Na ndio maana nikasema "Najua kuna wanaopitia makubwa zaidi yangu ila mambo madogo madogo kama haya psychologically ni harmful" .. anyway Asante kwa mchango wakoUpumbavu tu.. watu wana magonjwa ya kudumu wanavumilia we masikio unataka ujiue mattako kabisa wewe
Nashukuru mkuuKadri unavyokua yanapungua ukifikisha miaka 25 utasahau kabisa kama uliwahi kua bullied sababu ya hayo masikio, maana mwili utakua mkubwa umejaa nyama nyama kwa hiyo hata masikio hayataonekana,
Mara nyingi watu wenye huzuni maisha mwao hupenda ku bully wenzao wakiamini wanapata ahueni ya matatizo yao muhimu ni kuwadharau na kusonga mbele,
Usijali kitu mdogo wangu, dunia ni nzuri sana huna haja ya kujiua sababu kufa kwako sio mwisho wa hao kubully wengine, wataendelea kwa hivyo kifo chako hakitakua na maana.
Wewe ni Shujaa.
Usife kijinga.Na ndio maana nikasema "Najua kuna wanaopitia makubwa zaidi yangu ila mambo madogo madogo kama haya psychologically ni harmful" .. anyway Asante kwa mchango wako
Ubarikiwe sana mkuuPole na hongera ndugu kwa changamoto. Pole kwa sababu imekuwa ni mzigo kwa muda sasa. Hongera kwa sababu bado naona unaweza kucheka na kutabasamu licha ya hayo. Nianze kwa kusema ACHANA na wazo la kujiua. Kanuni moja ya maisha ni kuwa unaweza kugawa MAMLAKA yako kwa watu wengine kama UTAKUBALI furaha yako iongozwe na maoni waliyonayo juu yako; au unaweza kutwaa na kutawala MAMLAKA yako kama UTAKATAA kuongozwa na nini wasemacho watu kuhusu wewe. By any means simaanishi ni jambo rahisi lakini kama njia pekee ya kufika kisiwani ni mtumbwi, woga wa maji si jibu bali ni lazima ukubali kuwa jasiri. Rafiki - UNAWEZA. Funga vioo. Wanadamu hawataacha kusema. Acha waseme. Cheka na uchukulie easy kama ulivyofanya kwa jamaa mmojawapo. Hiyo ndiyo pona yako. Jiwekee malengo ya maisha yako na kakamaa kuyaendea hayo - ije mvua, lije jua. ACHANA NA WANADAMU BWANA! Aliyekuumba anakupenda na yapo mengi aliyoweka ndani yako. Hata mtu akisoma namna ulivyoandika post yako, aliye makini anaona kabisa kichwa chako kinafanya kazi. USIMPE MTU USUKANI WA KESHO YAKO. SHIKILIA USUKANI WAKO NA USONGE MBELE. Umebarikiwa na Aliye juu. Hiyo ni hakika kabisa.
Ni mengi tu bwana mdogo.Dunia Ina mengi hii we acha tu.Pole sana mkuu, ila mambo mbali mbali kama yapi ?
Binadamu sometimes tunachezewa tu kisaikolojia, mtu anaweza kukutamkia kuwa kitu fulani ni tatizo na wewe ukaathirika kabisa kisaikolojia.Hata ambao hatuna chura tunasimangwa kweli sio wewe tu hebu jiamini wewe mwanaume anatakiwa awe na sura mbaya ya kutishaaa
Asante sana mkuuKuna dogo walikuwa wamepanga nyumbani alikuwa na masikio lakini sio Kama yako ya kwake yalikuwa yamebana na yaani Kama akivaa miwani kunakuwa hakuna sehemu ya miwani kukaa na alikuwa na akili sana kwa maana kwamba akifocus na kitu anakijua kweli, alipokuwa mdogo alikomaa na dini na akaijua haswa na alipoanza secondary alikomaa na elimu haswa na alikuwa very bright bahati mbaya kadri alivyokuwa anakuwa mkubwa akaanza kujishtukia kuhusu masikio yake, hali ambayo ilianza kumfanya akae nyuma ya darasa ili wenzie wasione masikio yake, ikafikia hatua mtu akawa akiwa mbele yake basi atasubiri apitwe ili mtu asimuone masikio yake hakuna mtu aliyejali kwao ikafikia hatua akaamaua kuacha shule akiwa form four licha ya uwezo mzuri darasanina kushinda kavaa mizura tu mpaka sasa yupo kitaa tu Hana Cha maana lakini angepata ushauri wa kueleweka asingekatisha ndoto zake. Kwa upande wangu nadhani ukifika umri Fulani wa balehe unakua Kama kijana unajali sana kuhusu muonekano hata mimi niliwahi pitia hali hiyo kutokana na machunusi usoni ingawa sikupata bullying Ila nilikuwa najishtukia naamini baada ya kipindi hichi Cha makuzi kupita utaona kawaida tu vyovyote vile ulivyo. Ukiendekeza hali hiyo utashindwa kabisa kutongoza kwa kukosa kujiamini.Tafuta kitabu kinaitwa four agreement by Don Miguel kitaiusaidia sana
Nashukuru mkuuDuniani huwa hakuna jambo baya wala zuri.....! Ila kinachofanya jambo lionekana ni baya au zuri ni mtazamo wa watu tu....! Ndio maana hata kwenye jamii zetu tunatofautiana tamaduni, kuna tamaduni za jamii nyingine ni mbaya sana kwa jamii fulani lakini jamii husika inafurahis sana tamaduni zao, na ukiwambia kuwa tamaduni zenu ni mbaya hawatokuelewa....!
Na Sisi binadamu tulivyoumbwa tumepewa utashi wa kuamua jambo lolote kutoka ndani mwetu...! Kile kinachotawala akili yako ndicho utachokiishi katika maisha yako.
Sasa wewe inaonekana unapoteza muda kuifanya akili yako iwaze jinsi unavyofanyiwa ukatili wa kisaikolojia, na hali hiyo haitobadilika kamwe mpaka wewe mwenyewe ubadili mtazamo.....!
Kuanzia sasa akili yako iwe inawaza vile vitu unavyovipenda tu, vitu usivyovihitaji usivipe nafasi kabisa kwenye akili yako...! Kwa mfano unaweza ukawa unahitaji sana heshima na upendo toka kwa watu, sasa ili upate hiyo heshima na upendo inatakiwa kwanza ww uanze kujipenda na kujiheshimu...
Anza kujikubali na ujione wa kipekee sana hapa duniani, jiulize kwanini ww Mungu ameamua kukufanya tofauti na watu wengi? Bro wewe una bahati sana ujue, yaani katika mkusanyiko wa watu 1000 wewe unauwezo wa kuonekana kati ya wote. Hiyo ni bahati bro .
Ww ndio muamuzi wa maisha yako, wewe ndio muamuzi wa furaha yako, si baba yako wala mama yako.....! Anza kujipa thamani kwanza wewe mwenyewe, then sisi wengine ndio tuione hiyo thamani uliyoitengeneza....! Usitegemee kuonewa huruma Ikiwa ww mwenyewe hujiamini wala kujikubali.!
Asante mkuu1. Tafuta mtu ambae ana uelewa mpana wa mambo haya( anaweza kuwa mtaalamu) Mueleze tatzo lako
2.muone mtu ambae anaweza kukusikiliza na kukusaidia.
Kwanza mchunguze atalipokeaje swala lako
3. Sikushauri hili swala umuelezee mtu ambae hatakuwa na msaada. > Watu wengine hali yako wanaweza kuchukulia ni kitu cha kawaida, wakakupa majibu kama
"Tafuta hela kijana"
"We bado mdogo, soma"
"Hicho ni kitu kidogo, fanya mambo yako...."
"Mbona mimi Sina ............ Ila nafanya mambo yangu tuu"
Nk. Lakini kumbe wanakosea, depression, suicidal thoughts zinaweza kumpata mtu kama matokeo ya jambo lolote.
Mwingine ni body appearance tuu, mwingine ni economic reason, mwingine mi relationship problems.
Wakati huohuo kuna watu wengine watapitia matatizo hayo lakini bado watakuwa vizuri.
Bado kwenye jamii yetu elimu ya afya ya akili iko nyuma.
Hii inafanya wenzetu, wanaopatwa na matatizo haya, wasijue wapi wanapata msaada.(wengi wanakata tamaa ya kuishi)
Lakini pia, jamii haijui ni vipi inaweza kuwasaidia wenye matatizo haya
Mwisho tunaishia kuwatia moyo( hii haisaidii sana) au kuwavunja moyo.
Sawa mkuu ngoja nifanye hivoPole Sana noble.Dunia tupo wengi tunaopitia magumu ambayo yanatuacha na option moja tu.
Lakini usijidhuru kikubwa kubaliana na Hali kuwa wewe ni mtu tofauti.
Pitia uzi wangu kwenye bio uone ninachopitia pia lakini nipo najipa moyo tu