye nchi ya kifalme au kidikteta hilo linaweza kufanyika na baada ya muda nchi ikajitosheleza kwa ngano. Kwenye nchi ya kidemokrasia ngano ikiadimika wiki tu watu watangia barabarani na kuiangusha serikali. Wapinzani watapiga kelele za ajabu. Rais mwenye maono wa Liberia aliangushwa kwa namna hii na nchi ikachukuliwa na watu wazembe kama Samuel Doe. Ukisema tukuze textile industry yetu hivyo tulinde soko letu watu watazama barabarani na kukunyofoa madarakani. Waliotuletea demokrasia walijua vema wanachokifanya.

Kwenye nchi ya kidemokrasia ajenda kuu ya mtawala ni namna ya kubaki madarakani. Maamuzi yake yote yanazingatia kutimizwa kwa ajenda hii, hata kama yapo kinyume na maslahi ya nchi. Mfalme au dikteta anakuwa yupo imara madarakani. Anaweza kuwaza namna ya kukuza uchumi na hivyo kujiongezea kipato.

Nchi kama S Korea, Singapore, Malaysia na Shelisheli zimeweza kutoka kwenye umaskini kupitia madikteta.

Nchi kama UAE, KSA na Brunei zimeweza kufanya vizuri chini ya Ufame.

Bado hakuna nchi ya kidemokrasia iliyojitoa kwenye umaskini. Kila aina ya utawala ina mapungufu yake lakini demokrasia ni mfumo wa hovyo zaidi.

Habari kubwa kwenye nchi za kidemokrasia si za maendeleo, bali habari kuhusu michakato ya kidemokrasia.

DEMOKRASIA NA NCHI ZILIZOENDELEA

Nchi iliyoendelea na inayofuata demokrasia lazima itarudi kwenye umaskini. Nchi ya kidemokrasia iliyoendelea lazima itageuka ya kisocialist. Yaani wananchi wake watakuwa wanadai huduma kutoka kwa serikali kila leo hadi serikali itashindwa kuhudumia. Wananchi watataka afya bure. Mwanasiasa atakaye waahidi hilo wanamchagua. Kesho watadai elimu bure, kesho kutwa mishahara mikubwa, ruzuku wakulima nk nk. Nchi hizi zinajikuta zina matumizi makubwa kuliko mapato. Na wakati huo huo wanachi wakiwachagua wanasiasa wanaowaahidi kodi ndogo. Mwisho zinajikuta zina madeni wasiyoyaweza na deficit(nakisi) kwenye bajeti. Kaangalie nchi zinazodaiwa madeni ya kutisha, utakuta nchi za kidemokrasia zilizoendelea hasa ndizo zinaongoza kwa madeni, wala si nchi maskini zinazotangazwa kila leo. US deni lake ni asilimia 90 ya GDP yake. UK ni kama asilimia 250 wakati China ni kama 13%.

Hili la nchi kushindwa kumudu gharama limetokea kwa Argentina na nchi nyingi zilizoendelea zinaenda muelekeo huo.

Wafanyakazi wa nchi zilizoendelea na zinazofuata demokrasia wanaunda unions, na kudai mishahara mikubwa, benefits na haki nyingi. Matokeo yake gharama za uzalishaji zinakuwa kubwa na nchi kushindwa kushindana na bidhaa za kutoka mataifa mengine kama China. Matokeo yake viwanda vinafunga.

Gharama za kujenga miundombinu kwenye nchi za kidemokrasia ni kubwa sana. China imeziacha mbali sana nchi za magharibi kwenye suala la treni ziendazo kasi. Sababu kubwa ni mchakato mgumu na gharama kubwa za kufanya hivyo kwenye nchi za kidemokrasia. Kwenye nchi za kidemokrasia ukitaka kujenga kitu utakutana na red tapes za maana. Kila kikundi kitatoa sauti zao. Wenye ardhi watagoma reli isipite kwenye mapori yao au watadai fidia za ajabu na kukupeleka mahakamani juu.

Wengi wape lakini wakati mwingine wengi hukosea vibaya sana. Suala la Brexit ni mfano wa hili. Watu wengi walipiga kura UK ijiondoe EU. Leo hii baada ya athari kubwa za Brexit waingereza wengi wanajuta na kusema kuwa suala la Brexit halikuwa sawa. Mambo ya kitaalamu hayapaswi kuendeshwa kidemokrasia.

Demokrasia haifai kwa nchi maskini. Tukae chini tutafute mfumo mwingine.
Umeletwa mada nzuri sana kama unaishi katika mawazo yangu.
Asante sana kwa hoja nzuri zenye nguvu na mifano halisi kiasi kwamba kila mwenye akili ameelewa matatizo ya hili balaa linaloitwa demokrasia tulilowekewa na mabeberu toka ulaya.
Shida ni namna gani tunaweza kubadili mfumo huu muovu ambao unazidi kuzoeleka pamoja na kwamba ni mgumu kutekelezeka na kurudi kwenye utawala wetu wa asili
(utawala wa watemi na machifu )!
 
Umeletwa mada nzuri sana kama unaishi katika mawazo yangu.
Asante sana kwa hoja nzuri zenye nguvu na mifano halisi kiasi kwamba kila mwenye akili ameelewa matatizo ya hili balaa linaloitwa demokrasia tulilowekewa na mabeberu toka ulaya.
Shida ni namna gani tunaweza kubadili mfumo huu muovu ambao unazidi kuzoeleka pamoja na kwamba ni mgumu kutekelezeka na kurudi kwenye utawala wetu wa asili
(utawala wa watemi na machifu )!
Mnayo demokrasia?
Mko katika utawala wa kidemokrasia?
 
Kwa asilimia kubwa Africa haina demokrasia na bado inaongoza kwa umaskini na maendeleo duni.
Kule kutajwa tu kuwa ni Nchi zinazofuata Utawala wa kidemokrasia hata kama haki za kidemokrasia hazifuatwi tayari zimo kwenye matatizo kama alivyofafanua mleta hii mada !!
 
Kule kutajwa tu kuwa ni Nchi zinazofuata Utawala wa kidemokrasia hata kama haki za kidemokrasia hazifuatwi tayari zimo kwenye matatizo kama alivyofafanua mleta hii mada !!
Zikitajwa ni nchi za kidekteta kama hazina udikteta zinakuwa zimeondoka kwenye matatizo??
 
DEMOKRASIA NA NCHI MASIKINI

Leo nakuja tena na hii mada.
Kwanza ijulikane kuwa hakuna nchi masikini imewahi endelea ikIwa chini ya demokrasia. Ukifutilia historia utaona kuwa hakuna nchi imewahi kutoka kwenye umaskini ikiwa inaongozwa kidemokrasia. Nchi zote zilizofanikiwa kutoka kwenye umaskini zimeongozwa kidikteta au kifalme.

Demokrasia ni anasa ya matajiri. Nchi masikini ikiingia kwenye demokrasia inajichimbia kaburi. Kwanza sababu ni kuwa ni gharama kubwa sana kuendesha nchi ya kidemokrasia. Nchi ya kidemokrasia ina walaji wengi sana. Msomi mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya udikteta na demokrasia ni idadi ya watu unaotakiwa kuwaridhisha ili uendelee kushika madaraka. Idadi hiyo ni kubwa sana kwenye demokrasia. Wanaridhishwa kwa kupewa vyeo vingi vilivyoundwa kwa ajili yao. Na mzigo wote wa kuwalipa na kuwagharamia unaangukia nchi ambayo ni maskini.

Serikali ya kidemokrasia haiwezi kuja na sera za maendeleo ambazo zitawataka wananchi wafunge mikanda. Kuna wakati ili nchi iendelee ni lazima watu wafunge mikanda. Mfano nchi inaweza kusema hatutaagiza ngano ila tutahakikisha tunazalisha wenyewe kiasi cha kututosha. Kwenye nchi ya kifalme au kidikteta hilo linaweza kufanyika na baada ya muda nchi ikajitosheleza kwa ngano. Kwenye nchi ya kidemokrasia ngano ikiadimika wiki tu watu watangia barabarani na kuiangusha serikali. Wapinzani watapiga kelele za ajabu. Rais mwenye maono wa Liberia aliangushwa kwa namna hii na nchi ikachukuliwa na watu wazembe kama Samuel Doe. Ukisema tukuze textile industry yetu hivyo tulinde soko letu watu watazama barabarani na kukunyofoa madarakani. Waliotuletea demokrasia walijua vema wanachokifanya.

Kwenye nchi ya kidemokrasia ajenda kuu ya mtawala ni namna ya kubaki madarakani. Maamuzi yake yote yanazingatia kutimizwa kwa ajenda hii, hata kama yapo kinyume na maslahi ya nchi. Mfalme au dikteta anakuwa yupo imara madarakani. Anaweza kuwaza namna ya kukuza uchumi na hivyo kujiongezea kipato.

Nchi kama S Korea, Singapore, Malaysia na Shelisheli zimeweza kutoka kwenye umaskini kupitia madikteta.

Nchi kama UAE, KSA na Brunei zimeweza kufanya vizuri chini ya Ufame.

Bado hakuna nchi ya kidemokrasia iliyojitoa kwenye umaskini. Kila aina ya utawala ina mapungufu yake lakini demokrasia ni mfumo wa hovyo zaidi.

Habari kubwa kwenye nchi za kidemokrasia si za maendeleo, bali habari kuhusu michakato ya kidemokrasia.

DEMOKRASIA NA NCHI ZILIZOENDELEA

Nchi iliyoendelea na inayofuata demokrasia lazima itarudi kwenye umaskini. Nchi ya kidemokrasia iliyoendelea lazima itageuka ya kisocialist. Yaani wananchi wake watakuwa wanadai huduma kutoka kwa serikali kila leo hadi serikali itashindwa kuhudumia. Wananchi watataka afya bure. Mwanasiasa atakaye waahidi hilo wanamchagua. Kesho watadai elimu bure, kesho kutwa mishahara mikubwa, ruzuku wakulima nk nk. Nchi hizi zinajikuta zina matumizi makubwa kuliko mapato. Na wakati huo huo wanachi wakiwachagua wanasiasa wanaowaahidi kodi ndogo. Mwisho zinajikuta zina madeni wasiyoyaweza na deficit(nakisi) kwenye bajeti. Kaangalie nchi zinazodaiwa madeni ya kutisha, utakuta nchi za kidemokrasia zilizoendelea hasa ndizo zinaongoza kwa madeni, wala si nchi maskini zinazotangazwa kila leo. US deni lake ni asilimia 90 ya GDP yake. UK ni kama asilimia 250 wakati China ni kama 13%.

Hili la nchi kushindwa kumudu gharama limetokea kwa Argentina na nchi nyingi zilizoendelea zinaenda muelekeo huo.

Wafanyakazi wa nchi zilizoendelea na zinazofuata demokrasia wanaunda unions, na kudai mishahara mikubwa, benefits na haki nyingi. Matokeo yake gharama za uzalishaji zinakuwa kubwa na nchi kushindwa kushindana na bidhaa za kutoka mataifa mengine kama China. Matokeo yake viwanda vinafunga.

Gharama za kujenga miundombinu kwenye nchi za kidemokrasia ni kubwa sana. China imeziacha mbali sana nchi za magharibi kwenye suala la treni ziendazo kasi. Sababu kubwa ni mchakato mgumu na gharama kubwa za kufanya hivyo kwenye nchi za kidemokrasia. Kwenye nchi za kidemokrasia ukitaka kujenga kitu utakutana na red tapes za maana. Kila kikundi kitatoa sauti zao. Wenye ardhi watagoma reli isipite kwenye mapori yao au watadai fidia za ajabu na kukupeleka mahakamani juu.

Wengi wape lakini wakati mwingine wengi hukosea vibaya sana. Suala la Brexit ni mfano wa hili. Watu wengi walipiga kura UK ijiondoe EU. Leo hii baada ya athari kubwa za Brexit waingereza wengi wanajuta na kusema kuwa suala la Brexit halikuwa sawa. Mambo ya kitaalamu hayapaswi kuendeshwa kidemokrasia.

Demokrasia haifai kwa nchi maskini. Tukae chini tutafute mfumo mwingine.
Kama udictator ndio unaamini unaleta maendeleo, basj africa ilapaswa kuwa mbele sana kimaendeleo maana ndio imejaza madictator..
 
Uzi wa kijinga sana huu.

Inaonekana mleta mada umezaliwa kuanzia mwaka 2000 na kuendelea.

Hivi hujui Tanzania kuanzia 1969 - 1992 tulikuwa hatufuati mfumo wa kidemokrasia kama tuliokuwa nao sasa?

Tuliendelea?

Tumeendelea zaidi baada ya kukumbatia zaidi demokrasia au tulivyokuwa kipindi hicho?

Huwezi kumkuta mtu ambaye amekimbia North Korea anakwambia mfumo wa kidikteta ni mzuri

Wewe unaleta hizi hoja zako hapa kwa sababu you are priviledged individual ambaye hujawahi kuishi kwenye udikteta.

Again huu uzi ni wa kipuuzi mno
 
Umefafanua vizuri sana tena sana 👏👍.
Mimi nimeshachangia mada za namna hii mara nyingi ,
Lakini sina uwezo wa kufafanua kama ulivyofanya wewe,
Ila mimi nilikuwa mara zote nasema kwamba ili tuendelee kwa maendeleo ya kweli kabisa ni lazima aje kupatikana anayeitwa na mabeberu Dikiteta !

Lakini huyo anayeitwa Dikteta awe kwanza ni mcha Mungu, pili Muadilifu na mwenye maono 🙏

Na kusiwepo na hizi chaguzi za kila baada ya miaka mitano kwa ajili ya kiti hicho !

Wazungu ni wajanja wamelazimisha Demokrasia kwenye Nchi changa ili wakwapue mali zao kweri kweri 😳

Ukiisha Uchaguzi watu wanajipanga kwa Uchaguzi utakaofuata !
Business as usual !
Kidole kimoja hakivunji chawa, hapa ili kuendelea ikabidi Afrika karibia nzima iwe na madikteta na sio ilimradi tu madikteta ila madikteta wenye dira ya pamoja
 
NK ilikuwa bora kuliko SK balaah lilianza miaka mwisho wa miaka ya 80s na anguko la Soviet liliizika NK ukichanganya na vikwazo vingi alivyonavyo ndio balaah linazidi.

Ila wakorea wana akili za kuendelea no matter what sema tu vikwazo vinawavuta nyuma kidogo na ndio maana pamoja na vikwazo vyake ila kwa vipimo vingi NK ni bora kuliko nchi nyingi sana za Africa kwa sababu hatuna akili za kuendelea pamoja na kuwa huru nje ya vikwazo vya kimataifa.

Korea zote mbili zimendelezwa kwa udikteta.

East Asians mfumo wa kidikteta upo ndani ya maisha ya unachochochea ni uharaka zaidi wa maendeleo na ndio maana wachina,wajapan,wajorea wana hizi elements popote walipo duniani.

Si ajabu Singapore kuendelea ukikata kuthibitisha hili kamsikilize Lee Kuan Yew akizungumzia vitu gani vinavyowasukuma wachina popote walipo kufikia maendeleo ukihusiana na tamaduni zao.

Je, waafrika tuna hizo akili za kujali maendeleo kama wachina, wajapan,wachina kwa kutumia utamaduni wa kidikteta kimanufaa au tuna tumia udikteta kujinufaisha sisi wenyewe na jamaa zetu waliotuzunguka ? Swali la kujiuliza na kujijibu

Ni mwaka gani huo au at point in history ambao North Korea alikuwa better kiuchumi kuliko South Korea? Em tuelimishe?

Unaposema Korea zote mbili ziliendelezwa kwa udikteta unamaanisha nini?

Kama unamuongelea Park Chung Hee inaonekana huijui kabisa historia ya ile nchi and the science behind the miracle of Han RIver.
 
Uzi wa kijinga sana huu.

Inaonekana mleta mada umezaliwa kuanzia mwaka 2000 na kuendelea.

Hivi hujui Tanzania kuanzia 1969 - 1992 tulikuwa hatufuati mfumo wa kidemokrasia kama tuliokuwa nao sasa?

Tuliendelea?

Tumeendelea zaidi baada ya kukumbatia zaidi demokrasia au tulivyokuwa kipindi hicho?

Huwezi kumkuta mtu ambaye amekimbia North Korea anakwambia mfumo wa kidikteta ni mzuri

Wewe unaleta hizi hoja zako hapa kwa sababu you are priviledged individual ambaye hujawahi kuishi kwenye udikteta.

Again huu uzi ni wa kipuuzi mno
Unataka kusema sasa Tanzania inafuata demokrasia ?

Au unachanganya mabadiliko ya uendeshaji wa uchumi kwa kiasi ndio utofauti wa miaka ya enzi za mwalimu na sasa ?

By the way mabadiliko kadhaa ya uendeshaju wa uchumi hata China wakati wa Deng Xiaoping walifanya haina tofauti na wakati wa Mwinyi ila haimaanishi China waliachana na udikteta na kukumbatia demokrasia hata Tanzania haikuachana na udikteta na kukumbatia demokrasia.

Mfano nbona hiyo demokrasia iliyopo Zambia na Kenya hazijazifanya nchi hizo kuwa hata zaidi ya China ya kidikteta ?
 
Haueleweki unataka mfumo gani ufalme? Hizo nchi ni ndogo sana jaribu kutuletea ufalme hapa kama utaweza!

Kwa hizo nchi tajiri za demokrasia zilizaliwa tajiri ? Mfumo mzuri ndiyo umewapa huo utajiri hata nchi za Europe hazikuwa na demokrasia.

Kuna Korea mbili tuambie ipi tajiri yenye demokrasia au isiyo nayo?
Ametoa mfano wa nchi kama china na Korea! Na Mimi naongezea Japani ,Urusi na nchi za kiarabu zinazotawaliwa kifalme kama Saudi Arabia , Dubai , Kuwait , Emirates nk.
Hizo zote ni nchi tajiri kwa sababu huu upumbavu unaoita demokrasia hawataki kuusikia.
 
By the way mabadiliko kadhaa ya uendeshaju wa uchumi hata China wakati wa Deng Xiaoping walifanya haina tofauti na wakati wa Mwinyi ila haimaanishi China waliachana na udikteta na kukumbatia demokrasia hata Tanzania haikuachana na udikteta na kukumbatia demokrasia.
Sasa kwa nini bado Tanzania ni masikini kama haikuachana na udikteta na kukumbatia demokrasia??
 
Sasa kwa nini bado Tanzania ni masikini kama haikuachana na udikteta na kukumbatia demokrasia??
Umasikini wa Tanzania hauna mahusiano ya udikteta wala demokrasia ni masikini kwa sababu imejaza watu wa wajinga wajinga kama tu ilivyo nchi nyingi za Afrika.
 
Unataka kusema sasa Tanzania inafuata demokrasia ?

Au unachanganya mabadiliko ya uendeshaji wa uchumi kwa kiasi ndio utofauti wa miaka ya enzi za mwalimu na sasa ?

By the way mabadiliko kadhaa ya uendeshaju wa uchumi hata China wakati wa Deng Xiaoping walifanya haina tofauti na wakati wa Mwinyi ila haimaanishi China waliachana na udikteta na kukumbatia demokrasia hata Tanzania haikuachana na udikteta na kukumbatia demokrasia.

Mfano nbona hiyo demokrasia iliyopo Zambia na Kenya hazijazifanya nchi hizo kuwa hata zaidi ya China ya kidikteta ?

We are not fully developed democracy.

Lakini at some point tulikuwa hatufuati demokrasia kabisa na HATUKUENDELEA. So whats your point?

Unachukulia mfano wa China. Lakini ebu pitia G20 pale angalia ni nchi ngapi ambazo zina udikteta zimeingia kwenye ile list.

Acheni kutetea udikteta kama haujwahi kuishi kwenye huo mfumo.
 
Ni mwaka gani huo au at point in history ambao North Korea alikuwa better kiuchumi kuliko South Korea? Em tuelimishe?

Unaposema Korea zote mbili ziliendelezwa kwa udikteta unamaanisha nini?

Kama unamuongelea Park Chung Hee inaonekana huijui kabisa historia ya ile nchi and the science behind the miracle of Han RIver.
Mpaka miaka ya 60 NK ilikuwa mbele ya SK leta hiyo historia ya tofauti inayopinga udikteta na impact yake katika maendeleo ya SK.

Elezea hiyo historia ya SK unayoijua wewe hapa.
 
Ametoa mfano wa nchi kama china na Korea! Na Mimi naongezea Japani ,Urusi na nchi za kiarabu zinazotawaliwa kifalme kama Saudi Arabia , Dubai , Kuwait , Emirates nk.
Hizo zote ni nchi tajiri kwa sababu huu upumbavu unaoita demokrasia hawataki kuusikia.
Kwa nini Nepal, Jordan, Lesotho, Cambodia na Myanmar sio nchi tajiri?
 
Ametoa mfano wa nchi kama china na Korea! Na Mimi naongezea Japani ,Urusi na nchi za kiarabu zinazotawaliwa kifalme kama Saudi Arabia , Dubai , Kuwait , Emirates nk.
Hizo zote ni nchi tajiri kwa sababu huu upumbavu unaoita demokrasia hawataki kuusikia.


Usichanganye kutawaliwa kifalme na kukosa demokrasia

Pia Ungeendelea kuzitaja mkuu hizo nchi, NK ndo nini?

Uko tayari na mimi nikutajie nchi ambazo zina democracy ya kutosha na zina maendeleo makubwa kuliko hizo nchi ulizozitaja?
 
We are not fully developed democracy.

Lakini at some point tulikuwa hatufuati demokrasia kabisa na HATUKUENDELEA. So whats your point?

Unachukulia mfano wa China. Lakini ebu pitia G20 pale angalia ni nchi ngapi ambazo zina udikteta zimeingia kwenye ile list.

Acheni kutetea udikteta kama haujwahi kuishi kwenye huo mfumo.
Sijui ni ujinga gani unaotaka kuhararisha kuhusu Tanzania.

Countries: Argentina, Australia, Brazil, Canada, China, France, Germany, India, Indonesia, Italy, Japan, Mexico, Russia, Saudi Arabia, South Africa, South Korea, Turkey, the United Kingdom, and the United States

Nchi kariba zote hapa zina historia mbaya ya udikteta na impact yake katika maendeleo yao.
 
Back
Top Bottom