Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,540
Benki Kuu imetoa ripoti yake kwa ajili ya mwaka wa fedha 2007/2008 ambayo inaonyesha deni la Taifa kuongezeka kwa takriban 25% katika mwaka mmoja! Deni letu la nje bado ni kubwa ingawa deni la ndani linapungua.
Deni hili la Taifa ni 33% ya GDP ya nchi.
Je deni hili linaloongezeka kila siku ni nani atalilipa na ni lini litalipwa?
Ama ni kwa nini deni hili linalongezeka kutokana na kuendelea kukopa na riba itokanayo na mikopo ambayo tayari bado iko katika vitabu na majedwali ya mapato na matumizi ya nchi yetu?
Nimetatizwa sana na kauli ya Naibu Waziri wa Fedha Jeremiah Sumari ambaye amedai kuwa tusiwe na shaka kuhusu kuongezeka kwa deni hili na ni deni ambalo tunaweza kulihimili na kulilipa! Zaidi ni kitendo cha Sumari kudai kuwa kuna nchi nyingine ambazo zina uwiano mkubwa wa Deni lao la Taifa kuliko Tanzania hivyo hakuna haja ya kuogopa!
Je wewe Mtanzania mwenzangu unaipokeaje kauli hii ya kusema usiwe na wasiwasi tunaendelea kukopa huku hali halisi ni kuwa hatuna nguvu za kiuzalishaji mali na ukusanyaji mapato ambazo zitalipa Taifa pato la kuweza kujitegemea na kupunguza mzigo huu wa kutegemea mikopo na misaada kujiendesha?
Kama unaridhika na kauli ya Sumari, basi nakwambia wazi kuwa wewe utaendelea kuwa masikini na ombaomba na kamwe hutaweza kujitutumua na kujitegemea.
Kama umeshikwa na hasira kama Mchungaji ya kusikia kauli hasi kutoka kwa kiongozi mkubwa kama huyu, basi itakulazimu ujiulize ni vipi tunaendelea kukopa na hata kuongeza deni na ni nani anayetuongezea mzigo huu wa deni hili!
Je ni wewe Mtanzania au ni Viongozi ambao wamekosa mwamko wa kujenga uchumi unaojitegemea?
Tunapofikia mahali tunajigamba kuwa deni letu ni bora kuliko la Rwanda, Kenya hata Msumbiji, tujiulize je nao wana rasilimali sawa na zetu? je uzalishaji mali wetu wa ndani ni sawa? je mikopo na deni ni kutokana na matumizi sawa na kimaendeleo?
Nina uhakika kwa asilimia 85% kuwa sehemu kubwa ya mikopo (70%) imetumika kwa matumizi yasiyo ya lazima na yangeweza kupunguzwa.
Cha kutisha ni kuwa Tanzania si kwamba haina fedha wala uwezo wa kujitegemea, bali ni mazoea mabaya ya kukopa ambayo yamejenga mizizi mibaya inayoeta uzembe na hata ufisadi na hivyo dhana ya kuwa wabanifu na kutumia kwa uangalifu tulicho nacho haiko tena.
Tatizo kubwa la Serikali ya Tanzania ni matumizi yasiyo na kikomo wala kuwa na hamasa ya kubana matumizi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima au kama wenzetu wanavyoyaita Wasteful spending!
Mfano wa matumizi yasiyo na faida wala manufaa ni Serikali kung'ang'ania kuwa mshiriki wa uzalishaji mali katika sekta ambazo kuna ushindani tosha wa sekta binafsi. Hili husababisha kuanzishwa kwa mashirika, taasisi na miradi ambayo inaweza kufanya na watu binafsi na Serikali wajibu wake uwe ni kwenye uratibu.
La zaidi katika matumizi mabovu na yasiyo ya lazima ni kule kuhalalisha vitu ambavyo vinaweza kufanywa kwa kutumia teknolojia ya simu, barua pepe au watendaji wachache.
Mfano, kuna tabia kubwa ya kukimbilia kuandaa makongamano, semina, warsha na hata mikutano isiyo na ulazima ambayo hutumia fedha nyingi za walipa kodi na kudonoa fungu la misada na mikopo ambalo lilipaswa kutumika kwa miradi ya kimaendeleo na kuishia kuwa matumizi ya kawaida. Kwenye hivi vikao, kuna malipo ya usafiri na malazi, kushiriki kikao na mengineyo kwa ajili ya watu ambao hulipwa mishahara kwa kufanya kazi ambazo ni wajibu wao.
Ama misafara ya kila mtu inapofika mahali kiongozi anafanya ziara ya kutembelea sehemu, utakuta kuna zaidi ya watu 100 ambao kazi yao ni upambe kwa kudai eti wanapaswa kuandamana na kiongozi.
Sasa matumizi kama haya, yanaipunguzia Serikali mapato ukiongezea uzalishaji mali wetu ulio duni na wa kijima ambao hauna uwezo imara kusimama kidete katika ushindani wa kimataifa.
Rushwa na Takrima nayo ni mchangiaji mkubwa wa kukua kwa deni letu. Mwaka 2007, asilimia 20% ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya Bajeti zilipotea katika mazingira ya rushwa. Mwaka uliofuatia, Rushwa katika ufujaji wa bajeti uliongezeka kwa asilimia 10% hivyo kufanya upotevu wa Bajeti katika miaka miwili kuwa asilimia 50%!
Sasa kama tunapoteza mapato na kufuja hazina yetu kwa kiwango hiki, iweje Sumari atuambie tusiwe na wasiwasi tunapoona deni la Taifa linaongezeka?
Ninauliza ni nani atalilipa deni hili huku hata uzalishaji mali ni duni, rasilimali tunazitapanya na mapato kupitia kodi ni madogo kutokana na kutoa misamaha ya kodi na ukosefu wa uhakiki wa mapato ya wawekezaji?
Kama tungepunguza matumizi na mfumuko wa deni, tungeongeza kipato cha Mtanzania hata kwa asilimia 25% ya kima cha chini, hii ni zaidi ya shughuli nyingine za maendeleo na ulazima kama elimu, afya, miundombinu na hata nishati.
Kauli ya Sumari inanifanya niamini kuwa kamwe kama hatuta leta mabadiliko ya kweli ndani ya mfumo wetu wa kisiasa na utendaji kazi na maendeleo, tutaendelea kujilundikia madeni.
Sumari katuambia, pondamali kufa kwaja, je nawe wakubali hilo? mwanao na mjukuu wataishije?
Deni hili la Taifa ni 33% ya GDP ya nchi.
Je deni hili linaloongezeka kila siku ni nani atalilipa na ni lini litalipwa?
Ama ni kwa nini deni hili linalongezeka kutokana na kuendelea kukopa na riba itokanayo na mikopo ambayo tayari bado iko katika vitabu na majedwali ya mapato na matumizi ya nchi yetu?
Nimetatizwa sana na kauli ya Naibu Waziri wa Fedha Jeremiah Sumari ambaye amedai kuwa tusiwe na shaka kuhusu kuongezeka kwa deni hili na ni deni ambalo tunaweza kulihimili na kulilipa! Zaidi ni kitendo cha Sumari kudai kuwa kuna nchi nyingine ambazo zina uwiano mkubwa wa Deni lao la Taifa kuliko Tanzania hivyo hakuna haja ya kuogopa!
Je wewe Mtanzania mwenzangu unaipokeaje kauli hii ya kusema usiwe na wasiwasi tunaendelea kukopa huku hali halisi ni kuwa hatuna nguvu za kiuzalishaji mali na ukusanyaji mapato ambazo zitalipa Taifa pato la kuweza kujitegemea na kupunguza mzigo huu wa kutegemea mikopo na misaada kujiendesha?
Kama unaridhika na kauli ya Sumari, basi nakwambia wazi kuwa wewe utaendelea kuwa masikini na ombaomba na kamwe hutaweza kujitutumua na kujitegemea.
Kama umeshikwa na hasira kama Mchungaji ya kusikia kauli hasi kutoka kwa kiongozi mkubwa kama huyu, basi itakulazimu ujiulize ni vipi tunaendelea kukopa na hata kuongeza deni na ni nani anayetuongezea mzigo huu wa deni hili!
Je ni wewe Mtanzania au ni Viongozi ambao wamekosa mwamko wa kujenga uchumi unaojitegemea?
Tunapofikia mahali tunajigamba kuwa deni letu ni bora kuliko la Rwanda, Kenya hata Msumbiji, tujiulize je nao wana rasilimali sawa na zetu? je uzalishaji mali wetu wa ndani ni sawa? je mikopo na deni ni kutokana na matumizi sawa na kimaendeleo?
Nina uhakika kwa asilimia 85% kuwa sehemu kubwa ya mikopo (70%) imetumika kwa matumizi yasiyo ya lazima na yangeweza kupunguzwa.
Cha kutisha ni kuwa Tanzania si kwamba haina fedha wala uwezo wa kujitegemea, bali ni mazoea mabaya ya kukopa ambayo yamejenga mizizi mibaya inayoeta uzembe na hata ufisadi na hivyo dhana ya kuwa wabanifu na kutumia kwa uangalifu tulicho nacho haiko tena.
Tatizo kubwa la Serikali ya Tanzania ni matumizi yasiyo na kikomo wala kuwa na hamasa ya kubana matumizi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima au kama wenzetu wanavyoyaita Wasteful spending!
Mfano wa matumizi yasiyo na faida wala manufaa ni Serikali kung'ang'ania kuwa mshiriki wa uzalishaji mali katika sekta ambazo kuna ushindani tosha wa sekta binafsi. Hili husababisha kuanzishwa kwa mashirika, taasisi na miradi ambayo inaweza kufanya na watu binafsi na Serikali wajibu wake uwe ni kwenye uratibu.
La zaidi katika matumizi mabovu na yasiyo ya lazima ni kule kuhalalisha vitu ambavyo vinaweza kufanywa kwa kutumia teknolojia ya simu, barua pepe au watendaji wachache.
Mfano, kuna tabia kubwa ya kukimbilia kuandaa makongamano, semina, warsha na hata mikutano isiyo na ulazima ambayo hutumia fedha nyingi za walipa kodi na kudonoa fungu la misada na mikopo ambalo lilipaswa kutumika kwa miradi ya kimaendeleo na kuishia kuwa matumizi ya kawaida. Kwenye hivi vikao, kuna malipo ya usafiri na malazi, kushiriki kikao na mengineyo kwa ajili ya watu ambao hulipwa mishahara kwa kufanya kazi ambazo ni wajibu wao.
Ama misafara ya kila mtu inapofika mahali kiongozi anafanya ziara ya kutembelea sehemu, utakuta kuna zaidi ya watu 100 ambao kazi yao ni upambe kwa kudai eti wanapaswa kuandamana na kiongozi.
Sasa matumizi kama haya, yanaipunguzia Serikali mapato ukiongezea uzalishaji mali wetu ulio duni na wa kijima ambao hauna uwezo imara kusimama kidete katika ushindani wa kimataifa.
Rushwa na Takrima nayo ni mchangiaji mkubwa wa kukua kwa deni letu. Mwaka 2007, asilimia 20% ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya Bajeti zilipotea katika mazingira ya rushwa. Mwaka uliofuatia, Rushwa katika ufujaji wa bajeti uliongezeka kwa asilimia 10% hivyo kufanya upotevu wa Bajeti katika miaka miwili kuwa asilimia 50%!
Sasa kama tunapoteza mapato na kufuja hazina yetu kwa kiwango hiki, iweje Sumari atuambie tusiwe na wasiwasi tunapoona deni la Taifa linaongezeka?
Ninauliza ni nani atalilipa deni hili huku hata uzalishaji mali ni duni, rasilimali tunazitapanya na mapato kupitia kodi ni madogo kutokana na kutoa misamaha ya kodi na ukosefu wa uhakiki wa mapato ya wawekezaji?
Kama tungepunguza matumizi na mfumuko wa deni, tungeongeza kipato cha Mtanzania hata kwa asilimia 25% ya kima cha chini, hii ni zaidi ya shughuli nyingine za maendeleo na ulazima kama elimu, afya, miundombinu na hata nishati.
Kauli ya Sumari inanifanya niamini kuwa kamwe kama hatuta leta mabadiliko ya kweli ndani ya mfumo wetu wa kisiasa na utendaji kazi na maendeleo, tutaendelea kujilundikia madeni.
Sumari katuambia, pondamali kufa kwaja, je nawe wakubali hilo? mwanao na mjukuu wataishije?
ational debt stock increases
FARAJA MGWABATI, 29th August 2009 Daily News
THE national debt stock has increased by 23.1 per cent owing to exchange rate fluctuations, accumulated arrears, recording of new disbursements and new domestic debts.
According to the Bank of Tanzania (BoT) recent published annual report for 2007/08, the country's external debt increased by 25.4 per cent but the domestic debt decreased slightly.
Total debt as of June 2008 stood at 7.6 million US dollars (over 7.6bn/-) from 6.2 million dollars (over 6.2bn/-) registered at the end of 2007.
Commenting on the data, the Deputy Minister for Finance and Economic Affairs, Mr Jeremiah Sumari, said that the debt, which accounts for 33 per cent of the Gross Domestic Product (GDP), was still manageable compared to cases in some neighbouring countries.
He said the best way to service the debt is to honour the terms and conditions attached to it which Tanzania is comfortably in compliance with.
Sumari said that increase in National Debt should not scare people because it depends on the government's expenditure needs in a particular period."Let us not be worried by this increase. It is still manageable. Some countries have debts between 40 and 70 per cent of their GDP," he said.
However, the deputy minister said that the government is careful in its borrowing because it is aware that excessive practice means more spending-- which, consequently, increases the money in circulation and hence a rise in the inflation rate.
The BoT report indicates that the external debt which accounts for 77 per cent of the whole debt increased from 4.7 million dollars to 5.8 million dollars."Out of the total debt stock, principal and interest arrears were 1.1 million US dollars and 1.4 million dollars respectively," says the report.
The profile of disbursed outstanding debt (DOD) creditors indicates that multilateral, bilateral, commercial debt and export credit accounted for 58.4 per cent, 20.8 per cent, 13.8 per cent and 6.9 per cent respectively.
"
The high proportion of multilateral debt is attributed to the government's policy of borrowing concessional loans mainly offered by the International Development Association (IDA) and the African Development Fund (ADF).
However, the report indicates that there has been improvement on the country's indebtedness following debt relief obtained under the Enhanced HIPC Initiative and the Multilateral Debt Relief Initiative (MDRI).
The report shows that in the composition of DOD by borrower category, the Central Government remained higher at 79.9 per cent, while that of private and parastatal companies were 16.6 per cent and 3.5 per cent respectively.
BoT says the government securities accounted for 99.6 per cent of the total domestic debt stock.During the year under review, a total of 1.1bn/- fell due for payment. The amount represents an increase of 2.2 per cent compared to amount paid the previous year.