Amani Msumari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,830
- 972
Amani mtoto wa Msumari
Amani itawale kwenu.
Nimekaa na kutafakari sana kuhusu demokrasia. Jambo ambalo kwa hakika siwezi kulipinga ni ule ukweli kuwa, vyovyote vile, demokrasia ni jambo la muhimu sana kwenye jamii yoyote. Shida yangu iko kwenye dhana na maana ya demokrasia.
Dunia imepitia mambo mengi sana na hii ikazaa makubaliano ya kutenda mambo angalau kwa mfanano fulani (common practice). Hatahivyo, linapokuja suala la muktadha ni muhimu kuzingatiwa.
Hebu twendeni taratibu huku tukizitazama nchi ambazo zinajisema kuwa na demokrasia. Nchi za magharibi zipo kundi hili. Ukiangalia kwakina, utaona demokrasia yao imefungamanishwa na utamaduni, uchumi na mazingira yao.
Ni haki ya kila mtu kuwa huru kusema anachojisikia, hata kumdhalilisha Rais wa nchi, ni sawa tuu. Kwenye utamaduni wetu inaruhusiwa kumkosoa mtu mzima au kiongozi lakini kuna staha, miiko na taratibu za kufanya hivyo. Watu wetu wanaopiga kelele kuhusu demokrasia wanataka hii ibebwe kama ilivyo (copy and paste).
Ulaya na Marekani wanafanya hivyo, na sisi tufanye. HAPANA! uko wapi utamaduni wetu? Kwanini tulazimishe kuiga wengine? Kwetu, mtu mzima na kiongozi anautaratibu wake wa kumkosoa. Hatulazimiki kufanana nao.
Ulaya na nchi za magharibi huruhusiwi kumuadhibu mtoto wako. Ikifahamika, unachukuliwa hatua ikiwemo na kunyang'anywa mtoto kama itabidi. Wapiga chapuo wa demokrasia ya Magharibi wanataka haya kwetu. Copy & paste kama walivyotaka kulishughulikia janga la virusi vya korona.
Demokrasia ya magharibi inatambua haki za mtu ni pamoja na kufanya vile anavyojisikia kwenye mwili wake. Kama mwanaume ameona aolewe ni sawa tuu na sheria inamlinda na yuko huru kuonesha hivyo hadharani.
Napata taarifa kuwa huko ulaya na America ni kitu cha kwaida shuleni watoto wa jinsia moja kuwa wapenzi. Wazazi wao wapo, walimu wao wapo, serikali zao zipo na jamii zao zipo. Wenzetu hawa ndiko wanakokusudia kutupeleka.
Ukisoma historia, demokrasia inatajwa kuanzia Uingereza. Watu walikuwa wanapiga kura za wazi, baadae ikapendekezwa kura za siri ( secret ballots). Mchakato ulikuwa mrefu lakini ulioendana na mila, desturi na utamaduni wao. Sio lazima tufanane.
Huko magharibi kampeni zao za kisiasa sio tena kuleta maji, umeme, barabara, kujenga shule na hospitali. Wao wameshavuka huko. Sisi tunapambana kufika huko. Tunapambana huku tukilinda mila, desturi na taratibu zetu nzuri. Sio lazima tufanane.
Kama taifa, tunazo tunu zetu. Hizo ndio za kuangalia. Sisi hatusubiri kucheleweshwa na maadui wa ndani na nje. Sisi tumeamua kufa na kupona kufanya mambo yenye tija na maslahi kwa Tanzania na Afrika ya Leo na kesho.
Wenzetu wanaojitambua Kama akina Singapore, Taiwan, Russia, Malaysia,Japan n.k walishaliona hilo muda mrefu. Wanayo demokrasia waliyoitafsiri wao, kwaajili yao. Wananchi wao ni wazalendo kwelikweli. Wazalendo kwa vitendo.
Rejeeni mifano ya demokrasia iliyotafsiriwa na kulazimishwa huko Iraq,Libya, Tunisia, Egypt, Syria n.k.
Demokrasia yetu ni lazima iendana na mila, desturi na utamaduni wetu.
Amani Msumari
Tanga
Amani itawale kwenu.
Nimekaa na kutafakari sana kuhusu demokrasia. Jambo ambalo kwa hakika siwezi kulipinga ni ule ukweli kuwa, vyovyote vile, demokrasia ni jambo la muhimu sana kwenye jamii yoyote. Shida yangu iko kwenye dhana na maana ya demokrasia.
Dunia imepitia mambo mengi sana na hii ikazaa makubaliano ya kutenda mambo angalau kwa mfanano fulani (common practice). Hatahivyo, linapokuja suala la muktadha ni muhimu kuzingatiwa.
Hebu twendeni taratibu huku tukizitazama nchi ambazo zinajisema kuwa na demokrasia. Nchi za magharibi zipo kundi hili. Ukiangalia kwakina, utaona demokrasia yao imefungamanishwa na utamaduni, uchumi na mazingira yao.
Ni haki ya kila mtu kuwa huru kusema anachojisikia, hata kumdhalilisha Rais wa nchi, ni sawa tuu. Kwenye utamaduni wetu inaruhusiwa kumkosoa mtu mzima au kiongozi lakini kuna staha, miiko na taratibu za kufanya hivyo. Watu wetu wanaopiga kelele kuhusu demokrasia wanataka hii ibebwe kama ilivyo (copy and paste).
Ulaya na Marekani wanafanya hivyo, na sisi tufanye. HAPANA! uko wapi utamaduni wetu? Kwanini tulazimishe kuiga wengine? Kwetu, mtu mzima na kiongozi anautaratibu wake wa kumkosoa. Hatulazimiki kufanana nao.
Ulaya na nchi za magharibi huruhusiwi kumuadhibu mtoto wako. Ikifahamika, unachukuliwa hatua ikiwemo na kunyang'anywa mtoto kama itabidi. Wapiga chapuo wa demokrasia ya Magharibi wanataka haya kwetu. Copy & paste kama walivyotaka kulishughulikia janga la virusi vya korona.
Demokrasia ya magharibi inatambua haki za mtu ni pamoja na kufanya vile anavyojisikia kwenye mwili wake. Kama mwanaume ameona aolewe ni sawa tuu na sheria inamlinda na yuko huru kuonesha hivyo hadharani.
Napata taarifa kuwa huko ulaya na America ni kitu cha kwaida shuleni watoto wa jinsia moja kuwa wapenzi. Wazazi wao wapo, walimu wao wapo, serikali zao zipo na jamii zao zipo. Wenzetu hawa ndiko wanakokusudia kutupeleka.
Ukisoma historia, demokrasia inatajwa kuanzia Uingereza. Watu walikuwa wanapiga kura za wazi, baadae ikapendekezwa kura za siri ( secret ballots). Mchakato ulikuwa mrefu lakini ulioendana na mila, desturi na utamaduni wao. Sio lazima tufanane.
Huko magharibi kampeni zao za kisiasa sio tena kuleta maji, umeme, barabara, kujenga shule na hospitali. Wao wameshavuka huko. Sisi tunapambana kufika huko. Tunapambana huku tukilinda mila, desturi na taratibu zetu nzuri. Sio lazima tufanane.
Kama taifa, tunazo tunu zetu. Hizo ndio za kuangalia. Sisi hatusubiri kucheleweshwa na maadui wa ndani na nje. Sisi tumeamua kufa na kupona kufanya mambo yenye tija na maslahi kwa Tanzania na Afrika ya Leo na kesho.
Wenzetu wanaojitambua Kama akina Singapore, Taiwan, Russia, Malaysia,Japan n.k walishaliona hilo muda mrefu. Wanayo demokrasia waliyoitafsiri wao, kwaajili yao. Wananchi wao ni wazalendo kwelikweli. Wazalendo kwa vitendo.
Rejeeni mifano ya demokrasia iliyotafsiriwa na kulazimishwa huko Iraq,Libya, Tunisia, Egypt, Syria n.k.
Demokrasia yetu ni lazima iendana na mila, desturi na utamaduni wetu.
Amani Msumari
Tanga