Bavaria
JF-Expert Member
- Jun 14, 2011
- 53,092
- 53,496
Bora turudie maisha ya vibubu
Nadhani kukimbia tatizo sio solution, huwezi kuweka milion 100 kwenye kibubu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Bora turudie maisha ya vibubu
Tarehe 15 August saa 12 Asubuhi nimeibiwa laki 700,000/= kwa ATM ya NMB mtu akiwa Mbulu wakati me nipo Dar nimelala na kadi ipo kwenye draw ime-expire,kilichonishtua ni NMB MOBILE!!!!
Nikawafuata NMB wakaanza longo longo,oh mara huenda ni ndugu yangu,blah blah kibao,nimekomaa nao Sasa wanasema fraud unit yao na Police wanafuatilia na mfanya kazi wao Mbulu ni prime suspect,nivute subira!!!
Nadhani kukimbia tatizo sio solution, huwezi kuweka milion 100 kwenye kibubu
Wafanyakazi wa benki ndio wahusika wakubwa kwenye wizi wa aina hii. Nilishaibiwa pesa kutoka kwenye ATM bahati yangu sikuwapo tz na ushahidi nilikuwa nao. Cha kushangaza zaidi cctv haikuwa inafanya kazi wakati huyo mwizi akiiba. Sidhani kama mwizi anaweza temper na security cameras za bank bila usaidizi wa bank employees.
Hivi pesa zinazoibwa ni za personal Account only?
Wafanyakazi wa bank baadhi yao hujihusisha na wizi wa fedha za wateja wao na wizi mkubwa tu wa mapesa chungu nzima.
Mafanyakazi ya NMB ni majizi makubwa. Kuna mwaka fulani mkururo wa mafanyakazi majizi walifutwa kazi na wengine kukimbia na mamilioni ya fedha za wateja na mpaka sasa hawajulikani walipo. Kuna jamaa yangu aliwahi kupigwa sh laki 1.5 akwashtukia na kuwawakia...wakamwambia asubiri baada ya nusu saa...alipoenda kuangalia kwenye akaunti akakuta wame zirejesha. Ningekuwa mimi nisingekubali...lazima ningezaa na huyo mwizi... wamezidi bhana, aaah!
Ukiwa na pesa nyingi benki lazima uwe makini sana, hasa wale mamilionea ni rahisi sana kupigwa 3k, 5k, 8k, etc, na wasigundue. Hata akaunti za makampuni makubwa au serikali huchakachuliwa pesa nyingi sana ha hao majizi wa NMB....hii sio benki ya kuaminika hata kidogo...wafanyakazi wake ni MAFISADI kuliko unavyoweza kudhani....wana njaa kama za fisi mwenye njaa kali. Kuweni makini na wafanyakazi wa benki ya NMB kuliko hata hao cyber criminals wanaotumia IT kunyonya fedha. hawa wa NMB ni balaaaa...ni shidaaaaaaaa!!! Imagine mtu akinyonya 2k kutoka kwa wateja 20 atakuwa na bei gani? Si anaweza hata kujenga nyumaba kabisa? Ndio maana utakuta mfanyakzi wa benki mwenye mshahara wa laki 5 anaishi maisha mabayo hayaendani na mmshahara wake...kumbe ni wizi wa fedha za wateja ndio unawaweka mjini. Be careful with bank workers than cyber criminals!
Bahati mbaya Mkuu BAK hakuna atakayekubali ukweli huu. Kuna benk huwa wananikata elfu tani kila mwezi kuna mwezi karibia mara tatu nimekuta nimekatwa buku mbili mara buku tatu maana ile system yao ni kila transaction inayofanyika wana ku-alert kwa sms.......nimekaa kimya tu
Hizi ni pesa zako Mkuu Elli ambazo unazitolea jasho. Fuatilia bank ili ujue kitu kinachoendelea una kila haki ya kujua kama hayo makato ni ya kihalali au ni wizi. Kama yanafanywa na mfanyakazi wa bank ambaye si mwaminifu akifanya hivyo kila wiki kwa wateja 100 wa bank anajipatia pesa nzuri sana ya yeye kutanua kwa raha zake.
Bora turudie maisha ya vibubu
hili ndio nazungumzia watu wapewe terms and conditions za kufungua na kuendesha account pamoja na any fees associated with operation and maintenance of the account .... kimaandishi!!!!
Hivi pesa zinazoibwa ni za personal Account only?